< 2 Samweli 22 >

1 Daudi akamwimbia Yahwe maneno ya wimbo huu siku ile Yahwe alipomwokoa katika mkono wa adui zake wote na katika mkono wa Sauli.
David cantó las palabras de este cántico al Señor el día en que el Señor lo salvó de todos sus enemigos y de Saúl.
2 Akaomba hivi, “Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, aliyeniokoa.
Entonces cantó: El Señor es mi roca, mi fortaleza y mi salvador.
3 Mungu ni mwamba wangu. Yeye ni kimbilio langu. Ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, ngome yangu na kimbilio langu, aniokoaye na mabaya yote.
Él es mi Dios, mi roca que me protege. Él me protege del mal, su poder me salva, me mantiene seguro. Él es mi protector; es mi salvador; me libra de la violencia.
4 Nitamwita Yahwe, astahiliye kutukuzwa, nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Pido ayuda al Señor, merecedor de alabanza, y me salva de los que me odian.
5 Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maji ya uharibifu yakanishinda.
Las olas de la muerte me arrastran, las aguas de la destrucción me inundan;
6 Vifungo vya kuzimu vilinizunguka; kamba za mauti zikaninasa. (Sheol h7585)
El sepulcro enrolló sus cuerdas en torno a mí; la muerte me tendió trampas. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Yahwe; nilimwita Mungu wangu; akaisikia sauti yangu katika hekalu lake, na kilio changu cha msaada kikafika masikioni mwake.
En mi desesperación invoqué al Señor; clamé a mi Dios. Él escuchó mi voz desde su Templo; mi grito de auxilio llegó a sus oídos.
8 Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka. Misingi ya mbingu ikatetemeka na kutikiswa, kwa kuwa Mungu alikasirika.
La tierra se estremeció, los cimientos de los cielos temblaron por su cólera
9 Moshi ukatoka katika pua yake, na miale ya moto ikatoka katika kinywa chake. Makaa yakawashwa nayo.
Humo salía de sus narices, y fuego de su boca, carbones ardientes que ardían ante él.
10 Alizifungua mbingu akashuka, na giza totoro lilikuwa chini ya miguu yake.
Apartó los cielos y descendió, con nubes oscuras bajo sus pies.
11 Alipanda juu ya kerubi na kuruka. Alionekana katika mawingu ya upepo.
Montado en un ser celestial voló, abalanzándose sobre las alas del viento.
12 Naye akalifanya giza kuwa hema kumzunguka, akakusanya mawingu makubwa ya mvua angani.
Se escondió en las tinieblas, cubriéndose con negras nubes de lluvia.
13 Makaa ya moto yalidondoka mbele zake kutoka katika radi.
De su resplandor brotaron carbones ardientes.
14 Yahwe alishuka kutoka katika mbingu. Aliyejuu alipiga kelele.
El Señor tronó desde el cielo; resonó la voz del Altísimo.
15 Alipiga mishale na kuwatawanya adui zake—miale ya radi na kuwasambaratisha.
Disparó sus flechas, dispersando a sus enemigos, los derrotó con sus rayos.
16 Kisha njia za maji zikaonekana; misingi ya dunia ikawa wazi katika kilio cha vita ya Yahweh, katika sauti za pumzi ya pua zake.
El Señor rugió, y con el viento del aliento de su nariz se vieron los valles del mar y se descubrieron los cimientos de la tierra.
17 Kutoka juu alifika chini; akanishikilia! Aliniondoa katika vilindi vya maji.
Bajó su mano desde arriba y me agarró. Me sacó de las aguas profundas.
18 Aliniokoa kutoka kwa adui zangu wenye nguvu, kwao walionichukia, kwa maana walikuwa na nguvu sana kwangu.
Me rescató de mis poderosos enemigos, de los que me odiaban y eran mucho más fuertes que yo.
19 Walikuja kinyume changu siku ya shida yangu, lakini Yahwe alikuwa msaada wangu.
Se abalanzaron sobre mí en mi peor momento, pero el Señor me sostuvo.
20 Pia aliniweka mahali panapo nafasi. Aliniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Me liberó, me rescató porque es feliz conmigo.
21 Yahwe amenituza kwa kipimo cha haki yangu; amenirejesha kwa kiwango cha usafi wa mikono yangu.
El Señor me recompensó por hacer lo correcto; me pagó porque soy inocente.
22 Kwa maana nimezishika njia za Yahwe na sijafanya uovu kwa kugeuka kutoka kwa Mungu.
Porque he seguido los caminos del Señor; no he pecado apartándome de mi Dios.
23 Kwa kuwa maagizo yake yote ya haki yamekuwa mbele yangu; kwa kuwa sheria zake, sikujiepusha nazo.
He tenido presente todas sus leyes; no he ignorado sus mandamientos.
24 Nimekuwa bila hatia mbele zake pia, na nimejiepusha na dhambi.
Soy irreprochable a sus ojos; me guardo de pecar.
25 Kwa hiyo Yahwe amenirejesha kwa kiasi cha uadilifu wangu, kwa kipimo cha usafi wangu mbele zake.
El Señor me ha recompensado por hacer lo justo. Soy inocente ante sus ojos.
26 Kwa mwaminifu, unajionesha kuwa mwaminifu; kwake asiye na hatia; unajionesha kuwa hauna hatia.
Demuestras tu fidelidad a los que son fieles; demuestras integridad a los que son íntegros,
27 Kwa usafi unajionesha kuwa msafi, lakini kwa wakaidi unajionesha kuwa mkaidi.
Te muestras puro a los que son puros, pero te muestras astuto con los astutos.
28 Unaokoa walioteswa, lakini macho yako ni kinyume cha wenye kiburi, unawashusha chini.
Tú salvas a los humildes, pero tus ojos vigilan a los soberbios para abatirlos.
29 Kwa maana wewe ni taa yangu, Yahwe. Yahwe huangaza katika giza langu.
Tú, Señor, eres mi lámpara. El Señor ilumina mis tinieblas.
30 Maana kwa ajili yake ninaweza kupita vipingamizi; kwa msaada wa Mungu wangu naweza kuruka juu ya ukuta.
Contigo puedo abatir una tropa de soldados; contigo, Dios mío, puedo escalar un muro de la fortaleza.
31 Maana njia za Mungu ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi. Yeye ni ngao yao wanaomkimbilia.
El camino de Dios es absolutamente correcto. La palabra del Señor es digna de confianza. Es un escudo para todos los que acuden a él en busca de protección.
32 Maana ni nani aliye Mungu isipokuwa Yahwe? Na ni nani aliyemwamba isipokuwa Mungu?
Porque ¿quién es Dios sino el Señor? ¿Quién es la Roca, sino nuestro Dios?
33 Mungu ni kimbilio langu, na umwongoza katika njia yake mtu asiye na hatia.
Dios me hace fuerte y me mantiene seguro.
34 Huifanya myepesi miguu yangu kama kurungu na kuniweka katika vilima virefu.
Me hace seguro como el ciervo, capaz de caminar por las alturas con seguridad.
35 Huifundisha mikono yangu kwa vita, na viganja vyangu kupinda upinde wa shaba.
Me enseña a luchar en la batalla; me da la fuerza para tensar un arco de bronce.
36 Umenipa ngao ya wokovu wako, na matakwa yako yamenifanya mkuu.
Me protege con el escudo de su salvación; su ayuda me ha engrandecido.
37 Umeitengenezea miguu yangu nafasi chini yangu, hivyo miguu yangu haikujikwaa.
Me diste espacio para caminar y evitaste que mis pies resbalaran.
38 Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza. Sikurudi nyuma hadi walipoangamizwa.
Perseguí a mis enemigos y los alcancé. No me devolví hasta haberlos destruido.
39 Niliwararua na kuwasambaratisha; hawawezi kuinuka. Wameanguka chini ya miguu yangu.
Los derribé y no pudieron levantarse. Cayeron a mis pies.
40 Unaweka nguvu ndani yangu kama mkanda kwa vita; unawaweka chini yangu wanaoinuka kinyume changu.
Me hiciste fuerte para la batalla; hiciste que los que se levantaron contra mí se arrodillaran ante mí.
41 Ulinipa migongo ya shingo za adui zangu; niliwaangamiza kabisa wale wanaonichukia.
Hiciste que mis enemigos huyeran; destruí a todos mis enemigos.
42 Walilia kwa msaada, lakini hakuna aliyewaokoa; walimlilia Yahwe, lakini hakuwajibu.
Ellos clamaron por ayuda, pero nadie vino a rescatarlos. Incluso clamaron al Señor, pero él no les respondió.
43 Niliwaponda katika vipande kama mavumbi juu ya ardhi, niliwakanyaga kama matope mitaani.
Los convertí en polvo, como el polvo de la tierra. Los aplasté y los arrojé como lodo en la calle.
44 Umeniokoa pia kutoka katika mashutumu ya watu wangu. Umeniweka kama kichwa cha mataifa. Watu nisiowajua wananitumikia.
Me rescataste de los pueblos rebeldes; me mantuviste como gobernante de las naciones: gente que no conocía ahora me sirve.
45 Wageni walishurutishwa kuniinamia. Mara waliposikia kuhusu mimi, walinitii.
Los extranjeros se acobardan ante mí; en cuanto oyen hablar de mí, me obedecen.
46 Wageni walikuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
Se desalientan y salen temblando de sus fortalezas.
47 Yahwe anaishi! Mwamba wangu atukuzwe. Mungu na ainuliwe, mwamba wa wokovu wangu.
¡El Señor vive! ¡Bendita sea mi Roca! ¡Alabado sea el Dios que me salva!
48 Huyu ndiye Mungu anilipiaye kisasi, awawekaye watu chini yangu.
Dios me vindica, pone a los pueblos bajo mis pies,
49 Uniweka huru mbali na adui zangu. Hakika, uliniinua juu yao walioinuka kinyume changu. Uliniokoa kutoka kwa watu wenye ghasia.
Y me libera de los que me odian. Me mantiene a salvo de los que se rebelan contra mí, me salva de los hombres violentos.
50 Kwa hiyo nitakushukuru, Yahwe, kati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Por eso te alabaré entre las naciones, Señor; cantaré alabanzas sobre lo que tú eres.
51 Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na uonesha uaminifu wake wa kiagano kwa mtiwa mafuta wake, kwa Daudi na uzao wake daima.”
Has salvado al rey tantas veces, mostrando tu amor fiel a David, tu ungido, y a sus descendientes por siempre.

< 2 Samweli 22 >