< 2 Samweli 23 >
1 Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi-Daudi mwana wa Yese, mtu aliyeheshimiwa sana, aliyetiwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwandishi mzuri wa zaburi wa Israeli.
Mais voici les dernières paroles de David. David, fils d’Isaï, a parlé; l’homme institué le christ du Dieu de Jacob, l’excellent psalmiste d’Israël, a dit:
2 “Roho ya Yahwe alisema nami, na neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
L’Esprit du Seigneur s’est fait entendre par moi, et sa parole par ma langue.
3 Mungu wa Israeli alinena, Mwamba wa Israeli aliniambia, “Atawalaye kwa haki juu yangu, atawalaye katika hofu ya Mungu.
Le Dieu d’Israël m’a dit: le Fort d’Israël a parlé: le dominateur des hommes, le juste dominateur dans la crainte de Dieu sera
4 Atakuwa kama nuru ya asubuhi jua linapochomoza, asubuhi isiyo na mawingu, wakati mche mwororo unapochipua kutoka ardhini kupitia mwangaza wa mng'ao wa jua baada ya mvua.
Comme la lumière de l’aurore, qui, au soleil levant, le matin, brille sans nuages, et comme l’herbe qui germe de la terre par les pluies.
5 Hakika, je familia yangu haiko hivi mbele za Mungu? Je hajafanya nami agano la milele, taratibu la uhakika kwa kila njia? Je yeye haongezi wokovu wangu na kutimiza kila hitaji langu?
Et ma maison n’était pas si grande devant Dieu, pour qu’il fit avec moi un pacte éternel, ferme en toutes choses et assuré; car ce pacte est tout mon salut et toute ma volonté; et rien n’en provient qui ne porte ses fruits.
6 Lakini yasiyofaa yote yatakuwa kama miiba na kutupwa mbali, kwa maana haiwezekani kukusanywa kwa mikono.
Mais les prévaricateurs seront extirpés tous comme des épines que l’on n’arrache pas avec les mains.
7 Ayagusaye ni lazima atumie chombo cha chuma au au fumo la mkuki. Ni lazima yachomwe mahali yalipo.
Et si quelqu’un veut les toucher, il s’arme de fer, et d’un bois de lance, et brûlées par le feu, elles sont consumées jusqu’à néant.
8 Haya ni majina ya askari wa Daudi: Yashobeamu Mhakmoni alikuwa kiongozi wa mashujaa. Aliua watu mia nne wakati mmoja.
Voici le nom des braves de David. Celui qui était assis dans la chaire, le plus sage, le premier entre les trois; c’est lui qui, comme le petit ver le plus tendre du bois, tua huit cents hommes en une seule fois.
9 Baada yake alikuwa Elieza mwana wa Dodo, mwana wa mwahohi, mmoja wa mashujaa watatu wa Daudi. Alikuwepo walipowashinda Wafilisti waliokuwa wamekusanyika kwa vita, na wakati watu wa Israeli walipokuwa wamekimbia.
Après lui, Éléazar, Ahohite, fils de son oncle paternel, était entre les trois braves qui étaient avec David, lorsqu’ils insultèrent les Philistins, et qu’ils s’assemblèrent en ce lieu pour le combat.
10 Elieza akasimama na kuwapiga Wafilisti mpaka mkono wake ukachoka, mpaka mkono wake ukang'ang'ania mpini wa upanga wake. Siku hiyo Yahwe akatoa ushindi mkuu. Jeshi likarejea kwa ajili ya kuteka tu nyara za waliouawa na Elieza.
Et lorsque les hommes d’Israël eurent monté, lui se présenta, et battit les Philistins, jusqu’à ce que sa main se lassât et demeurât attachée à son glaive; et le Seigneur donna une grande victoire à Israël en ce jour-là, et le peuple, qui avait fui, retourna pour enlever les dépouilles des morts.
11 Baada yake alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti wakajikusanya pamoja palipokuwa na shamba la dengu, na jeshi likawakimbia.
Et après lui venait Semma, fils d’Agé, d’Arari. Et les Philistins s’assemblèrent au poste; car il y avait là un champ plein de lentilles. Et lorsque le peuple se fut enfui devant les Philistins,
12 Lakini Shama akasimama katikati ya shamba na kulitetea. Aliwauwa Wafilisti, na Yahwe akaleta ushindi mkuu.
Semma se tint au milieu du champ, le défendit et battit les Philistins; et le Seigneur accorda une grande victoire.
13 Watatu kati ya askari thelathini walishuka kwa Daudi nyakati za mavuno, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Mrefai.
Et déjà auparavant étaient descendus les trois qui étaient les premiers entre les trente, et ils étaient venus au temps de la moisson vers David, dans la caverne d’Odollam; mais le camp des Philistins était placé dans la Vallée des Géants.
14 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, wakati Wafilisti walikuwa wanaimilk Bethlehemu.
Et David était dans la forteresse; mais l’armée des Philistins était alors à Bethléhem.
15 Daudi alitamani maji na akasema, “Kama ingekuwa mtu mmoja angenipa maji ya kunywa kutoka kisima kilichopo Bethlehemu, kisima kilichopo langoni!”
David donc fit un souhait, et dit: Oh! si quelqu’un me donnait à boire de l’eau de la citerne qui est à Bethléhem, près de la porte:
16 Hivyo mashujaa hawa watatu wakapita kati ya jeshi la Wafilisti na kuchota maji katika kisima cha Bethlehemu, kilichopo langoni. Wakachukua maji na kuyaleta kwa Daudi, lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake akayamwaga mbele za Yahwe.
Les trois braves passèrent donc à travers le camp des Philistins, et puisèrent de l’eau dans la citerne de Bethléhem qui était près de la porte, et l’apportèrent à David; et David n’en voulut pas boire, mais il l’offrit en libations au Seigneur,
17 Kisha akasema, “Iwe mbali nami, Yahwe, kwamba niyanywe haya. Je ninywe damu ya watu waliohatarisha maisha yao?” Hivyo akakataa kuyanywa. Haya ni mambo yaliyofanywa na mashujaa watatu.
Disant: Que le Seigneur me soit propice, pour que je ne fasse pas cela: boirai-je le sang de ces hommes qui sont allés la chercher, et le péril de leurs âmes? Il ne voulut donc pas boire. Voilà ce que firent ces trois hommes très vigoureux.
18 Abishai, nduguye Yoabu na mwana wa Seruya, alikuwa akida wa watatu. Alipigana kwa mkuki wake na watu mia tatu na akawauwa wote mara. Mara kwa mara alitajwa kati ya mashujaa watatu.
Abisaï aussi, frère de Joab, fils de Sarvia, était le premier de trois autres: c’est lui qui leva sa lance contre trois cents, qu’il tua: il était renommé parmi ces trois,
19 Hakuwa maarufu kuliko wale watatu? Alifanywa akida wao. Lakini, umaarufu wake haukulingana na umaarufu wa wale mashujaa watatu.
Et le plus noble d’entre ces trois, et leur chef; mais il n’atteignait pas les premiers.
20 Benaya kutoka Kabseeli mwana wa Yehoyada; alikuwa mtu hodari aliyefanya matendo makuu. Aliwauwa wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka shimoni na kuuwa simba wakati wa theruji.
Ensuite Banaïas de Cabséel, fils de Joïada, homme très vaillant, et aux grands exploits; c’est lui qui tua les deux lions de Moab, et lui qui descendit et tua le lion au milieu de la citerne, dans les jours de la neige.
21 Na alimwua Mmisri aliyekuwa mtu mnene sana. Mmisri alikuwa na mkuki mkononi, lakini Benaya alipigana naye kwa fimbo tu. Aliuchukua mkuki mkononi mwa Mmisri na kisha kumwua nao.
C’est lui qui tua l’Egyptien: homme digne d’être en spectacle et ayant en main une lance; c’est pourquoi, lorsqu’il fut descendu vers lui avec sa verge, il arracha de force la lance de la main de l’Egyptien, et le tua de sa lance.
22 Benaya mwana wa Yehoyada alifanya matendo haya, naye alitajwa kati ya mashujaa watatu.
Voilà ce que fit Banaïas, fils de Joïada.
23 Alikuwa na heshima kuliko mashujaa thelathini kwa ujumla wao, lakini hakuwa na heshima kama wale mashujaa watatu. Hata hivyo Daudi alimweka kuwa mlinzi wake.
Et il était renommé entre les trois vaillants les plus nobles entre les trente; cependant il n’atteignait pas les trois premiers; et David le fit son conseiller intime.
24 Wafuatao ni wale watu thelathini: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
Asaël, frère de Joab, était entre les trente; Eléhanan de Bethléhem, fils de l’oncle paternel d’Asaël;
25 Shama Mharodi, Elika Mharodi,
Semma de Harodi, Elica de Harodi,
26 Helesi Mpeloni, Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi,
Hélès de Phalti, Hira, fils d’Accès de Thécua;
27 Abi Ezeri Mwanathothi, Mebunai Mhushathi,
Abiézer d’Anathoth, Mobonnaï de Husati,
28 Salmoni Mhahoi, Maharai Mnetofathi;
Selmon, l’Ahohite, Maharaï, le Nétophathite;
29 Helebu mwana wa Baana, Mnetofathi, Itai mwana wa Rabai kutoka Gibea ya Wabenjamini,
Héled, fils de Baana, lui aussi Nétophatite, Ithaï, fils de Ribaï de Gabaath des enfants de Benjamin;
30 Benaya Mpirathoni, Hidai wa mabonde ya Gaashi.
Banaï, le Pharathonite, Heddaï du torrent de Gaas,
31 Abieliboni Mwarbathi, Azmawethi Mbarhumi,
Abialbon, l’Arbathite, Azmaveth de Béromi,
32 Eliaba Mshalboni, wana wa Yasheni, Yonathani mwana wa Shama Mharari;
Eliaba de Salaboni. Les fils de Jassen, Jonathan,
33 Ahiamu mwana wa Sharari Mharari,
Semma d’Orori; Ahiam, fils de Sarar, l’Arorite;
34 Elifeleti mwana wa Ahasbai Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli Mgiloni,
Eliphélet, fils d’Aasbaï, fils de Machati; Eliam, fils d’Achitophel, le Gélonite,
35 Hezro Mkarmeli, Parai Mwarbi,
Hesraï du Carmel, Pharaï d’Arbi,
36 Igali mwana wa Nathani kutoka Soba, Bani kutoka kabila la Gadi,
Igaal, fils de Nathan de Soba, Bonni de Gadi,
37 Zeleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
Sélec d’Ammoni, Naharaï, le Bérothite, écuyer de Joab, fils de Sarvia,
38 Ira Mwithri, Garebu Mwithri,
Ira, le Jéthrite, Gareb, lui aussi Jéthrite,
39 Uria Mhiti - jumla yao thelathini na wanane.
Urie, l’Héthéen. En tout trente-sept.