< 2 Samweli 22 >
1 Daudi akamwimbia Yahwe maneno ya wimbo huu siku ile Yahwe alipomwokoa katika mkono wa adui zake wote na katika mkono wa Sauli.
Devit ni, Sawl hoi a taran pueng e kut thung hoi BAWIPA ni a rungngang nah hnin vah, BAWIPA e hmaitung a sak e lanaw teh:
2 Akaomba hivi, “Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, aliyeniokoa.
BAWIPA teh kaie lungsong, kaie rapan, kai na kahloutsakkung bawi.
3 Mungu ni mwamba wangu. Yeye ni kimbilio langu. Ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, ngome yangu na kimbilio langu, aniokoaye na mabaya yote.
Ka thaonae kaie Cathut, kai ni ka kâuep e, ka bahling hoi kai rungngangnae ki, ka rapanim kânguenae lah ao. Kaie rapan lah na o. Rektapnae thung hoi na rungngang haw.
4 Nitamwita Yahwe, astahiliye kutukuzwa, nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Pholen han kamcu e BAWIPA teh ka kaw vaiteh, taran kut dawk hoi na rungngang han.
5 Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maji ya uharibifu yakanishinda.
Duenae tuicapa ni na kalup teh Cathut banglah noutnahoehnae tuicapa ni na taki sak.
6 Vifungo vya kuzimu vilinizunguka; kamba za mauti zikaninasa. (Sheol )
Sheol lungmathoenae ni na kalup awh teh, duenae karapnaw ni sut na pawp. (Sheol )
7 Katika shida yangu nalimwita Yahwe; nilimwita Mungu wangu; akaisikia sauti yangu katika hekalu lake, na kilio changu cha msaada kikafika masikioni mwake.
Ka lungreithai navah, BAWIPA ka kaw teh, ka Cathut koevah ka hram. Bawkim dawk hoi ka lawk a thai teh, ka hramnae lawk hah a hnâ thung a kâen.
8 Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka. Misingi ya mbingu ikatetemeka na kutikiswa, kwa kuwa Mungu alikasirika.
Hatnavah, a lungkhueknae lahoi talai a kâhuetsak, kalvan du ditouh lengleng a kâhuet.
9 Moshi ukatoka katika pua yake, na miale ya moto ikatoka katika kinywa chake. Makaa yakawashwa nayo.
A hnawng dawk hoi hmaikhu a tâco teh, a pahni dawk hoi hmaikaknae lahoi, hmaisaan kaman sak.
10 Alizifungua mbingu akashuka, na giza totoro lilikuwa chini ya miguu yake.
Ama ni kalvan hai a pakui teh, a khoktabei rahim kho lah a hmo.
11 Alipanda juu ya kerubi na kuruka. Alionekana katika mawingu ya upepo.
Cherubim a kâcui teh a kamleng. Bokheiyah, kahlînaw e rathei van a hmu awh.
12 Naye akalifanya giza kuwa hema kumzunguka, akakusanya mawingu makubwa ya mvua angani.
A hmonae hah ama kalupkung lah a sak teh, tui hoi katha poung e tâmainaw a pâkhueng teh,
13 Makaa ya moto yalidondoka mbele zake kutoka katika radi.
a hma lae angnae lahoi hmaisaan a kaman sak.
14 Yahwe alishuka kutoka katika mbingu. Aliyejuu alipiga kelele.
BAWIPA teh kalvan vah a cairing teh, ka lentoe poung e Cathut ni lawk a dei.
15 Alipiga mishale na kuwatawanya adui zake—miale ya radi na kuwasambaratisha.
Licung samtang a pathui teh, ahnimanaw a kâkayei sak. Sumpapalik sak teh ahnimanaw hah a rawk sak.
16 Kisha njia za maji zikaonekana; misingi ya dunia ikawa wazi katika kilio cha vita ya Yahweh, katika sauti za pumzi ya pua zake.
BAWIPA ni yuenae hoi a hnawng dawk hoi kahlî a tâco sak e lahoi, tuipui a dengnae koehoi talaivan adu ungnae hah koung a kamnue sak.
17 Kutoka juu alifika chini; akanishikilia! Aliniondoa katika vilindi vya maji.
A rasangnae hmuen koehoi a kut a kâyap teh, tui moikapap thung hoi na rasa.
18 Aliniokoa kutoka kwa adui zangu wenye nguvu, kwao walionichukia, kwa maana walikuwa na nguvu sana kwangu.
A thakasaipoung e taran kut thung hoi na rungngang. Ahnimouh ni kai na hmuhma awh teh, kai hlak a thasai awh.
19 Walikuja kinyume changu siku ya shida yangu, lakini Yahwe alikuwa msaada wangu.
A rucatnae koe ka phanae tueng dawk, na ngang awh nakunghai, BAWIPA teh kaie kânguenae lah ao.
20 Pia aliniweka mahali panapo nafasi. Aliniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Kai hah kalenpounge hmuen koe na ceikhai awh teh, kai dawk a lunghawi dawkvah, na hlout sak.
21 Yahwe amenituza kwa kipimo cha haki yangu; amenirejesha kwa kiwango cha usafi wa mikono yangu.
BAWIPA ni ka lannae patetlah na tawkphu na poe teh, ka kut a thoung e patetlah na patho.
22 Kwa maana nimezishika njia za Yahwe na sijafanya uovu kwa kugeuka kutoka kwa Mungu.
Bangkongtetpawiteh, BAWIPA e a lamthung hah pou ka dawn teh, kaie Cathut koehoi yon hoi kahmat boihoeh.
23 Kwa kuwa maagizo yake yote ya haki yamekuwa mbele yangu; kwa kuwa sheria zake, sikujiepusha nazo.
A lawkcengnae pueng hah ka hmaitung vah ao. A phunglam ka cettakhai boihoeh.
24 Nimekuwa bila hatia mbele zake pia, na nimejiepusha na dhambi.
A hmaitung hai toun hane kawi lah kaawm hoeh. Ka payonpakainae dawk hoi na hlout sak.
25 Kwa hiyo Yahwe amenirejesha kwa kiasi cha uadilifu wangu, kwa kipimo cha usafi wangu mbele zake.
Hatdawkvah, ka lannae patetlah na pathung. A mithmu vah kathounge patetlah na patho.
26 Kwa mwaminifu, unajionesha kuwa mwaminifu; kwake asiye na hatia; unajionesha kuwa hauna hatia.
Pahrennae ka tawn e koe pahrennae ka tawn e patetlah na kamnue teh, tamikalan koe tamikalan lah na kamnue van han.
27 Kwa usafi unajionesha kuwa msafi, lakini kwa wakaidi unajionesha kuwa mkaidi.
Tamikathoung koe, kathounge lah na kamnue vaiteh, tami lungkapataknaw koe a lungpatanae lahoi na kamnue van han.
28 Unaokoa walioteswa, lakini macho yako ni kinyume cha wenye kiburi, unawashusha chini.
Kârahnoum e tami hah na rungngang teh, kâoupnaw na pabo hanelah pou na khet.
29 Kwa maana wewe ni taa yangu, Yahwe. Yahwe huangaza katika giza langu.
Oe BAWIPA, nang teh kaie hmaiim lah na o. BAWIPA ni kaie hmonae a ang sak han.
30 Maana kwa ajili yake ninaweza kupita vipingamizi; kwa msaada wa Mungu wangu naweza kuruka juu ya ukuta.
Kai ni nang na kângue e lahoi ransahu ka tâ teh, rapan hai ka yawngtapue thai.
31 Maana njia za Mungu ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi. Yeye ni ngao yao wanaomkimbilia.
Cathut e a lamthung teh a kuep. Yuemkamcu lawk teh tanouk lah ao. Kâuepnaw pueng hanelah bahling lah ao.
32 Maana ni nani aliye Mungu isipokuwa Yahwe? Na ni nani aliyemwamba isipokuwa Mungu?
BAWIPA hoeh e laipalah Cathut alouke ao maw. Cathut laipalah, lungsong alouke ao maw.
33 Mungu ni kimbilio langu, na umwongoza katika njia yake mtu asiye na hatia.
Cathut teh ka thaonae hoi ka kângue e lah ao, ka lamthung a hmacawn sak.
34 Huifanya myepesi miguu yangu kama kurungu na kuniweka katika vilima virefu.
Ka khok heh sayuk e a khok patetlah a hue a rang sak teh, a hmuen karasang e koe na o sak.
35 Huifundisha mikono yangu kwa vita, na viganja vyangu kupinda upinde wa shaba.
Ka kut teh tarantuk nahan a cangkhai. Hottelah rahum licung hai ka sawn thai.
36 Umenipa ngao ya wokovu wako, na matakwa yako yamenifanya mkuu.
Nama ni rungngangnae saiphei hah na poe teh, a lungsawnae lahoi kai teh na tawm rasang e lah ka o.
37 Umeitengenezea miguu yangu nafasi chini yangu, hivyo miguu yangu haikujikwaa.
Kai ni ka cei nahane lamthung na pacei teh, ka khoknaw hai thawn hoeh.
38 Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza. Sikurudi nyuma hadi walipoangamizwa.
Ka tarannaw ka pha teh ka thei, koung ka thei hoehroukrak kai ni ka ban hoeh.
39 Niliwararua na kuwasambaratisha; hawawezi kuinuka. Wameanguka chini ya miguu yangu.
Kaie ka khok rahim a rawp awh teh, a thaw thai awh hoeh nahanelah, katinkaawi teh ka thei.
40 Unaweka nguvu ndani yangu kama mkanda kwa vita; unawaweka chini yangu wanaoinuka kinyume changu.
Bangkongtetpawiteh, tarantuk sak hanelah, nang ni thaonae hoi na pathoup teh, kai na katuknaw hah kaie rahim na sung sak.
41 Ulinipa migongo ya shingo za adui zangu; niliwaangamiza kabisa wale wanaonichukia.
Kai na ka hmuhma e a lahuennaw hah kai koe na poe teh, nama ni kai na katuknaw hah hnuklah na kamlang sak.
42 Walilia kwa msaada, lakini hakuna aliyewaokoa; walimlilia Yahwe, lakini hakuwajibu.
A hram awh ei, ka rungngang hane tami awmhoeh. BAWIPA teh a khet awh ei, pato awh hoeh.
43 Niliwaponda katika vipande kama mavumbi juu ya ardhi, niliwakanyaga kama matope mitaani.
Hatnavah, kai ni ahnimanaw hah vaiphu patetlah reppasei lah ka phawm teh, lam dawk songnawng patetlah ka coungroe awh teh, kaheikalai awh.
44 Umeniokoa pia kutoka katika mashutumu ya watu wangu. Umeniweka kama kichwa cha mataifa. Watu nisiowajua wananitumikia.
Nang ni ka taminaw hoi hawihoehnae dawk hoi na rungngang teh, Jentelnaw e kaukkung lah na o sak nahanelah, na ring e ka panuek boihoeh e naw ni, kaimae thaw a tawk awh han.
45 Wageni walishurutishwa kuniinamia. Mara waliposikia kuhusu mimi, walinitii.
Jentelnaw hah kai koe a kâpoe awh vaiteh, a thai awh tahma ka lawk a ngai awh han.
46 Wageni walikuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
Jentelnaw a tâco awh han.
47 Yahwe anaishi! Mwamba wangu atukuzwe. Mungu na ainuliwe, mwamba wa wokovu wangu.
BAWIPA teh yungyoe a hring. Kaie lungsong, pholennae lah awm seh. Kaie rungngangnae lungsong Cathut teh, tawmrasang e lah awm naseh.
48 Huyu ndiye Mungu anilipiaye kisasi, awawekaye watu chini yangu.
Kai koe lah moi ka pathung pouh e hoi miphun pueng kaie rahim ka pabawt e teh katâkung Cathut doeh.
49 Uniweka huru mbali na adui zangu. Hakika, uliniinua juu yao walioinuka kinyume changu. Uliniokoa kutoka kwa watu wenye ghasia.
Tarannaw e kut dawk hoi, na hlout sak. Kai na ka taran naw e a lathueng vah, na tawm teh, ka mathoutmakainaw e kut dawk hoi na hlout sak.
50 Kwa hiyo nitakushukuru, Yahwe, kati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Hatdawkvah, Oe BAWIPA, kai teh Jentelnaw koevah, lunghawinae lawk ka dei vaiteh, na min pholennae la ka sak han.
51 Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na uonesha uaminifu wake wa kiagano kwa mtiwa mafuta wake, kwa Daudi na uzao wake daima.”
Cathut teh a siangpahrang hanelah, rungngangnae imrasang lah ao teh, satui a awi e Devit hoi a canaw koe lathueng vah yungyoe hoi yungyoe totouh, pahren lungmanae a kamnue sak.