< 2 Samweli 17 >
1 Kisha Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Niruhusu sasa nichague watu elfu kumi na mbili nami nitaondoka na kumfuatia Daudi usiku huu.
阿希托費耳向說:「讓我選拔一萬二千人,今夜起程去追趕達味。
2 Nitampata kwa ghafla wakati amechoka na dhaifu nami nitamstukiza kwa hofu. Watu waliopamoja naye watakimbia nami nitamshambulia mfalme peke yake.
正當他困乏疲倦時,我忽然趕到,使他驚惶失措,隨從他的人,必會逃散,我只把君王一人殺了,
3 Nitawarejesha watu wote kwako kama bibi harusi ajavyo kwa bwana wake, na watu wote watakuwa katika amani chini yako.”
然後人民來歸順你,像新娘回到新郎那裏;你只須害一人的性命,全民眾就都和平無事了」。
4 Alichokisema Ahithofeli kikampendeza mfalme na wazee wote wa Israeli.
阿貝沙隆和以色列的眾長老,對這提議都很贊成。
5 Kisha Absalomu akasema, “Sasa mwiteni pia Hushai Mwarki ili tusikie yeye pia anasemavyo.”
阿貝沙隆說:「讓把阿爾基人胡瑟召來,我們也願聽聽他說什麼」。
6 Hushai alipofika kwa Absalomu, Absalomu akamweleza kile ambacho Ahithofeli alikuwa amesema na kisha akamwuliza Hushai, “Je tufanye alivyosema Ahithofeli? Ikiwa hapana, tueleze kile unachoshauri.”
胡瑟來到阿貝沙隆前,阿貝沙隆向他說:「阿希托費耳說出這樣的話,我們應按他的主意去行嗎﹖請你提議吧! 」
7 Hivyo Hushai akamwambia Absalomu, “Ushauri aliotoa Ahithofeli siyo mzuri kwa wakati huu.”
胡瑟回答阿貝沙隆說:「阿希托費耳這次所出的計謀卻是不妙」。
8 Hushai akaongeza, “Unamjua baba yako na kwamba watu wake ni mashujaa na kwa sasa wanauchungu, ni kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake mwituni. Baba yako ni mtu wa vita; hatalala na jeshi usiku huu.
胡瑟接著說:「你知道你父親和隨從他的人,都是勇將,現在心情惱怒,好像田野間喪子的母熊;何況,你父親又是歷戰陣的人,夜間決不會讓軍民安睡。
9 Tazama, kwa wakati huu pengine amejificha katika shimo fulani au mahali pengine. Itakuwa kwamba baadhi ya watu wako watakapokuwa wameuawa mwanzoni mwa shambulio hata kila mtu atakayesikia atasema, mauaji yamefanyika kwa askari wanaomfuata Absalomu.'
他現在必藏在一個山洞裏,或另一個地方;若起初我們的人就有傷亡,人們聽見必要說:跟隨阿貝沙隆的人,慘遭失敗;
10 Kisha hata askari jasiri zaidi ambao moyo wao ni kama moyo wa simba, wataogopa kwa kuwa Israeli yote inajua kwamba baba yako ni mtu mwenye nguvu na kwamba watu alionao ni wenye nguvu sana.
那麼,連性情兇猛如獅子的壯士,也要灰心喪膽,因為全以色列人都知道你父親是個勇將,跟隨他的人,也都是驍勇的人。
11 Hivyo ninashauri kwamba Israeli wote wakutanike kwako pamoja kutoka Dani hadi Beersheba, wengi kama mchanga ufuoni mwa bahari na kwamba wewe mwenyewe uende vitani.
我的計劃,是先把所有的以色列人集合在你身邊,從丹直到貝爾舍巴,像海邊沙粒那樣多,然後由你親自率領,前去征討;
12 Kisha tutampata popote atakapokuwa nasi tutamfunika kama umande uangukavyo juu ya nchi. Hatutamwachia hata mmoja aliye hai kati ya watu wake wala yeye mwenyewe.
他不論到那裏,我們也突然到那裏;像露一樣襲擊他,使他和跟隨他的人一個也不留下。
13 Ikiwa ataingia ndani ya mji kisha Israeli wote tutaleta kamba juu ya mji huo na kuukokotea mtoni, hata kusionekane hata jiwe moja dogo lililosalia.”
若他退入一座城內,全以色列就帶著繩索去攻擊那城,將那城拉到山谷裏,連一塊小石也不剩下」。
14 Kisha Absalomu na watu wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai Mwarki ni jema kuliko lile la Ahithofeli. Yahwe aliwafanya wakatae shauri jema la Ahithofeli ili kumwangamiza Absalomu.
阿貝沙隆和全以色列人都說:「阿爾基人胡瑟的計謀比阿希托費耳的更為可取」。原是上主決定了要破壞阿希托費耳是好計謀,為給阿彼瑟降下災禍。
15 Kisha Hushai akawambia Sadoki na Abiathari makuhani, “Ahithofeli alimshauri Absalomu na wazee wa Israeli hivi na hivi, lakini mimi nimeshauri vinginevyo.
隨後,胡瑟報告匝多克和厄貝雅塔爾說:「阿希托費耳給阿貝沙隆和以色列長老出了那樣的計謀,我卻出了這樣的計謀。
16 Sasa basi, nendeni haraka na mmtaarifu Daudi kusema, 'Usipige kambi usiku huu katika vivuko vya Araba, lakini kwa namna yoyote vukeni, tofauti na hapo mfalme atamezwa pamoja na watu wote walio pamoja naye.”
現在,快派人去報告達味說:今夜不可在曠野的渡口露宿,要趕快過河,免得君王和隨從他的人民都遭殲滅」。
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwako katika chemichemi za En Rogeli. Hivyo kijakazi mmoja alikuwa akienda na kuwapasha habari waliyopaswa kuifahamu, ili kwamba wasihatarishe maisha yao kwa kuonwa wakiingia mjini. Ujumbe ulipofika ndipo huenda na kumtaarifu mfalme Daudi.
那時,約納堂和阿希瑪茲已在洛革泉傍等候,因怕被人看見,不敢進城;有個使女出來給他們傳信,他們就去報告達味君王。
18 Lakini kijana mmoja akawaoni mara akamwambia Absalomu. Hivyo Yonathani na Ahimaasi wakaenda kwa haraka na wakaingia katika nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu, aliyekuwa na kisima katika ua wake wakaingia humo.
但有一個少年人看見了他們,便向阿貝沙隆報告了;他們二人就急速逃匿,來到巴胡陵的一個人家裏,他院子裏有一口井,他們便下到井裏。
19 Mke wa mtu huyo akachukua kifuniko na kukikufunika kwenye mlango wa kisima kisha akaanika nafaka juu yake, hivyo hakuna aliyejua kwamba Yonathani na Ahimaasi walikuwa kisimani.
那家的婦女取了一個蓋子蓋在井口上,蓋子上又撒了些麥粒,免得有人注意。
20 Watu wa Absalomu wakaja kwa mwanamke na kumwuliza, “Ahimaasi na Yonathani wako wapi?” Mwanamke akawaambia, “Wamevuka mto.” Hivyo baada ya kuwatafuta bila kuwaona kurejea Yerusalemu.
阿貝沙隆的差役來到那家的婦女前問說:「阿希瑪茲和約納堂在哪裏﹖那婦女答說:「他們早過了蓄水池」。差役就去搜索他們,卻沒有找著,便回了耶路撒冷。
21 Ikawa baada yao kuondoka Yonathani na Ahimaasi wakatoka ndani ya kisima. Wakaenda kumtaarifu mfalme Daudi; wakamwambia, “Inuka na uvuke maji haraka kwa maana Ahithofeli ametoa mashauri haya na haya juu yako.”
差役走了以後,兩人就為井裏上來;去給達味君王報信,對達味說:「起身,趕快過河,因為阿希托費耳為害你們出了這樣的計謀」。
22 Kisha Daudi akainuka pamoja na watu wote walikuwa pamoja naye, nao wakauvuka Yordani. Hata ilipofika alfajiri hakuna hata mmoja aliyesalia kwa kutouvuka Yordani.
達味和隨從他的人就起身過了約旦河。到天亮時,沒有一個沒有過約旦河的。
23 Ikawa Ahithofeli alipoona kwamba ushauri wake haukufuatwa, akapanda punda wake na kuondoka. Akaenda nyumbani katika mji wake mwenyewe, akaweka mambo yake katika utaratibu na kisha akajinyonga. Kwa hiyo akafa na kuzikwa katika kaburi la baba yake.
阿希托費耳看見人不依從他的計謀,就備上驢,動身回家,回了本城,安排了自己的家務以後,就上吊死了。人將他埋在他父親的墳墓裏。
24 Ndipo Daudi akaja Mahanaimu. Lakini Absalomu yeye akavuka Yordani yeye pamoja na watu wote wa Israeli waliokuwa pamoja naye.
阿貝沙隆率領以色列人過約旦河時,達味已到了瑪哈納因。
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Naye huyo Amasa alikuwa mwana wa Yetheri Mwishmaeli, aliyekuwa amelala na Abigaili, aliyekuwa binti Nahashi na dada wa Seruya, mamaye Yoabu.
阿貝沙隆派阿瑪撒代約阿布為統帥。阿瑪撒是依市瑪耳人依特辣的兒子。依特辣曾走近過葉瑟的女兒,約阿布的母親,責魯雅的姐妹阿彼蓋耳。
26 Kisha Israeli na Absalomu wakapiga kambi katika nchi ya Gileadi.
以色列人同阿貝沙隆在基肋阿得一帶紮了營。
27 Ikawa wakati Daudi alipokuwa amekuja Mahanaimu, huyo Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni na Makiri mwana wa Amieli wa kutoka Lo Debari, na Berzilai Mgileadi wa Rogelimu,
當達味來到瑪哈納因時,納哈士的兒子芍彼,由阿孟人民的辣巴城,阿米爾的兒子瑪基爾由羅德巴爾城,基肋阿得人巴爾齊來由洛革林城,
28 wakaleta magodoro na mabulangeti, mabakuri na vyungu, na ngano, unga wa shayiri, nafaka zilizokaangwa, maharage, dengu,
帶來了床、鋪蓋、杯盤、炊具、小麥、麵粉、炒麥、豆子、扁豆、
29 asali, siagi, kondoo na samli, ili kwamba Daudi na watu waliokuwa pamoja naye waweze kula. Kwani walisema, “Watu wana njaa, wamechoka na wana kiu huko nyikani.”
蜂蜜、奶油、奶餅、牛肉和羊肉,供給達味和他的的人吃用,因為他們想:這些人經過了曠野,必定感到飢餓和疲勞。