< 2 Wafalme 6 >
1 Wana wa manabii wakamwambia Elisha, “Sehemu ambayo tunayoishi na wewe ni ndogo sana kwa ajili ya wote.
Et les fils des prophètes dirent à Élisée: Tu vois que le lieu où nous habitons devant toi est trop étroit pour nous.
2 Tafadhali, tuache tuende Yordani, na umwache kila mtu akate mti hapo ambako tunaweza kuishi.” Elisha akajibu, “unaweza kwenda mbele.”
Allons, s’il te plaît, jusqu’au Jourdain, et nous y prendrons chacun une pièce de bois, et nous y bâtirons un lieu pour y habiter. Et il dit: Allez.
3 Mmoja wao akasema, “Nenda na watumishi wako tafadhali.” Elisha akajibu, “Nitaenda.”
Et l’un d’eux dit: Consens, je te prie, à venir avec tes serviteurs. Et il dit: J’irai.
4 Kwa hiyo akaenda pamoja nao, na wakati walipokuja Yordani, wakaanza kukata miti.
Et il alla avec eux; et ils vinrent au Jourdain, et coupèrent des arbres.
5 Lakini mmoja wao alipokuwa akikata, kichwa cha shoka kikaangukia kwenye maji; akalia kwa sauti na kusema, “la hasha, bwana wangu, kilikuwa kimeazimwa!”
Et il arriva, comme l’un d’eux abattait une pièce de bois, que le fer tomba dans l’eau; et il s’écria et dit: Hélas, mon maître! il était emprunté!
6 Basi mtu wa Mungu akasema, “kiliangukia wapi?” Yule mtu akamwonyesha Elisha ile sehemu. akakata fimbo, akarusha kwenye maji, na kufanya chuma kuelea.
Et l’homme de Dieu dit: Où est-il tombé? Et il lui montra l’endroit; et [Élisée] coupa un morceau de bois, et l’y jeta, et fit surnager le fer;
7 Elisha akasema, “Kichukue.” Basi yule mtu akafikisha mkono wake na kukinyakua.
et il dit: Enlève-le. Et il étendit sa main, et le prit.
8 Basi mfalme wa Shamu alikuwa akipigana vita dhidi ya Israel. Akafanya shauri na watumishi wake, akisema, “kambi yangu itakuwa sehemu flani na flani.”
Or le roi de Syrie faisait la guerre contre Israël; et il tint conseil avec ses serviteurs, disant: En tel et tel lieu sera mon camp.
9 Basi huyo mtu wa Mungu akamtuma kwa mfalme wa Israeli, akisema, “Kuwa makini usipite ile sehemu, kwa kuwa ndipo Washamu wanakoshukia hapo.”
Et l’homme de Dieu envoya au roi d’Israël, disant: Garde-toi de passer par ce lieu-là; car les Syriens y sont descendus.
10 Mfalme wa Israeli akatuma mjumbe kwenda pale sehemu ambayo mtu wa Mungu alipaongelea na kumtahadharisha. Zaidi ya mara moja au mbili, wakati mfalme alipoenda pale, alikuwa kwenye ulinzi wake.
Et le roi d’Israël envoya au lieu au sujet duquel l’homme de Dieu lui avait parlé et l’avait averti, et il y fut gardé. [Cela eut lieu] non pas une fois, ni deux fois.
11 Huyo mfalme wa Shamu alikasirishwa kuhusu haya maonyo, na akawaita watumishi wake na kuwaambia, “Je hamtaniambia ni nani miongoni mwetu aliye upande wa Israeli?”
Et le cœur du roi de Syrie fut agité à cause de cela; et il appela ses serviteurs, et leur dit: Ne me déclarerez-vous pas qui d’entre nous est pour le roi d’Israël?
12 Hivyo mmoja wa watumishi wake akasema, “Hapana, bwana wangu, mfalme, kwa ajili ya Elisha yule nabii katika Israeli humwambia yule mfalme wa Israeli maneno ambayo uyaongeayo kwenye kitanda chako cha kulala!”
Et l’un de ses serviteurs [lui] dit: Personne, ô roi, mon seigneur! mais Élisée, le prophète qui est en Israël, déclare au roi d’Israël les paroles que tu dis dans ta chambre à coucher.
13 Yule mfalme akajibu, “Nenda na uone Elisha alipo hivyo naweza kutuma watu na kumkamata.” Akaambiwa, “Tazama yuko Dothani.”
Et il dit: Allez, et voyez où il est, et j’enverrai et je le prendrai. Et on lui rapporta, disant: Le voilà à Dothan.
14 Kwa hiyo yule mfalme akatuma farasi kwenda Donathi, magari ya farasi, na jeshi kubwa. Wakaja usiku na kuzunguka ule mji.
Et il y envoya des chevaux, et des chars, et de grandes forces; et ils allèrent de nuit, et environnèrent la ville.
15 Wakati yule mtumishi wa mtu wa Mungu alipoamka mapema na kutoka nje, kumbe, jeshi kubwa pamoja na farasi na magari ya farasi yameuzunguka mji. Mtumishi wake akamwabia, “Kumbe, bwana wangu! Tutafanya nini?”
Et celui qui servait l’homme de Dieu se leva de bon matin et sortit: et voici, une armée entourait la ville, et des chevaux, et des chars. Et son jeune homme lui dit: Hélas! mon seigneur, comment ferons-nous?
16 Elisha akajibu, “usiogope, wale walio na sisi ni zaidi kuliko wale walio nao.”
Et il dit: Ne crains pas; car ceux qui sont avec nous sont en plus grand nombre que ceux qui sont avec eux.
17 Elisha akajibu na kusema, “Yahwe, nakuomba kwamba utamfungua macho yake ili kwamba aweze kuona.” Ndipo Yahwe alipofungua macho ya mtumishi, na akaona. Kumbe, ule mlima ulikuwa umejaa farasi na magari ya farasi ya moto yamemzunguka Elisha!
Et Élisée pria, et dit: Éternel, je te prie, ouvre ses yeux, afin qu’il voie. Et l’Éternel ouvrit les yeux du jeune homme, et il vit: et voici la montagne était pleine de chevaux et de chars de feu autour d’Élisée.
18 Wakati hao Washami walipomshukia chini, Elisha aliomba kwa Yahwe na kusema, “Uwapige hawa watu kwa upofu, nakuomba.” Hivyo Yahwe akawafanya vipofu, kama Elisha alivyoomba.
Et [les Syriens] descendirent vers Élisée; et il pria l’Éternel, et dit: Je te prie, frappe cette nation de cécité. Et il les frappa de cécité, selon la parole d’Élisée.
19 Kisha Elisha akawaambia Washami, “Hii njia sio, pia mji huu sio. Nifuateni mimi, na nitawaleta kwa yule mtu ambaye mnayemtafuta.” Ndipo akawaongoza kweda Samaria.
Et Élisée leur dit: Ce n’est pas ici le chemin, et ce n’est pas ici la ville; venez après moi, et je vous mènerai vers l’homme que vous cherchez. Et il les mena à Samarie.
20 Hata walipokwisha kufika Samaria, Elisha akasema, “Yahwe, fungua macho ya hawa watu ili waweze kuona.” Yahwe akawafungua macho yao na wakaona, na kumbe, walikuwa katikati ya mji wa Samaria.
Et il arriva, quand ils furent entrés à Samarie, qu’Élisée dit: Éternel, ouvre les yeux à ces [hommes], afin qu’ils voient. Et l’Éternel ouvrit leurs yeux, et ils virent: et voici, [ils étaient] au milieu de Samarie.
21 Yule mfalme wa Israeli akamwambia Elisha, wakati alipowaona, “Baba yangu, niwaue? Niwaue?”
Et le roi d’Israël dit à Élisée, quand il les vit: Frapperai-je, frapperai-je, mon père?
22 Elisha akajibu, “Usiwaue. Ungeweza kuwaua wale ambao uliokuwa umewachukua mateka kwa upanga na upinde wako? Weka mkate na maji mbele yao, ili kwamba waweze kula na kunywa, na kwenda kwa bwana wao.”
Et il dit: Tu ne frapperas point; ceux que tu aurais faits captifs avec ton épée et ton arc, les frapperais-tu? Mets du pain et de l’eau devant eux; et qu’ils mangent et boivent, et qu’ils s’en aillent vers leur seigneur.
23 Ndipo mfalme akaandaa chakula kingi kwa ajili yao, na wakati walipokula na kunywa, akawapeleka mbali, na walirudi kwa bwana wao. Lile kundi la jeshi la Wasahami halikurudi kwa mda mrefu katika nchi ya Israeli.
Et il leur prépara un grand festin, et ils mangèrent et burent; et il les renvoya, et ils s’en allèrent vers leur seigneur. Et les bandes des Syriens ne revinrent plus dans le pays d’Israël.
24 Baadaye baada ya huyu Ben Hadadi mfalme wa Shamu kukusanya majeshi yake yote na kuiteka Samaria na kuizingira.
Et il arriva, après cela, que Ben-Hadad, roi de Syrie, rassembla toute son armée, et monta, et assiégea Samarie.
25 Hivyo kulikuwa na njaa kubwa katika Samaria. Kumbe, wakauzingira hadi kichwa cha punda kilipouzwa kwa vipande themanini vya fedha, na sehemu ya nne ya sehemu ya kibaba cha kinyesi cha njiwa kwa vipande vitano vya fedha.
Et il y eut une grande famine dans Samarie; et voici, ils la serraient de près, jusqu’à ce que la tête d’un âne fut à 80 [sicles] d’argent, et le quart d’un kab de fiente de pigeon à cinq [sicles] d’argent.
26 Wakati mfalme wa Israeli alipokuwa akipita karibu na ukuta, mwanamke mmoka akamlilia akisema, “Nisaidie, bwana wangu, mfalme.”
Et il arriva, comme le roi d’Israël passait sur la muraille, qu’une femme lui cria, disant: Sauve-moi, ô roi, mon seigneur!
27 Akasema, “Kama Yahwe hawezi kukusaidia, je nitakusaidiaje? je kuna kitu chochote kinakuja kutoka sehemu ya kupuria nafaka au shinikizoni?”
Et il dit: Si l’Éternel ne te sauve pas, comment te sauverais-je? Serait-ce au moyen de l’aire ou de la cuve?
28 Mfalme akaendelea, “Nini kinakusumbua?” Akajibu, “Huyu mwanamke ameniambia, 'Mtoe mtoto wako ili tuweze kumla leo, na tutamla wakwangu kesho.”
Et le roi lui dit: Qu’as-tu? Et elle dit: Cette femme-là m’a dit: Donne ton fils, et nous le mangerons aujourd’hui; et demain nous mangerons mon fils.
29 Hivyo tulimchemsha mtoto wangu na kumla, na siku ya pili yake nikamwambia, “Mtoe mtoto wako ili tuweze kumla, lakini alikuwa amemficha mtoto wake.”
Et nous avons bouilli mon fils, et nous l’avons mangé; et le jour après, je lui ai dit: Donne ton fils, et nous le mangerons. Et elle a caché son fils.
30 Basi mfalme aliposikia yale maneno ya yule mwanamke, akayachana mavazi yake (sasa alikuwa akitembelea kwenye ukuta), na watu wakatazama na kuona kwamba alikuwa amevaa nguo ya gunia chini, dhidi ya ngozi yake.
Et aussitôt que le roi entendit les paroles de la femme, il déchira ses vêtements. Et comme il passait sur la muraille, le peuple le vit: et voici, il avait un sac sur sa chair, en dedans.
31 Kisha akasema, “Mungu afanye hivyo kwangu, na zaidi pia, kama kichwa cha Elisha mwana wa Shafati kitabaki juu yake leo.”
Et [le roi] dit: Ainsi Dieu me fasse, et ainsi il y ajoute, si la tête d’Élisée, fils de Shaphath, demeure sur lui aujourd’hui!
32 Basi Elisha alikuwa ameketi kwenye nyumba yake, na wazee walikuwa wamekaa pamoja naye. Yule mfalme akamtuma mtu wa mbele yake, lakini wakati mjumbe alipokuja kwa Elisha, akawaambia wazee, “Ona jinsi huyu mwana wa muuaji alivytumwa kuchukua kichwa changu? Tazama, wakati yule mjumbe atakapokuja, funga mlango, na uushikilie huo mlango funga dhidi yake asiingie. Je sio sauti ya bwana wake nyuma mguuni pake?”
Et Élisée était assis dans sa maison, et les anciens étaient assis avec lui, et [le roi] envoya un homme devant lui. Avant que le messager arrive auprès de lui, [Élisée] dit aux anciens: Voyez-vous que ce fils d’un meurtrier envoie pour m’ôter la tête? Voyez quand le messager entrera; fermez la porte, et repoussez-le avec la porte: n’est-ce pas le bruit des pieds de son maître après lui?
33 Wakati alipokuwa bado akiongea pamoja nao, kumbe, yule mjumbe alishuka kwake. Mfalme akasema, “Kumbe, masumbuko haya yatoka kwa Yahwe. Kwa nini nimsubiri Yahwe tena?”
Il parlait encore avec eux, quand voici, le messager descendit vers lui. Et [le roi] dit: Voici, ce mal est de par l’Éternel; pourquoi m’attendrais-je encore à l’Éternel?