< 2 Samweli 18 >

1 Daudi akawahesabu askari waliokuwa pamoja naye na akaweka akida wa elfu na akida wa mia juu yao.
And David numbered the people that were with him, and he set over them captains of thousands and captains of hundreds.
2 Kisha Daudi akalipeleka jeshi, thelusi moja chini ya Yoabu, thelusi nyingine chini ya Abishai mwana wa Seruya, ndugu wa Yoabu, na thelusi nyingine tena chini ya Itai Mgiti. Mfalme akaliambia jeshi, “kwa hakika mimi mwenyewe pia nitakwenda pamoja nanyi.
And David sent forth the people a third part under the command of Joab, and a third part under the command of Abishai the son of Zeruyah, Joab's brother, and a third part under the command of Ittai the Gittite. And the king said unto the people, I myself also will without fail go forth with you.
3 Lakini watu wakasema, “Wewe usiende vitani, kwani ikiwa tutakimbia hawatatujari sisi, ama nusu yetu wakifa hawatajari. Lakini wewe ni zaidi ya elfu kumi yetu sisi! Kwa hiyo ni afadhari zaidi ukitusaidia ukiwa mjini.”
But the people said, Thou shalt not go forth; for if we should have to flee away, they will not care for us; and if half of us die, they will not care for us; for now thou art worth ten thousand of us: therefore now it is better that thou shouldst be a succor to us out of the city.
4 Hivyo mfalme akawajibu, “Nitafanya lolote lionekanalo jema machoni penu.” Mfalme akasimama kati ya lango la mji wakati jeshi lilipoondoka katika mamia na katika maelfu.
And the king said unto them, What seemeth good in your eyes will I do. And the king placed himself by the side of the gate, and all the people went out by hundreds and by thousands.
5 Mfalme akawaagiza Yoabu, Abishai, na Itai kusema, “Mmtendee huyo kijana, Absalomu, kwa upole kwa ajili yangu.” Watu wote wakasikia jinsi mfalme alivyowaagiza maakida kuhusu Absalomu.
And the king commanded Joab and Abishai and Ittai, saying, Deal gently for my sake with the young man, with Abshalom. And all the people heard when the king charged all the captains with respect to Abshalom.
6 Hivyo jeshi likaenda nyikani dhidi ya Israeli; vita ikaenea katika msitu wa Efraimu.
So the people went out into the field against Israel: and the battle took place in the forest of Ephraim.
7 Jeshi la Israeli likashindwa mbele ya askari wa Daudi; kulikuwa na machinjo makuu kwa watu elfu ishirini siku hiyo.
And the people of Israel were smitten there before David's servants, and the slaughter was great there on that day—twenty thousand men.
8 Vita ikaenea katika eneo lote na watu wengi wakaangamizwa na msitu kuliko upanga.
And the battle became extended there over the face of all the country: and the forest devoured yet more of the people than the sword had devoured on that day.
9 Ikatukia kwamba Absalomu akakutana na askari wa Daudi. Absalomu alikuwa amepanda juu ya nyumbu wake na nyumbu akapita chini ya matawi manene ya mti wa mwaloni, na kichwa chake kikanaswa katika matawi ya mti. Akaachwa akining'inia kati ya nchi na anga wakati nyumbu alipoendelea mbele.
And Abshalom happened to come before the servants of David. And Abshalom was riding upon a mule, and the mule came under the thick boughs of a great oak, and his head caught hold of the oak, and he was left hanging between the heaven and the earth: and the mule that was under him passed on.
10 Mtu mmoja akaona lililotukia na akamwambia Yoabu, “Tazama, nilimwona Absalomu akining'inia katika mwaloni!”
And a certain man saw, and told it to Joab, and said, Behold, I have seen Abshalom hanging on an oak.
11 Yoabu akamwambia aliyemwambia kuhusu Absalomu, “Tazama! Ulimwona! Kwa nini haukumpiga hata chini. Ningekupa shekeli kumi za fedha na mkanda.”
And Joab said unto the man that told him, And, behold, thou sawest him: why then didst thou not smite him there to the ground? and it would have been obligatory on me to give thee ten shekels of silver and a girdle.
12 Yule mtu akamjibu Yoabu, “Hata kama ningepewa shekeli elfu za fedha hata hivyo nisingeinua mkono wangu juu ya mwana wa mfalme, kwa maana sisi sote tulimsikia mfalme akiwaagiza wewe, Abishai na Itai kusema, mtu asimguse huyo kijana Absalomu.'
And the man said unto Joab, And though I should weigh on my hands a thousand shekels of silver, I would not stretch forth my hand against the king's son; for before our ears did the king charge thee and Abishai and Ittai, saying, Take heed, whoever it be, of the young man, of Abshalom.
13 Ikiwa ningehatarisha maisha yangu kwa uongo(na hakuna jambo linalofichika kwa mfalme), ungejitenga nami.”
Or should I even have acted with falsehood against my own life, since there is no matter which can be hidden from the king; thou wouldst surely have placed thyself aloof.
14 Ndipo Yoabu aliposema, “sitakusubiri.” Kisha akachukua mishale mitatu mkononi mwake na akairusha katika moyo wa Absalomu wakati yu ngali hai na amening'inia katika mwaloni.
Then said Joab, I will not wait thus before thee. And he took three darts in his hand, and thrust them into the heart of Abshalom, who was yet alive in the midst of the oak.
15 Kisha vijana kumi waliochukua slaha za Yoabu wakamzunguka Absalomu, wakampiga na kumwua.
And ten young men, Joab's armor-bearers, encompassed and smote Abshalom, and slew him.
16 Kisha Yoabu akapiga tarumbeta na jeshi likarudi kutoka kuwafuatia Israeli, hivyo Yoabu akalirudisha jeshi.
And Joab blew the cornet, and the people returned from pursuing after Israel; for Joab restrained the people.
17 Wakamchukua Absalomu na kumtupa katika shimo kubwa msituni; wakaufukia mwili wake chini ya rundo kubwa la mawe, wakati Israeli wote walipokimbia kila mtu nyumbani kwake.
And they took Abshalom, and cast him down in the forest, into the large pit, and erected upon him a very great heap of stones: and all Israel fled, every one, to his tents.
18 Wakati Absalomu alipokuwa yu ngali hai alijijengea nguzo kubwa ya jiwe katika Bonde la Mfalme, kwani alisema, “Sina mwana wa kuchukua kumbukumbu ya jina langu.” Akaiita nguzo kwa jina lake, hivyo inaitwa Mnara wa Absalomu hata leo.
Now Abshalom had taken and reared up for himself in his lifetime, the pillar, which is in the king's dale; for he said, I have no son, so as to keep my name in remembrance; and he called the pillar after his own name: and it was called Abshalom's monument, even until this day.
19 Kisha Ahimaasi mwana wa Sadoki akasema, “Niruhusu niende kwa mfalme na habari njema, jinsi Yahwe alivyomwokoa kutoka mkono wa adui zake.”
And Achima'az the son of Zadok said, Do let me run, I pray thee, and bear the king tidings, that the Lord hath done him justice from the power of his enemies.
20 Yoabu akamjibu, “Wewe hautakuwa mchukua habari leo; utafanya hivyo siku nyingine. Leo hautachukua habari yoyote kwa maana mwana wa mfalme ameuawa.”
And Joab said unto him, Thou art not the man to bear [good] tidings this day, and thou shalt bear tidings another day; but this day thou shalt bear no tidings, because the king's son is dead.
21 Ndipo Yoabu akamwambia Mkushi, “Nenda umwambia mfalme ulichokiona.” Mkushi akamwinamia Yoabu, na kisha akakimbia.
Then said Joab to the Cushi, Go tell the king what thou hast seen, And Cushi bowed himself unto Joab, and ran.
22 Kisha tena, Ahimaasi mwana wa Sadoki akamwambia Yoabu, “Pamoja na yote yanayoweza kutokea, tafadhari niruhusu nami pia niende nimfuate Mkushi.” Yoabu akajibu, “Mwanangu kwa nini unataka kwenda, hautapata thawabu yoyote kwa ajili ya habari hii?”
Then said Achima'az the son of Zadok yet again to Joab, Be it as it may, let me, I pray thee, run also after the Cushi. And Joab said, Wherefore is it that thou wilt run, my son, seeing that thou hast no profitable tidings?
23 “Vyovyote itakavyokuwa niache niende,” Ahimaasi alijibu. Hivyo Yoabu akamjibu, “Nenda.” Ndipo Ahimaasi akakimbia kwa njia ya tambarare na akampita Mkushi.
But be it as it may, let me run. And he said unto him, Run. And Achima'az ran by the way of the plain, and passed the Cushi.
24 Basi Daudi alikuwa amekaa kati ya lango la ndani na lango la nje. Na mlinzi alikuwa juu ya lango ukutani naye akainua macho yake. Alipokuwa akiangalia, akamwona mtu anakaribia huku akikimbia peke yake.
And David was sitting between the two gates: and the watchman went up to the roof of the gate, upon the wall, and as he lifted up his eyes, he saw, and behold, a man was running alone.
25 Mlinzi akaita kwa sauti na kumwambia mfalme. Ndipo mfalme akasema, “Ikiwa yupo peke yake ana habari katika kinywa chake.” Mkimbiaji akasogea na kuukaribia mji.
And the watchman cried, and told it to the king. And the king said, If he be alone, there are tidings in his mouth. And he came nearer and nearer continually.
26 Kisha mlinzi akaona mtu mwingine aliyekuwa anakimbia, naye akamwambia bawabu; kusema, “Tazama, kuna mtu mwingine anakimbia peke yake.” Mfalme akasema, “Yeye pia analeta habari.”
And the watchman saw another man running: and the watchman called unto the gate-keeper, and said, Behold, here is a man running alone. And the king said, Also this one bringeth tidings.
27 Ndipo mlinzi akasema, Nadhani kukimbia kwake mtu aliye mbele ni kama kukimbia kwake Ahimaasi mwana wa Sadoki.” Mfalme akasema, “Yeye ni mtu mwema naye anakuja na habari njema.”
And the watchman said, I regard the running of the foremost as the running of Achima'az the son of Zadok. And the king said, That is a good man, and with good tidings must he come.
28 Ndipo Ahimaasi akaita na kumwambia mfalme, “Yote ni mema.” Kisha akainama yeye mwenyewe uso wake chini mbele ya mfalme na kusema, Atukuzwe Yahwe Mungu wako, aliyewatoa watu walioinua mkono wao kinyume cha bwana wangu mfalme.”
And Achima'az called, and said unto the king, Peace. And he prostrated himself to the king with his face to the earth, and said, Blessed be the Lord thy God, who hath surrendered the men that had lifted up their hand against my Lord the king.
29 Hivyo mfalme akauliza, “Je huyo kijana Absalomu hajambo?” Ahimaasi akajibu, “Wakati Yoabu ananituma kwako mfalme, mimi mtumishi wa mfalme, niliona fujo kubwa sana lakini sikutambua ilihusu nini.”
And the king said, Is the young man Abshalom safe? And Achima'az answered, I saw the greatest crowd when Joab sent off the king's servant, and thy servant; but I know not what hath happened.
30 Mfalme akamwambia, “Geuka usimame kando.” Hivyo Ahimaasi akageuka na kusimama.
And the king said, Turn aside, place thyself here. And he turned aside, and remained standing.
31 Mara Mkushi akafika na kusema, “Kuna habari njema kwa bwana wangu mfalme kwa kuwa leo Yahwe amekulipia kisasi kwa wale wote walioinuka kinyume chako.”
And, behold, the Cushi came [next]; and the Cushi said, Let my lord the king receive the tidings, that the Lord hath done thee justice this day from the power of all those that had risen up against thee.
32 Ndipo mfalme akamwuliza, “Je huyo kijana Absalomu ni mzima?” Mkushi akajibu, “Adui wa bwana wangu mfalme na wote wainukao kukudhuru na wawe kama huyo kijana.”
And the king said unto the Cushi, Is the young man Abshalom safe? And the Cushi answered, May like the young man be the enemies of my Lord the king, and all that have risen up against thee for evil.
33 Ndipo mfalme alipohuzunishwa sana naye akaenda chumbani juu ya lango na kulia. Kadili alivyokwenda aliomboleza, mwanangu Absalomu, mwanangu, mwanangu Absalomu! afadhari ningekufa badala yako, Absalomu, mwanangu, mwanangu!”
And the king was much moved, and he went up to the upper chamber of the gate, and wept: and thus he said as he went, O my son Abshalom, my son, my son Abshalom! who would grant that I had died in thy stead, O Abshalom, my son, my son!

< 2 Samweli 18 >