< 2 Samweli 10 >
1 Ikawa baadaye mfalme wa watu wa Amoni akafa, na Hanuni mwanaye akawa mfalme mahali pake.
Now after this, death came to the king of the children of Ammon, and Hanun, his son, became king in his place.
2 Daudi akasema, “Nitaonesha fadhiri Hanuni mwana wa Nahashi, kwa kuwa baba yake alinifadhiri.” Hivyo Daudi akatuma watumishi wake kumfariji Hanuni kwa habari ya baba yake. Watumishi wake wakaingia katika nchi ya watu wa Amoni.
And David said, I will be a friend to Hanun, the son of Nahash, as his father was a friend to me. So David sent his servants, to give him words of comfort on account of his father. And David's servants came into the land of the children of Ammon.
3 Lakini viongozi wa watu wa Amoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “Je unathani kwa hakika Daudi anamweshimu baba yako hata ametuma watu kukutia moyo? Daudi hajawatuma watumishi wake kwako ili kuuangalia mji, kuupeleleza, ili kuupindua?
But the chiefs of the children of Ammon said to Hanun their lord, Does it seem to you that David is honouring your father by sending comforters to you? has he not sent his servants to go through the town and make secret observation of it, and overcome it?
4 Hivyo Hanuni akawachukuwa watumishi wa Daudi, akawanyoa nusu ya ndevu zao, akachana mavazi yao hadi kwenye matako, naye akawaacha waende zao.
So Hanun took David's servants, and after cutting off half the hair on their chins, and cutting off the skirts of their robes up to the middle, he sent them away.
5 Daudi alipoelezwa kuhusu hili, akatuma watu kwenda kuwalaki, kwa kuwa walikuwa wamefedheheshwa sana. Mfalme akawambia, “Kaeni Yeriko mpaka ndevu zenu zitakapoota, ndipo mrudi.”
When David had news of it, he sent men out with the purpose of meeting them on their way, for the men were greatly shamed: and the king said, Go to Jericho till your hair is long again, and then come back.
6 Watu wa Amoni walipoona kwamba wamenuka kwa Daudi, wakatuma wajumbe na kuwaajiri Washami wa Bethi Rehobu na Soba, askari elfu ishirini waendao kwa mguu, na mfalme wa Maaka pamoja na watu elfu, na watu wa Tobu elfu kumi na mbili.
And when the children of Ammon saw that they had made themselves hated by David, they sent to the Aramaeans of Beth-rehob and Zobah, and got for payment twenty thousand footmen, and they got from the king of Maacah a thousand men, and from Tob twelve thousand.
7 Daudi aliposikia, akamtuma Yoabu na jeshi lote la askari.
And hearing of this, David sent Joab and all the army and the best fighting-men.
8 Waamoni wakatoka na wakafanya mistari ya vita katika maingilio ya lango la mji wao, wakati Washami wa Soba na wale wa Rehobu, na watu wa Tobu na Maaka, wakasimama peke yao uwandani.
And the children of Ammon came out and put their forces in position at the way into the town: and the Aramaeans of Zobah and of Rehob, with the men of Tob and Maacah, were by themselves in the field.
9 Yoabu alipoona mistari ya vita ikimkabili pote mbele na nyuma, alichagua baadhi ya waisraeli wajuao kupigana vizuri na akawapanga dhidi ya Washami.
Now when Joab saw that their forces were in position against him in front and at his back, he took the best of the men of Israel and put them in line against the Aramaeans;
10 Na sehemu iliyosalia ya jeshi, akawaweka chini ya Abishai nduguye, naye akawaweka katika mistari ya vita dhidi ya jeshi la Amoni.
And the rest of the people he put in position against the children of Ammon, with Abishai, his brother, at their head.
11 Yoabu akasema, “ikiwa Washami watakuwa na nguvu zaidi juu yangu, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini ikiwa jeshi la Amoni litakuwa na nguvu zaidi juu yako, nitakuja kukuokoa.
And he said, If the Aramaeans are stronger and get the better of me, then you are to come to my help; but if the children of Ammon get the better of you, I will come to your help.
12 Iweni na nguvu, nasi tujioneshe kuwa wenye nguvu kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu, kwa maana Yahwe atatenda yapendezayo kwa ajili ya kusudi lake.
Take heart, and let us be strong for our people and for the towns of our God, and may the Lord do what seems good to him.
13 Hivyo Yoabu na askari wa jeshi lake wakasonga mbele katika vita dhidi ya Washami, waliolazimika kukimbia mbele ya jeshi la Israeli.
Then Joab and the people with him went forward to the fight against the Aramaeans, and they went in flight before him.
14 Jeshi la Amoni lilipoona kwamba Washami wamekimbia, nao pia wakakimbia kutoka kwa Abishai wakarudi ndani ya mji. Ndipo Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na akarejea Yerusalemu.
And when the children of Ammon saw the flight of the Aramaeans, they themselves went in flight from Abishai, and came into the town. So Joab went back from fighting the children of Ammon and came to Jerusalem.
15 Washami walipoona kwamba wameshindwa na Israeli, walijikusanya pamoja tena.
And when the Aramaeans saw that Israel had overcome them, they got themselves together.
16 Kisha Hadareza akatuma kuleta vikosi vya Washami ng'ambo ya Mto Frati. Wakaja Helamu pamoja na Shobaki, mkuu wa jeshi la Hadareza juu yao.
And Hadadezer sent for the Aramaeans who were on the other side of the River: and they came to Helam, with Shobach, the captain of Hadadezer's army, at their head.
17 Daudi alipoambiwa, aliwakusanya Israeli wote pamoja, akavuka Yordani, na akafika Helamu. Washami wakajipanga katika mistari ya vita dhidi ya Daudi na wakapigana naye.
And word of this was given to David: and he got all Israel together and went over Jordan and came to Helam. And the Aramaeans put their forces in position against David, and made an attack on him.
18 Washami wakakimbia mbele ya Israeli. Daudi akaua askari mia saba wa magari na askari wa farasi elfu arobaini. Shobaki mkuu wa jeshi lao alijeruhiwa na akafa huko.
And the Aramaeans went in flight before Israel; and David put to the sword the men of seven hundred Aramaean war-carriages and forty thousand footmen, and Shobach, the captain of the army, was wounded, and came to his death there.
19 Wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadareza walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Israeli na wakawa watumishi wao. Hivyo washami wakaogopa kuwasaidia watu wa Amoni tena.
And when all the kings who were servants of Hadadezer saw that they were overcome by Israel, they made peace with Israel and became their servants. So the Aramaeans, in fear, gave no more help to the children of Ammon.