< 2 Wafalme 8 >

1 Basi, Elisha alikuwa amemwambia yule mwanamke ambaye alimfufulia mtoto wake. Akamwambia, “Inuka na uenede pamoja na nyumba yako, na uishi popote uwezapo katika nchi nyingine, kwa sababu Yahwe ameiita njaa ambayo itakuja katika hii nchi kwa miaka saba.”
Élisée avait parlé à la femme dont il avait rendu la vie au fils, en disant: « Lève-toi, va, toi et ta famille, et reste quelque temps où tu pourras, car Yahvé a annoncé une famine. Elle s'abattra sur le pays pendant sept ans. »
2 Basi yule mwanamke akainuka na akatii lile neno la mtumishi wa Mungu. Akaenda na nyumba yake na kuishi kwenye nchi ya Wafilisti miaka saba.
La femme se leva, et fit ce que l'homme de Dieu lui avait dit. Elle partit avec sa famille, et elle vécut sept ans dans le pays des Philistins.
3 Ikafika kama mwishoni mwa miaka saba yule mwanamke akarudi kutoka kwenye ile nchi ya Wafilisti, na kwenda kwa mfalme kumuomba nyumba yake na kwa ajili ya nchi yake.
Au bout de sept ans, la femme revint du pays des Philistins. Elle sortit pour demander au roi sa maison et son pays.
4 Basi mfalme alikuwa anaongea na Gehazi yule mtumishi wa Mungu, akisema, “Tafadhali niambie yale mambo makubwa ambayo Elisha ameyafanya.”
Or, le roi parlait avec Guéhazi, le serviteur de l'homme de Dieu, en disant: « Je te prie de me raconter toutes les grandes choses qu'Élisée a faites. »
5 Basi alipokuwa akimwambia yule mfalme jinsi gani Elisha alivyomfufua yule mtoto aliyekufa, huyo mwanamke ambaye mtoto wake aliyekuwa amefufuliwa akaja kumuomba yule mfalme kwa ajili ya nyumba yake na nchi yake. Gehazi akasema, “Bwana wangu, mfalme, huyu ndiye yule mwanamke, na huyu ndiye mtoto wake, ambaye Elisha amemfufua.”
Comme il racontait au roi comment il avait rendu la vie à celui qui était mort, voici que la femme dont il avait rendu la vie au fils supplia le roi pour sa maison et pour son pays. Guéhazi dit: « Mon seigneur, ô roi, voici la femme et voici son fils qu'Élisée a rendu à la vie. »
6 Wakati yule mfalme alipomuuliza yule mwanamke kuhusu mtoto wake, alimwelezea yule mfalme. Ndipo mfalme akamwagizia ofisa makini, akisema, “Mrudishie vyote vilivyokuwa vyake na mavuno yake yote ya kwenye mashamba tangu siku alipoondoka hadi sasa.”
Le roi interrogea la femme, et elle lui répondit. Alors le roi lui nomma un officier, en disant: « Restaure tout ce qui lui appartenait, et tous les fruits des champs depuis le jour où elle a quitté le pays, jusqu'à maintenant. »
7 Elisha akaja Damaskasi ambako Ben Hadadi yule mfalme wa Shamu alikuwa anaumwa. Yule mfalme aliambiwa, “Yule mtu wa Mungu amekuja hapa.”
Elisée arriva à Damas, et Benhadad, le roi de Syrie, était malade. On lui dit: « L'homme de Dieu est venu ici. »
8 Mfalme akamwambia Hazaeli, “Chukua zawadi kwenye mkono wako na uende ukakutane na mtu wa Mungu, na ukazungumze na Yahwe kupitia yeye, ukisema, “Je nitapona huu ugonjwa wangu?”
Le roi dit à Hazaël: « Prends un présent dans ta main, va à la rencontre de l'homme de Dieu, et interroge par lui Yahvé en disant: « Vais-je guérir de cette maladie? »"
9 Basi Hazaeli akaenda kuonana naye na kuchukua zawadi zake za kila kitu kizuri cha Damskasi, akabeba ngamia arobaini. Hivyo Hazaeli akaja na kusimama mbele ya Elisha na kusema, “Mtoto wako Ben Hadadi mfalme wa Shamu amenituma kwako, kusema, “Je nitapona huu ugonjwa?”
Hazaël alla au-devant de lui et prit avec lui un présent, de tout ce qu'il y avait de bon à Damas, quarante charges de chameaux, puis il vint se placer devant lui et dit: « Ton fils Benhadad, roi de Syrie, m'a envoyé vers toi, en disant: « Vais-je guérir de cette maladie? »
10 Elisha akamwambia, “Nenda, kwa Ben Hadadi, 'Utapona hakika,' lakini Yahwe amenionyesha kwamba atakufa hahkika.”
Élisée lui dit: « Va, dis-lui: « Tu vas guérir », mais l'Éternel m'a montré qu'il allait mourir. »
11 Basi Elisha akamtumbulia macho Hazaeli hadi alipojisikia aibu, na yule mtu wa Mungu akalia machozi.
Il fixa son regard sur lui, jusqu'à ce qu'il ait honte. Alors l'homme de Dieu pleura.
12 Hazaeli akauliza, kwa nini unalia, bwana wangu?” Akajibu, “Kwa sababu najua uovu ambao utakaoufanya kwa watu wa Israeli. Utazichoma moto ngome zao kwa moto, na utawaua vijana wao kwa upanga, kuwaseta vipande vipande watoto wao wachanga, na kuwapasua mimba zao wanawake wenye mimba.”
Hazaël dit: « Pourquoi pleures-tu, mon seigneur? » Il répondit: « Parce que je sais le mal que tu feras aux enfants d'Israël. Vous mettrez le feu à leurs forteresses, vous tuerez leurs jeunes gens par l'épée, vous mettrez en pièces leurs petits enfants et vous déchirerez leurs femmes enceintes. »
13 Hazaeli akajibu, Ni nani mtumwa wako, ambaye atafanya jambo hili kubwa? Yeye ni mbwa tu.” Elisha akajibu, “Yahwe amenionyesha kwamba utakuwa mfalme juu ya Shamu.”
Hazaël dit: « Mais qu'est-ce que ton serviteur, qui n'est qu'un chien, pour qu'il puisse faire cette grande chose? » Elisée répondit: « Yahvé m'a montré que tu seras roi de Syrie. »
14 Ndipo Hazaeli akamwacha Elisha na kuja kwa bwana wake, ambaye alimwambia, “Je Elisha alikwambiaje?” Akajibu, “Ameniambia kwamba utapona bila shaka.”
Puis il se sépara d'Élisée et vint vers son maître, qui lui dit: « Que t'a dit Élisée? » Il a répondu: « Il m'a dit que vous alliez sûrement guérir. »
15 Basi siku ya pili yake Hazaeli akachukua blangeti na kulichovya kwenye maji, na kulitandaza kwenye uso wa Ben Hadadi hivyo akafa. Basi Hazaeli akawa mfalme katika sehemu sehemu yake.
Le lendemain, il prit un linge épais, le trempa dans l'eau et l'étendit sur le visage du roi, de sorte qu'il mourut. Hazaël régna à sa place.
16 Katika mwaka wa kumi na tano wa Yoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Yehoramu akaanza kutawala. Alikuwa mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda. Alianza wakati Yehoshafati alikuwa mfalme wa Yuda.
La cinquième année de Joram, fils d'Achab, roi d'Israël, Josaphat étant alors roi de Juda, Joram, fils de Josaphat, roi de Juda, commença à régner.
17 Yoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na mbili alipoanza kutawala, na alitawala kwa mda wa miaka minane katika Yerusalemu.
Il avait trente-deux ans lorsqu'il devint roi. Il régna huit ans à Jérusalem.
18 Yoramu akatembea kwenye njia ya huyo mfalme wa Israeli, kama walivyokuwa wakifanya kwenye nyumba ya Ahabu; kwa kuwa alikuwa na binti wa Ahabu kama mke wake, na alifanya uovu usoni kwa Yahwe.
Il marcha dans la voie des rois d'Israël, comme la maison d'Achab, car il avait épousé la fille d'Achab. Il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel.
19 Walakini, kwa sababu ya mtumishi wake Daudi, Yahwe hakutaka kuiharibu Yuda, tangu alipomwambia kwamba atampatia wazao.
Cependant, l'Éternel ne voulut pas détruire Juda, à cause de David, son serviteur, car il lui avait promis de lui donner une lampe pour ses enfants, pour toujours.
20 Katika siku za Yoramu, Edomu akaasi kutoka chini ya mkono wa Yuda, na wakamfanya mfalme juu yao wenyewe.
De son temps, Édom se révolta de dessous la main de Juda, et se fit un roi.
21 Basi Yehoramu akaenda na maamri jeshi na magari ya farasi yote. Ilitokea kwamba akaamka usiku na kushambulia na kuwazunguka Waedomu, waliokuwa wamemzunguka na wale maamri jeshi wa magari ya farasi. Ndipo wanajeshi wa Yehoramu wakakimbilia wajumbani kwao.
Et Joram passa à Zaïr, et tous ses chars avec lui; et il se leva de nuit et frappa les Édomites qui l'entouraient avec les chefs des chars; et le peuple s'enfuit dans ses tentes.
22 Hivyo Edomu aliasi dhidi ya utawala wa Yuda katika siku hizi. Libna pia aliasi katika kipindi hicho hicho.
Ainsi Édom se révolta de dessous la main de Juda jusqu'à ce jour. En même temps, Libna se révolta.
23 Kwa mambo mengine yamhusuyo Yehoramu, yote aliyoyafanya, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Yuda?
Le reste des actes de Joram, et tout ce qu'il a fait, n'est-ce pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
24 Yehoramu akafa na kuzikwa pamoja na baba zake, na akalala pamoja na baba zake katika mji wa Daudi. Ndipo Ahazi mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.
Joram se coucha avec ses pères et fut enterré avec ses pères dans la ville de David; et Achazia, son fils, régna à sa place.
25 Katika mwaka wa kumi na mbili wa Yohoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.
La douzième année de Joram, fils d'Achab, roi d'Israël, Achazia, fils de Joram, roi de Juda, commença à régner.
26 Ahazi alikuwa ana umri wa miaka ishirini na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala kwa mda wa mwaka mmoja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Athalia; alikuwa mtoto wa Omri, mfalme wa Israeli.
Achazia avait vingt-deux ans lorsqu'il devint roi, et il régna un an à Jérusalem. Le nom de sa mère était Athalie, fille d'Omri, roi d'Israël.
27 Ahazia alitembelea katika nyumba ya Ahabu; alifanya yale yaliyo maovu katika uso wa Yahwe, kama nyumba ya Ahabu ilivyokuwa ikifanya, kwa kuwa Ahazia alikuwa mkwe kwenye nyumba ya Aabu.
Il marcha dans la voie de la maison d'Achab et fit ce qui est mal aux yeux de Yahvé, comme la maison d'Achab, car il était le gendre de la maison d'Achab.
28 Ahazia akaenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu, kupigana dhidi ya Hazaeli, mfalme wa Shamu, katika Ramath Geleadi. Washami wakamjeruhi Yoramu.
Il alla avec Joram, fils d'Achab, à la guerre contre Hazaël, roi de Syrie, à Ramoth Galaad, et les Syriens blessèrent Joram.
29 Mfalme Yoramu akarudi ili auguzwe huko Yezreeli kwenye yale majeraha ambayo Washami walimpatia huko Rama. Wakati alipopigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Hivyo Ahazi mwana wa Yehoramu, mfalme Yuda, akashuka kwa Yezreeli kumuona Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu Yoramu alikuwa amejeruhiwa.
Le roi Joram revint se faire guérir à Jizreel des blessures que les Syriens lui avaient faites à Rama, lorsqu'il combattait contre Hazaël, roi de Syrie. Achazia, fils de Joram, roi de Juda, descendit voir Joram, fils d'Achab, à Jizreel, car il était malade.

< 2 Wafalme 8 >