< 2 Samweli 11 >

1 Ikawa wakati wa majira ya kipupwe, wakati ambapo kwa kawaida wafalme huenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu, mtumishi wake, na jeshi lote la Israeli. Wakaliaribu jeshi la Amoni na kuuhusuru Raba. Lakini Daudi akakaa Yerusalemu.
U početku slijedeće godine, u doba kad kraljevi izlaze u rat, posla David Joaba i s njim svoje ljude i svega Izraela: oni pobiše Amonce i podsjedoše Rabu. A David osta u Jeruzalemu.
2 Hivyo ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi akaamka kutoka kitandani na akatembea katika dari la kasri. Akiwa pale akamwona mwanamke aliyekuwa akioga, mwanamke yule alikuwa mzuri sana kwa mwonekano.
A jednoga dana predveče usta David sa svoje postelje i prošeta se po krovu svoje palače. Opazi s krova ženu gdje se kupa. Ta žena bijaše izvanredno lijepa.
3 Hivyo Daudi akatuma na kuuliza watu waliomfahamu yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, “Je huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, naye si mke wa Uria mhiti?
David se propita za tu ženu i rekoše mu: “Pa to je Bat-Šeba, kći Eliamova i žena Urije Hetita!”
4 Daudi akatuma wajumbe nao wakamchukua; akaja kwake, na akalala naye(kwani ndo alikuwa amejitakasa kutoka siku zake). Kisha akarudi nyumbani kwake.
Nato David posla glasnika da je dovedu k njemu. Kad je došla, leže on s njom, upravo kad se bila očistila od svoje nečistoće. Zatim se ona vrati svojoj kući.
5 Mwanamke akawa mjamzito, naye akatuma na kumwambia Daudi; akasema, “mimi ni mjamzito.”
Žena zatrudnje te poruči Davidu: “Trudna sam!”
6 Kisha Daudi akatuma watu kwa Yoabu kusema, “Umtume kwangu Uria mhiti.” Hivyo Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
Tada David posla poruku Joabu: “Pošalji k meni Uriju Hetita!” I Joab posla Uriju k Davidu.
7 Uria alipofika, Daudi akamuuliza hali ya Yoabu. Jinsi jeshi lilivyokuwa likiendelea, na jinsi vita vilivyokuwa vinaendelea.
Kad je Urija došao k njemu, zapita ga David kako je Joab, kako je vojska i kako napreduje rat.
8 Daudi akamwambia Uria, “Shuka nyumbani kwako, unawe miguu yako. “Hivyo Uria akaondoka katika kasri la mfalme, mfalme akamtumia zawadi kwa Uria.
Potom David reče Uriji: “Siđi u svoju kuću i operi svoje noge!” Urija iziđe iz kraljeva dvora, a za njim ponesoše dar s kraljeva stola.
9 Lakini Uria akalala pamoja na watumishi wa bwana wake katika lango la kasri, wala hakushuka nyumbani kwake.
Ali Urija osta da spava pred vratima kraljeva dvora sa stražarima svoga gospodara i ne ode svojoj kući.
10 Daudi alipoambiwa, “Uria hakushuka nyumbani kwake,” akamwambia Uria, Je haukutoka safarini? Kwa nini haukushuka nyumbani kwako?”
Javiše to Davidu govoreći: “Urija nije otišao svojoj kući!” Tada David upita Uriju: “Zar nisi došao s puta? Zašto ne ideš svojoj kući?”
11 Uria akamjibu Daudi, “Sanduku, na Israeli na Yuda wamo kwenye mahema, na Yoabu na watumishi wa bwana wangu wamepiga hema uwandani. Jinsi gani basi mimi naweza kwenda nyumbani kwangu kula kunywa na kulala na mke wangu? kwa hakika kama uishivyo, sitafanya hivyo.
A Urija odgovori Davidu: “Kovčeg, Izrael i Juda borave pod šatorima, moj gospodar Joab i straža moga gospodara borave na otvorenu polju, a ja da uđem u svoju kuću da jedem i da pijem i da spavam sa svojom ženom? Živoga mi Jahve, i tako mi tvoga života, zaista neću učiniti nešto takvo!”
12 Hivyo Daudi akamwambia Uria, “Ukae leo pia, kesho nitakuacha uende.” Kwa hiyo uria akakaa Yerusalemu siku hiyo na iliyofuata.
Tada David reče Uriji: “Ostani još danas ovdje, a sutra ću te otpustiti.” Tako Urija osta u Jeruzalemu onaj dan.
13 Daudi alipomwita, alikula na kunywa pamoja naye, Daudi akamfanya alewe. Wakati wa jioni Uria akaenda kulala kitandani pake pamoja na watumish wa bwana wake; hakushuka nyumbani kwake.
Sutradan David pozva Uriju da jede i da pije pred njim i on ga opi. A uvečer Urija iziđe i leže na svoju postelju sa stražama svoga gospodara, ali svojoj kući nije otišao.
14 Hivyo asubuhi Daudi akamwandikia Yoabu barua, naye akaituma kwa mkono wa Uria.
Ujutro David napisa pismo Joabu i posla ga po Uriji.
15 Ndani ya barua Daudi aliandika hivi, “Mweke Uria mbele ya vita vikali sana, na kisha, mmwache, ili apigwe na afe.
A u tom pismu pisao je ovako: “Postavite Uriju naprijed, gdje je najžešći boj, pa uzmaknite iza njega: neka bude pogođen i neka pogine!”
16 Hivyo Yoabu alipoona mji ukizingirwa, alimweka Uria katika sehemu aliyojua askari adui wenye nguvu wangekuwa wakipigana.
Zato Joab, opsjedajući grad, postavi Uriju na mjesto gdje je znao da stoje najhrabriji ratnici.
17 Wakati watu wa mji walipotoka na kupigana dhidi ya jeshi la Yoabu, baadhi ya askari wa Daudi wakaanguka, na Uria Mhiti pia akauwawa.
Kad su onda građani provalili van i pobili se s Joabom, pade nekoliko od njegove vojske, od Davidovih ljudi, a pogibe i Urija Hetit.
18 Wakati Yoabu alipotuma neno kwa mfalme kuhusu hali ya vita,
Potom Joab posla čovjeka i javi Davidu sve što se dogodilo u boju.
19 alimwagiza mjumbe, kusema, “Utakapomaliza kumwambia mfalme kuhusu hali ya vita,
I zapovjedi glasniku ovako: “Kad pripovjediš kralju sve što se dogodilo u boju,
20 yawezekana mfalme akakasirika, naye akakwambia, 'Kwa nini mlipigana na mji kwa karibu hivyo, hamkujua kwamba wangeweza kushambulia kutokea ukutani?
možda će se kralj razljutiti pa ti kazati: 'Zašto ste se primakli tako blizu gradu da navalite? Zar niste znali da se obično izmeću strijele sa zida?
21 Ni nani aliyemwua Abimeleki mwana wa Yerubeshethi? Siye mwanamke aliyerusha jiwe la kusagia juu yake kutoka ukutani, hata akafa huko Thebesi? Kwanini basi mliukaribia ukuta jinsi hiyo? Nawe umjibu, 'Uria mtumishi wako amekufa pia.”
Tko je ubio Abimeleka, sina Jerubaalova? Nije li jedna žena bacila na njega mlinski kamen, ozgo sa zida, te je poginuo u Tebesu? Zašto ste se primakli tako blizu zidu?' Ako ti tako kaže, a ti mu reci: 'Poginuo je i tvoj sluga Urija Hetit.'”
22 Hivyo mjumbe akaondoka na kwenda kwa Daudi akamwambia kila jambo ambalo Yoabu alimtuma kusema.
Glasnik krenu na put, dođe k Davidu i pripovjedi mu sve što mu je naložio Joab. A David planu gnjevom na Joaba i reče glasniku: “Zašto ste se primakli tako blizu zidu? Tko je ubio Abimeleka, sina Jerubaalova? Nije li jedna žena bacila na njega mlinski kamen, ozgo sa zida, te je poginuo u Tebesu? Zašto ste se primakli tako blizu zidu?”
23 Na mjumbe akamwambia Daudi, “Mwanzoni adui walikuwa na nguvu kuliko sisi; walitukabili uwandani, lakini tukawarudisha nyuma kwenye maingilio ya lango.
Glasnik odgovori Davidu: “Ti su ljudi silovito udarali na nas i izašli su protiv nas na otvoreno polje. Mi smo ih potisnuli natrag do gradskih vrata,
24 Na wapiga mishale wao wakawarushia watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watumishi wa mfalme wameuawa, na mtumishi wako Uria mhiti pia ameuawa.”
ali su strijelci sa zida stali izmetati strijele na tvoje ljude te ih je poginulo nekoliko između kraljevih slugu; tako je poginuo i tvoj sluga Urija Hetit.”
25 Kisha Daudi akamwambia mjumbe, “Mwambie hivi Yoabu, 'Usiruhusu jamba hili likuhuzunishe, kwa maana upanga huangamiza huyu kama uangamizavyo na mwingine. Vifanye vita vyako kuwa vyenye nguvu zaidi dhidi ya mji, na uuteke.' Mtie moyo Yoabu.”
Tada David reče glasniku: “Ovako reci Joabu: 'Nemoj to uzimati toliko k srcu, jer mač proždire sad ovoga, sad onoga. Udaraj još jače na grad i obori ga!' Tako ćeš mu vratiti srčanost!”
26 Hivyo mke Uria aliposikia kwamba mme wake amekufa, akaomboleza sana kwa ajili yake.
Kad je Urijina žena čula da je poginuo njezin muž Urija, žalila je za svojim mužem.
27 Huzuni yake ilipoisha, Daudi akatuma na kumchukua kwake katika kasri lake, naye akawa mkewe na akamzalia mwana. Lakini alichokifanya Daudi hakikumpendeza Yahwe.
A kad je prošlo vrijeme žalosti, posla David po nju i uze je u svoj dvor, i ona mu posta ženom. I rodi mu sina. Ali djelo koje učini David bijaše zlo u očima Jahvinim.

< 2 Samweli 11 >