< 2 Samweli 22 >

1 Daudi akamwimbia Yahwe maneno ya wimbo huu siku ile Yahwe alipomwokoa katika mkono wa adui zake wote na katika mkono wa Sauli.
Davide rivolse al Signore le parole di questo canto, quando il Signore lo liberò dalla mano di tutti i suoi nemici, specialmente dalla mano di Saul.
2 Akaomba hivi, “Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, aliyeniokoa.
«Il Signore è la mia roccia, la mia fortezza, il mio liberatore, Egli disse:
3 Mungu ni mwamba wangu. Yeye ni kimbilio langu. Ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, ngome yangu na kimbilio langu, aniokoaye na mabaya yote.
il mio Dio, la mia rupe in cui mi rifugio, il mio scudo, la mia salvezza, il mio riparo! Sei la mia roccaforte che mi salva: tu mi salvi dalla violenza.
4 Nitamwita Yahwe, astahiliye kutukuzwa, nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Invoco il Signore, degno di ogni lode, e sono liberato dai miei nemici.
5 Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maji ya uharibifu yakanishinda.
Mi circondavano i flutti della morte, mi atterrivano torrenti esiziali.
6 Vifungo vya kuzimu vilinizunguka; kamba za mauti zikaninasa. (Sheol h7585)
Mi avviluppavano le funi degli inferi; mi stavano davanti i lacci della morte. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Yahwe; nilimwita Mungu wangu; akaisikia sauti yangu katika hekalu lake, na kilio changu cha msaada kikafika masikioni mwake.
Nell'angoscia ho invocato il Signore, ho gridato al mio Dio, Egli ha ascoltato dal suo tempio la mia voce; il mio grido è giunto ai suoi orecchi.
8 Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka. Misingi ya mbingu ikatetemeka na kutikiswa, kwa kuwa Mungu alikasirika.
Si scosse la terra e sobbalzò; tremarono le fondamenta del cielo; si scossero, perché egli si era irritato.
9 Moshi ukatoka katika pua yake, na miale ya moto ikatoka katika kinywa chake. Makaa yakawashwa nayo.
Fumo salì dalle sue narici; dalla sua bocca uscì un fuoco divoratore; carboni accesi partirono da lui.
10 Alizifungua mbingu akashuka, na giza totoro lilikuwa chini ya miguu yake.
Egli piegò i cieli e discese; una nube oscura era sotto i suoi piedi.
11 Alipanda juu ya kerubi na kuruka. Alionekana katika mawingu ya upepo.
Cavalcò un cherubino e volò; si librò sulle ali del vento.
12 Naye akalifanya giza kuwa hema kumzunguka, akakusanya mawingu makubwa ya mvua angani.
Si avvolse di tenebra tutto intorno; acque scure e dense nubi erano la sua tenda.
13 Makaa ya moto yalidondoka mbele zake kutoka katika radi.
Per lo splendore che lo precedeva arsero carboni infuocati.
14 Yahwe alishuka kutoka katika mbingu. Aliyejuu alipiga kelele.
Il Signore tuonò nei cieli, l'Altissimo emise la sua voce.
15 Alipiga mishale na kuwatawanya adui zake—miale ya radi na kuwasambaratisha.
Scagliò frecce e li disperse; vibrò folgori e li mise in fuga.
16 Kisha njia za maji zikaonekana; misingi ya dunia ikawa wazi katika kilio cha vita ya Yahweh, katika sauti za pumzi ya pua zake.
Apparvero le profondità marine; si scoprirono le basi del mondo, come effetto della tua minaccia, Signore, del soffio violento della tua ira.
17 Kutoka juu alifika chini; akanishikilia! Aliniondoa katika vilindi vya maji.
Dall'alto stese la mano e mi prese; mi fece uscire dalle grandi acque.
18 Aliniokoa kutoka kwa adui zangu wenye nguvu, kwao walionichukia, kwa maana walikuwa na nguvu sana kwangu.
Mi liberò dai miei robusti avversari, dai miei nemici più forti di me.
19 Walikuja kinyume changu siku ya shida yangu, lakini Yahwe alikuwa msaada wangu.
Mi affrontarono nel giorno della mia rovina, ma il Signore fu il mio sostegno.
20 Pia aliniweka mahali panapo nafasi. Aliniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Egli mi trasse al largo; mi liberò, perché oggetto della sua benevolenza.
21 Yahwe amenituza kwa kipimo cha haki yangu; amenirejesha kwa kiwango cha usafi wa mikono yangu.
Il Signore mi ricompensò secondo la mia giustizia, mi trattò secondo la purità delle mie mani.
22 Kwa maana nimezishika njia za Yahwe na sijafanya uovu kwa kugeuka kutoka kwa Mungu.
Perché mi sono mantenuto nelle vie del Signore, non sono stato empio, lontano dal mio Dio,
23 Kwa kuwa maagizo yake yote ya haki yamekuwa mbele yangu; kwa kuwa sheria zake, sikujiepusha nazo.
perché tutti i suoi decreti mi sono dinanzi e non ho allontanato da me le sue leggi.
24 Nimekuwa bila hatia mbele zake pia, na nimejiepusha na dhambi.
Sono stato irreprensibile nei suoi riguardi; mi sono guardato dall'iniquità.
25 Kwa hiyo Yahwe amenirejesha kwa kiasi cha uadilifu wangu, kwa kipimo cha usafi wangu mbele zake.
Il Signore mi trattò secondo la mia giustizia, secondo la purità delle mie mani alla sua presenza.
26 Kwa mwaminifu, unajionesha kuwa mwaminifu; kwake asiye na hatia; unajionesha kuwa hauna hatia.
Con il pio ti mostri pio, con il prode ti mostri integro;
27 Kwa usafi unajionesha kuwa msafi, lakini kwa wakaidi unajionesha kuwa mkaidi.
con il puro ti mostri puro, con il tortuoso ti mostri astuto.
28 Unaokoa walioteswa, lakini macho yako ni kinyume cha wenye kiburi, unawashusha chini.
Tu salvi la gente umile, mentre abbassi gli occhi dei superbi.
29 Kwa maana wewe ni taa yangu, Yahwe. Yahwe huangaza katika giza langu.
Sì, tu sei la mia lucerna, Signore; il Signore illumina la mia tenebra.
30 Maana kwa ajili yake ninaweza kupita vipingamizi; kwa msaada wa Mungu wangu naweza kuruka juu ya ukuta.
Sì, con te io posso affrontare una schiera, con il mio Dio posso slanciarmi sulle mura.
31 Maana njia za Mungu ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi. Yeye ni ngao yao wanaomkimbilia.
La via di Dio è perfetta; la parola del Signore è integra; egli è scudo per quanti si rifugiano in lui.
32 Maana ni nani aliye Mungu isipokuwa Yahwe? Na ni nani aliyemwamba isipokuwa Mungu?
C'è forse un dio come il Signore; una rupe fuori del nostro Dio?
33 Mungu ni kimbilio langu, na umwongoza katika njia yake mtu asiye na hatia.
Dio mi cinge di forza, rende sicura la mia via.
34 Huifanya myepesi miguu yangu kama kurungu na kuniweka katika vilima virefu.
Ha reso simili i miei piedi a quelli delle cerve; mi ha fatto stare sulle alture.
35 Huifundisha mikono yangu kwa vita, na viganja vyangu kupinda upinde wa shaba.
Ha addestrato la mia mano alla guerra; ha posto un arco di bronzo nelle mie braccia.
36 Umenipa ngao ya wokovu wako, na matakwa yako yamenifanya mkuu.
Mi hai dato lo scudo della tua salvezza, la tua sollecitudine mi fa crescere.
37 Umeitengenezea miguu yangu nafasi chini yangu, hivyo miguu yangu haikujikwaa.
Fai largo davanti ai miei passi; le mie gambe non vacillano.
38 Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza. Sikurudi nyuma hadi walipoangamizwa.
Inseguo e raggiungo i miei nemici, non desisto finché non siano distrutti.
39 Niliwararua na kuwasambaratisha; hawawezi kuinuka. Wameanguka chini ya miguu yangu.
Li colpisco ed essi non possono resistere; cadono sotto i miei piedi.
40 Unaweka nguvu ndani yangu kama mkanda kwa vita; unawaweka chini yangu wanaoinuka kinyume changu.
Mi cingi di forza per la battaglia; hai fatto piegare sotto di me i miei avversari.
41 Ulinipa migongo ya shingo za adui zangu; niliwaangamiza kabisa wale wanaonichukia.
Mi mostri i nemici di spalle, così io distruggo quelli che mi odiano.
42 Walilia kwa msaada, lakini hakuna aliyewaokoa; walimlilia Yahwe, lakini hakuwajibu.
Gridano, ma nessuno li salva, verso il Signore, che a loro non risponde.
43 Niliwaponda katika vipande kama mavumbi juu ya ardhi, niliwakanyaga kama matope mitaani.
Li disperdo come polvere della terra, li calpesto come fango delle piazze.
44 Umeniokoa pia kutoka katika mashutumu ya watu wangu. Umeniweka kama kichwa cha mataifa. Watu nisiowajua wananitumikia.
Tu mi liberi dalle contese del popolo; mi poni a capo di nazioni; un popolo non conosciuto mi serve.
45 Wageni walishurutishwa kuniinamia. Mara waliposikia kuhusu mimi, walinitii.
I figli degli stranieri mi onorano appena sentono, mi obbediscono.
46 Wageni walikuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
I figli degli stranieri vengono meno, lasciano con spavento i loro nascondigli.
47 Yahwe anaishi! Mwamba wangu atukuzwe. Mungu na ainuliwe, mwamba wa wokovu wangu.
Viva il Signore! Sia benedetta la mia rupe! Sia esaltato il Dio della mia salvezza!
48 Huyu ndiye Mungu anilipiaye kisasi, awawekaye watu chini yangu.
Dio fa vendetta per me e mi sottomette i popoli.
49 Uniweka huru mbali na adui zangu. Hakika, uliniinua juu yao walioinuka kinyume changu. Uliniokoa kutoka kwa watu wenye ghasia.
Tu mi liberi dai miei nemici, mi innalzi sopra i miei avversari, mi liberi dall'uomo violento.
50 Kwa hiyo nitakushukuru, Yahwe, kati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Perciò ti loderò, Signore, fra i popoli canterò inni al tuo nome.
51 Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na uonesha uaminifu wake wa kiagano kwa mtiwa mafuta wake, kwa Daudi na uzao wake daima.”
Egli concede una grande vittoria al suo re, la grazia al suo consacrato, a Davide e ai suoi discendenti per sempre».

< 2 Samweli 22 >