< 2 Wafalme 9 >

1 Nabii Elisha akamwita mmoja wa watoto wa manabii na kumwambia, “Vaa kwa kwa safari, halafu chukua hii chupa ndogo ya mafuta kwenye mikono yako na uende Romoth Geliadi.
And Elisha the prophet he summoned one from [the] sons of the prophets and he said to him gird up loins your and take [the] flask of oil this in hand your and go Ramoth Gilead.
2 Wakati utakapofika, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi, na uende ukaingie na kumfanya ainuke kutoka miongoni mwa rafiki zake, na ukampeleke katika chumba cha ndani.
And you will go there towards and look for there Jehu [the] son of Jehoshaphat [the] son of Nimshi and you will go and you will make rise him from among brothers his and you will bring him a room in a room.
3 Kisha chukua ile chupa ya mafuta na imiminie kwenye kichwa chake na kusema, 'Yahwe anasema hivi: “Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. “Halafu fungua mlango, na kukimbia; usichelewe.”
And you will take [the] flask of oil and you will pour [it] on head his and you will say thus he says Yahweh I anoint you to king to Israel and you will open the door and you will flee and not you must delay.
4 Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Romoth Geliadi.
And he went the young man the young man the prophet Ramoth Gilead.
5 Wakati alipofika, kumbe, wale manahodha wa lile jeshi walikuwa wamekaa. Hivyo yule nabii kijana akasema, “Nimekuja mara moja naneno kwako, nahodha.” Yehu akajibu, “kwa yupi katika sisi?” Yule nabii kijana akajibu, “Kwako nahodha.”
And he came and there! [the] commanders of the army [were] sitting and he said a word [belongs] to me to you O commander and he said Jehu to whom? from all of us and he said to you O commander.
6 Basi Yehu akainuka na kwenda kwenye nyumba, na yule nabii akammiminia mafuta kwenye kichwa chake na kumwambia Yehu, “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: 'Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Yahwe, juu ya Isaraeli.
And he arose and he went the house towards and he poured the oil to head his and he said to him thus he says Yahweh [the] God of Israel I anoint you to king to [the] people of Yahweh to Israel.
7 Wewe lazima uiue familia ya Ahabu bwana wako, ili niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe, ambao waliokuwa wameuawa kwa mkono wa Yezebeli.
And you will strike down [the] house of Ahab master your and I will avenge [the] blood of - servants my the prophets and [the] blood of all [the] servants of Yahweh from [the] hand of Jezebel.
8 Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu, yeyote awe mtumwa au mtu huru.
And it will perish all [the] house of Ahab and I will cut off to Ahab [one who] urinates on a wall and shut up and freed in Israel.
9 Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama nyumba ya Yerobohamu mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
And I will make [the] house of Ahab like [the] house of Jeroboam [the] son of Nebat and like [the] house of Baasha [the] son of Ahijah.
10 Mbwa watamla Yezebeli katika Yezreeli, na hakutakuwa na mtu wa kumzika.” Kisha nabii akafungua mlango na kukimbia.
And Jezebel they will devour the dogs in [the] territory of Jezreel and there not [will be one who] buries [her] and he opened the door and he fled.
11 Kisha Yehu akatoka kwenda kwa watumishi wa bwana wake, na mmoja akamwambia, “Je kila kitu kiko sawa? Kwa nini huyu mwenda wazimu amekuja kwako?” Yehu akawajibu, “Mnamjua huyo mtu na mambo asemayo.”
And Jehu he went out to [the] servants of master his and someone said to him ¿ peace why? did he come the mad [man] this to you and he said to them you you know the man and talk his.
12 Wakasema, “Huo ni uongo. Tuambie.” Yehu akajibu, “Alisema hivi na vile juu yangu, na pia akasema, 'hivi ndivyo Yahwe asemavyo: Nimekumiminia mafuta kama mfalme juu ya Israeli.””
And they said falsehood tell please to us and he said like this and like this he said to me saying thus he says Yahweh I anoint you to king to Israel.
13 Kisha kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu juu ya madaraja. Wakapiga baragumu na kusema, “Yehu ni mfalme.”
And they hurried and they took each garment his and they put [them] under him to [the] bone of the steps and they gave a blast on the trumpet and they said he is king Jehu.
14 Katika njia hii Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akafanya njama juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiilinda Ramothi Gileadi, yeye na Israeli yote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu,
And he conspired Jehu [the] son of Jehoshaphat [the] son of Nimshi against Joram and Joram he had been watching at Ramoth Gilead he and all Israel from before Hazael [the] king of Aram.
15 lakini mfalme Yoramu alikuwa amesharudi kwa Yezreeli ili kuponywa yale majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami, wakati akiwa anapigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akawaambia watumishi wa Yoramu, “kama hili ndilo wazo lako, kisha usimwache mtu aondoke na kwenda nje ya mji, ili aende kupeleka habari hii Yezreeli.”
And he had returned Jehoram the king to get himself healed in Jezreel from the wounds which they wounded him [the] Arameans when fought he with Hazael [the] king of Aram and he said Jehu if there [is] mind your may not he go out an escapee from the city to go (to tell *Q(k)*) in Jezreel.
16 Basi Yehu akaendesha gari la farasi mpaka Yezreeli; kwa kuwa Yoramu alikuwa amelala huko. Basi Ahazi mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka chini kuonana na Yoramu.
And he rode in a chariot Jehu and he went Jezreel towards for Joram [was] lying there and Ahaziah [the] king of Judah he had come down to see Joram.
17 Mlinzi alikuwa amesimama juu ya mnara katika Yezreeli, akaliona lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo; akasema, “Naona kundi la watu wanakuja.” Yoramu akasema, “Chukua mwendesha farasi, na umtume akakutane nao; mwambie aseme, “Je mnakuja kwa amani?””
And the watchman [was] standing on the tower in Jezreel and he saw [the] crowd of Jehu when came he and he said a crowd I [am] seeing and he said Jehoram take a horseman and send [him] to meet them and he may say ¿ peace.
18 Hivyo mwendesha farasi akatoka kumlaki; akasema, “Mfalme asema hivi: Je mnakuja kwa amani?”' Basi Yehu akasema, “Wewe una nini na amani? Geuka na unifuate nyuma.” Kisha yule mlinzi akamwambia mfalme, Yule mjumbe ameshaonana nao, lakini anarudi.”
And he went [the] rider of the horse to meet him and he said thus he says the king ¿ peace and he said Jehu what? [is] to you and to peace go around to after me and he reported the watchman saying he came the messenger to they and not he has turned back.
19 Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao na kusema, “Mfalme asema hivi: 'Je mnakuja na amani?”' Yehu akajibu, “Wewe una nini na amani? Geuka na kunifuata nyuma.
And he sent a rider of a horse second and he came to them and he said thus he says the king peace and he said Jehu what? [is] to you and to peace go around to after me.
20 Tena yule mlinzi akatoa taarifa, “Amekwisha kuonana nao, lakini hatorudi. Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo; anaendesha kwa kasi.”
And he reported the watchman saying he came to to them and not he has turned back and the driving [is] like [the] driving of Jehu [the] son of Nimshi for with madness he drives.
21 Hivyo Yoramu akasema, “Andaa gari langu la farasi liwe tayari.” Wakaandaa gari lake la farasi, na Yoramu mfalme wa Israeli na Ahazi mfalme wa Yuda akaendesha, kila mmoja kwenye gari lake la farasi, kumlaki Yehu. Wakamkuta kwenye mali ya Nabothi Myezreeli.
And he said Jehoram harness and someone harnessed chariot his and he went out Jehoram [the] king of Israel and Ahaziah [the] king of Judah each in chariot his and they went out to meet Jehu and they found him in [the] portion of land of Naboth the Jezreelite.
22 Wakati Yoramu alipomuona Yehu, alisema, “Je unakuja katika hali ya amani, Yehu?” Akajibu, “Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?”
And it was when saw Jehoram Jehu and he said ¿ peace O Jehu and he said what? [is] peace until [the] prostitutions of Jezebel mother your and sorceries her many.
23 Basi Yoramu akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia na kumwambia Ahazia, “Kuna udanganyifu, Ahazia.
And he turned around Jehoram hands his and he fled and he said to Ahaziah treachery O Ahaziah.
24 Ndipo Yehu akauvuta upinde wake kwa nguvu zake zote na kumpiga Yoramu kati ya mabega yake; mshale ukaenda kwenye moyo wake, akaanguka chini kwenye gari lake la farasi.
And Jehu he filled hand his with bow and he struck Jehoram between arms his and it came out the arrow from heart his and he sank down in chariot his.
25 Ndipo Yehu akamwambia Bidkari nahodha wake, “Mchukue na mtupie kwenye shamba la Nabothi Myezreeni. Fikiria kuhusu vile ambavyo wewe na mimi tulivyoendesha pamoja baada ya Ahabu baba yake, Yahwe aliuweka juu unabii dhidi yake:
And he said to Bidkar (officer his *Q(K)*) pick [him] up throw him in [the] portion of [the] field of Naboth the Jezreelite for remember I and you [were] riding pairs behind Ahab father his and Yahweh he lifted up on him the oracle this.
26 Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya watoto wake - asema Yahwe - na nitahakikisha unalipia hili shamba - asema Yahwe. Sasa basi, mchukue na mtupe kwenye hili shamba, sawa sawa na neno la Yahwe.”
If not [the] blood of Naboth and [the] blood of sons his I saw yesterday [the] utterance of Yahweh and I will repay to you on the portion of land this [the] utterance of Yahweh and therefore pick [him] up throw him on the portion of land according to [the] word of Yahweh.
27 Wakati Ahazi yule mfalme wa Yuda alipoliona hili, akakimbia kwa njia ya Bethi Hagani. Lakini Yehu akamfuata, na kusema, “Muulie humo kwenye gari la farasi,” na wakampiga mahali pa kupandia Guri, karibu na Ebleamu. Ahazi akakimbilia Megido na kufia pale.
And Ahaziah [the] king of Judah he saw and he fled [the] direction Beth Haggan and he pursued after him Jehu and he said also him strike down him into the chariot at [the] ascent of Gur which [is] with Ibleam and he fled Megiddo and he died there.
28 Watumishi wake wakaubeba mwili wake kwa magari ya farasi kwenda Yerusalemu na kumzika kwenye kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
And they caused to ride him servants his Jerusalem towards and they buried him in grave his with ancestors his in [the] city of David.
29 Basi ilikuwa mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu huyo Ahazia akaanza kutawala juu ya Yuda.
And in year one [plus] ten year of Joram [the] son of Ahab he had become king Ahaziah over Judah.
30 Wakati Yahu alipokuja kwa Yezebeli, Yezebeli akasikia juu ya hilo, akapaka wanja kwenye macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri, na kuchungulia kwenye dirisha.
And he went Jehu Jezreel towards and Jezebel she heard and she set with eye-paint eyes her and she made good head her and she looked down through the window.
31 Kadiri Yehu alipokuwa akiingia kwenye lango, akamwambia, “Je unakuja kwa amani, wewe Zimri, muuaji wa bwana wako?”
And Jehu he came in the gate and she said ¿ peace O Zimri [the] murderer of master his.
32 Yehu akatazama juu ya dirisha na kusema, “Ni nani yuko upande wangu? Nani?” Matowashi wawili au watatu wakachungulia nje.
And he lifted up face his to the window and he said who? [is] with me who? and they looked down to him two three court-officials.
33 Basi Yehu aksema, “Mtupeni chini.” Hivyo wakamtupa Yezebeli chini, na damu yake nyingine ikamwagika kwenye ukuta na farasi, na Yehu akamkanyaga kanyaga chini ya miguu.
And he said (let fall her *Q(K)*) and they let fall her and it spattered some of blood her to the wall and to the horses and he trampled her.
34 Basi Yehu akaingia hiyo sehemu, akala na kunywa. Kisha akasema, “Mtazamani sasa huyu mwanamke aliyelaaniwa na kumzika, kwa kuwa ni binti wa mfalme.”
And he went and he ate and he drank and he said attend to please the accursed [woman] this and bury her for [was] a daughter of a king she.
35 Wakaenda kumzika, lakini hawakumkuta ila fuvu, miguu, na viganga vya mikono yake.
And they went to bury her and not they found in her that except the skull and the feet and [the] palms of the hands.
36 Basi wakarudi na kumwambia Yehu. Akasema, “Hili ndilo neno la Yahwe ambalo ameliongea kupitia Eliya Mtishbi, likisema, 'Katika nchi Yezreeli mbwa ataula mwili wa Yezebeli,
And they returned and they told to him and he said [is] [the] word of Yahweh it which he spoke by [the] hand of servant his Elijah the Tishbite saying in [the] territory of Jezreel they will devour the dogs [the] flesh of Jezebel.
37 na mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema, “Huyu ni Yezebeli.””
(And it will be *Q(k)*) [the] corpse of Jezebel like dung on [the] surface of the field in [the] territory of Jezreel that not people will say this [is] Jezebel.

< 2 Wafalme 9 >