< 2 Samweli 12 >

1 Kisha Yahwe akamtuma Nathani kwa Daudi. Akaja kwake na kusema, “Kulikuwa na watu wawili katika mji. Mmoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa masikini.
Rəbbee Natan peyğambar Davudne k'anyaqa g'ıxele. Natan mang'une k'anyaqa arı, inəxüd eyhe: – Sa şaharee q'öyre insan vooxhe. Manbışda sa karnana manasar kar deşda eyxhe.
2 Yule tajiri alikuwa na kundi la ng'ombe na kondoo wengi sana,
Karnane insanıqa geed çavra-vəq'ə eyxhe.
3 lakini maskini hakuwa na chochote isipokuwa mwanakondoo, aliyekuwa amemnunua na kumlisha na kumlea. Akakua pamoja naye na pamoja na watoto wake. Yule mwanakondoo hata alikula naye na kunywa kutoka katika kikombe chake, naye akalala katika mikono yake na alikuwa kama binti kwake.
Kar deşdang'uqamee alivşu xəp qaa'ane vughulyne bederıle ğayrı, vuççud eyxhe deş. Mang'vee mana beder cune uşaxaaşika sacigee xəp qaa'a vuxha. Mançin mang'une xılençe kar oyxhan ıxha, mang'une k'oleençed xhyan ulyoğa ıxha. G'alyuvxhasıb mana mang'ul oo g'ulyoxha vuxha. Mana mang'unemee yişşene cigee vuxha.
4 Siku moja tajiri akapata mgeni, lakini yeye hakuwa tiyari kuchukua mnyama kutoka katika kundi lake la ng'ombe au kundi la kondoo ili kumwandalia chakula. Badala yake alichukua mwanakondoo wa masikini na akampika kwa ajili ya mgeni wake.
Sayəqees karnane insanısqa menne cigabışeençe mihman arayle. Karnane insanıs cong'əə arıyne mihmannemee otxhuniy ha'asva cune çavra-vəq'əyke həyvan avqu givk'as qiviykkanna. Mang'vee hark'ın kar deşing'una beder avqu abı, cong'əə arıyne mihmanıs otxhuniy ha'a.
5 Hasira ya Daudi ikawaka dhidi ya tajiri yule, naye akamwambia Nathani kwa hasira, “Kama Yahwe aishivyo, mtu aliyelitenda jambo hili anastahili kufa.
Davudna mane insanılqa qəl avqu, Natanık'le eyhen: – Vorne Rəbbilqan k'ın ixhen, man hı'iyne insanıs qik'uyud avaak'a.
6 Ni lazima alipe mwanakondoo mara nne zaidi kwa ajili ya kile alichokifanya, na kwa sababu hakuwa na huruma kwa mtu maskini.
Rəhı'm hidyav'u, məxbına iş g'avcuva, mang'vee mane bederıl-alla yoq'nəqees geed kar qeles.
7 Ndipo Nathani akamwambia Daudi, “Wewe ndiye yule mtu! Yahweh, Mungu wa Israeli, asema, 'Nilikutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli, na nilikuokoa kutoka katika mkono wa Sauli.
Natanee Davuduk'le eyhen: – Mana insan ğu vorna! İzrailyne Allahee Rəbbee inəxüdud eyhe: «Zı ğu İzrailyna paççah xhinne g'əyxı', Zı ğu Şaulne xılençe g'attixhan hı'ı.
8 Nikakupa nyumba ya bwana wako, na wake zake mikononi mwako. Nilikupa pia nyumba ya Israeli na Yuda. Na ikiwa hayo yalikuwa kidogo zaidi kwako, ningeweza kukuongezea mengine zaidi.
Zı vas yiğne xərıng'un xav huvu. Mang'un yadar Zı yiğne xhılibışeeqa quvu. Zı vas İzrailiniy Yahudayn milletbı huvu. Man vak'le k'ılda g'acuxhee, Zı vas mançile hexxanıd helesınniy.
9 Hivyo basi kwa nini umedharau maagizo ya Yahwe, hata ukafanya yaliyo maovu mbele zake? Umeua Uria Mhiti kwa upanga na umechukua mkewe kuwa mke wako. Uliua kwa upanga wa jeshi la Amoni.
Nya'a ğu Rəbbine ulesqa pisba qööna iş hav'u? Nya'a ğu Mang'un cuvab g'eliqqa huvu? Q'etbışda eyxhene Uriyne xhunaşşeyke vas xhunaşşe hee'esva, ğu mana g'ılıncıqqa huvu. Ğu mana Ammonbışde xıleka gik'u.
10 Hivyo basi upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa kuwa umenidharau na umemchukua mke wa Uria mhiti kuwa mke wako.'
G'iyniyke şaqa yiğne xaake mısacad g'ılınc əq'əna qixhes deş. Ğu Yizın cuvab g'eliqqa huvu, Q'etbışda eyxhene Uriyne xhunaşşeyke vas xhunaşşe hey'ı».
11 Yahwe asema, 'Tazama, nitaleta maafa dhidi yako kutoka katika nyumba yako mwenyewe. Nitachukua wake zako, mbele ya macho yako na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako wakati wa mchana.
Rəbbee inəxüdud eyhe: «Zı vakın divan yiğne xaabınbışisqacad qaqqas alikkas. Zı yiğne ulene ögil, yiğın yadar alyapt'ı, vas delesne insanısqa qevles. Manar yiğne-yiğın, ulek'le g'ece-g'ece yiğne yadaaşika g'alixhas.
12 Kwa maana wewe ulitenda dhambi hii sirini, lakini mimi nitatenda jambo hili wakati wa mchana mbele za Israeli wote.
Ğu man kar dyugulenda hı'ı, Zımee man kar yiğene yı'q'ı'hne gahıl gırgıne İzrailybışde ulene ögil ha'as alikkas».
13 Ndipo Daudi alipomwambia Nathani, “Nimemtenda dhambi Yahwe.” Nathani akamjibu Daudi, “Yahwe naye ameiachilia dhambi yako. Hautakufa.
Davudee Natanık'le eyhen: – Zı Rəbbine ögil bınah hav'u. Nataneeyid sak'ı, Davuduk'le eyhen: – Rəbbee yiğna bınah havaakal hav'una, ğu qik'as deş.
14 Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umemdharau Yahwe, mtoto aliyezaliwa kwako hakika atakufa.”
Ğu məxdın kar hı'iyle qiyğa, Rəbbine duşmanaaşisser Mana k'ap'ik'ıle avqa qa'as əxə. Mançil-allar vake ıxhana dix qik'asda, axvas deş.
15 Kisha Nathani akaondoka na kwenda kwake. Yahwe akampiga mtoto ambaye mke wa Uria alimzaa kwa Daudi, naye akaugua sana.
Mançile qiyğa Natan cune xaaqa siyk'al. Rəbbee, Davudna dix ık'iyk'ara'ana. Man uşax qik'uyne Uriyeyne xhunaşşeyken ıxha.
16 Kisha Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya kijana. Daudi akafunga naye akaingia ndani na kulala usiku wote juu ya sakafu.
Davudee uşaxnemee Allahıs düə haa'a. Mana sivacı xəmbı cune gozee q'ərane ç'iyel alğa'a.
17 Wazee wa nyumba yake wakainuka na kusimama kando yake, ili wamwinue kutoka sakafuni. Lakini hakuinuka, na hakula pamoja nao.
Sarayn ağsaqqalar mana ç'iyele oza qa'asva qabı k'ane ulyoozar. Mana ozar qexhe deş, karıd oyxhan deş.
18 Ikawa siku ya saba mtoto akafa. Watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia kwamba mtoto amekufa, kwa maana walisema, “Tazama, wakati mtoto alipokuwa hai tuliongea naye, lakini hakuisikiliza sauti yetu. Atakuwaje ikiwa tutamwambia kwamba kijana amekufa?!”
Yighıd'esde yiğıl uşax qek'an. Davudun nukarar uşax qik'uva mang'uk'le eyhes qəvəyq'ənanbı. Manbışisqa məxüd qayle: – Uşax üç'ürnang'a, şi mana ittunçil aqqeyir, mang'vee şal k'ırı alixhxhı deş. Həşde uşax qik'uva şi mang'uk'le nəxüdne eyhes? Sayid cuk sa kar ha'a.
19 Daudi alipoona kwamba watumishi wake walikuwa wakinong'onezana, Akatambua kwamba mtoto amekufa. Akawauliza, “Je mtoto amekufa?” Wakajibu, “Amekufa.”
Davuduk'le cune nukaraaşe ğud-ğud haa'a g'avxhumee, uşax qik'uva ats'axhxhen. Mang'vee manbışike «Uşax qik'uynneva?» qiyghan. Manbışe «Ho'ova» eyhe.
20 Kisha Daudi akainuka kutoka sakafuni naye akaoga, akajipaka mafuta, na kubadili mavazi yake. Akaenda katika hema la kukutania na akaabudu pale, kisha akarudu katika kasri lake. Akataka chakula kiletwe, wakamwandalia, naye akala.
Man g'ayxhı, Davud ç'iyele oza qıxha, əyxı'r-səyxı'r vuk'lelqa zeytunun q'ışid qadğu, tanalinbıd badal hı'ı, Rəbbine xaaqa hark'ın, Mang'us kyoyzarna. Qiyğa mana mançe cune xaaqa sak'ı, cus otxhuniy heleva eyhe. Cus oxhanas hucooyiy huvu, mang'vee oyxhanan.
21 Ndipo watumishi wake walipomwambia, “Kwa nini umefanya jambo hili? Ulifunga na kulia kwa ajili ya mtoto wakati alipokuwa hai, lakini mtoto alipokufa, ukainuka na kula.”
Nukaraaşe mang'uke qiyghanan: – Ğu in ha'an kar hucoone? Uşax üç'ürnang'a, ğu sivacı geşşu-gyaxvananiy, həşde uşax qik'umee, ğu oza qıxha kar otxhan girğıl?
22 Daudi akajibu, “Wakati mtoto alipokuwa hai nilifunga na kulia. Nilisema, Ni nani ajuaye kwamba Yahwe angeweza kunihurumia mtoto akaishi au sivyo?
Davudee manbışis inəxdın alidghıniy qele: – Uşax üç'ürnang'a, zı sivacı geşşu-gyaxvananiy. Zalygena ixhee, Rəbbis zı qiykkın, uşax gidek'avaniy eyhe.
23 Lakini sasa amekufa, hivyo nifungie nini? Je naweza kumrudisha tena? Nitakwenda kwake, lakini yeye hawezi kunirudia.”
Həşde uşax qik'uyn, zı nişisne siv aqqas? Nya'a mana zasse yı'q'əlqa sak'al ha'as əxəyee? Mana zasqa sak'alas deş, zı mang'usqa əlyhəəs.
24 Daudi akamfariji Bethsheba mkewe, akaingia kwake, na akalala naye. Baadaye akazaa mtoto wa kiume, naye akaitwa Selemani. Yahwe akampenda
Qiyğa Davudee xhunaşşeys Bat-Şevays yik'bı hele, ikkeç'u məng'ı'ka g'ılexha. Mana vuxhne ayxu dix uxooxa. Davudee mang'un do Sıleyman giyxhe. Rəbbis man uşax ıkkiykanan.
25 naye akatuma neno kupitia nabii Nathani kumwita Yedidia, kwa sababu Yahwe alimpenda.
Mang'vee maqa Natan peyğambar g'ıxele, mangv'eeyid uşaxın do Yedidiyah (Rəbbis ıkkanna) giyxhe.
26 Basi Yoabu akapigana na Raba, mji wa kifalme wa watu wa Amoni, naye akaiteka ngome yake.
Yoavee Ammonbı vooxhene Rabba eyhene şaharılqa cuna g'oşun k'yoohar hav'u, maana paççahna g'ala avqaaqqa.
27 Hivyo Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi na kusema, “Nimepigana na Raba, nami nimeshikilia sehemu inayosambaza maji ya mji.
Qiyğa Yoavee Davudne k'anyaqa ina xabar ana insanar g'uxoole: – Şi Rabba eyhene şaharılqa k'yophur, manbışe xhyan havacen cigabı aqqı.
28 Kwa hiyo sasa likusanye jeshi lililosalia uhuzingire mji na kuuteka, kwa maana ikiwa nitauteka, utaitwa kwa jina langu.”
Həşdiyle ğu avxuna g'oşun sav'u, arı mane şaharın hiqiy-alladın cigabı aqqe. Qiyğab vuc şahar alept'e. Deşxheene, zı mana şahar avqee, mançis yizın do heles.
29 Hivyo Daudi akalikusanya jeshi lote na kwenda Raba; akapigana nao na kuuteka.
Davudeeyib avxuna g'oşun sav'u, Rabbeeqa arı, dəv'əyka mana avqaaqqana.
30 Daudi akachukua taji ya dhahabu kutoka katika kichwa cha mfalme wao iliyokuwa na uzito wa talanta, na ilikuwa na jiwe la thamani ndani yake. Taji ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Kisha akachukua nyara za mji kwa wingi.
Mang'vee manbışde paççahne vuk'lele tac alyaat'u, cune vuk'lelqa giyxhe. Man tac k'ınəəğəyke hı'ı ıxha, çina yı'q'vaalab sa talant vuxha. Mançine hiqiy-allançed gıranın g'ayebıyiy gitk'ın. Davudee mane şahareençe geed gıranın kar qığa'a.
31 Akawatoa watu waliokuwa mjini naye akawalazimisha kufanya kazi kwa misumeno, sululu na shoka; lakini pia akawalazimisha kutengeneza matofali. Daudi akailazimisha miji yote ya watu wa Amoni kufanya kazi hiyo. Kisha Daudi na jeshi lote wakarudi Yerusalemu
Mane şahareedın millet mang'vee qığatxhu, ayxaaka, yivayne kılıngıkayiy yak'uka işbı gaces ilekka. Qiyğale xhinne manbışisqa karpıç ha'as ilekka ıxha. Davudee Ammonbışde gırgıne şaharbışik man hı'iyle qiyğa, qığeç'u cune g'oşunuka İyerusalimqa ayk'an.

< 2 Samweli 12 >