< 2 Samweli 10 >

1 Ikawa baadaye mfalme wa watu wa Amoni akafa, na Hanuni mwanaye akawa mfalme mahali pake.
And it was after thus and he died [the] king of [the] people of Ammon and he reigned Hanun son his in place his.
2 Daudi akasema, “Nitaonesha fadhiri Hanuni mwana wa Nahashi, kwa kuwa baba yake alinifadhiri.” Hivyo Daudi akatuma watumishi wake kumfariji Hanuni kwa habari ya baba yake. Watumishi wake wakaingia katika nchi ya watu wa Amoni.
And he said David I will do covenant loyalty - with Hanun [the] son of Nahash just as he did father his with me covenant loyalty and he sent David to comfort him by [the] hand of servants his concerning father his and they came [the] servants of David [the] land of [the] people of Ammon.
3 Lakini viongozi wa watu wa Amoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “Je unathani kwa hakika Daudi anamweshimu baba yako hata ametuma watu kukutia moyo? Daudi hajawatuma watumishi wake kwako ili kuuangalia mji, kuupeleleza, ili kuupindua?
And they said [the] leaders of [the] people of Ammon to Hanun lord their ¿ honoring [is] David father your in view your for he has sent to you comforters ¿ not in order to explore the city and to spy on it and to overthrow it has he sent David servants his to you.
4 Hivyo Hanuni akawachukuwa watumishi wa Daudi, akawanyoa nusu ya ndevu zao, akachana mavazi yao hadi kwenye matako, naye akawaacha waende zao.
And he took Hanun [the] servants of David and he shaved half of beard their and he cut off robes their at the middle to buttocks their and he sent away them.
5 Daudi alipoelezwa kuhusu hili, akatuma watu kwenda kuwalaki, kwa kuwa walikuwa wamefedheheshwa sana. Mfalme akawambia, “Kaeni Yeriko mpaka ndevu zenu zitakapoota, ndipo mrudi.”
And people told to David and he sent to meet them for they were the men humiliated very and he said the king remain at Jericho until it will grow back beard your and you will return.
6 Watu wa Amoni walipoona kwamba wamenuka kwa Daudi, wakatuma wajumbe na kuwaajiri Washami wa Bethi Rehobu na Soba, askari elfu ishirini waendao kwa mguu, na mfalme wa Maaka pamoja na watu elfu, na watu wa Tobu elfu kumi na mbili.
And they saw [the] people of Ammon that they had made themselves odious with David and they sent [the] people of Ammon and they hired Aram Beth Rehob and Aram Zobah twenty thousand foot soldier[s] and [the] king of Maacah one thousand man and [the] man of Tob two [plus] ten thousand man.
7 Daudi aliposikia, akamtuma Yoabu na jeshi lote la askari.
And he heard David and he sent Joab and all the army the warriors.
8 Waamoni wakatoka na wakafanya mistari ya vita katika maingilio ya lango la mji wao, wakati Washami wa Soba na wale wa Rehobu, na watu wa Tobu na Maaka, wakasimama peke yao uwandani.
And they went out [the] people of Ammon and they deployed battle [the] entrance of the gate and Aram Zobah and Rehob and [the] man of Tob and Maacah to alone them [were] in the open country.
9 Yoabu alipoona mistari ya vita ikimkabili pote mbele na nyuma, alichagua baadhi ya waisraeli wajuao kupigana vizuri na akawapanga dhidi ya Washami.
And he saw Joab that it was against him [the] face of the battle from before and from behind and he chose some of all [the] chosen [men] (of Israel *Q(K)*) and he deployed [them] to meet Aram.
10 Na sehemu iliyosalia ya jeshi, akawaweka chini ya Abishai nduguye, naye akawaweka katika mistari ya vita dhidi ya jeshi la Amoni.
And [the] rest of the people he put in [the] hand of Abishai brother his and he deployed [them] to meet [the] people of Ammon.
11 Yoabu akasema, “ikiwa Washami watakuwa na nguvu zaidi juu yangu, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini ikiwa jeshi la Amoni litakuwa na nguvu zaidi juu yako, nitakuja kukuokoa.
And he said if it will be [too] strong Aram for me and you will become of me deliverance and if [the] people of Ammon they will be [too] strong for you and I will come to deliver you.
12 Iweni na nguvu, nasi tujioneshe kuwa wenye nguvu kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu, kwa maana Yahwe atatenda yapendezayo kwa ajili ya kusudi lake.
Be strong so we may show ourselves strong for people our and for [the] cities of God our and Yahweh he will do the good in view his.
13 Hivyo Yoabu na askari wa jeshi lake wakasonga mbele katika vita dhidi ya Washami, waliolazimika kukimbia mbele ya jeshi la Israeli.
And he drew near Joab and the people which [was] with him for battle in Aram and they fled from before him.
14 Jeshi la Amoni lilipoona kwamba Washami wamekimbia, nao pia wakakimbia kutoka kwa Abishai wakarudi ndani ya mji. Ndipo Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na akarejea Yerusalemu.
And [the] people of Ammon they saw that it had fled Aram and they fled from before Abishai and they went the city and he returned Joab from on [the] people of Ammon and he came Jerusalem.
15 Washami walipoona kwamba wameshindwa na Israeli, walijikusanya pamoja tena.
And it saw Aram that it was defeated before Israel and they gathered themselves together.
16 Kisha Hadareza akatuma kuleta vikosi vya Washami ng'ambo ya Mto Frati. Wakaja Helamu pamoja na Shobaki, mkuu wa jeshi la Hadareza juu yao.
And he sent Hadadezer and he brought out Aram which [was] from [the] other side of the River and they came Helam and Shobach [the] commander of [the] army of Hadadezer [was] before them.
17 Daudi alipoambiwa, aliwakusanya Israeli wote pamoja, akavuka Yordani, na akafika Helamu. Washami wakajipanga katika mistari ya vita dhidi ya Daudi na wakapigana naye.
And it was told to David. And he gathered all Israel and he passed over the Jordan and he came Helam towards and they deployed Aram to meet David and they did battle with him.
18 Washami wakakimbia mbele ya Israeli. Daudi akaua askari mia saba wa magari na askari wa farasi elfu arobaini. Shobaki mkuu wa jeshi lao alijeruhiwa na akafa huko.
And it fled Aram from before Israel and he killed David of Aram seven hundred charioteer[s] and forty thousand horsemen and Shobach [the] commander of army its he struck down and he died there.
19 Wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadareza walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Israeli na wakawa watumishi wao. Hivyo washami wakaogopa kuwasaidia watu wa Amoni tena.
And they saw all the kings [the] servants of Hadadezer that they were defeated before Israel and they made peace with Israel and they served them and they were afraid Aram to deliver again [the] people of Ammon.

< 2 Samweli 10 >