< 2 Wafalme 23 >
1 Hivyo mfalme akawatuma wajumbe waliokuwa wamemzunguka wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.
Kral Yoşiya haber gönderip Yahuda ve Yeruşalim'in bütün ileri gelenlerini yanına topladı.
2 Kisha mfalme akapanda hadi kwenye nyumba ya Yahwe, na watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu pamoja naye, na makuhani, manabii, na watu wote, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Kisha akasoma katika masikioni kwao maneno yote ya kitabu cha agano ambalo lililokuwa limepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
Sonra Yahudalılar, Yeruşalim'de yaşayanlar, kâhinler, peygamberler, büyük küçük herkesle birlikte RAB'bin Tapınağı'na çıktı. RAB'bin Tapınağı'nda bulunmuş olan Antlaşma Kitabı'nı baştan sona kadar herkesin duyacağı biçimde okudu.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yahwe, kutembea pamoja na Yahwe na kukumbuka maagizo yake, kanuni zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kuthibitisha maneno ya hili agano ambalo lililokuwa limeandikwa kwenye hiki kitabu. Hivyo watu wote wakakubaliana kusimama kwenye agano
Sütunun yanında durarak RAB'bin yolunu izleyeceğine, buyruklarını, öğütlerini, kurallarını candan ve yürekten uygulayacağına, bu kitapta yazılı antlaşmanın koşullarını yerine getireceğine ilişkin RAB'bin huzurunda antlaşma yaptı. Bütün halk bu antlaşmayı onayladı.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia yule kuhani mkuu, makuhani chini yake, na walinzi wa lango watoe kwenye hekalu vyombo vilivyokuwa vimetengenezwa kwa ajili ya Baali na Ashera, na kwa ajili ya nyota zote za mbinguni. Akivichoma moto Yerusalimu kwenye mashamba ya bonde la Kidroni na kubeba majivu yake kwenda Betheli.
Kral Yoşiya Baal, Aşera ve gök cisimleri için yapılmış olan bütün eşyaları RAB'bin Tapınağı'ndan çıkarmak üzere Başkâhin Hilkiya'ya, kâhin yardımcılarına ve kapı nöbetçilerine buyruk verdi. Bunları Yeruşalim'in dışına çıkarıp Kidron Vadisi'nde yaktı, küllerini Beytel'e götürdü.
5 Akawaondoa makuhani waliokuwa wanaabudu miungu ambao wafalme wa Yuda waliwachagua ili kwa ajili ya kufukiza ubani katika mahali pa juu kwenye miji ya Yuda na sehemu zinazoizunguka Yerusalemu-wale waliokuwa wanchoma ubani kwa Baali, kwa juana kwa mwezi, kwa sayari, na kwa nyota zote za mbinguni.
Yahuda krallarının kentlerde ve Yeruşalim'in çevresindeki tapınma yerlerinde buhur yaksınlar diye atamış olduğu putperest kâhinleri, Baal'a, güneşe, aya, takımyıldızlara –bütün gök cisimlerine– buhur yakanları ortadan kaldırdı.
6 Akaiondoa Ashera kutoka kwenye hekalu la Yahwe, nje ya Yerusalemu hata bonde la Kidroni na kuichoma hapo. Akaipiga kwenye mavumbi na kuiyatupa yale mavumbi kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
Aşera putunu RAB'bin Tapınağı'ndan çıkarıp Yeruşalim'in dışında Kidron Vadisi'nde yaktı, ezip toza çevirdi. Bu tozu sıradan halkın mezarlarına serpti.
7 Akavisafisha vyumba vya makahaba ambao walikuwa kwenye hekalu la Yahwe, ambako wanawake waliposhonea nguo kwa ajili ya Ashera
Fuhuş yapan kadın ve erkeklerin RAB'bin Tapınağı alanındaki odalarını yıktı. Kadınlar orada Aşera için kumaş dokurlardı.
8 Yosia akawaleta makuhani wote nje ya miji ya Yuda na kupanajisi mahali pa juu ambako makuhani walipokuwa wakichomea ubani, kutoka Geba hata Bersheba. Akapaharibu mahala pa juu kwenye malango ambayo yaliyokuwa ya kuingilia kwenda kwenye lango la Yoshua (liwali wa mji), upande wa kushoto wa lango la mji.
Yoşiya Yahuda kentlerinden bütün kâhinleri getirtti. Geva'dan Beer-Şeva'ya kadar kâhinlerin buhur yaktıkları tapınma yerlerini kirletti. Adını kent yöneticisinden alan Yeşu Kapısı'nın girişinde, kentin ana kapısının solunda kalan kapılardaki tapınma yerlerini de yıktı.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu hawakuruhusiwa kuhudumu kwenye madhabahu ya Yahwe katika Yerusalemu, wakala mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Tapınma yerlerinin kâhinleri, Yeruşalim'deki RAB'bin sunağına çıkmaz, ancak öbür kâhinlerle birlikte mayasız ekmek yerlerdi.
10 Yosia akainajisi Tofethi, ambayo ipo kwenye bonde la Ben Hinomu, ili kwamba mtu yeyote asimuweke mtoto wake wa kiume au binti yake kwenye moto kama sadaka kwa Molaki.
Yoşiya, kimse oğlunu ya da kızını ilah Molek için ateşte kurban etmesin diye, Ben-Hinnom Vadisi'ndeki Tofet'i kirletti.
11 Akawachukua farasi ambao wafalme wa Yuda waliokuwa wametolewa kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye eneo la lango la uingilia kwenye hekalu la Yahwe, karibu na chumba cha Nathani Meleki, msimamizi mkuu wa nyumba ya mfalme. Yosia akayachoma yale magari ya farasi ya jua
Yahuda krallarının güneşe adamış olduğu atları RAB'bin Tapınağı'nın girişinden kaldırdı. Atlar tapınağın avlusunda, hadım Natan-Melek'in odasının yanındaydı. Yoşiya güneşe adanmış savaş arabalarını da ateşe verdi.
12 Yosia mfalme akayaharibu madhabahu yaliyokuwa kwenye dari ya juu ya chumba cha Ahazi, ambacho wafalme wa Yuda walikitengeneza, na madhabahu ambayo Manase aliyatengeneza kwenye behewa mbili za nyumba ya Yahwe. Yosia akazivunga vipande vipande na kuvitupa kwenye bonde la Kidroni.
Ahaz'ın yukarı odasının damında Yahuda krallarının yaptırdığı sunakları da, RAB'bin Tapınağı'nın iki avlusunda Manaşşe'nin yaptırdığı sunakları da yıktı; onları kırıp parçalayarak tozlarını Kidron Vadisi'ne saçtı.
13 Mfalme akapaangamiza mahali pa juu magharibi mwa Yerusalemu, kusini mwa mlima wa uharibifu ambapo Sulemani mfalme wa Israeli alipajenga kwa ajili ya Ashtorithi, chukizo la Wamoabu; sanamu za karaha za Wasidoni; kwa Kemoshi, sanamu za karaha wa Moabu; na kwa Moleki, sanamu wa karaha wa watu wa Amoni.
Yeruşalim'in doğusunda, Yıkım Dağı'nın güneyinde İsrail Kralı Süleyman'ın Saydalılar'ın iğrenç putu Aştoret, Moavlılar'ın iğrenç putu Kemoş ve Ammonlular'ın iğrenç putu Molek için yaptırmış olduğu tapınma yerlerini kirletti.
14 Akazivunja nguzo za jiwe kuwa vipande vipande na kuziangusha chini nguzo za Ashera na kuzijaza zile sehemu kwa mifupa ya watu.
Dikili taşları, Aşera putlarını parçaladı; yerlerini insan kemikleriyle doldurdu.
15 Yosia pia akaiteketeza kabisa madhabahu iliyokuwa Betheli na mahali pa juu ambako Yeroboamu mwana wa Nebati (ambaye aliwafanya Waisraeli kuasi) aliijenga. Pia aliichoma moto ile madhabahu na mahali pa juu na kupapiga hadi pakawa vumbi. Pia akaichoma moto nguzo ya Ashera.
Bundan başka İsrail'i günaha sürükleyen Nevat oğlu Yarovam'ın yaptırdığı Beytel'deki tapınma yerini ve sunağı bile yıktı. Tapınma yerini ateşe verip toz duman etti. Aşera putunu yaktı.
16 Yosia alipotazama kwenye lile eneo, akagundua kwamba yale makaburi yalikuwa juu ya mlima. Akawatuma watu kuichukua mifupa kutoka kwenye yale makaburi; kisha akaichoma kwenye madhabahu, akainajisi. Hii ilitokana na neno la Yahwe ambalo mtu wa Mungu aliliongea, yule mtu aliyekuwa ameongea haya mambo kabla.
Yoşiya çevresine bakındı. Tepedeki mezarları görünce, adamlarını gönderip mezarlardaki kemikleri çıkarttı. Olacakları önceden bildiren Tanrı adamının açıkladığı RAB'bin sözü uyarınca, kemikleri sunağın üzerinde yakarak sunağı kirletti.
17 Kisha akasema, “Ni ukumbusho wa nani ule ninao uona?” Mtu wa ule mji akamwambia, “Lile ni kaburi la mtu wa Mungu ambaye alikuja kutoka Yuda na kuongea kuhusu haya mambo ambayo ameyafanya dhidi ya madhabahu ya Betheli.”
Kral, “Orada görünen anıt nedir?” diye sordu. Kent halkı, “Orası Yahuda'dan gelen ve senin Beytel'deki sunağa yaptıklarını bildiren Tanrı adamının mezarıdır” diye yanıtladı.
18 Hivyo Yosia akasema, “Mwacheni. Mtu asihamishe mifupa yake.” Hivyo wakaacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya nabii ambaye alikuja kutoka Samaria.
Kral, “Ona dokunmayın” dedi, “Kimse onun kemiklerini rahatsız etmesin.” Böylece Tanrı adamının kemiklerine de, Samiriye'den gelmiş olan peygamberin kemiklerine de dokunmadılar.
19 Kisha Yosia akahamisha nyumba zote za mahali pa juu ambazo zilikuwa katika mji wa Samaria, ambazo wafalme wa Israeli walizokuwa wamezitengeneza, na ambazo zilizokuwa zimemgadhabisha Yahwe kwa hasira.
Yoşiya Beytel'de yaptığı gibi, İsrail krallarının Samiriye kentlerinde yaptırdığı RAB'bi öfkelendiren tapınma yerlerindeki bütün yapıları ortadan kaldırdı.
20 Aliwafanyia kile ambacho kilikuwa kimefanyika katika Betheli. Aliwachinja makuhani wote wa mahali pa juu ya madhabahu na aliichoma mifupa ya watu juu yao. Kisha akarudi Yerusalemu.
O kentlerdeki tapınma yerlerinin bütün kâhinlerini sunakların üzerinde kurban etti. Sunakların üzerinde insan kemikleri yaktıktan sonra Yeruşalim'e döndü.
21 Kisha mfalme akawaamuru watu wote, akisema, “Itunzeni Pasaka ya Yahwe Mungu wenu, kama ilivyoandikwa kwenye hiki kitabu cha agano.”
Kral, “Tanrınız RAB için Fısıh Bayramı'nı bu Antlaşma Kitabı'nda yazılanlara uygun biçimde kutlayın” diye halka buyruk verdi.
22 Hiyo Pasaka haijawahi kufanyika tangu siku za waamuzi ambao waliiongoza Israeli, wala katika siku zote za wafalme wa Israeli au Yuda.
İsrail'e önderlik etmiş olan hâkimler döneminden bu yana, ne İsrail, ne de Yahuda kralları döneminde, böyle bir Fısıh Bayramı kutlanmamıştı.
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia hii Pasaka ya Yahwe ilisheherekewa katika Yerusalemu.
RAB için düzenlenen bu Fısıh Bayramı Kral Yoşiya'nın krallığının on sekizinci yılında Yeruşalim'de kutlandı.
24 Yosia pia akawafukuza wale ambao waliokuwa wameongea na wafu au na roho. Pia aliifukuza miungu ya sananmu, sanamu, na vitu vyote ambavyo ni chukizo vilivyokuwa vinaonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, hivyo kwa kuthibitisha yale maneno ya sheria ambayo iliyokuwa imeandikwa kwenye kitabu cha Hilkia yule kuhani aliyekuwa amepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
Bundan başka Yoşiya, Kâhin Hilkiya'nın RAB'bin Tapınağı'nda bulduğu kitapta yazılı yasanın ilkelerini yerine getirmek amacıyla, cincileri, ruhçuları, aile putlarını, öteki putları, ayrıca Yahuda ve Yeruşalim'de görülen bütün iğrençlikleri silip süpürdü.
25 Kabla ya Yosia, hapakuwa na mfalme kama yeye, aliyekuwa amemwelekea yahwe kwa moyo wake wote, roho yake yote, na nguvu zake zote, ambaye alifuata sheria zote za Musa. Hapakuwa na mfalme kama Yosia aliyeinuka baada ya yeye.
Ne ondan önce, ne de sonra onun gibi candan ve yürekten var gücüyle RAB'be yönelen ve Musa'nın yasasına uyan bir kral çıktı.
26 Walakini, Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake, ambayo ilikuwa dhidi ya Yuda kwa waabudu wapagani wote pamoja ambao Manase aliokuwa amemgadhibisha.
Oysa Manaşşe işlediği suçlarla RAB'bi öyle öfkelendirmişti ki, RAB Yahuda'ya karşı alevlenen öfkesinden vazgeçmedi
27 Hivyo Yahwe akasema, “Pia nitaiondoa Yuda usoni kwangu, kama nilivyoiondoa Israeli, na nitautupilia mbali huu mji ambao nilio uchagua, Yerusalemu, na ile nyumba ambayo niliyokuwa nimesema, 'Jina langu litakuwa humo.”'
ve “İsrail'i nasıl huzurumdan attımsa, Yahuda'yı da öyle atacağım” dedi, “Seçtiğim bu kenti, Yeruşalim'i ve ‘Orada bulunacağım’ dediğim tapınağı kendimden uzaklaştıracağım.”
28 Kama kwa mambo mengine yanayo muhusu Yosia, kila kitu alichofanya, je vimeandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
Yoşiya'nın krallığı dönemindeki öteki olaylar ve bütün yaptıkları Yahuda krallarının tarihinde yazılıdır.
29 Katika siku zake, Farao Neko, mfalme wa Misri, alienda kupigana dhidi ya mfalme wa Ashuru huko mto Frati. Mfalme Yosia akaenda kuonana na Neco katika mapigano, na Neko akamuua huko Megido.
Yoşiya'nın krallığı sırasında Mısır Firavunu Neko Asur Kralı'na yardım etmek üzere Fırat'a doğru yola çıktı. Kral Yoşiya da Neko'nun üzerine yürüdü. Megiddo'da karşılaştılar. Neko Yoşiya'yı öldürdü.
30 Watumishi wa Yosia wakambeba kwenye gari la farasi akiwa amekufa kutoka Migido, kumleta Yerusalemu, na kumzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta, na kumfanya kuwa mfalme katika mahali pake.
Görevlileri Yoşiya'nın cesedini savaş arabasıyla Megiddo'dan Yeruşalim'e getirip mezarına gömdüler. Yahuda halkı Yoşiya'nın oğlu Yehoahaz'ı meshederek babasının yerine kral yaptı.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na tatu alipoanza kutawala, na alitawala miezi mitatu katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Hamutali; alikuwa binti wa Yeremia wa Libana.
Yehoahaz yirmi üç yaşında kral oldu ve Yeruşalim'de üç ay krallık yaptı. Annesi Livnalı Yeremya'nın kızı Hamutal'dı.
32 Yehoahazi alifanya yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama kila kitu ambacho babu zake walichokifanya.
Yehoahaz ataları gibi RAB'bin gözünde kötü olanı yaptı.
33 Farao Neko akamfunga gerezani huko Ribla katika nchi ya Hamathi, hivyo asiweze kutawala katika Yerusalemu. Kisha Neko akaitoza Yuda talanta mia moja za fedha na talanta moja ya dhahabu.
Yeruşalim'de krallık yapmasın diye, Firavun Neko, Hama ülkesinde, Rivla'da Yehoahaz'ı zincire vurdu. Ülke halkını yüz talant gümüş ve bir talant altın ödemekle yükümlü kıldı.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia mfalme katika mahali pa Yosia baba yake, na kubadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua mfalme Yehoahazi kwenda Misri, na Yehoahazi akafia huko.
Firavun Neko Yoşiya'nın oğlu Elyakim'i babasının yerine kral yaptı ve adını değiştirip Yehoyakim koydu. Sonra Yehoahaz'ı alıp Mısır'a döndü. Yehoahaz orada öldü.
35 Yehoyakimu akalipa fedha na dhahabu kwa Farao. Ili akutane na amri ya Farao, Yehoyakimu akaitoza nchi na kulazimisha kila mtu miongoni mwa watu wa nchi wamlipe fedha na dhahabu kulingana na makadirio yao.
Yehoyakim firavunun istediği altın ve gümüşü ödedi. Bu parayı bulmak için firavunun buyruğuna uyarak ülkeyi vergiye bağladı. Firavun Neko'ya verilmek üzere Yahuda halkından herkesin gücü oranında altın ve gümüş topladı.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, na alitawala miaka kumi na moja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Zebida; alikuwa binti wa Pedaia wa Ruma.
Yehoyakim yirmi beş yaşında kral oldu ve Yeruşalim'de on bir yıl krallık yaptı. Annesi Rumalı Pedaya'nın kızı Zevuda'ydı.
37 Yehoyakimu akafanya yale yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama waliyoyafanya babu zake.
Yehoyakim ataları gibi RAB'bin gözünde kötü olanı yaptı.