< 2 Samweli 24 >
1 Kisha hasira ya Yahwe ikawaka dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi kinyume chao kusema, “Nenda, ukawahesabu Israeli na Yuda.”
Yahweh was angry with the Israeli people again, so he incited David to cause trouble for them. He said to David, “Send [some men] to count the people of Israel and Judah.”
2 Mfalme akamwambia Yoabu, jemedari wa jeshi, aliyekuwa pamoja naye, “Nenda upite katika kabila zote za Israeli, toka Dani mpaka Beersheba, uwahesabu watu wote, ili niweze kujua idadi kamili ya watu wanaofaa kwa vita.”
So the king said to Joab, the commander of his army, “Go [with your officers] through all the tribes of Israel, from Dan [city in the far north] to Beersheba [town in the far south], and count the people, in order that I may know how many people [there are who are able to be soldiers in the army].”
3 Yoabu akamwambia mfalme, “Yahwe Mungu wako na aizidishe hesabu ya watu mara mia, na macho ya bwana wangu mfalme yaone ikifanyika. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme analitaka jambo hili?
But Joab replied to the king, “Your Majesty, I wish/desire that Yahweh our God will cause there to be 100 times as many people [in Israel] as there are now, and I wish/desire that you would see that happen [before you die]. But why do you want us to do this?”
4 Walakini neno la mfalme lilikuwa la mwisho dhidi ya Yoabu na dhidhi ya majemedari wa jeshi. Hivyo Yoabu na majemedari wakatoka mbele ya mfalme kuwahesabu watu wa Israeli.
But the king commanded Joab and his officers to do it. So they left the king and went out to count the people of Israel.
5 Wakavuka Yordani na kupiga kambi karibu na Aroeri, kusini mwa mji bondeni. Kisha wakasafiri kupitia Gadi mpaka Yazeri.
They crossed the Jordan [River] and set up their tents south of Aroer [town], in the middle of the valley, in the territory [that was given to the tribe] of Gad. From there they went [north] to Jazer [city]
6 Wakaja Gileadi na nchi ya Tahtimu Hodshi, kisha Dani, Jaani na karibu kuelekea Sidoni.
Then they went [north] to [the] Gilead [region] and to Kadesh [city], in the land where the Heth people-group lived. Then they went to Dan [city in the far north of Israel], and then further west, to Sidon [city near the Mediterranean Sea].
7 Wakafika ngome ya Tiro na miji yote ya Wahivi na Wakanaani. Kisha wakaenda Negebu katika Yuda huko Beersheba.
Then they went [south] to Tyre, a city with high walls around it, and to all the cities where the Hiv and Canaan people-groups live. Then they went [east] to Beersheba, in the southern part of Judah.
8 Walipokuwa wamepita katika nchi yote, wakarejea Yerusalemu mwishoni mwa miezi tisa na siku ishirini.
After nine months and 20 days, when they had finished going throughout the land [and counting the people], they returned to Jerusalem.
9 Ndipo Yoabu alipotoa taarifa ya hesabu kamili kwa mfalme kuhusu watu wawezao kupigana vita. Katika Israeli kulikuwa na watu 800, 000 jasiri wawezao kutoa upanga, na wale wa Yuda walikuwa watu 500, 000.
They reported to the king the number of people that they had counted. There were 800,000 men in Israel and 500,000 men in Judah who were able to become soldiers in the army [MTY].
10 Ndipo moyo wa Daudi ukamchoma alipokuwa amewahesabu watu. Hivyo akamwambia Yahwe, “Kwa kufanya hivi nimetenda dhambi sana. Sasa, Yahwe, uiondoe hatia ya mtumishi wako, kwani nimetenda kwa upumbavu.”
But after David’s men had counted the people, David regretted [IDM] that he had told them to do that. [One night] he said to Yahweh, “I have committed a very big sin. Please forgive me, because what I have done is very foolish.”
11 Daudi alipoinuka asubuhi, neno la Yahwe likamjia nabii Gadi, mwonaji wa Daudi, kusema,
When David got up the next morning, Yahweh gave a message to the prophet Gad. He said to him,
12 Nenda umwambie Daudi; 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: “Ninakupa mambo matatu. Uchague mojawapo.”
“Go and tell this to David: ‘I am allowing you to choose one of three things [to punish you]. I will do whichever one you choose.’”
13 Hivyo Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je miaka mitatu ya njaa ije katika nchi yako? au miezi mitatu ukimbie kutoka kwa adui zako huku wakikufuatia? au kuwe na tauni ya siku tatu katika nchi yako? Amua sasa jibu gani nimrudishie aliyenituma.”
So Gad went to David and told him [what Yahweh had said]. He said to David, “You can choose whether there will be three years of famine in your land, or three months of your [army] running away from your enemies, or three days when there will be a (plague/very severe illness) in your land. You think about it and choose [which one you want, and tell me], and I will return to Yahweh and tell him what your answer is.”
14 Ndipo Daudi alipomwambia Gadi, “Nipo katika shida kubwa. Haya na tuanguke katika mikono ya Yahwe kuliko kuanguka katika mikono ya mwanadamu, kwani matendo yake ya rehema ni makuu sana.”
David said to Gad, “All those are very terrible things for me to choose between! But allow Yahweh to punish [MTY] me, because he is very merciful. Do not allow humans to punish me, [because they will not be merciful].”
15 Hivyo akatuma tauni juu ya Israeli kuanzia asubuhi kwa muda ulioamriwa, na watu sabini na tano elfu kutoka Dani mpaka Beersheba wakafa.
So Yahweh sent a plague on the Israeli people. It started that morning and did not stop until the time that he had chosen/set. All over the land, from Dan to Beersheba, there were 70,000 Israelis who died [because of the plague].
16 Malaika aliponyosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili kuuharibu, Yahwe akabadili nia yake kuhusu madhara, na akamwambia malaika aliyekuwa tiyari kuwaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako sasa.” Wakati huo malaika wa Yahwe alikuwa amesimama katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.
When [Yahweh’s] angel stretched out his hand toward Jerusalem to destroy [the people by this plague], Yahweh changed his mind about punishing [any more] people. He said to the angel who was killing them [with the plague], “Stop what you are doing [IDM]! That is enough!” [When he said that, ] the angel was standing at the ground where Araunah, from the Jebus people-group, threshed grain.
17 Daudi alipomwona malaika aliyekuwa amewapiga watu, akamwambia Yahwe kusema, “Nimetenda dhambi, na nimetenda kwa upumbavu. Lakini kondoo hawa, wamefanya nini? Tafadhari, mkono wako na uniadhibu mimi na familia ya baba yangu!”
When David saw the angel who was causing the people to become sick and die, he said to Yahweh, “Truly, I am the one who has committed the sin. I have done a very wicked thing, but these people are [as innocent as] sheep [MET]. They have certainly not [RHQ] done anything [that is wrong]. So you should punish [IDM] me and my family, [not these people]!”
18 Kisha Gadi akaja siku hiyo kwa Daudi na kumwambia, “Kwea na ujenge madhabahu kwa ajili ya Yahwe katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.”
That day Gad came to David and said to him, “Go up to the place where Araunah threshes grain, and build an altar to [worship] Yahweh there.”
19 Hivyo Daudi akakwea kama Gadi alivyomwelekeza kufanya, kama Yahwe alivyokuwa ameagiza.
So David did what Gad told him to do, which was what Yahweh had commanded, [and he went up there].
20 Arauna akatazama na kumwona mfalme na watumishi wake wakikaribia. Ndipo Arauna akaondoka na kumsujudia mfalme uso wake mpaka juu ya ardhi.
When Araunah looked down and saw the king and his officials coming toward him, he prostrated himself on the ground in front of the king, with his face touching the ground.
21 Kisha Arauna akasema, “Kwa nini bwana wangu mfalme amekuja kwangu, mtumishi wake? Daudi akajibu, “Kununua uwanja wako wa kupuria, ili nimjengee Yahwe madhabahu, ili kwamba tauni iondolewe kwa watu.”
Araunah said, “Your Majesty, why have you come to me?” David replied, “[I have come] to buy this ground where you thresh grain, in order to build an altar to Yahweh [and offer sacrifices on it], in order that he will stop the plague.”
22 Arauna akamwambia Daudi, “Chukua liwe lako, bwana wangu mfalme. Ulifanyie lolote lolote lililojema machoni pako. Tazama, ng'ombe kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na miganda ya kupuria na nira kwa kuni.
Araunah replied to David, “Your Majesty, offer to Yahweh whatever you wish/want. Here, take my oxen to use for the offering that will be completely burned on the altar. And here, take their yokes and the boards [that I use] for the threshing, [and use them] for the wood that you will burn.
23 Haya yote bwana wangu mfalme, mimi Arauna nakupa.” Kisha akamwambia mfalme, “Yahwe Mungu wako na awe nawe.”
I, Araunah, am giving all this to you, the king.” Then he said, “I desire/hope that Yahweh our God will accept your offering.”
24 Mfalme akamwambia Arauna, “Hapana, nahimiza kukinunua kwa thamani yake. Sitatoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe chochote nisichokigharimia.” Hivyo Daudi akakinunua kiwanja cha kupuria na ng'ombe kwa shekeli hamsini za fedha.
But the king said to Araunah, “No, [I will not take these things as a gift.] I will pay you for it. I will not take sacrifices that have cost me nothing, and offer them to Yahweh to be completely burned on the altar.” So he paid 50 pieces of silver to Araunah for the oxen and the ground.
25 Daudi akajenga madhabahu kwa Yahwe pale na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Hivyo wakamsihi Yahwe kwa niaba ya nchi, hivyo akaizuia tauni katika katika Israeli yote.
Then David built an altar to Yahweh, and he offered [the oxen] to be completely burned on the altar, and he also offered sacrifices to maintain fellowship with Yahweh. Then, Yahweh answered David’s prayers, and he caused the plague in Israel to end.