< 2 Samweli 10 >

1 Ikawa baadaye mfalme wa watu wa Amoni akafa, na Hanuni mwanaye akawa mfalme mahali pake.
Hathnukkhu, Ammon siangpahrang teh a due. A capa Hanun ni a na pa e yueng lah siangpahrang a tawk.
2 Daudi akasema, “Nitaonesha fadhiri Hanuni mwana wa Nahashi, kwa kuwa baba yake alinifadhiri.” Hivyo Daudi akatuma watumishi wake kumfariji Hanuni kwa habari ya baba yake. Watumishi wake wakaingia katika nchi ya watu wa Amoni.
Devit ni Hanun e a na pa Nahash teh kai koe ahawinae a sak dawkvah, pahrennae ka kamnue sak van han telah ati. A na pa a due nah lungpahawi hanelah a sannaw a patoun teh, Devit e sannaw teh Ammonnaw e ram koe a pha awh.
3 Lakini viongozi wa watu wa Amoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “Je unathani kwa hakika Daudi anamweshimu baba yako hata ametuma watu kukutia moyo? Daudi hajawatuma watumishi wake kwako ili kuuangalia mji, kuupeleleza, ili kuupindua?
Ammon miphun kacuenaw ni amamae a bawipa Hanun koevah, Devit ni na barilawa dawkvah, nang koe lungmawng nahanelah, tami a patoun e na yuem maw. Devit ni hete khopui a raphoe thai nahan ka tuet hanelah nang koe a patoun awh nahoehmaw telah atipouh awh.
4 Hivyo Hanuni akawachukuwa watumishi wa Daudi, akawanyoa nusu ya ndevu zao, akachana mavazi yao hadi kwenye matako, naye akawaacha waende zao.
Hanun ni Devit e a sannaw a man teh, a pâkhamuen tangawn a ngaw pouh. A khohna hai a laheibaw totouh a a pouh hnukkhu a cei sak.
5 Daudi alipoelezwa kuhusu hili, akatuma watu kwenda kuwalaki, kwa kuwa walikuwa wamefedheheshwa sana. Mfalme akawambia, “Kaeni Yeriko mpaka ndevu zenu zitakapoota, ndipo mrudi.”
Hote kamthang hah Devit ni a thai toteh, ahnimanaw teh a kaya poung dawkvah, ahnimanaw dawn sak hanelah a patoun teh, nangmouh teh pâkhamuen a saw hoehroukrak Jeriko kho dawkvah awm awh. Hahoi torei bout tho awh telah atipouh.
6 Watu wa Amoni walipoona kwamba wamenuka kwa Daudi, wakatuma wajumbe na kuwaajiri Washami wa Bethi Rehobu na Soba, askari elfu ishirini waendao kwa mguu, na mfalme wa Maaka pamoja na watu elfu, na watu wa Tobu elfu kumi na mbili.
Ammonnaw ni vah, maimouh teh Devit e hmaitung panuettho e lah o awh han tie a panue awh teh, taminaw a patoun awh teh, Bethrekhob kho hoi Aramzobah kho e Siria ransa 20,000, hoi siangpahrang Maakah e tami 1,000, hoi Tob ram e tami 12,000 touh hah a hlai awh.
7 Daudi aliposikia, akamtuma Yoabu na jeshi lote la askari.
Devit ni hote kamthang a thai toteh, Joab hoi athakaawme ransanaw hah a patoun.
8 Waamoni wakatoka na wakafanya mistari ya vita katika maingilio ya lango la mji wao, wakati Washami wa Soba na wale wa Rehobu, na watu wa Tobu na Maaka, wakasimama peke yao uwandani.
Ammonnaw hah a tâco awh teh, kho longkha koe a tungpup awh. Aramzobah kho, Rehob, Tob kho hoi ka tho e Siria tami hoi Maakah siangpahrang e taminaw teh aloukcalah law vah ao awh.
9 Yoabu alipoona mistari ya vita ikimkabili pote mbele na nyuma, alichagua baadhi ya waisraeli wajuao kupigana vizuri na akawapanga dhidi ya Washami.
A hnukhma lahoi tuk hane na kâcai awh tie Joab ni a thai navah, Isarelnaw thung dawk hoi kahawi kahawi e a rawi teh, Sirianaw tuk hanelah namranlah a tumpup awh.
10 Na sehemu iliyosalia ya jeshi, akawaweka chini ya Abishai nduguye, naye akawaweka katika mistari ya vita dhidi ya jeshi la Amoni.
Aloukenaw pueng hah a hmaunawngha Abisai kut dawk koung a hruek teh, Ammon tami tuk hanelah a tumpup sak awh.
11 Yoabu akasema, “ikiwa Washami watakuwa na nguvu zaidi juu yangu, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini ikiwa jeshi la Amoni litakuwa na nguvu zaidi juu yako, nitakuja kukuokoa.
Siria taminaw ni kai na tâ pawiteh, nangmouh ni na kabawp han. Ammonnaw ni nangmanaw na tâ pawiteh, kaimouh ni na kabawp han.
12 Iweni na nguvu, nasi tujioneshe kuwa wenye nguvu kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu, kwa maana Yahwe atatenda yapendezayo kwa ajili ya kusudi lake.
Tarankahawi lah awm awh. Ka taminaw hoi mamae Cathut khonaw hanelah thapatung awh nateh, tuk awh. BAWIPA ni a ngainae patetlah a sak han doeh atipouh.
13 Hivyo Yoabu na askari wa jeshi lake wakasonga mbele katika vita dhidi ya Washami, waliolazimika kukimbia mbele ya jeshi la Israeli.
Ama koe kaawm e taminaw hoi Siria taminaw tuk hanelah a pâtam awh teh, Sirianaw a yawng awh.
14 Jeshi la Amoni lilipoona kwamba Washami wamekimbia, nao pia wakakimbia kutoka kwa Abishai wakarudi ndani ya mji. Ndipo Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na akarejea Yerusalemu.
Sirianaw a yawng awh e Ammonnaw ni a hmu awh navah, ahnimouh hai Abisai hmalah a yawng awh teh, kho thung vah a kâen awh. Joab hai Ammon ram hoi a tâco teh Jerusalem kho lah a cei.
15 Washami walipoona kwamba wameshindwa na Israeli, walijikusanya pamoja tena.
Sirianaw ni Isarelnaw e a hmalah amamanaw a sung e a kâpanue awh navah bout a kamkhueng awh.
16 Kisha Hadareza akatuma kuleta vikosi vya Washami ng'ambo ya Mto Frati. Wakaja Helamu pamoja na Shobaki, mkuu wa jeshi la Hadareza juu yao.
Hadadezer ni tami a patoun teh, tui namran lah kaawm e Sirianaw a thokhai teh, Hadadezer ransa kacue e Shobak ni a hrawi awh teh, Helam kho lah a cei awh.
17 Daudi alipoambiwa, aliwakusanya Israeli wote pamoja, akavuka Yordani, na akafika Helamu. Washami wakajipanga katika mistari ya vita dhidi ya Daudi na wakapigana naye.
Hote kong Devit koe a dei pouh. Isarelnaw pueng koung a pâkhueng teh, Jordan tui a raka awh teh, Helam kho a pha awh. Sirianaw ni Devit tuk hanelah a kampawp awh teh a tuk awh.
18 Washami wakakimbia mbele ya Israeli. Daudi akaua askari mia saba wa magari na askari wa farasi elfu arobaini. Shobaki mkuu wa jeshi lao alijeruhiwa na akafa huko.
Sirianaw teh Isarelnaw e hmalah hoi a yawng awh. Devit ni Siria tami leng dawk kâcuinaw 700 hoi marangransanaw 40,000 touh a thei. Ransabawi Shobak hai a thei awh teh hawvah a due.
19 Wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadareza walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Israeli na wakawa watumishi wao. Hivyo washami wakaogopa kuwasaidia watu wa Amoni tena.
Hadadezer koe san ka toung e siangpahrangnaw pueng teh, Isarelnaw e hmaitung vah amamanaw a sung e a kâpanue awh navah, Isarelnaw hoi roumnae a sak awh teh, a thaw a tawk pouh awh. Hottelah Sirianaw ni Ammonnaw hah bout kabawm ngai awh hoeh toe.

< 2 Samweli 10 >