< 2 Wafalme 25 >

1 Ilitokea kwamba katika mwaka wa tisa wa utawala wa mfalme Sedekia, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya huo mwezi, Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuja pamoja na jeshi lake lote kwa ajili ya kupigana dhidi ya Yerusalemu. Akaweka kambi kuelekeana nayo, na wakajenga ukuta kuizunguka.
Alors, dans la neuvième année de son règne, le dixième mois et le dixième jour du mois, Nabuchodonozor, roi de Babylone, marcha avec toute son armée contre Jérusalem; il campa sous ses murs et on éleva des retranchements sur tout son circuit.
2 Hivyo mji huo ulizungukwa mpaka miaka kumi na moja ya utawala wa Sedekia.
La ville subit le siège jusqu’à la onzième année du règne de Sédécias.
3 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa huo mwaka, njaa ilikuwa kali sana kwenye huo mji kwamba hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu wa nchi.
Le neuf du mois, la famine sévit dans la ville et les gens du peuple manquèrent de pain.
4 Wakati huo ule mji ulikuwa umebomoka ndani, na wapiganaji wote wakakimbia usiku kwa njia ya lango kati ya kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wote wameuzunguka mji. Mfalme akaenda kuelekea upande wa Araba.
Alors la ville fut ouverte par une brèche; aussitôt tous les gens de guerre s’échappèrent de nuit par la porte du double rempart attenante au parc du roi, tandis que les Chaldéens cernaient la ville, et prirent la direction de la Plaine.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuata mfalme Sedekia na kumchukua katika tambarare ya bonde la Mto Yoradani karibu na Yeriko. Jeshi lake lote lilitawanyika wakamwacha.
L’Armée chaldéenne se mit à la poursuite du roi et l’atteignit dans la plaine de Jéricho, alors que sa propre armée s’était débandée en l’abandonnant.
6 Wakamkamata mfalme na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, ambapo walipitisha hukumu juu yake.
On fit le roi prisonnier et on l’amena auprès du roi de Babylone à Ribla, où l’on prononça sa sentence.
7 Kama kwa watoto wa Sedekia, wakawachinja mbele ya macho yake. Kisha akamtoa macho Sedekia, wakamfunga pingu, na kumpeleka hadi Babeli.
D’Abord on égorgea les fils de Sédécias à sa vue, puis on lui creva les yeux, on le jeta dans les fers et on le transporta à Babylone.
8 Basi katika mwezi wa tano, katika siku ya saba ya mwezi, ambapo ulikuwa mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, mtumishi wa mfalme wa Babeli na amrijeshi wa walinzi wake, wakaja hadi Yerusalemu.
Le septième jour du cinquième mois, qui correspond à la dix-neuvième année du règne de Nabuchodonozor, roi de Babylone, Nebouzaradan, chef des gardes, serviteur du roi de Babylone, entra dans Jérusalem.
9 Akaichoma moto nyumba ya Yahwe, nyumba ya mfalme, na nyumba zote za Yeruselemu; pia kila jengo la muhimu katika mji akayachoma.
Il mit le feu au temple du Seigneur et au palais du roi; de même, il livra aux flammes toutes les maisons de Jérusalem, à savoir toute maison d’un personnage important.
10 Kama kwa kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu, jeshi lote la Wababeli ambao walikuwa chini ya amrishi wa walinzi wakaziharibu.
Et les remparts qui entouraient Jérusalem, toute l’armée chaldéenne, placée sous les ordres du chef des gardes, les démolit.
11 Basi watu waliokuwa wamebaki ambao walikuwa wameondoka katika mji, wale waliokuwa wameasi kwa mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu-Nebuzadani, amiri jeshi wa mlinzi, wakachukuliwa kwenda utumwani.
Nebouzaradan, chef des gardes, envoya en exil le reste de la population qui était demeurée dans la ville, les transfuges qui s’étaient jetés entre les bras du roi de Babylone et le surplus de la multitude.
12 Lakini amiri jeshi wa mlinzi aliwaacha baadhi ya maskini wa nchi ili wafanye kazi kwenye shamba la mizabibu na kulima.
Le chef des gardes ne laissa dans le pays que des gens de la basse classe comme vignerons et laboureurs.
13 Na zile nguzo za shaba ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, na misimamio na bahari ya chuma ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, Wakaldayo wakazivunja vipande vipande na kubeba shaba kuirudisha Babeli.
Les colonnes d’airain qui se trouvaient dans la maison de Dieu, les supports et la Mer d’airain du temple, les Chaldéens les brisèrent et en emportèrent l’airain à Babylone.
14 Masufuria, mabeleshi, makasi, vijiko, na vyombo vyote vya shaba ambavyo kuhani alivyokuwa amevitunza kwenye hekalu-Wakaldayo wakavichukua vyote.
Ils prirent aussi les cendriers, les pelles, les couteaux, les cuillers, et tous les ustensiles d’airain qui servaient au culte.
15 Masufuria ya kuhamisha majivu na mabakuli ambayo yalikuwa yametengenezwa kwa dhahabu, na yale yaliyotengenezwa kwa fedha-yule nahodha wa mlinzi wa mfalme akavichukua pia.
Le chef des gardes s’empara encore des brasiers et des bassins, tant en or qu’en argent.
16 Zile nguzo mbili, ile bahari, na vile vitako ambavyo Suleimani alivitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yahwe shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani.
Quant aux deux colonnes, à la Mer unique et aux supports que Salomon avait faits pour le temple du Seigneur, le poids de l’airain de tous ces objets ne peut être évalué.
17 Urefu wa ile nguzo ya kwanza ulikuwa ridhaa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake. Na urefu wa kichwa ulikuwa ridhaa tatu, pamoja na mapambo ya wavu na makomamanga yote yakizunguka kwenye hicho kichwa, vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa shaba. Na ile nguzo nyingine ilikuwa vivyo hivyo kama ile ya kwanza pamoja na wavu wake.
La hauteur d’une des colonnes était de dix-huit coudées; elle était surmontée d’un chapiteau d’airain haut de trois coudées et entouré d’un treillage et de grenades, le tout en airain. Telle la deuxième colonne, treillage compris.
18 Yule amiri jeshi wa mlinzi akamchukua Seraya kuhani mkuu, pamoja za Sefania, yule kuhani wa pili, na walinzi watatu wa kwenye lango.
Le chef des gardes s’assura de la personne de Seraïa, le grand-prêtre, de Cephania, le grand prêtre suppléant, et des trois gardiens du seuil.
19 Kutoka mjini akamchukua mlinzi, afisa mmoja ambaye aliyekuwa msimamizi wa maaskari, na watu watano ambao walikuwa wakimshauri mfalme, ambao walikuwa bado katika mji. Pia alimchukua mfungwa wa afisa jeshi la mfalme, kwa ajili ya kuandika watu kwenye jeshi, pamoja na watu sitini muhimu kutoka hiyo nchi ambao walikuwa katika mji.
Des habitants de la ville, il arrêta un officier, préposé aux gens de guerre, cinq des conseillers intimes du roi qui furent surpris dans la ville, le secrétaire, chef du recrutement, chargé d’enrôler la population du pays, ainsi que soixante hommes de cette population qui se trouvaient dans la ville.
20 Kisha Nebuzaradani, amiri wa mlinzi, akawachukua na kuwapeleka kwa mfalme Babeli huko Ribla.
Nebouzaradan, chef des gardes, emmena tous ces prisonniers et les conduisit au roi de Babylone à Ribla.
21 Mfalme wa Babeli akawaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Kwa njia hii, Yuda akaiacha nchi yake kwenda utumwani.
Le roi de Babylone les fit frapper et mettre à mort à Ribla, dans le district de Hamat. Ainsi s’accomplit l’exil de Juda loin de son sol.
22 Na wale watu waliokuwa wamebakia katika nchi ya Yuda, wale ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwaacha, akamuweka Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, msimamizi wao.
Quant à la population restée dans le pays de Juda, et que Nabuchodonozor, roi de Babylone, y avait laissée, il mit à sa tête Guedalia, fils d’Ahikam, fils de Chafan.
23 Kisha wakati maamiri wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemfanya Gedalia kuwa liwali, wakaenda kwa Gedalia huko Mispa. Hawa watu walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka-wao na watu wao.
Lorsque les chefs d’armée et leurs hommes apprirent que Nabuchodonozor avait nommé Ghedalia gouverneur, ils se rendirent auprès de celui-ci à Miçpa, à savoir Ismaël, fils de Netania, Johanan, fils de Karéah, Seraïa, fils de Tanhoumet, de Netofa, et Yaazania, fils du Maakhatite, eux et leurs hommes.
24 Gedalia akafanya kiapo kwa watu wake na kuwaambia, “Msiwaogope Wakaldayo. Muishi katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vema kwenu.”
Ghedalia leur fit un serment à eux et à leurs hommes en disant: "Ne craignez rien des serviteurs des Chaldéens; demeurez dans le pays, soyez soumis au roi de Babylone, et vous vous en trouverez bien."
25 Lakini ilitokea kwamba katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, kutoka familia ya kifalme, wakaja na watu kumi na kumshambulia Gedalia. Gedalia akafa, pamoja na watu wa Yuda na Wababeli ambao walikuwa pamoja nae huko Mizpa.
Mais le septième mois, Ismaël, fils de Netania, fils d’Elichama, de la race royale, vint accompagné de dix hommes, et ils frappèrent à mort Ghedalia, ainsi que les Judéens et les Chaldéens qui étaient avec lui à Miçpa.
26 Kisha wale watu wote, kutoka chini kwenda juu, na maamiri wa jeshi, wakainuka na kwenda Misri, kwasababu walikuwa wanawaogopa Wababeli.
Aussitôt tout le peuple, grands et petits, et les chefs d’armée se mirent en route et entrèrent en Egypte par crainte des Chaldéens.
27 Ilitokea baadaye katika mwaka wa thelathini na saba wa utumwa wa Yekonia mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, Evil-merodaki mfalme wa Babeli akamtoa Yekonia mfalme wa Yuda kutoka gerezani. Hii ilitokea katika mwaka ambao Evil-Merodaki alipoanza kutawala.
La trente-septième année de l’exil de Joïachin, roi de Juda, le douzième mois et le vingt-septième jour du mois, Evil-Merodac, roi de Babylone, dans l’année même de son avènement, gracia Joïachin, roi de Juda, et le libéra de la maison de détention.
28 Akaongea naye kwa ukarimu na kumpatia kiti kizuri zaidi kuliko kile cha wafalme wengine ambao walikuwa pamoja naye Babeli.
Il lui parla avec bienveillance et lui donna un siège placé au-dessus du siège des rois qui étaient avec lui à Babylone.
29 Evil-Merodaki akamvua Yekonia nguo za gerezani,
Il lui fit changer ses vêtements de détention et l’admit constamment à sa table, toute sa vie durant.
30 na Yekinia akala siku zote kwenye meza ya mfalme katika maisha yake yote yaliyokuwa yamebakia.
Son entretien, entretien permanent, lui fut assuré de la part du roi, suivant les besoins de chaque jour, tant qu’il vécut.

< 2 Wafalme 25 >