< 2 Samweli 13 >

1 Ikawa baada ya hayo kwamba Amnoni mwana wa Daudi, akamtamani sana Tamari dada yake wa kambo aliyekuwa mzuri, alikuwa tumbo moja na Absalome, mwana wingine wa Daudi.
И бысть по сих, и у Авессалома сына Давидова бе сестра добра взором зело, имя же ей Фамарь, и возлюби ю Амнон сын Давидов:
2 Amnoni akasononeka sana kiasi cha kuugua kwa ajili ya Tamari dada yake. Tamari alikuwa bikra, na hivyo ilionekana haiwezekani Amnoni kufanya neno lolote kwake.
и скорбяше Амнон, яко и разболетися (ему) сестры своея ради Фамары, зане дева бяше сия, и не удобно бе пред очима Амнонима что сотворити ей.
3 Lakini Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yehonadabu mwana wa Shama, nduguye Daudi.
И бе Амнону друг, имя же ему Ионадав, сын Самаа брата Давидова, и Ионадав муж мудр зело.
4 Yehonadabu alikuwa mtu mwelevu sana. Akamwambia Amnoni, “Kwa nini, mwana wa mfalme, unadhoofika kila siku? Kwa nini uniambii? Ndipo Amnoni akamjibu, “Nampenda Tamari, dada yake Absalome ndugu yangu.”
И рече ему (Ионадав): что ти, яко ты тако болиши, сыне царев, утро утро? И не возвещаеши ми? И рече ему Амнон: Фамару сестру Авессалома брата моего аз люблю.
5 Ndipo Yehonadabu akamwambia, “Lala kitandani mwako na ujifanye kuwa mgonjwa. Wakati baba yako atakapo kuja kukuona, mwambie, Tafadhari mtume dada yangu Tamari aandaye chakula mbele yangu, ili kwamba nikione na kula kutoka mkononi mwake?”
И рече ему Ионадав: лязи на постели твоей и разболися, и внидет отец твой видети тя, и речеши к нему: да приидет ныне Фамарь сестра моя, и да ми даст ясти, и да сотворит пред очима моима снедь, да увижду и вкушу от рук ея.
6 Hivyo Amnoni akalala na kujifanya kuwa mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia mfalme, “Tafadhari mtume Tamari dada yangu aandaye chakula kwa ajili ya ugonjwa wangu mbele yangu ili kwamba nikile kutoka mkononi mwake.
И ляже Амнон и разболеся: и вниде царь видети его. И рече Амнон к царю: да приидет ныне Фамарь сестра моя ко мне и да испечет два пряжма пред очима моима, и имам ясти от руку ея.
7 Ndipo Daudi katika kasri lake akatuma neno kwa Tamari, kusema, “Nenda katika nyumba ya nduguyo Amnoni na umwandalie chakula. Hivyo
И посла Давид к Фамаре в дом, глаголя: иди ныне в дом Амнона брата твоего и сотвори ему снедь.
8 Tamari akaenda katika nyumba ya Amnoni nduguye alipokuwa amelala. Akachukua donge na kulifinyanga na kuandaa mkate mbele zake, kisha akauoka.
И иде Фамарь в дом Амнона брата своего, и той лежаше. И взя тесто, и смеси, и устрои пред очима его, и испече пряжма:
9 Akachukua kikaangio na kumpa mkate, lakini akakataa kula. Kisha Amnoni akawambia waliokuwepo, “Kila mtu na aondoke.” Hivyo kila mmoja akaondoka.
и взя сковраду и изложи пред него, и не восхоте ясти. И рече Амнон: изжените вся мужы от мене. И изгнаша вся мужы от него.
10 Amnoni akamwambia Tamari, “Lete chakula chumbani kwangu nikile katika mkono wako.” Tamari akachukua mkate aliokuwa ameuandaa, na kuuleta katika chumba cha Amnoni kaka yake.
И рече Амнон к Фамаре: внеси ми снедь во внутреннюю храмину, и ям от руку твоею. И взя Фамарь пряжма, яже испече, и внесе Амнону брату своему во внутреннюю храмину,
11 Alipoleta chakula kwake, Amnoni akamshikilia na kumwambia, “Njoo, ulale nami, dada yangu.”
и представи ему да яст. И ят ю, и рече ей: гряди, лязи со мною, сестро моя.
12 Yeye akamjibu, “Hapana, kaka yangu, usinilazimishe, kwani hakuna jambo kama hili linapaswa kufanyika katika Israeli. Usifanye jambo la aibu kiasi hiki!
И рече ему: ни, брате мой, не обругай мене, понеже не сотворится тако во Израили, не сотвори безумия сего:
13 Nitakwenda wapi ili nijiepushe na aibu ambayo jambo hili litaileta juu ya maisha yangu? Na tendo hili litakuonesha kuwa mpumbavu usiye na aibu katika Israeli yote. Tafadhari, ninakuomba uongee na mfalme. Yeye atakuruhusu unioe.”
и аз камо скрыю безчестие мое? И ты будеши яко един от безумных во Израили: и ныне глаголи к царю, да не отлучит мене от тебе.
14 Lakini Amnoni hakuweza kumsikiliza. Kwa kuwa alikuwa zaidi akamkamata na akalala naye.
И не восхоте Амнон послушати гласа ея, и преодоле ей, и смири ю, и преспа с нею.
15 Kisha Amnoni akamchukia Tamari kwa chuki kuu. Akamchukia zaidi ya jinsi alivyokuwa amemtamani. Amnoni akamwambia, “Inuka na uondoke.”
И возненавиде ю Амнон ненавистию великою зело, яко велиим ненавидением возненавиде ю паче любве, еюже любляше ю, и рече ей Амнон: востани и отиди.
16 Lakini yeye akamjibu, “Hapana! kwa maana uovu wa kunifanya ni uondoke ni mbaya zaidi ya kile ulichonitenda!” Lakini Amnoni hakumsikiliza.
И рече ему Фамарь: (ни, брате, ) яко злоба болши есть последняя паче первыя, юже сотворил еси со мною, еже отслати мене. И не восхоте Амнон слышати гласа ея.
17 Badala yake, akamwita mtumishi wake na akasema, “Mwondoe mwanamke huyu mbele yangu, na uufunge mlango nyuma yake.”
И призва отрока своего, приставника дому своего, и рече ему: отсли ныне сию от мене вон, и заключи двери вслед ея.
18 Hivyo mtumishi wake akamtoa na kufunga mlango. Tamari alikuwa amevaa vazi lilinakishiwa kwani ndivyo binti za wafalme waliobikra valivyokuwa wakivaa.
И бе риза на ней испещрена, понеже тако облачахуся дщери царевы, сущыя девицы, во одежды своя. И изведе ю вон слуга его и затвори двери вслед ея.
19 Tamari akaweka majivu juu ya kichwa chake na akalirarua vazi lake
И взя Фамарь пепел, и насыпа на главу свою, и одежду испещренную растерза на себе, и возложи руце свои на главу свою, и идущи идяше и вопияше.
20 Absalome, kaka yake, akamwambia, “Amnoni, kaka yako, amekuwa nawe? Lakini sasa nyamaza, dada yangu. Yeye ni kaka yako. Usiliweke hili moyoni.” Hivyo Tamari akakaa peke yake katika nyumba ya Absalomu kaka yake.
И рече к ней Авессалом брат ея: еда Амнон брат твой бысть с тобою? И ныне, сестро моя, умолчи, яко брат твой есть: не полагай на сердцы твоем еже глаголати слово сие. И седе Фамарь вдовствующи в дому Авессалома брата своего.
21 Mfalme Daudi aliposikia haya yote, alikasirika sana.
И слыша царь Давид вся словеса сия, и разгневася зело, и не опечали духа Амнона сына своего, понеже любляше его, яко первенец бе ему.
22 Absalome hakusema chochote kwa Amnoni, kwa maana Absalome alimchukia kwa kile alichokifanya, kumdhalilisha Tamari, dada yake.
И не глагола Авессалом со Амноном ни о добре, ни о зле, понеже возненавиде Авессалом Амнона того ради, понеже Фамару сестру его обругал.
23 Ikawa baada ya miaka miwili mizima Absalomu akawa na wakatao kondoo manyoya wakifanya kazi huko Baali Hazori, ulioko karibu na Efraim, naye Absalomu akawaarika wana wote wa mfalme kufika huko.
И бысть по двух летех дний, и беша стригуще (овцы) Авессаломовы (раби) в Веласоре близ Ефрема: и призва Авессалом вся сыны царевы.
24 Absalomu akamwendea mfalme na kusema, “Tazama sasa, mtumishi wako anao wakatao kondoo manyoya. Tafadhari, naomba mfalme na watumishi wake waende nami, mtumishi wako.”
И прииде Авессалом ко царю и рече: се, ныне стригут рабу твоему, да идет убо царь и отроцы его с рабом твоим.
25 Mfalme akamjibu Absalomu, “hapana mwanangu, tusiende sisi yote kwani tutakuwa mzigo kwako.” Absalomu akamhakikishia mfalme, lakini yeye asikubali kwenda, ila alimbariki Absalomu.
И рече царь ко Авессалому: ни, сыне мой, да не пойдем вси мы, и да не отяготим тя. И нуждаше его: и не восхоте (царь) ити, и благослови его.
26 Kisha Absalomu akasema, “kama sivyo, basi tafadhari mwache ndugu yangu Amnoni aende nasi.” Mfalme akamuliza, “Kwa nini Amnoni aende nanyi?”
И рече Авессалом к нему: аще же ни, поне да идет с нами Амнон брат мой. И рече ему царь: почто идет с тобою Амнон?
27 Absalomu akamsihi Daudi, hivyo akamruhusu Amnoni na wana wengine wa mfalme kwenda naye.
И принуди его Авессалом, и отпусти с ним Амнона и вся сыны царевы. И сотвори Авессалом пир, якоже творит пир царь.
28 Absalomu akawaamuru watumishi wake kusema, “Sikilizeni kwa makini. Amnoni atakapokuwa amelewa mvinyo, na nitakapowambia, 'Mpigeni Amnoni,' msiogope mwueni. Je siyo mimi niliyewamru? Mwe jasiri na hodari.”
И заповеда Авессалом отроком своим, глаголя: видите егда возблажает сердце Амноне от вина, и реку вам: поразите Амнона, и умертвите его: не убойтеся, яко не аз ли есмь повелеваяй вам? Мужайтеся и будите в сыны силы.
29 Hivyo watumishi wa Absalome wakamtendea Amnoni kama walivyoamriwa. Kisha wana wote wa mfalme wakainuka na kila mmoja akapanda nyumbu wake akakimbia.
И сотвориша отроцы Авессаломли Амнону, якоже заповеда им Авессалом. И восташа вси сынове царевы, и вседе кийждо на мска своего, и бежаша.
30 Hata ikawa wakati wakiwa njiani habari zikafika kwa Daudi kusema, “Absalomu ameua wana wote wa mfalme na hakuna hata mmoja aliyesalia.”
И бысть, сущым им на пути, и слух дойде до Давида, глаголя: изби Авессалом вся сыны царевы, и не избысть от них ни един.
31 Kisha mfalme akainuka na kurarua mavazi yake na kujilaza juu ya sakafu; watumishi wake wote wakasimama karibu naye mavazi yao yameraruriwa.
И воста царь, и растерза ризы своя, и ляже на земли, и вси отроцы его предстоящии ему растерзаша ризы своя.
32 Yehonadabu mwana wa Shama, nduguye Daudi, akajibu na kusema, “Bwana wangu asidhani kuwa vijana wote ambao ni wana wa mfalme wameuawa, kwa maana ni Amnoni pekee ndiye aliyeuawa. Absalomu alilipanga jambo hili tangu siku ile Amnoni alivyomwaribu Tamari, dada yake.
И рече Ионадав, сын Самаа брата Давидова, и рече: да не речет господин мой царь, яко вся отроки сыны царевы уби, но Амнон есть един убиен, яко той из уст Авессалому не исхождаше, отнележе обруга сестру его Фамару:
33 Kwa hiyo basi, bwana wangu mfalme asiiweke taarifa hii moyoni, kudhani kwamba wana wote wa mfalme wameuawa, kwani aliyeuawa ni Amnoni peke yake.”
и ныне да не полагает господин мой царь словесе на сердцы своем, глаголя: вси сынове царевы умроша: яко Амнон един умре.
34 Absalomu akakimbia. Mtumishi aliyekuwa akiangalia akainua macho yake na kuona watu wengi wakija njiani kando ya kilima upande wake wa magharibi.
И побеже Авессалом. И воздвиже отрок страж очеса своя и виде: и се, людие мнози идуще путем вслед его со страны гор в низхождение. И прииде страж и возвести царю и рече: мужы видех от пути Оронска со страны горы.
35 Kisha Yehonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wanakuja. kama mtumishi wako alivyosema.”
И рече Ионадав ко царю: се, сынове царевы приходят: по словеси раба твоего, тако бысть.
36 Ikawa mara alipomaliza kusema wana wa mfalme wakafika, wakainua sauti zao na kulia. Na mfalme pamoja na watumishi wake wote pia wakalia kwa uchungu.
И бысть егда сконча глаголя, и се, сынове царевы приидоша и воздвигоша глас свой и плакаша: и сам царь и вси отроцы его плакаша плачем великим зело.
37 Lakini Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Mfalme akaomboleza kila siku kwa ajili ya mwanaye.
И Авессалом убеже, и прииде ко Фолму сыну Емиуда, царю Гедсурску, в землю Хамаахадску. И плакаше Давид царь о сыне своем вся дни.
38 Hivyo Absalomu akakimbia na kwenda Geshuri na akakaa huko kwa miaka mitatu.
И Авессалом убеже, и иде в Гедсур, и бе тамо три лета.
39 Moyo wa mfalme Daudi ukatamani kwenda kumwona Absalomu, kwa maana alikuwa amefarijika kwa habari ya kifo cha Amnoni.
И остави царь Давид изыти вслед Авессалома, яко утешися о Амноне, яко умре.

< 2 Samweli 13 >