< 2 Wafalme 25 >

1 Ilitokea kwamba katika mwaka wa tisa wa utawala wa mfalme Sedekia, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya huo mwezi, Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuja pamoja na jeshi lake lote kwa ajili ya kupigana dhidi ya Yerusalemu. Akaweka kambi kuelekeana nayo, na wakajenga ukuta kuizunguka.
漆德克雅為王九年十月十日,巴比倫王拿步高率領全軍前進攻耶路撒冷,紮營圍城,在城四周建築了壁壘,
2 Hivyo mji huo ulizungukwa mpaka miaka kumi na moja ya utawala wa Sedekia.
圍攻京城,直到漆德克雅為王十一年。
3 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa huo mwaka, njaa ilikuwa kali sana kwenye huo mji kwamba hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu wa nchi.
是年四月九日,城中發生了嚴重的飢荒,當地人民已沒有食糧,
4 Wakati huo ule mji ulikuwa umebomoka ndani, na wapiganaji wote wakakimbia usiku kwa njia ya lango kati ya kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wote wameuzunguka mji. Mfalme akaenda kuelekea upande wa Araba.
京城遂被攻破。加加丁人還在圍攻城時,君王和全體士兵,夜間出了靠近御園的雙牆城門,逃往阿辣巴。
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuata mfalme Sedekia na kumchukua katika tambarare ya bonde la Mto Yoradani karibu na Yeriko. Jeshi lake lote lilitawanyika wakamwacha.
加色丁軍隊便追趕君王,在耶利哥曠野追上了;此時他的軍隊都已離開他散了。
6 Wakamkamata mfalme na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, ambapo walipitisha hukumu juu yake.
加色丁軍隊擒獲了君王,帶他去黎貝拉去見巴比倫王。巴比倫王就宣判他的罪案,
7 Kama kwa watoto wa Sedekia, wakawachinja mbele ya macho yake. Kisha akamtoa macho Sedekia, wakamfunga pingu, na kumpeleka hadi Babeli.
且在漆德克雅眼前殺了他的兒子,也剜了他的眼,給他帶上鎖鏈,送往巴比倫去。
8 Basi katika mwezi wa tano, katika siku ya saba ya mwezi, ambapo ulikuwa mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, mtumishi wa mfalme wa Babeli na amrijeshi wa walinzi wake, wakaja hadi Yerusalemu.
巴比倫王拿步高為王十九年五月七日,巴比倫王的大臣,衛隊長乃步匝辣當來到了耶路撒冷,
9 Akaichoma moto nyumba ya Yahwe, nyumba ya mfalme, na nyumba zote za Yeruselemu; pia kila jengo la muhimu katika mji akayachoma.
燒毀了上主的殿、王宮和耶路撒冷所有的民房;凡是高大的建築都用火燒了。
10 Kama kwa kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu, jeshi lote la Wababeli ambao walikuwa chini ya amrishi wa walinzi wakaziharibu.
跟隨衛長的所有加色丁軍隊,拆毀了耶路撒冷周圍是城牆。
11 Basi watu waliokuwa wamebaki ambao walikuwa wameondoka katika mji, wale waliokuwa wameasi kwa mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu-Nebuzadani, amiri jeshi wa mlinzi, wakachukuliwa kwenda utumwani.
城中剩下的人民和已投降巴比倫王的人,以及其餘的平民,衛隊長乃步匝辣當都擄了去,
12 Lakini amiri jeshi wa mlinzi aliwaacha baadhi ya maskini wa nchi ili wafanye kazi kwenye shamba la mizabibu na kulima.
只留下當地一部分最窮的平民作園丁和農夫。
13 Na zile nguzo za shaba ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, na misimamio na bahari ya chuma ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, Wakaldayo wakazivunja vipande vipande na kubeba shaba kuirudisha Babeli.
加色丁人又將上主殿前的銅柱,和上主殿內的銅座、銅海都打碎,把銅運往巴比倫;
14 Masufuria, mabeleshi, makasi, vijiko, na vyombo vyote vya shaba ambavyo kuhani alivyokuwa amevitunza kwenye hekalu-Wakaldayo wakavichukua vyote.
此外,鍋、鏟、蠟剪、香盤,以及行禮的一切銅器,全都帶走;
15 Masufuria ya kuhamisha majivu na mabakuli ambayo yalikuwa yametengenezwa kwa dhahabu, na yale yaliyotengenezwa kwa fedha-yule nahodha wa mlinzi wa mfalme akavichukua pia.
提爐、杯爵,凡是純金純銀的,衛隊長都拿走了。
16 Zile nguzo mbili, ile bahari, na vile vitako ambavyo Suleimani alivitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yahwe shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani.
撒羅滿為上主的殿所製造的兩根柱子,一個銅海和一些盆座,這一切器皿所用的銅,重量無法估計。
17 Urefu wa ile nguzo ya kwanza ulikuwa ridhaa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake. Na urefu wa kichwa ulikuwa ridhaa tatu, pamoja na mapambo ya wavu na makomamanga yote yakizunguka kwenye hicho kichwa, vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa shaba. Na ile nguzo nyingine ilikuwa vivyo hivyo kama ile ya kwanza pamoja na wavu wake.
一根柱子高十八肘,上端有同柱頭,高五肘,柱頭四周有網子和石榴,全是銅的;另一根柱子,也有網子。
18 Yule amiri jeshi wa mlinzi akamchukua Seraya kuhani mkuu, pamoja za Sefania, yule kuhani wa pili, na walinzi watatu wa kwenye lango.
隊長又擒獲了大司祭色辣雅、副大司祭責法尺雅和三個門丁;
19 Kutoka mjini akamchukua mlinzi, afisa mmoja ambaye aliyekuwa msimamizi wa maaskari, na watu watano ambao walikuwa wakimshauri mfalme, ambao walikuwa bado katika mji. Pia alimchukua mfungwa wa afisa jeshi la mfalme, kwa ajili ya kuandika watu kwenye jeshi, pamoja na watu sitini muhimu kutoka hiyo nchi ambao walikuwa katika mji.
由城中擄去了一個管理軍隊的宦官,五個在城內搜到的君王的親信,一個徵募當地人民的軍長的書記.和城中搜到的六十個當地平民。
20 Kisha Nebuzaradani, amiri wa mlinzi, akawachukua na kuwapeleka kwa mfalme Babeli huko Ribla.
衛隊長乃步匝辣當捉住他們,帶到黎貝拉去見巴比倫王;
21 Mfalme wa Babeli akawaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Kwa njia hii, Yuda akaiacha nchi yake kwenda utumwani.
巴比倫王就在哈瑪特地的黎貝拉將他們殺了;從此,猶大人由本鄉被擄去充軍。
22 Na wale watu waliokuwa wamebakia katika nchi ya Yuda, wale ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwaacha, akamuweka Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, msimamizi wao.
巴比倫王拿步高對留在猶大地的人民,派定了沙番的孫子,阿希甘的兒子革達里雅作他們的首長。
23 Kisha wakati maamiri wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemfanya Gedalia kuwa liwali, wakaenda kwa Gedalia huko Mispa. Hawa watu walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka-wao na watu wao.
眾軍長和他們的士兵一聽說巴比倫王委派了革達里雅為首長,乃塔尺雅的兒子依市瑪耳,卡勒亞的兒子約哈南,乃托法人堂胡默特的兒子色辣雅,瑪阿加人的兒子雅匝尼雅和他們的士兵,都來到米茲帕見革達里雅。
24 Gedalia akafanya kiapo kwa watu wake na kuwaambia, “Msiwaogope Wakaldayo. Muishi katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vema kwenu.”
革達里雅遂對他們和他們的士兵起誓說:「你們不要害怕加色丁人的臣僕,安心住在此地,服事巴比倫王,就必能相安無事」。
25 Lakini ilitokea kwamba katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, kutoka familia ya kifalme, wakaja na watu kumi na kumshambulia Gedalia. Gedalia akafa, pamoja na watu wa Yuda na Wababeli ambao walikuwa pamoja nae huko Mizpa.
但是到了七月,王家的後裔厄里沙瑪的孫子,乃塔尼雅的兒子依市瑪耳帶了十個人前來,殺了革達里雅,和與他同在米茲帕的猶大人及加色丁人。
26 Kisha wale watu wote, kutoka chini kwenda juu, na maamiri wa jeshi, wakainuka na kwenda Misri, kwasababu walikuwa wanawaogopa Wababeli.
於是所有的人民,不分貴賤大小和眾軍長,因為害怕加色丁人,都起身逃往埃及去了。
27 Ilitokea baadaye katika mwaka wa thelathini na saba wa utumwa wa Yekonia mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, Evil-merodaki mfalme wa Babeli akamtoa Yekonia mfalme wa Yuda kutoka gerezani. Hii ilitokea katika mwaka ambao Evil-Merodaki alipoanza kutawala.
猶大王耶苛尼雅被擄後第三十七年十二月二十七日,巴比倫王厄威耳默洛達客在他登極元年,大赦猶大王耶苛尼雅,放他出獄,
28 Akaongea naye kwa ukarimu na kumpatia kiti kizuri zaidi kuliko kile cha wafalme wengine ambao walikuwa pamoja naye Babeli.
親切與他交談,令他坐在與他一同在巴比倫的眾王之上。
29 Evil-Merodaki akamvua Yekonia nguo za gerezani,
耶苛尼雅脫去囚服,以後一生日日與王共進飲食。
30 na Yekinia akala siku zote kwenye meza ya mfalme katika maisha yake yote yaliyokuwa yamebakia.
他的生活費用,在他有生之日,每天不斷由巴比倫王供應。

< 2 Wafalme 25 >