< 2 Samweli 20 >
1 Ikatukia pia kuwa katika eneo lilelile kulikuwa mfanya fujo jina lake Sheba mwana wa Bikri Mbenjamini. Akapiga tarumbeta na kusema, “Sisi hatuna sehemu katika Daudi, wala hatuna urithi katika mwana wa Yese. Haya kila mtu na aende nyumbani kwake, Israeli.”
Il arriva aussi que là était un homme de Bélial, du nom de Séba, fils de Bochri, homme de Jémini, et il sonna de la trompette, et dit: Nous n’avons point de part avec David, ni d’héritage avec le fils d’Isaï; retourne en tes tabernacles, ô Israël.
2 Hivyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana wa Bikri. Lakini watu wa Yuda wakamfuata mfalme wao kwa karibu sana, kutoka Yordani njia yote hadi Yerusalemu.
Et tout Israël se sépara de David, et suivit Séba, fils de Bochri; mais les hommes de Juda restèrent près de leur roi, depuis le Jourdain jusqu’à Jérusalem.
3 Daudi alipofika katika kasri lake huko Yerusalemu, akawachukua masuria aliokuwa amewaacha kulitunza kasri, na akawaweka katika nyumba chini ya uangalizi. Aliwaandalia mahitaji yao lakini hakulala nao tena. Hivyo walikuwa wametengwa hadi siku ya kufa kwao, waliishi kama wajane.
Et lorsque le roi fut venu en sa maison à Jérusalem, il prit les dix femmes qu’il avait laissées pour garder la maison, les donna en garde, leur fournissant les aliments; et il ne s’approcha plus d’elles: mais elles étaient enfermées jusqu’au jour de leur mort, vivant en veuves.
4 Kisha mfalme akamwambia Amasa, “Uwaite watu wa Yuda ndani ya siku hizi tatu; wewe pia uwepo hapa.”
Or, le roi dit à Amasa: Appelle près de moi tous les hommes de Juda pour le troisième jour, et toi, sois présent.
5 Hivyo Amasa akaenda kuwaalika watu wote wa Yuda kwa pamoja, lakini akatumia muda mrefu kulika mfalme alivyokuwa amemwamuru.
Amasa donc s’en alla pour appeler Juda, et il tarda au-delà de l’ordre que lui avait donné le roi.
6 Hivyo Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatufanyia madhara zaidi ya Absalomu. Chukua watumishi wa bwana wako, askari wangu, na umfuatie asije akaingia katika mji wenye ngome na kututoroka.”
Or David dit à Abisaï: Maintenant Séba, fils de Bochri, nous affligera plus qu’Absalom: prends donc les serviteurs de ton seigneur, et poursuis-le, de peur qu’il ne trouve des villes fortifiées, et qu’il ne nous échappe.
7 Ndipo watu wa Yoabu wakamfuatia, pamoja na Wakerethi na Wapelethi na mashujaa wote. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
Les hommes de Joab sortirent donc avec lui, les Céréthiens aussi et les Phélétiens; et tous les hommes vigoureux sortirent de Jérusalem pour poursuivre Séba, fils de Bochri.
8 Walipokuwa katika jiwe kubwa lililoko Gibeoni, Amasa akaja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa silaha ya vita aliyokuwa ameivaa, alikuwa pia na upanga uliokuwa umefungwa na mkanda katika kiuno chake. Kadili alivyoendelea mbele upanga ukadondoka.
Et lorsqu’ils furent près de la grande pierre qui est à Gabaon, Amasa, venant, les rencontra. Or, Joab était vêtu d’une tunique étroite, selon la mesure de son habit, et par-dessus ceint d’un glaive pendant à ses côtés dans son fourreau, et fait de manière qu’il pouvait par un léger mouvement sortir et frapper.
9 Hivyo Yoabu akamwambia Amasa, “Haujambo binamu yangu?” Kwa utaratibu Yoabu akakishika kidevu cha Amasa kwa mkono wake wa kulia ili ambusu.
C’est pourquoi Joab dit à Amasa: Salut, mon frère. Et de sa main droite, il prit le menton d’Amasa, comme pour le baiser.
10 Amasa hakutambua kwamba kulikuwa na jambia katika mkono wa kushoto wa Yoabu. Yoabu akamchoma Amasa tumboni na matumbo yake yakadondoka chini. Wala Yoabu hakumpiga tena, na Amasa akafa. Hivyo Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
Or Amasa ne prit point garde au glaive qu’avait Joab, qui le frappa dans le côté, et répandit ses entrailles sur la terre; et il ne le frappa point d’un second coup, et Amasa mourut. Ensuite Joab et Abisaï son frère poursuivirent Séba, fils de Bochri.
11 Kisha mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa naye akasema, “Aliye upande wa Yoabu na aliyeupande wa Daudi na amfuate Yoabu.”
Cependant quelques hommes des compagnons de Joab, s’étant arrêtés près du cadavre d’Amasa, dirent: Voilà celui qui a voulu être de la suite de David à la place de Joab.
12 Amasa akawa anagalagala katika damu yake katikati ya njia. Mtu yule alipoona kwamba watu wote wamesimama, akambeba Amasa na kumweka shambani kando ya njia. Akatupa vazi juu yake kwa maana aliona kila mmoja aliyekuja alisimamaa pale.
Et Amasa, couvert de sang, gisait au milieu de la voie. Mais un certain homme vit que tout le peuple s’arrêtait pour le voir; il poussa Amasa de la voie dans le champ, et le couvrit d’un vêtement, afin que les passants ne s’arrêtassent pas à cause de lui.
13 Baada ya Amasa kuondolewa njiani watu wote wakamfuata Yoabu katika kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
Amasa donc ôté de la voie, tout homme passait, suivant Joab, pour poursuivre Séba, fils de Bochri.
14 Sheba akazipita kabila zote za Israeli mpaka Abeli wa Beth Maaka, na katika nchi yote ya Berite ambao pia walijikusanya pamoja pia na kumfuatia Sheba.
Mais celui-ci avait passé à travers toutes les tribus d’Israël, à Abéla et à Bethmaacha; et tous les hommes choisis s’étaient assemblés auprès de lui.
15 Walimpata na kumzingira huko Abeli wa Bethi Maaka. Wakajenga buruji ya kuhusuru mji nyuma ya ukuta. Jeshi lote lilokuwa pamoja na Yoabu likaugongagonga ukuta ili uanguke.
C’est pourquoi Joab et les siens vinrent, et l’assiégèrent à Abéla et à Bethmaacha; et ils environnèrent la ville de fortifications, et la ville fut investie: or, toute la multitude qui était avec Joab s’efforçait de détruire les murs.
16 Ndipo mwanamke mwerevu akapiga kelele kutoka ndani ya mji, “Sikiliza, Yoabu, tafadhari sikiliza! Sogea karibu nami ili niongee nawe.”
Et une femme sage de la ville s’écria: Ecoutez, écoutez; dites à Joab: Approche-toi d’ici, et je te parlerai.
17 Hivyo Yoabu akakaribia, mwanamke akamwambia, “Je wewe ni Yoabu? Akajibu, “ni mimi.” mwanamke akamwambia, “Sikiliza maneno ya mtumishi wako.” Akajibu, “Nasikiliza.”
Lorsque Joab se fut approché d’elle, elle lui dit: C’est toi qui es Joab? Et celui-ci répondit: Moi. Elle lui parla ainsi: Ecoute les paroles de ta servante. Joab répondit: J’écoute.
18 Ndipo aliposema,”Hapo zamani ilisemwa, 'Bila shaka tafuteni ushauri huko Abeli,' na kwamba ushauri huo utakata maneno.
Et elle de nouveau: Ce mot, dit-elle, se disait dans un ancien proverbe: Ceux qui interrogent, qu’ils interrogent à Abéla; et c’est ainsi qu’ils arrivaient au but.
19 Sisi ni mji ulio miongoni mwa miji yenye nguvu na aminifu sana katika Israeli. Mnataka kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kuumeza urithi wa Yahwe?”
N’est-ce pas moi qui réponds la vérité en Israël, et toi, tu demandes à bouleverser une cité, et à détruire une mère en Israël? Pourquoi renverses-tu l’héritage du Seigneur?
20 Ndipo Yoabu alipojibu na kusema, “Iwe mbali, iwe mbali nami, hata nikameze au kuharibu.
Et répondant, Joab dit: Loin de moi, loin de moi cela! je ne renverse, ni ne démolis.
21 Hiyo si kweli. Lakini mtu kutoka katika nchi ya milima ya Efraimu, aitwaye Sheba mwana wa Bikri, ameinua mkono wake kinyume cha mfalme, kinyume cha Daudi. Mtoeni yeye nami nitauacha mji.” Mwanamke akamwambia Yoabu, “Utarushiwa kichwa chake kutoka juu ya ukuta.”
La chose n’est pas ainsi; mais un homme de la montagne d’Ephraïm, Séba, fils de Bochri par son surnom, a levé sa main contre le roi David: livrez-le seul, et nous nous retirerons de la ville. Et la femme dit à Joab: Voilà que sa tête te sera envoyée par-dessus le mur.
22 Kisha mwanamke akawaendea watu wote wa mji kwa hekima yake. Wakakiondoa kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumrushia Yoabu. Ndipo alipopiga tarumbeta na watu wa Yoabu wakauacha mji kila mtu nyumbani kwake. Na Yoabu akarejea Yerusalemu kwa mfalme.
Elle s’avança donc vers tout le peuple, et parla sagement; et ayant coupé la tête de Séba, fils de Bochri, ils la jetèrent à Joab. Et celui-ci sonna de la trompette, et ils se retirèrent de la ville, chacun en ses tabernacles; mais Joab retourna à Jérusalem près du roi.
23 Yoabu alikuwa juu ya jeshi lote la Israeli na Benaya mwana wa Yehoiada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi.
Joab donc fut chef de toute l’armée d’Israël, mais Banaïas, fils de Joïada, des Céréthiens et des Phéléthiens,
24 Adoramu alikuwa juu ya watu waliofanya kazi ya shokoa na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mkumbushaji.
Et Aduram, des tributs; et Josaphat, fils d’Ahilud, tenait les registres.
25 Sheva alikuwa mwandishi, na Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani.
Siva était scribe, et Sadoc et Abiathar, prêtres.
26 Ira wa Yairi alikuwa mhudumu mkuu wa Daudi.
Mais Ira, le Jaïrite, était prêtre de David.