< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya haya Daudi akamuuliza Yahwe, “Je naweza kuupandia mmojawapo wa miji ya Yuda?” Yahweh akamjibu, “Panda.” Daudi akauliza, “Niuendee mji upi? Yahwe akajibu, “Hebroni”
And after these things David consulted the Lord, saying: Shall I go up into one of the cities of Juda? And the Lord said to him: Go up. And David said: Whither shall I go up? And he answered him: Into Hebron.
2 Hivyo Daudi akakwea pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
So David went up, and his two wives, Achinoam the Jezrahelitess, and Abigail the wife of Nabal of Carmel:
3 Daudi akawaleta watu waliokuwa pamoja naye, na kila mmoja akaleta familia yake katika mji wa Hebroni walipoanza kuishi.
And the men also that were with him, David brought up every man with his household: and they abode in the towns of Hebron.
4 Kisha watu wa Yuda wakaja na kumtia Daudi mafuta kuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Wakamwambia Daudi, “Watu wa Yabeshi Gileadi wamemzika Sauli.”
And the men of Juda came, and anointed David there, to be king over the house of Juda. And it was told David, that the men of Jabes Galaad had buried Saul.
5 Hivyo Daudi akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi Gileadi akawambia, “Mbarikiwe na Yahwe, kwa kuwa mmeonesha utiifu huu kwa bwana wenu Sauli mliyemzika.
David therefore sent messengers to the men of Jabes Galaad, and said to them: Blessed be you to the Lord, who have shewn this mercy to your master Saul, and have buried him.
6 Sasa Yahwe awadhihirishie utiifu na uaminifu wa kiagano. Nami pia nitawaonesha wema kwa sababu ya yale mliyoyafanya.
And now the Lord surely will render you mercy and truth, and I also will, requite you for this good turn, because you have done this thing.
7 Sasa basi, mikono yenu itiwe nguvu; mwe jasiri kwa maana Sauli bwana wenu amekufa, na nyumba yote ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalime wao.
Let your hands be strengthened, and be ye men of valour: for although your master Saul be dead, yet the house of Juda hath anointed me to be their king.
8 Lakini Abneri mwana wa Neri, mkuu wa jeshi la Sauli, akamchukuwa Ishboshethi mwana wa Sauli akamleta Mahanaimu.
But Abner the son of Ner, general of Saul’s army, took Isboseth the son of Saul, and led him about through the camp?
9 Akamfanya Ishboshethi mfalme juu ya Gileadi, Asheri, Yezreeli, Efraimu, Benjamini na juu ya Israeli yote.
And made him king over Galaad, and, over Gessuri, and over Jezrahel, and over Ephraim, and over Benjamin, and over all Israel.
10 Ishiboshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala juu ya Israeli, akatawala miaka miwili. Lakini nyumba ya Yuda ikaambatana na Daudi.
Isboseth the son of Saul was forty years old when he began to reign over, Israel, and he reigned two years: and only the house of Juda followed David.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ni miaka saba na miezi sita.
And the number of the days that David abode, reigning in Hebron over the house of Juda, was seven years and six months.
12 Abneri mwana wa Neri na watumishi wa Ishboshethi mwana wa Sauli walitoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
And Abner the son of Ner, and the servants of Isboseth the son of Saul, went out from the camp to Gabaon.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watumishi wa Daudi wakatoka na kukutana nao katika bwawa la Gibeoni. Wakakaa pale, kundi moja upande huu wa bwawa na kundi lingine upande wa pili.
And Joab the son of Sarvia, and the servants of David went out, and met them by the pool of Gabaon. And when they were come together, they sat down over against one another: the one on the one side of the pool, and the other on the other side.
14 Abneri akamwambia Yoabu, “haya, vijana na wainuke na kushindana mbele yetu.” Yoabu akajibu, “haya na wainuke.”
And Abner said to Joab: Let the young men rise, and play before us. And Joab answered: Let them rise.
15 Ndipo vijana walipoinuka na kukutana, kumi na wawili kwa ajili ya Banjamini na Ishboshethi mwana wa Sauli, na kumi na wawili kutoka kwa watumishi wa Daudi.
Then there arose and went over twelve in number of Benjamin, of the part of Isboseth the son of Saul, and twelve of the servants of David.
16 Kila mtu akakamata kichwa cha adui yake na kupiga upanga wake katika ubavu wa adui yake, wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale pakaitwa kwa Kiebrania, “Helkath Hazzurim,” yaani “konde la upanga,” lililopo Gibeoni.
And every one catching his fellow, by the head, thrust his sword into the side of his adversary, and they fell down together: and the name of the place was called: The field of the valiant, in Gabaon.
17 Vita ikawa kali sana siku ile na Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watumishi wa Daudi.
And there was a very fierce battle that day: and Abner was put to flight, with the men of Israel, by the servants of David.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwepo pale: Yoabu, Abishai na Asaheli.
And there were the three sons of Sarvia there, Joab, and Abisai, and Asael: now Asael was a most swift runner, like one of the roes that abide in the woods.
19 Asaheli alikuwa mwepesi miguuni kama paa. Akamfuatilia Abneri kwa karibu bila kugeuka upande wowote.
And Asael pursued after Abner, and turned not to the right hand nor to the left from following Abner.
20 Abneri akaangalia nyuma yake na kusema, “Ni wewe Asaheli?” Akajibu, “ni mimi.”
And Abner looked behind him, and said: Art thou Asael? And he answered: I am.
21 Abneri akamwambia, “Geuka upande wako wa kuria au kushoto umshike mmojawapo wa vijana na kuchukua silaha yake.” Lakini Asaheli hakugeuka.
And Abner said to him: Go to the right hand or to the left, and lay hold on one of the young men and take thee his spoils. But Asael would not leave off following him close.
22 Ndipo Abneri alipomwambia tena Asaheli, “Simama usinifuate. Kwa nini nikupige hata chini? Nitautazamaje uso wa Yoabu ndugu yako?”
And again Abner said to Asael: Go off, and do not follow me, lest I be obliged to stab thee to the ground, and I shall not be able to hold up my face to Joab thy brother.
23 Lakini Asaheli hakukubari kugeuka. na hivyo Abneri akamchoma kwa nchi ya mkuki wake, hata ukatokea upande wa pili. Asaheli akaanguka chini akafa. Hata ikawa kila mmoja aliyefika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa, alisimama hapo hapo.
But he refused to hearken to him, and would not turn aside: wherefore Abner struck him with his spear with a back stroke in the groin, and thrust him through, and he died upon the spot: and all that came to the place where Asael fell down and died stood still.
24 Lakini Yoabu na Abishai wakamfuatilia Abneri. Wakati jua linazama walikuwa wamefika mlima wa Amma, uliopo karibu na Gia katika njia ielekeayo nyika ya Gibeoni.
Now while Joab and Abisai pursued after Abner, the sun went down: and they came as far as the hill of the aqueduct, that lieth over against the valley by the way of the wilderness in Gabaon.
25 Wabenjamini wakajikusanya nyuma ya Abneri na kusimama juu ya kilima.
And the children of Benjamin gathered themselves together to Abner: and being joined in one body, they stood on the top of a hill.
26 Kisha Abneri akamwita Yoabu na kusema, “Je ni lazima upanga uendelee kurarua daima? Je haujui kwamba mwisho wake utakuwa mchungu? Hata line ndipo uwaambie watu wako waache kuwafuatia ndugu zao?”
And Abner cried out to Joab, and said: Shall thy sword rage unto utter destruction? knowest thou not that it is dangerous to drive people to despair? how long dost thou defer to bid the people cease from pursuing after their brethren?
27 Yoabu akajibu, “Kama Mungu aishivyo, usingesema hivyo, askari wangu wangewafuatia ndugu zao hata asubuhi!”
And Joab said: As the Lord liveth, if thou hadst spoke sooner, even in the morning the people should have retired from pursuing after their brethren.
28 Ndipo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wote wakasimama na hawakuendelea kuwafuata Israeli tena wala hawakupigana tena.
Then Joab sounded the trumpet, and all the army stood still, and did not pursue after Israel any farther, nor fight any more.
29 Abneri na watu wake wakasafiri usiku wote kupitia Araba. Wakavuka Yordani, wakatembea asubuhi yote iliyofuata, na hata wakafika Mahanaimu.
And Abner and his men walked all that night through the plains: and they passed the Jordan, and having gone through all Beth-horon, came to the camp.
30 Yoabu akarudi kutoka katika kumfuatia Abneri. Akawakusanya watu wake wote, ambopo Asahali na askari wengine kumi na tisa wa Daudi walipungua.
And Joab returning, after he had left Abner, assembled all the people: and there were wanting of David’s servants nineteen men, beside Asael.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wameua watu 360 wa Benjamini na Abneri.
But the servants of David had killed of Benjamin, and of the men that were with Abner, three hundred and sixty, who all died.
32 Kisha wakamchukua Asahali na kumzika katika kaburi la baba yake, lililokuwapo Bethlehemu. Yoabu na watu wake wakasafiri usiku wote, kukacha wakati wanafika Hebroni.
And they took Asael, and buried him in the sepulchre of his father in Bethlehem, and Joab, and the men that were with him, marched all the night, and they came to Hebron at break of day.

< 2 Samweli 2 >