< 2 Samweli 11 >
1 Ikawa wakati wa majira ya kipupwe, wakati ambapo kwa kawaida wafalme huenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu, mtumishi wake, na jeshi lote la Israeli. Wakaliaribu jeshi la Amoni na kuuhusuru Raba. Lakini Daudi akakaa Yerusalemu.
and to be to/for turn [the] year to/for time to come out: come ([the] messenger *LBH(a+C)*) and to send: depart David [obj] Joab and [obj] servant/slave his with him and [obj] all Israel and to ruin [obj] son: descendant/people Ammon and to confine upon Rabbah and David to dwell in/on/with Jerusalem
2 Hivyo ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi akaamka kutoka kitandani na akatembea katika dari la kasri. Akiwa pale akamwona mwanamke aliyekuwa akioga, mwanamke yule alikuwa mzuri sana kwa mwonekano.
and to be to/for time [the] evening and to arise: rise David from upon bed his and to go: walk upon roof house: home [the] king and to see: see woman to wash: wash from upon [the] roof and [the] woman pleasant appearance much
3 Hivyo Daudi akatuma na kuuliza watu waliomfahamu yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, “Je huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, naye si mke wa Uria mhiti?
and to send: depart David and to seek to/for woman and to say not this Bathsheba Bathsheba daughter Eliam woman: wife Uriah [the] Hittite
4 Daudi akatuma wajumbe nao wakamchukua; akaja kwake, na akalala naye(kwani ndo alikuwa amejitakasa kutoka siku zake). Kisha akarudi nyumbani kwake.
and to send: depart David messenger and to take: take her and to come (in): come to(wards) him and to lie down: lay down with her and he/she/it to consecrate: consecate from uncleanness her and to return: return to(wards) house: home her
5 Mwanamke akawa mjamzito, naye akatuma na kumwambia Daudi; akasema, “mimi ni mjamzito.”
and to conceive [the] woman and to send: depart and to tell to/for David and to say pregnant I
6 Kisha Daudi akatuma watu kwa Yoabu kusema, “Umtume kwangu Uria mhiti.” Hivyo Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
and to send: depart David to(wards) Joab to send: depart to(wards) me [obj] Uriah [the] Hittite and to send: depart Joab [obj] Uriah to(wards) David
7 Uria alipofika, Daudi akamuuliza hali ya Yoabu. Jinsi jeshi lilivyokuwa likiendelea, na jinsi vita vilivyokuwa vinaendelea.
and to come (in): come Uriah to(wards) him and to ask David to/for peace: greeting Joab and to/for peace: greeting [the] people and to/for peace: greeting [the] battle
8 Daudi akamwambia Uria, “Shuka nyumbani kwako, unawe miguu yako. “Hivyo Uria akaondoka katika kasri la mfalme, mfalme akamtumia zawadi kwa Uria.
and to say David to/for Uriah to go down to/for house: home your and to wash: wash foot your and to come out: come Uriah from house: home [the] king and to come out: come after him tribute [the] king
9 Lakini Uria akalala pamoja na watumishi wa bwana wake katika lango la kasri, wala hakushuka nyumbani kwake.
and to lie down: sleep Uriah entrance house: home [the] king with all servant/slave lord his and not to go down to(wards) house: home his
10 Daudi alipoambiwa, “Uria hakushuka nyumbani kwake,” akamwambia Uria, Je haukutoka safarini? Kwa nini haukushuka nyumbani kwako?”
and to tell to/for David to/for to say not to go down Uriah to(wards) house: home his and to say David to(wards) Uriah not from way: journey you(m. s.) to come (in): come why? not to go down to(wards) house: home your
11 Uria akamjibu Daudi, “Sanduku, na Israeli na Yuda wamo kwenye mahema, na Yoabu na watumishi wa bwana wangu wamepiga hema uwandani. Jinsi gani basi mimi naweza kwenda nyumbani kwangu kula kunywa na kulala na mke wangu? kwa hakika kama uishivyo, sitafanya hivyo.
and to say Uriah to(wards) David [the] ark and Israel and Judah to dwell in/on/with booth and lord my Joab and servant/slave lord my upon face: surface [the] land: country to camp and I to come (in): come to(wards) house: home my to/for to eat and to/for to drink and to/for to lie down: lay down with woman: wife my alive your and alive soul your if: surely no to make: do [obj] [the] word: thing [the] this
12 Hivyo Daudi akamwambia Uria, “Ukae leo pia, kesho nitakuacha uende.” Kwa hiyo uria akakaa Yerusalemu siku hiyo na iliyofuata.
and to say David to(wards) Uriah to dwell in/on/with this also [the] day and tomorrow to send: depart you and to dwell Uriah in/on/with Jerusalem in/on/with day [the] he/she/it and from morrow
13 Daudi alipomwita, alikula na kunywa pamoja naye, Daudi akamfanya alewe. Wakati wa jioni Uria akaenda kulala kitandani pake pamoja na watumish wa bwana wake; hakushuka nyumbani kwake.
and to call: call to to/for him David and to eat to/for face: before his and to drink and be drunk him and to come out: come in/on/with evening to/for to lie down: lay down in/on/with bed his with servant/slave lord his and to(wards) house: home his not to go down
14 Hivyo asubuhi Daudi akamwandikia Yoabu barua, naye akaituma kwa mkono wa Uria.
and to be in/on/with morning and to write David scroll: document to(wards) Joab and to send: depart in/on/with hand: power Uriah
15 Ndani ya barua Daudi aliandika hivi, “Mweke Uria mbele ya vita vikali sana, na kisha, mmwache, ili apigwe na afe.
and to write in/on/with scroll: document to/for to say to give [obj] Uriah to(wards) opposite face: before [the] battle [the] strong and to return: return from after him and to smite and to die
16 Hivyo Yoabu alipoona mji ukizingirwa, alimweka Uria katika sehemu aliyojua askari adui wenye nguvu wangekuwa wakipigana.
and to be in/on/with to keep: look at Joab to(wards) [the] city and to give: put [obj] Uriah to(wards) [the] place which to know for human strength there
17 Wakati watu wa mji walipotoka na kupigana dhidi ya jeshi la Yoabu, baadhi ya askari wa Daudi wakaanguka, na Uria Mhiti pia akauwawa.
and to come out: come human [the] city and to fight with Joab and to fall: kill from [the] people from servant/slave David and to die also Uriah [the] Hittite
18 Wakati Yoabu alipotuma neno kwa mfalme kuhusu hali ya vita,
and to send: depart Joab and to tell to/for David [obj] all word: deed [the] battle
19 alimwagiza mjumbe, kusema, “Utakapomaliza kumwambia mfalme kuhusu hali ya vita,
and to command [obj] [the] messenger to/for to say like/as to end: finish you [obj] all word: deed [the] battle to/for to speak: speak to(wards) [the] king
20 yawezekana mfalme akakasirika, naye akakwambia, 'Kwa nini mlipigana na mji kwa karibu hivyo, hamkujua kwamba wangeweza kushambulia kutokea ukutani?
and to be if to ascend: rise rage [the] king and to say to/for you why? to approach: approach to(wards) [the] city to/for to fight not to know [obj] which to shoot from upon [the] wall
21 Ni nani aliyemwua Abimeleki mwana wa Yerubeshethi? Siye mwanamke aliyerusha jiwe la kusagia juu yake kutoka ukutani, hata akafa huko Thebesi? Kwanini basi mliukaribia ukuta jinsi hiyo? Nawe umjibu, 'Uria mtumishi wako amekufa pia.”
who? to smite [obj] Abimelech son: child Jerubbesheth not woman to throw upon him millstone chariot: millstone from upon [the] wall and to die in/on/with Thebez to/for what? to approach: approach to(wards) [the] wall and to say also servant/slave your Uriah [the] Hittite to die
22 Hivyo mjumbe akaondoka na kwenda kwa Daudi akamwambia kila jambo ambalo Yoabu alimtuma kusema.
and to go: went [the] messenger and to come (in): come and to tell to/for David [obj] all which to send: depart him Joab
23 Na mjumbe akamwambia Daudi, “Mwanzoni adui walikuwa na nguvu kuliko sisi; walitukabili uwandani, lakini tukawarudisha nyuma kwenye maingilio ya lango.
and to say [the] messenger to(wards) David for to prevail upon us [the] human and to come out: come to(wards) us [the] land: country and to be upon them till entrance [the] gate
24 Na wapiga mishale wao wakawarushia watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watumishi wa mfalme wameuawa, na mtumishi wako Uria mhiti pia ameuawa.”
(and to shoot *Q(K)*) ([the] to shoot *Q(k)*) to(wards) servant/slave your from upon [the] wall and to die from servant/slave [the] king and also servant/slave your Uriah [the] Hittite to die
25 Kisha Daudi akamwambia mjumbe, “Mwambie hivi Yoabu, 'Usiruhusu jamba hili likuhuzunishe, kwa maana upanga huangamiza huyu kama uangamizavyo na mwingine. Vifanye vita vyako kuwa vyenye nguvu zaidi dhidi ya mji, na uuteke.' Mtie moyo Yoabu.”
and to say David to(wards) [the] messenger thus to say to(wards) Joab not be evil in/on/with eye: appearance your [obj] [the] word: thing [the] this for like/as this and like/as this to eat [the] sword to strengthen: strengthen battle your to(wards) [the] city and to overthrow her and to strengthen: strengthen him
26 Hivyo mke Uria aliposikia kwamba mme wake amekufa, akaomboleza sana kwa ajili yake.
and to hear: hear woman: wife Uriah for to die Uriah man: husband her and to mourn upon master: husband her
27 Huzuni yake ilipoisha, Daudi akatuma na kumchukua kwake katika kasri lake, naye akawa mkewe na akamzalia mwana. Lakini alichokifanya Daudi hakikumpendeza Yahwe.
and to pass [the] mourning and to send: depart David and to gather her to(wards) house: home his and to be to/for him to/for woman: wife and to beget to/for him son: child and be evil [the] word: thing which to make: do David in/on/with eye: appearance LORD