< 2 Wafalme 6 >
1 Wana wa manabii wakamwambia Elisha, “Sehemu ambayo tunayoishi na wewe ni ndogo sana kwa ajili ya wote.
Les fils des prophètes dirent à Élisée: « Voici, le lieu où nous habitons et où nous nous réunissons avec toi est trop petit pour nous.
2 Tafadhali, tuache tuende Yordani, na umwache kila mtu akate mti hapo ambako tunaweza kuishi.” Elisha akajibu, “unaweza kwenda mbele.”
Je t'en prie, allons jusqu'au Jourdain, et que chacun prenne une poutre de là, et que nous nous fassions là un lieu où nous pourrons vivre. » Il a répondu: « Vas-y! »
3 Mmoja wao akasema, “Nenda na watumishi wako tafadhali.” Elisha akajibu, “Nitaenda.”
L'un d'eux dit: « Je vous prie de bien vouloir accompagner vos serviteurs. » Il répondit: « Je vais y aller. »
4 Kwa hiyo akaenda pamoja nao, na wakati walipokuja Yordani, wakaanza kukata miti.
Il partit donc avec eux. Lorsqu'ils arrivèrent au Jourdain, ils coupèrent du bois.
5 Lakini mmoja wao alipokuwa akikata, kichwa cha shoka kikaangukia kwenye maji; akalia kwa sauti na kusema, “la hasha, bwana wangu, kilikuwa kimeazimwa!”
Mais comme l'un d'eux abattait un arbre, la tête de la hache tomba dans l'eau. Alors il s'écria: « Hélas, mon maître! Car il a été emprunté. »
6 Basi mtu wa Mungu akasema, “kiliangukia wapi?” Yule mtu akamwonyesha Elisha ile sehemu. akakata fimbo, akarusha kwenye maji, na kufanya chuma kuelea.
L'homme de Dieu demanda: « Où est-elle tombée? » Il lui montra l'endroit. Il coupa un bâton, le jeta dedans et fit flotter le fer.
7 Elisha akasema, “Kichukue.” Basi yule mtu akafikisha mkono wake na kukinyakua.
Il dit: « Prends-le. » Il tendit la main et le prit.
8 Basi mfalme wa Shamu alikuwa akipigana vita dhidi ya Israel. Akafanya shauri na watumishi wake, akisema, “kambi yangu itakuwa sehemu flani na flani.”
Or le roi de Syrie était en guerre contre Israël; il tenait conseil avec ses serviteurs, disant: « Mon camp sera dans tel ou tel endroit. »
9 Basi huyo mtu wa Mungu akamtuma kwa mfalme wa Israeli, akisema, “Kuwa makini usipite ile sehemu, kwa kuwa ndipo Washamu wanakoshukia hapo.”
L'homme de Dieu envoya dire au roi d'Israël: « Prends garde de ne pas passer par ce lieu, car les Syriens y descendent. »
10 Mfalme wa Israeli akatuma mjumbe kwenda pale sehemu ambayo mtu wa Mungu alipaongelea na kumtahadharisha. Zaidi ya mara moja au mbili, wakati mfalme alipoenda pale, alikuwa kwenye ulinzi wake.
Le roi d'Israël se rendit au lieu que l'homme de Dieu lui avait indiqué et dont il l'avait averti, et il s'y sauva, ni une fois ni deux.
11 Huyo mfalme wa Shamu alikasirishwa kuhusu haya maonyo, na akawaita watumishi wake na kuwaambia, “Je hamtaniambia ni nani miongoni mwetu aliye upande wa Israeli?”
Le cœur du roi de Syrie fut très troublé à ce sujet. Il appela ses serviteurs et leur dit: « Ne me montrerez-vous pas lequel d'entre nous est pour le roi d'Israël? »
12 Hivyo mmoja wa watumishi wake akasema, “Hapana, bwana wangu, mfalme, kwa ajili ya Elisha yule nabii katika Israeli humwambia yule mfalme wa Israeli maneno ambayo uyaongeayo kwenye kitanda chako cha kulala!”
Un de ses serviteurs dit: « Non, mon seigneur, ô roi; mais Élisée, le prophète qui est en Israël, rapporte au roi d'Israël les paroles que tu prononces dans ta chambre. »
13 Yule mfalme akajibu, “Nenda na uone Elisha alipo hivyo naweza kutuma watu na kumkamata.” Akaambiwa, “Tazama yuko Dothani.”
Il dit: « Va voir où il est, afin que j'envoie le chercher. » On lui a dit: « Voici, il est à Dothan. »
14 Kwa hiyo yule mfalme akatuma farasi kwenda Donathi, magari ya farasi, na jeshi kubwa. Wakaja usiku na kuzunguka ule mji.
Il y envoya donc des chevaux, des chars et une grande armée. Ils arrivèrent de nuit et entourèrent la ville.
15 Wakati yule mtumishi wa mtu wa Mungu alipoamka mapema na kutoka nje, kumbe, jeshi kubwa pamoja na farasi na magari ya farasi yameuzunguka mji. Mtumishi wake akamwabia, “Kumbe, bwana wangu! Tutafanya nini?”
Le serviteur de l'homme de Dieu s'était levé tôt et était sorti, et voici qu'une armée avec des chevaux et des chars entourait la ville. Son serviteur lui dit: « Hélas, mon maître! Que ferons-nous? »
16 Elisha akajibu, “usiogope, wale walio na sisi ni zaidi kuliko wale walio nao.”
Il répondit: « N'aie pas peur, car ceux qui sont avec nous sont plus nombreux que ceux qui sont avec eux. »
17 Elisha akajibu na kusema, “Yahwe, nakuomba kwamba utamfungua macho yake ili kwamba aweze kuona.” Ndipo Yahwe alipofungua macho ya mtumishi, na akaona. Kumbe, ule mlima ulikuwa umejaa farasi na magari ya farasi ya moto yamemzunguka Elisha!
Élisée pria et dit: « Yahvé, ouvre-lui les yeux, afin qu'il voie. » Yahvé ouvrit les yeux du jeune homme, et il vit; et voici que la montagne était pleine de chevaux et de chars de feu autour d'Elisée.
18 Wakati hao Washami walipomshukia chini, Elisha aliomba kwa Yahwe na kusema, “Uwapige hawa watu kwa upofu, nakuomba.” Hivyo Yahwe akawafanya vipofu, kama Elisha alivyoomba.
Lorsqu'ils descendirent vers lui, Élisée pria Yahvé et dit: « Je te prie de frapper ce peuple de cécité. » Il les a frappés de cécité selon la parole d'Elisée.
19 Kisha Elisha akawaambia Washami, “Hii njia sio, pia mji huu sio. Nifuateni mimi, na nitawaleta kwa yule mtu ambaye mnayemtafuta.” Ndipo akawaongoza kweda Samaria.
Élisée leur dit: « Ce n'est pas ici le chemin, et ce n'est pas ici la ville. Suivez-moi, et je vous conduirai à l'homme que vous cherchez. » Il les conduisit en Samarie.
20 Hata walipokwisha kufika Samaria, Elisha akasema, “Yahwe, fungua macho ya hawa watu ili waweze kuona.” Yahwe akawafungua macho yao na wakaona, na kumbe, walikuwa katikati ya mji wa Samaria.
Lorsqu'ils furent entrés dans la Samarie, Élisée dit: « Yahvé, ouvre les yeux de ces hommes, afin qu'ils voient. » Yahvé leur ouvrit les yeux, et ils virent; et voici, ils étaient au milieu de la Samarie.
21 Yule mfalme wa Israeli akamwambia Elisha, wakati alipowaona, “Baba yangu, niwaue? Niwaue?”
Le roi d'Israël dit à Élisée, lorsqu'il les vit: « Mon père, dois-je les frapper? Dois-je les frapper? »
22 Elisha akajibu, “Usiwaue. Ungeweza kuwaua wale ambao uliokuwa umewachukua mateka kwa upanga na upinde wako? Weka mkate na maji mbele yao, ili kwamba waweze kula na kunywa, na kwenda kwa bwana wao.”
Il répondit: « Tu ne les frapperas pas. Frapperais-tu de ton épée et de ton arc ceux que tu as emmenés en captivité? Mets devant eux du pain et de l'eau, qu'ils mangent et boivent, puis va chez ton maître. »
23 Ndipo mfalme akaandaa chakula kingi kwa ajili yao, na wakati walipokula na kunywa, akawapeleka mbali, na walirudi kwa bwana wao. Lile kundi la jeshi la Wasahami halikurudi kwa mda mrefu katika nchi ya Israeli.
Il leur prépara un grand festin. Après qu'ils eurent mangé et bu, il les renvoya et ils s'en allèrent chez leur maître. Ainsi, les bandes de Syrie cessèrent d'attaquer le pays d'Israël.
24 Baadaye baada ya huyu Ben Hadadi mfalme wa Shamu kukusanya majeshi yake yote na kuiteka Samaria na kuizingira.
Après cela, Benhadad, roi de Syrie, rassembla toute son armée, monta et assiégea Samarie.
25 Hivyo kulikuwa na njaa kubwa katika Samaria. Kumbe, wakauzingira hadi kichwa cha punda kilipouzwa kwa vipande themanini vya fedha, na sehemu ya nne ya sehemu ya kibaba cha kinyesi cha njiwa kwa vipande vitano vya fedha.
Il y eut une grande famine à Samarie. On l'assiégea jusqu'à ce qu'on vendît la tête d'un âne pour quatre-vingts pièces d'argent et le quart d'un kab de fumier de colombe pour cinq pièces d'argent.
26 Wakati mfalme wa Israeli alipokuwa akipita karibu na ukuta, mwanamke mmoka akamlilia akisema, “Nisaidie, bwana wangu, mfalme.”
Comme le roi d'Israël passait sur la muraille, une femme lui cria: « Au secours, mon seigneur, ô roi! »
27 Akasema, “Kama Yahwe hawezi kukusaidia, je nitakusaidiaje? je kuna kitu chochote kinakuja kutoka sehemu ya kupuria nafaka au shinikizoni?”
Il dit: « Si Yahvé ne te secourt pas, où pourrais-je trouver du secours pour toi? De l'aire de battage, ou du pressoir? »
28 Mfalme akaendelea, “Nini kinakusumbua?” Akajibu, “Huyu mwanamke ameniambia, 'Mtoe mtoto wako ili tuweze kumla leo, na tutamla wakwangu kesho.”
Alors le roi lui demanda: « Quel est ton problème? » Elle répondit: « Cette femme m'a dit: 'Donne ton fils, pour que nous le mangions aujourd'hui, et nous mangerons mon fils demain'.
29 Hivyo tulimchemsha mtoto wangu na kumla, na siku ya pili yake nikamwambia, “Mtoe mtoto wako ili tuweze kumla, lakini alikuwa amemficha mtoto wake.”
Nous avons donc fait bouillir mon fils et nous l'avons mangé; et le lendemain, je lui ai dit: 'Donne ton fils, pour que nous le mangions'; et elle a caché son fils. »
30 Basi mfalme aliposikia yale maneno ya yule mwanamke, akayachana mavazi yake (sasa alikuwa akitembelea kwenye ukuta), na watu wakatazama na kuona kwamba alikuwa amevaa nguo ya gunia chini, dhidi ya ngozi yake.
Lorsque le roi entendit les paroles de la femme, il déchira ses vêtements. Or il passait sur la muraille, et le peuple regardait, et voici, il avait un sac en dessous de son corps.
31 Kisha akasema, “Mungu afanye hivyo kwangu, na zaidi pia, kama kichwa cha Elisha mwana wa Shafati kitabaki juu yake leo.”
Alors il dit: « Que Dieu me fasse ainsi, et plus encore, si la tête d'Élisée, fils de Shaphat, reste aujourd'hui sur lui. »
32 Basi Elisha alikuwa ameketi kwenye nyumba yake, na wazee walikuwa wamekaa pamoja naye. Yule mfalme akamtuma mtu wa mbele yake, lakini wakati mjumbe alipokuja kwa Elisha, akawaambia wazee, “Ona jinsi huyu mwana wa muuaji alivytumwa kuchukua kichwa changu? Tazama, wakati yule mjumbe atakapokuja, funga mlango, na uushikilie huo mlango funga dhidi yake asiingie. Je sio sauti ya bwana wake nyuma mguuni pake?”
Mais Élisée était assis dans sa maison, et les anciens étaient assis avec lui. Le roi envoya un homme de devant lui; mais avant que le messager n'arrive, il dit aux anciens: « Voyez-vous comment ce fils de meurtrier a envoyé enlever ma tête? Voici, quand le messager viendra, fermez la porte, et maintenez la porte fermée contre lui. Le bruit des pieds de son maître n'est-il pas derrière lui? »
33 Wakati alipokuwa bado akiongea pamoja nao, kumbe, yule mjumbe alishuka kwake. Mfalme akasema, “Kumbe, masumbuko haya yatoka kwa Yahwe. Kwa nini nimsubiri Yahwe tena?”
Comme il parlait encore avec eux, voici que le messager descendit vers lui. Et il dit: « Voici, ce malheur vient de Yahvé. Pourquoi attendrais-je Yahvé plus longtemps? »