< 2 Samweli 12 >

1 Kisha Yahwe akamtuma Nathani kwa Daudi. Akaja kwake na kusema, “Kulikuwa na watu wawili katika mji. Mmoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa masikini.
And YHWH sends Nathan to David, and he comes to him, and says to him: “Two men have been in one city, one rich and one poor.
2 Yule tajiri alikuwa na kundi la ng'ombe na kondoo wengi sana,
The rich has very many flocks and herds,
3 lakini maskini hakuwa na chochote isipokuwa mwanakondoo, aliyekuwa amemnunua na kumlisha na kumlea. Akakua pamoja naye na pamoja na watoto wake. Yule mwanakondoo hata alikula naye na kunywa kutoka katika kikombe chake, naye akalala katika mikono yake na alikuwa kama binti kwake.
but the poor one has nothing, except one little ewe-lamb which he has bought and keeps alive. And it grows up together with him and with his sons. It eats of his morsel, and it drinks from his cup, and it lies in his bosom, and it is as a daughter to him.
4 Siku moja tajiri akapata mgeni, lakini yeye hakuwa tiyari kuchukua mnyama kutoka katika kundi lake la ng'ombe au kundi la kondoo ili kumwandalia chakula. Badala yake alichukua mwanakondoo wa masikini na akampika kwa ajili ya mgeni wake.
And a traveler comes to the rich man, and he spares to take from his own flock, and from his own herd, to prepare for the traveling [man] who has come to him; and he takes the ewe-lamb of the poor man and prepares it for the man who has come to him.”
5 Hasira ya Daudi ikawaka dhidi ya tajiri yule, naye akamwambia Nathani kwa hasira, “Kama Yahwe aishivyo, mtu aliyelitenda jambo hili anastahili kufa.
And the anger of David burns against the man exceedingly, and he says to Nathan, “YHWH lives, surely the man who is doing this [is] a son of death,
6 Ni lazima alipe mwanakondoo mara nne zaidi kwa ajili ya kile alichokifanya, na kwa sababu hakuwa na huruma kwa mtu maskini.
and [for] the ewe-lamb he repays fourfold, because that he has done this thing, and because that he had no pity.”
7 Ndipo Nathani akamwambia Daudi, “Wewe ndiye yule mtu! Yahweh, Mungu wa Israeli, asema, 'Nilikutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli, na nilikuokoa kutoka katika mkono wa Sauli.
And Nathan says to David, “You [are] the man! Thus said YHWH, God of Israel: I anointed you for king over Israel, and I delivered you out of the hand of Saul;
8 Nikakupa nyumba ya bwana wako, na wake zake mikononi mwako. Nilikupa pia nyumba ya Israeli na Yuda. Na ikiwa hayo yalikuwa kidogo zaidi kwako, ningeweza kukuongezea mengine zaidi.
and I give to you the house of your lord, and the wives of your lord, into your bosom, and I give the house of Israel and Judah to you; and if [that is] too little, then I add such and such [things] to you.
9 Hivyo basi kwa nini umedharau maagizo ya Yahwe, hata ukafanya yaliyo maovu mbele zake? Umeua Uria Mhiti kwa upanga na umechukua mkewe kuwa mke wako. Uliua kwa upanga wa jeshi la Amoni.
Why have you despised the word of YHWH, to do evil in His eyes? You have struck Uriah the Hittite by the sword, and you have taken his wife for a wife for yourself, and you have slain him by the sword of the sons of Ammon.
10 Hivyo basi upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa kuwa umenidharau na umemchukua mke wa Uria mhiti kuwa mke wako.'
And now, the sword does not turn aside from your house for all time, because you have despised Me, and take the wife of Uriah the Hittite to be for a wife for yourself;
11 Yahwe asema, 'Tazama, nitaleta maafa dhidi yako kutoka katika nyumba yako mwenyewe. Nitachukua wake zako, mbele ya macho yako na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako wakati wa mchana.
thus said YHWH: Behold, I am raising up calamity against you, out of your [own] house, and have taken your wives before your eyes, and given [them] to your neighbor, and he has lain with your wives before the eyes of this sun;
12 Kwa maana wewe ulitenda dhambi hii sirini, lakini mimi nitatenda jambo hili wakati wa mchana mbele za Israeli wote.
for you have done [it] in secret, and I do this thing before all Israel, and before the sun.”
13 Ndipo Daudi alipomwambia Nathani, “Nimemtenda dhambi Yahwe.” Nathani akamjibu Daudi, “Yahwe naye ameiachilia dhambi yako. Hautakufa.
And David says to Nathan, “I have sinned against YHWH.” And Nathan says to David, “Also—YHWH has caused your sin to pass away; you do not die;
14 Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umemdharau Yahwe, mtoto aliyezaliwa kwako hakika atakufa.”
only, because you have caused the enemies of YHWH to greatly despise by this thing, also—the son who is born to you surely dies.”
15 Kisha Nathani akaondoka na kwenda kwake. Yahwe akampiga mtoto ambaye mke wa Uria alimzaa kwa Daudi, naye akaugua sana.
And Nathan goes to his house, and YHWH strikes the boy, whom the wife of Uriah has borne to David, and it is incurable;
16 Kisha Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya kijana. Daudi akafunga naye akaingia ndani na kulala usiku wote juu ya sakafu.
and David seeks God for the youth, and David keeps a fast, and has gone in and lodged, and lain on the earth.
17 Wazee wa nyumba yake wakainuka na kusimama kando yake, ili wamwinue kutoka sakafuni. Lakini hakuinuka, na hakula pamoja nao.
And [the] elderly of his house rise against him, to raise him up from the earth, and he has not been willing, nor has he eaten bread with them;
18 Ikawa siku ya saba mtoto akafa. Watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia kwamba mtoto amekufa, kwa maana walisema, “Tazama, wakati mtoto alipokuwa hai tuliongea naye, lakini hakuisikiliza sauti yetu. Atakuwaje ikiwa tutamwambia kwamba kijana amekufa?!”
and it comes to pass on the seventh day, that the boy dies, and the servants of David fear to declare to him that the boy is dead, for they said, “Behold, in the boy being alive we spoke to him, and he did not listen to our voice; and how do we say to him, The boy is dead? Then he has done evil.”
19 Daudi alipoona kwamba watumishi wake walikuwa wakinong'onezana, Akatambua kwamba mtoto amekufa. Akawauliza, “Je mtoto amekufa?” Wakajibu, “Amekufa.”
And David sees that his servants are whispering, and David understands that the boy is dead, and David says to his servants, “Is the boy dead?” And they say, “Dead.”
20 Kisha Daudi akainuka kutoka sakafuni naye akaoga, akajipaka mafuta, na kubadili mavazi yake. Akaenda katika hema la kukutania na akaabudu pale, kisha akarudu katika kasri lake. Akataka chakula kiletwe, wakamwandalia, naye akala.
And David rises from the earth, and bathes and anoints [himself], and changes his raiment, and comes into the house of YHWH, and bows himself, and comes to his house, and asks and they place bread for him, and he eats.
21 Ndipo watumishi wake walipomwambia, “Kwa nini umefanya jambo hili? Ulifunga na kulia kwa ajili ya mtoto wakati alipokuwa hai, lakini mtoto alipokufa, ukainuka na kula.”
And his servants say to him, “What [is] this thing you have done? Because of the living boy you have fasted and you weep, and when the boy is dead you have risen and eat bread.”
22 Daudi akajibu, “Wakati mtoto alipokuwa hai nilifunga na kulia. Nilisema, Ni nani ajuaye kwamba Yahwe angeweza kunihurumia mtoto akaishi au sivyo?
And he says, “While the boy is alive I have fasted and I weep, for I said, Who knows [if] YHWH pities me and the boy has lived?
23 Lakini sasa amekufa, hivyo nifungie nini? Je naweza kumrudisha tena? Nitakwenda kwake, lakini yeye hawezi kunirudia.”
And now, he has died, why [is] this—I fast? Am I able to bring him back again? I am going to him, and he does not return to me.”
24 Daudi akamfariji Bethsheba mkewe, akaingia kwake, na akalala naye. Baadaye akazaa mtoto wa kiume, naye akaitwa Selemani. Yahwe akampenda
And David comforts his wife Bathsheba, and goes in to her, and lies with her, and she bears a son, and he calls his name Solomon; and YHWH has loved him,
25 naye akatuma neno kupitia nabii Nathani kumwita Yedidia, kwa sababu Yahwe alimpenda.
and sends by the hand of Nathan the prophet, and calls his name Jedidiah, because of YHWH.
26 Basi Yoabu akapigana na Raba, mji wa kifalme wa watu wa Amoni, naye akaiteka ngome yake.
And Joab fights against Rabbah of the sons of Ammon, and captures the royal city,
27 Hivyo Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi na kusema, “Nimepigana na Raba, nami nimeshikilia sehemu inayosambaza maji ya mji.
and Joab sends messengers to David and says, “I have fought against Rabbah—I have also captured the city of waters;
28 Kwa hiyo sasa likusanye jeshi lililosalia uhuzingire mji na kuuteka, kwa maana ikiwa nitauteka, utaitwa kwa jina langu.”
and now, gather the rest of the people, and encamp against the city, and capture it, lest I capture the city, and my name has been called on it.”
29 Hivyo Daudi akalikusanya jeshi lote na kwenda Raba; akapigana nao na kuuteka.
And David gathers all the people, and goes to Rabbah, and fights against it, and captures it;
30 Daudi akachukua taji ya dhahabu kutoka katika kichwa cha mfalme wao iliyokuwa na uzito wa talanta, na ilikuwa na jiwe la thamani ndani yake. Taji ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Kisha akachukua nyara za mji kwa wingi.
and he takes the crown of their king from off his head, and its weight [is] a talent of gold, and precious stones, and it is on the head of David; and he has brought out the spoil of the city—very much;
31 Akawatoa watu waliokuwa mjini naye akawalazimisha kufanya kazi kwa misumeno, sululu na shoka; lakini pia akawalazimisha kutengeneza matofali. Daudi akailazimisha miji yote ya watu wa Amoni kufanya kazi hiyo. Kisha Daudi na jeshi lote wakarudi Yerusalemu
and he has brought out the people who [are] in it, and sets [them] to the saw, and to cutting instruments of iron, and to axes of iron, and has caused them to pass over into the brick-kiln; and so he does to all the cities of the sons of Ammon; and David turns back, and all the people, to Jerusalem.

< 2 Samweli 12 >