< 2 Wafalme 3 >

1 Basi katika mwaka wa kumi na nane wa Yehoshefati mfalme wa Yuda, Yoramu mwana wa Ahabu alianza kutawala juu ta Israeli katika Samaria; alitawala miaka kumi na miwili.
Or la dix-huitième année de Josaphat Roi de Juda, Joram fils d'Achab avait commencé à régner sur Israël en Samarie, et il régna douze ans.
2 Alifanya yaliyo maovo usoni kwa Yahwe, lakini si kama baba yake na mama yake; kwa kuwa aliiondoa ile nguzo ya mungu wa Baali ambayo baba yake aliitengeneza.
Et fit ce qui déplaît à l'Eternel, non pas toutefois comme [avaient fait] son père et sa mère, car il ôta la statue de Bahal que son père avait faite.
3 Hata hivyo alishikilia dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli kufanya dhambi; wala hakuziacha mbali nao.
Mais il adhéra aux péchés de Jéroboam fils de Nébat, par lesquels il avait fait pécher Israël, [et] ne se détourna point d'aucun d'eux.
4 Basi Mesha mfalme wa Moabu alifuga kondoo. Alikuwa akimpatia mfalme wa Israeli kondoo 100, 000 na manyoya ya kondoo dume 100, 000.
Or Mésah, Roi de Moab, se mêlait de bétail, et payait au Roi d'Israël cent mille agneaux, et cent mille moutons [portant] laine.
5 Ila baada ya Ahabu kufa, yule mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli.
Mais aussitôt qu'Achab fut mort, il arriva que le Roi de Moab se rebella contre le Roi d'Israël.
6 Hivyo Mfalme Joramu alikaondoka Samaria katika muda huo kuwahamasisha Waisraeli wote kwa ajili ya vita.
C'est pourquoi le Roi Joram sortit ce jour-là de Samarie, et dénombra tout Israël.
7 Akatuma mjumbe kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda, akisema, “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je mtakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?” Yehoshafati akajibu, “Nitaenda. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
Puis il alla, et envoya vers Josaphat Roi de Juda, pour lui dire: Le Roi de Moab s'est rebellé contre moi, ne viendras-tu pas avec moi à la guerre contre Moab? et il répondit: J'y monterai; fais ton compte de moi comme de toi, de mon peuple comme de ton peuple, et de mes chevaux comme de tes chevaux.
8 Ndipo akasema, “Tutawashambulia kwa njia gani?” Yehoshafati akajibu, “Kwa njia ya jangwa la Edemu.
Ensuite il dit: Par quel chemin monterons-nous? Et il répondit: Par le chemin du désert d'Edom.
9 Hivyo huyo mfalme wa Israeli, Yuda, na Edomu wakazunguka kwa mda wa siku saba. Hapakuwa na maji kwa ajili ya jeshi lao, wala kwa farasi au wanyama.
Ainsi le Roi d'Israël, et le Roi de Juda, et le Roi d'Edom partirent, et tournoyèrent par le chemin durant sept jours, jusqu'à ce qu'ils n'eurent plus d'eau pour le camp, ni pour les bêtes qu'ils menaient.
10 Basi mfalme wa Israeli akasema, “Hii ni nini? Yahwe amewaita wafalme watatu ili kutekwa mikononi mwa Moabu?”
Et le Roi d'Israël dit: Ha! Ha! certainement l'Eternel a appelé ces trois Rois pour les livrer entre les mains de Moab.
11 Lakini Yehoshafati akasema, “je hakuna nabii wa Yahwe, ambaye tunaweza kufanya shauri kuhusu Yahwe kupitia yeye?” Mtumishi mmoja wa wafalme wa Israeli akajibu na kusema, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa, ambaye alikuwa akimimina maji kwenye mikono ya Eliya.”
Et Josaphat dit: N'y a-t-il point ici quelque Prophète de l'Eternel, afin que par son moyen nous consultions l'Eternel? Et un des serviteurs du Roi d'Israël répondit, et dit: Il y a ici Elisée fils de Saphat, qui versait de l'eau sur les mains d'Elie.
12 Yehoshafati akasema, “Neno la Yahwe liko pamoja nami.” Hivyo mfalme wa Israeli, Yehoshaphati, na mfalme wa Edomu wakashuka chini kwenda kwake.
Alors Josaphat dit: La parole de l'Eternel est avec lui; et le Roi d'Israël, et Josaphat, et le Roi d'Edom descendirent vers lui.
13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nifanye nini kwa ajili yako? Nenda kwa manabii wa baba na mama yako.” Ndipo mfalme wa Israeli akamwambia, “Hapana, kwa sababu Yahwe amewaita hawa wafalme watatu pamoja ili kuruhusu jeshi la Moabu liwateke.”
Mais Elisée dit au Roi d'Israël: Qu'y a-t-il entre moi et toi? va-t'en vers les prophètes de ton père, et vers les prophètes de ta mère. Et le Roi d'Israël lui répondit: Non; car l'Eternel a appelé ces trois Rois pour les livrer entre les mains de Moab.
14 Elisha akajibu, “Kama Yawhe wa majeshi aishivo, ambaye nimesimama mbele zake, hakika kama nisingemheshimu uwepo wa Yehoshafati mfalme wa Yeda, Nisingevuta usikivu kwako, au hata kukutazama.
Et Elisée dit: L'Eternel des armées, devant lequel je me tiens, est vivant, que si je n'avais de la considération pour Josaphat le Roi de Juda, je n'aurais aucun égard pour toi, et ne t'aurais même pas vu.
15 Lakini sasa niletee mwanamuziki.” Ndipo alipokuja mpiga muziki alipocheza, mkono wa Yahwe ukaja juu ya Elisha.
Mais maintenant amenez-moi un joueur d'instruments. Et comme le joueur jouait des instruments, la main de l'Eternel fut sur Elisée;
16 Akasema, “'Yahwe asema hivi, 'Fanya hili bonde la mto mkavu lijae mahandaki.'
Et il dit: Ainsi a dit l'Eternel: Qu'on coupe par des fossés toute cette vallée.
17 Kwa kuwa Yahwe asema hivi, 'Hutaona upepo, wala hamtaona mvua, bali hili bonde la mto litajaa maji, na mtakunywa, ninyi na mifugo yenu na wanyama wenu wote.'
Car ainsi a dit l'Eternel: Vous ne verrez ni vent, ni pluie, et néanmoins cette vallée sera remplie d'eaux, et vous boirez, vous et vos bêtes.
18 Hiki ni kitu rahisi usoni mwa Yahwe. Pia atawapa ushindi juu ya hao Wamoabu.
Encore cela est peu de chose pour l'Eternel; car il livrera Moab entre vos mains;
19 Mtaiteka kila ngome ya mji na kila mji mzuri, kukata kila mti mzuri, kusimamisha chemichemi zote za maji, na kuharibu kila sehemu nzuri ya nchi na miamba.”
Et vous détruirez toutes les villes fortes, et toutes les villes principales, et vous abattrez tous les bons arbres, et vous boucherez toutes les fontaines d'eaux, et vous gâterez avec des pierres tous les meilleurs champs.
20 Hivyo asubuhi karibia na mda wa kutoa sadaka ya kuteketeza, yakaja maji kutoka uelekeo wa Edomu; nchi ikajaa maji.
Il arriva donc au matin, environ l'heure qu'on offre l'oblation, qu'on vit venir des eaux du chemin d'Edom, en sorte que ce lieu-là fut rempli d'eaux.
21 Ndipo wakati Wamoabu wote waliposikia kwamba wafalme wamekuja kupigana dhidi yao, walikusanyika pamoja, wote waliotakiwa kubeba silaha, na wakasimama mpakani.
Or tous les Moabites ayant appris que ces Rois-là étaient montés pour leur faire la guerre, s'étaient assemblés à cri public, depuis tous ceux qui étaient en âge de porter les armes, et au-dessus, et ils se tinrent sur la frontière.
22 Walitembea asubuhi na mapema na jua likang'aa kwenye maji. Wakati Wamoabu walipoyaona yale maji yaliyowaelekea, yanaonekana mekundu kama damu.
Et le lendemain ils se levèrent de bon matin, et comme le soleil fut levé sur les eaux, les Moabites virent vis-à-vis d'eux les eaux rouges comme du sang.
23 Wakatamka kwa hasira, “Hii ni damu! Yamkini hao wafalme wameharibiwa, na wameuna wao kwa wao! Sasa basi, Moabu, ngoja tuende tukawateke nyara!”
Et ils dirent: C'est du sang; certainement ces Rois-là se sont entre-tués, et chacun a frappé son compagnon; maintenant donc, Moabites, au butin.
24 Wakati walipokuja kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakawashtukiza na kuwashambulia Wamoabi, ambao walikimbia mbele yao. Hilo jeshi la Israeli waliwakimbiza hao Wamoabu hadi kwao wakiwaua.
Ainsi ils vinrent au camp d'Israël, et les Israëlites se levèrent, et frappèrent les Moabites, lesquels s'enfuirent devant eux; puis ils entrèrent au pays, et frappèrent Moab.
25 Waliiharibu miji, na kila aina ya amani ya nchi kila mtu alirusha jiwe mpaka ulipojaa. Walizuia kila chemichemi ya maji na kukata chini miti mizuri yote. Kir-haresethi tu ndiyo ilichwa na mawe yake. Lakini hao maaskari wakawashambulia na makombeo wakiwazunguka na kuishambulia.
Ils détruisirent les villes; et chacun jetait des pierres dans les meilleurs champs, de sorte qu'ils les en remplirent; ils bouchèrent toutes les fontaines d'eaux, et abattirent tous les bons arbres, jusqu'à ne laisser que les pierres à Kir-haréseth, laquelle les tireurs de fronde environnèrent, et battirent.
26 Ndipo Mfalme Mesha wa Moabu alipoona kwamba ameshindwa, alichukua watu hodari wa upanga mia saba pamoja naye kwenda kwa mfalme wa Edomu, lakini walishindwa.
Et le Roi de Moab voyant qu'il n'était pas le plus fort, prit avec lui sept cents hommes dégainant l'épée, pour enfoncer jusqu'au Roi d'Edom; mais ils ne purent.
27 Ndipo akamchukua mtoto wake wa kwanza, ambaye angetawala baada ya yeye, na akamuudhi kwa kumtoa kama sadaka ya kuteketezwa juu ya ukuta. Hivyo, kulikuwa na hasira kubwa dhidi ya Israeli, na hao Waisraeli, na Jeshi la Israeli likamuacha mfalme Mesha na kurudi kwenye nchi yao.
Alors il prit son fils premier-né, qui devait régner en sa place, et l'offrit en holocauste sur la muraille, et il y eut une grande indignation en Israël; ainsi ils se retirèrent de lui, et s'en retournèrent en leur pays.

< 2 Wafalme 3 >