< 2 Samweli 1 >

1 Baada ya kifo cha Sauli, Daud alirudi kutoka kuwashambulia Waamaleki na akakaa Siklagi kwa siku mbili.
After Saul died, David [and the men who were with him] returned to Ziklag [town] after defeating the descendants of Amalek. They stayed in Ziklag for two days.
2 Siku ya tatu, mtu mmoja alikuja kutoka kambi ya Sauli nguo zake zikiwa zimeraruliwa na akiwa na vumbi juu ya kichwa chake. Alipofika kwa Daudi alinamisha uso wake chini akajifanya yeye mwenyewe kuwa si kitu.
On the third day, unexpectedly a man arrived there who had come from where Saul’s army was camped. He had torn his clothes and put dust on his head [to show that he was grieving]. He came to David, and prostrated himself on the ground [in front of David to show respect for him].
3 Daudi akamuliza, “Unatoka wapi?” Yeye akajibu, “Nimeponyoka kutoka kambi ya Israeli.”
David asked him, “Where have you come from?” The man replied, “I escaped from where the Israeli army had been camped.”
4 Daudi akamwambia, “Tafadhari nieleze jinsi mambo yalivyokuwa.” Akajibu, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wameanguka, na wengi wao wameuawa. Sauli na Yonathani mwanawe pia wameuawa.”
David asked him, “What happened? Tell me [about the battle]!” The man replied, “The Israeli soldiers ran away from the battle. Many of them were killed. And Saul and his son Jonathan (are dead/were also killed).”
5 Daudi akamwuliza kijana, “unajuaje kuwa Sauli na Yonathani mwanawe wameuawa?”
David said to the young man, “How do you know that Saul and his son Jonathan are dead?”
6 Yule kijana akajibu, “Kwa bahati nilikuwa juu ya Mlima Gilboa, na pale alikuwepo Sauli ameegemea mkuki wake, na magari ya farasi na waongozaji walikuwa karibu kumkamata.
The young man replied, “It happened that I was on Gilboa Mountain [where the battle occurred], and I saw Saul, leaning on his spear. The [enemy] chariots and their drivers had come very close to Saul.
7 Sauli alipogeuka aliniona na akaniita. Nikajibu, 'Mimi hapa.'
Saul turned around and saw me, and he called out to me. I answered him and said, ‘What do you want me to do?’
8 Akaniuliza, 'Wewe ni nani?' Nikamjibu, 'Mimi ni Mwamaleki,'
He replied, ‘Who are you?’ I replied, ‘I am a descendant of Amalek.’
9 Akaniambia, Tafadhari simama juu yangu uniuwe, kwa kuwa shida kubwa imenipata, lakini uhai ungalimo ndani yangu.'
Then he said to me, ‘Come over here and kill me. I am still alive, but I am enduring a lot of pain.’
10 Hivyo nilisimama juu yake nikamuuwa, kwa maana nilijua kwamba asingeweza kuishi baada ya kuwa ameanguka. Ndipo nikachukuwa taji iliyokuwa juu ya kichwa chake na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, na nimevileta hapa kwako, bwana wangu.”
So I went to him and killed him, because I knew that he was wounded very badly and would (not continue to live/soon die). I took the crown that was on his head and the band/bracelet that was on his arm, and I have brought them to you.”
11 Kisha Daudi akararua mavazi yake, na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafanya vilevile.
Then David and all the men who were with him tore their clothes [to show that they were very sad].
12 Walilia, wakaomboleza na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli, Yonathani mwanawe, watu wa Yahwe, na kwa ajili ya nyumba ya Israeli kwa maana wameanguka kwa upanga.
They mourned for Saul and his son Jonathan, and they cried and (fasted/abstained from eating food) until it was evening. They also mourned for all the army of Yahweh, and for all the Israeli people, because many of their soldiers had been killed in the battle [MTY].
13 Daudi akamwambia yule kijana, “Unatokea wapi?” Akajibu, mimi ni kijana wa mgeni Mwamaleki.”
Then David asked the young man who had told him [about the battle], “Where are you from?” He replied, “My father is a descendant of Amalek, but we live in Israel.”
14 Daudi akamwambia, “Kwa nini haukuogopa kumwua mfalme, mtiwa mafuta wa Yahwe kwa mkono wako?”
David asked him, “(Why were you not afraid [that you would be punished if you] killed Saul, whom Yahweh had appointed [MTY] [to be the king]?/You should have been afraid [that you would be punished if you] killed Saul, whom Yahweh had appointed [MTY] [to be the king].) [RHQ]
15 Daudi akamwita mmojawapo wa vijana na akamwambia, “Nenda ukamuue.” Hivyo kijana huyo akaenda na kumpiga hata ata chini, Mwamaleki akafa.
You yourself said, ‘I killed the man whom Yahweh appointed to be the king.’ So you have caused yourself to be guilty [MTY] of causing your own death!” Then David summoned one of his soldiers and said to him, “Kill him!” So the soldier killed him by striking him [with a sword].
16 Ndipo Daudi akamwambia Mwamaleke aliyekufa, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako kwa kuwa kinywa chako kimeshuhudia dhidi yako kusema, Nimemuua mfalme mtiwa mafuta wa Yahwe.
17 Ndipo Daudi akaimba wimbo wa maombolezo juu ya Sauli na Yonathani mwanawe.
Then David composed/wrote this sad song about Saul and Jonathan,
18 Akawaamuru watu kuufundisha wimbo wa Bow kwa wana wa Yuda, ambao umeandikwa katika Kitabu cha Yashari.
and he commanded that it be taught to the people of Judah. [The song is called] ‘The Bow [and Arrow]’ and it has been written in the Book of Jashar:
19 “Utukufu wako, Israel, umeondolewa, umeondolewa juu ya mahali pako pa juu! Jinsi mwenye nguvu alivyoanguka!
“You Israeli people, your glorious [MTY] leaders have been killed on the mountains! [It is very sad that] those mighty men have died!
20 Msiiseme katika Gathi, msiitangaze katika mitaa ya Ashikeloni, ili binti za wafilisti wasifurahi, ili binti za wasiotailiwa wasisherehekee.
“Do not tell it [to our enemies in the Philistia area]; do not tell to the people who live in Gath [city] what happened; do not proclaim it in the streets of Ashkelon [city], because if you tell them, [even] the women in that area will be happy; do not allow those (pagan women/women who do not know God) to rejoice.
21 Milima ya Gilboa, kusiwe na umande au mvua juu yenu. wala mashamba yasitoe nafaka kwa ajili ya sadaka, kwa maana hapo ngao ya mwenye nguvu imeharibiwa. Ngao ya Sauli haiwezi tena kutiwa mafuta.
I hope/desire that there will be no rain or dew on the mountains of [the] Gilboa [area] [APO], and that no grain will grow in the fields there, because there the shield of Saul, the mighty [king], fell on the ground. No one rubbed [olive] oil on Saul’s shield;
22 Kutoka katika damu ya waliouawa, kutoka katika miili ya wenye nguvu, upinde wa Yonathani haukurudi nyuma, na upanga wa Sauli haukurudi patupu.
instead, it was stained with the blood of those whom he had killed, and the fat of mighty enemy soldiers was smeared on it. Jonathan [PRS] did not retreat carrying his bow [and arrows], and Saul always [defeated his enemies when he fought them] with his sword. [PRS, LIT]
23 Sauli na Yonathani walikuwa wakipendwa na walikuwa wenye neema maishani, hata wakati wa mauti yao walikuwa pamoja. Walikuwa na kasi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
“Saul and Jonathan were loved and they pleased many people. They were together [LIT] while they lived and when they died. [In battles] they were swifter than eagles and they were stronger than lions.
24 Enyi binti wa Israeli lieni juu ya Sauli, aliyewavika mavazi ya thamani pamoja na vito vya thamani, na aliyetia mapambo ya dhahabu katika mavazi yenu.
“You Israeli women, cry about Saul; He provided beautiful scarlet/red clothes for you and he gave you gold ornaments/jewelry to fasten on those clothes.
25 Jinsi wenye nguvu walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa juu ya mahali pako pa juu.
“[It is very sad that] this mighty soldier has died! Jonathan has been killed on the mountains/hills.
26 Nimesikitishwa sana kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu. Ulikuwa mpendwa wangu sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, ukipita upendo wa wanawake.
Jonathan, my dear friend, I grieve for you; you were very dear to me. You loved me in a wonderful manner; it was better than the way that a woman loves [her husband and her children].
27 Jinsi wenye nguvu walivyoanguka na silaha za vita zimeteketea!”
“It is very sad that those mighty men have died, and their weapons are now abandoned!

< 2 Samweli 1 >