< 2 Wafalme 23 >

1 Hivyo mfalme akawatuma wajumbe waliokuwa wamemzunguka wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.
So the king sent messengers who gathered to him all the elders of Judah and of Jerusalem.
2 Kisha mfalme akapanda hadi kwenye nyumba ya Yahwe, na watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu pamoja naye, na makuhani, manabii, na watu wote, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Kisha akasoma katika masikioni kwao maneno yote ya kitabu cha agano ambalo lililokuwa limepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
Then the king went up to the house of Yahweh, and all the men of Judah and all the inhabitants of Jerusalem with him, and the priests, prophets, and all the people, from small to great. He then read in their hearing all the words of the book of the Covenant that had been found in the house of Yahweh.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yahwe, kutembea pamoja na Yahwe na kukumbuka maagizo yake, kanuni zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kuthibitisha maneno ya hili agano ambalo lililokuwa limeandikwa kwenye hiki kitabu. Hivyo watu wote wakakubaliana kusimama kwenye agano
The king stood by the pillar and made a covenant before Yahweh, to walk after Yahweh and to keep his commandments, his regulations, and his statutes, with all his heart and all his soul, to confirm the words of this covenant that were written in this book. So all the people agreed to stand by the covenant.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia yule kuhani mkuu, makuhani chini yake, na walinzi wa lango watoe kwenye hekalu vyombo vilivyokuwa vimetengenezwa kwa ajili ya Baali na Ashera, na kwa ajili ya nyota zote za mbinguni. Akivichoma moto Yerusalimu kwenye mashamba ya bonde la Kidroni na kubeba majivu yake kwenda Betheli.
The king commanded Hilkiah the high priest, the priests under him, and the gatekeepers to bring out of the temple of Yahweh all the vessels that were made for Baal and Asherah, and for all the stars of heaven. He burned them outside Jerusalem in the fields in the Kidron Valley and carried their ashes to Bethel.
5 Akawaondoa makuhani waliokuwa wanaabudu miungu ambao wafalme wa Yuda waliwachagua ili kwa ajili ya kufukiza ubani katika mahali pa juu kwenye miji ya Yuda na sehemu zinazoizunguka Yerusalemu-wale waliokuwa wanchoma ubani kwa Baali, kwa juana kwa mwezi, kwa sayari, na kwa nyota zote za mbinguni.
He got rid of the idolatrous priests whom the kings of Judah had chosen to burn incense at the high places in the cities of Judah and in the places around Jerusalem—those who burned incense to Baal, to the sun and the moon, to the planets, and to all the stars of heaven.
6 Akaiondoa Ashera kutoka kwenye hekalu la Yahwe, nje ya Yerusalemu hata bonde la Kidroni na kuichoma hapo. Akaipiga kwenye mavumbi na kuiyatupa yale mavumbi kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
He brought out the Asherah pole from the temple of Yahweh, outside Jerusalem to the Kidron Valley and burned it there. He beat it to dust and threw that dust onto the graves of the common people.
7 Akavisafisha vyumba vya makahaba ambao walikuwa kwenye hekalu la Yahwe, ambako wanawake waliposhonea nguo kwa ajili ya Ashera
He cleared out the rooms of the cultic prostitutes who were in the temple of Yahweh, where the women wove garments for Asherah.
8 Yosia akawaleta makuhani wote nje ya miji ya Yuda na kupanajisi mahali pa juu ambako makuhani walipokuwa wakichomea ubani, kutoka Geba hata Bersheba. Akapaharibu mahala pa juu kwenye malango ambayo yaliyokuwa ya kuingilia kwenda kwenye lango la Yoshua (liwali wa mji), upande wa kushoto wa lango la mji.
Josiah brought all the priests out of the cities of Judah and defiled the high places where the priests had burned incense, from Geba to Beersheba. He destroyed the high places at the gates that were at the entrance to the gate of Joshua (the city governor), on the left side of the city gate.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu hawakuruhusiwa kuhudumu kwenye madhabahu ya Yahwe katika Yerusalemu, wakala mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Although the priests of those high places were not allowed to serve at the altar of Yahweh in Jerusalem, they ate unleavened bread among their brothers.
10 Yosia akainajisi Tofethi, ambayo ipo kwenye bonde la Ben Hinomu, ili kwamba mtu yeyote asimuweke mtoto wake wa kiume au binti yake kwenye moto kama sadaka kwa Molaki.
Josiah defiled Topheth, which is in the Valley of Ben Hinnom, so that no one might cause his son or his daughter to pass through the fire as a sacrifice to Molech.
11 Akawachukua farasi ambao wafalme wa Yuda waliokuwa wametolewa kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye eneo la lango la uingilia kwenye hekalu la Yahwe, karibu na chumba cha Nathani Meleki, msimamizi mkuu wa nyumba ya mfalme. Yosia akayachoma yale magari ya farasi ya jua
He took away the horses that the kings of Judah had given to the sun. They had been in an area at the entrance to the temple of Yahweh, near the room of Nathan-Melek, the chamberlain. Josiah burned the chariots of the sun.
12 Yosia mfalme akayaharibu madhabahu yaliyokuwa kwenye dari ya juu ya chumba cha Ahazi, ambacho wafalme wa Yuda walikitengeneza, na madhabahu ambayo Manase aliyatengeneza kwenye behewa mbili za nyumba ya Yahwe. Yosia akazivunga vipande vipande na kuvitupa kwenye bonde la Kidroni.
Josiah the king destroyed the altars that were on the roof of the upper chamber of Ahaz, which the kings of Judah had made, and the altars that Manasseh had made in the two courts of the temple of Yahweh. Josiah smashed them into pieces and threw them into the Kidron Valley.
13 Mfalme akapaangamiza mahali pa juu magharibi mwa Yerusalemu, kusini mwa mlima wa uharibifu ambapo Sulemani mfalme wa Israeli alipajenga kwa ajili ya Ashtorithi, chukizo la Wamoabu; sanamu za karaha za Wasidoni; kwa Kemoshi, sanamu za karaha wa Moabu; na kwa Moleki, sanamu wa karaha wa watu wa Amoni.
The king ruined the high places east of Jerusalem, south of the mount of corruption that Solomon the king of Israel had built for Ashtoreth, the detestable idol of the Sidonians; for Chemosh, the detestable idol of Moab; and for Molech, the detestable idol of the people of Ammon.
14 Akazivunja nguzo za jiwe kuwa vipande vipande na kuziangusha chini nguzo za Ashera na kuzijaza zile sehemu kwa mifupa ya watu.
He broke the stone pillars into pieces and cut down the Asherah poles and he filled those places with the bones of human beings.
15 Yosia pia akaiteketeza kabisa madhabahu iliyokuwa Betheli na mahali pa juu ambako Yeroboamu mwana wa Nebati (ambaye aliwafanya Waisraeli kuasi) aliijenga. Pia aliichoma moto ile madhabahu na mahali pa juu na kupapiga hadi pakawa vumbi. Pia akaichoma moto nguzo ya Ashera.
Josiah also completely destroyed the altar that was at Bethel and the high place that Jeroboam son of Nebat (the one who made Israel to sin) had constructed. He also burned that altar and the high place and beat it to dust. He also burned the Asherah pole.
16 Yosia alipotazama kwenye lile eneo, akagundua kwamba yale makaburi yalikuwa juu ya mlima. Akawatuma watu kuichukua mifupa kutoka kwenye yale makaburi; kisha akaichoma kwenye madhabahu, akainajisi. Hii ilitokana na neno la Yahwe ambalo mtu wa Mungu aliliongea, yule mtu aliyekuwa ameongea haya mambo kabla.
As Josiah looked over the area, he noticed the graves that were on the hillside. He sent men to take the bones from the graves; then he burned them on the altar, which defiled it. This was according to the word of Yahweh which the man of God had spoken, the man who spoke of these things beforehand.
17 Kisha akasema, “Ni ukumbusho wa nani ule ninao uona?” Mtu wa ule mji akamwambia, “Lile ni kaburi la mtu wa Mungu ambaye alikuja kutoka Yuda na kuongea kuhusu haya mambo ambayo ameyafanya dhidi ya madhabahu ya Betheli.”
Then he said, “What monument is that I see?” The men of the city told him, “That is the grave of the man of God who came from Judah and spoke about these things that you have just done against the altar of Bethel.”
18 Hivyo Yosia akasema, “Mwacheni. Mtu asihamishe mifupa yake.” Hivyo wakaacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya nabii ambaye alikuja kutoka Samaria.
So Josiah said, “Let it alone. No one should move his bones.” So they let his bones alone, along with the bones of the prophet who had come from Samaria.
19 Kisha Yosia akahamisha nyumba zote za mahali pa juu ambazo zilikuwa katika mji wa Samaria, ambazo wafalme wa Israeli walizokuwa wamezitengeneza, na ambazo zilizokuwa zimemgadhabisha Yahwe kwa hasira.
Then Josiah removed all the houses on the high places that were in the cities of Samaria, which the kings of Israel had made, and that provoked Yahweh to anger. He did to them exactly what had been done at Bethel.
20 Aliwafanyia kile ambacho kilikuwa kimefanyika katika Betheli. Aliwachinja makuhani wote wa mahali pa juu ya madhabahu na aliichoma mifupa ya watu juu yao. Kisha akarudi Yerusalemu.
He slaughtered all the priests of the high places on the altars and he burned human bones on them. Then he returned to Jerusalem.
21 Kisha mfalme akawaamuru watu wote, akisema, “Itunzeni Pasaka ya Yahwe Mungu wenu, kama ilivyoandikwa kwenye hiki kitabu cha agano.”
Then the king commanded all the people, saying, “Keep the Passover to Yahweh your God, as it is written in this Book of the Covenant.”
22 Hiyo Pasaka haijawahi kufanyika tangu siku za waamuzi ambao waliiongoza Israeli, wala katika siku zote za wafalme wa Israeli au Yuda.
Such a Passover celebration had never been held from the days of the judges who ruled Israel, nor in all the days of the kings of Israel or Judah.
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia hii Pasaka ya Yahwe ilisheherekewa katika Yerusalemu.
But in the eighteenth year of King Josiah this Passover of Yahweh was celebrated in Jerusalem.
24 Yosia pia akawafukuza wale ambao waliokuwa wameongea na wafu au na roho. Pia aliifukuza miungu ya sananmu, sanamu, na vitu vyote ambavyo ni chukizo vilivyokuwa vinaonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, hivyo kwa kuthibitisha yale maneno ya sheria ambayo iliyokuwa imeandikwa kwenye kitabu cha Hilkia yule kuhani aliyekuwa amepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
Josiah also banished those who talked with the dead or with spirits. He also banished the fetishes, the idols, and all the disgusting things that were seen in the land of Judah and in Jerusalem, so as to confirm the words of the law which were written in the book that Hilkiah the priest had found in the house of Yahweh.
25 Kabla ya Yosia, hapakuwa na mfalme kama yeye, aliyekuwa amemwelekea yahwe kwa moyo wake wote, roho yake yote, na nguvu zake zote, ambaye alifuata sheria zote za Musa. Hapakuwa na mfalme kama Yosia aliyeinuka baada ya yeye.
Before Josiah, there had been no king like him, who turned to Yahweh with all his heart, all his soul, and all his might, who followed all the law of Moses. Nor did any king like Josiah arise after him.
26 Walakini, Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake, ambayo ilikuwa dhidi ya Yuda kwa waabudu wapagani wote pamoja ambao Manase aliokuwa amemgadhibisha.
Nevertheless, Yahweh did not turn away from the burning of his fierce anger, which burned against Judah because of all that Manasseh had done to provoke him to anger.
27 Hivyo Yahwe akasema, “Pia nitaiondoa Yuda usoni kwangu, kama nilivyoiondoa Israeli, na nitautupilia mbali huu mji ambao nilio uchagua, Yerusalemu, na ile nyumba ambayo niliyokuwa nimesema, 'Jina langu litakuwa humo.”'
So Yahweh said, “I will also remove Judah out of my sight, as I have removed Israel, and I will throw away this city that I have chosen, Jerusalem, and the house of which I said, 'My name will be there.'”
28 Kama kwa mambo mengine yanayo muhusu Yosia, kila kitu alichofanya, je vimeandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
As for the other matters concerning Josiah, everything that he did, are they not written in the book of the events of the kings of Judah?
29 Katika siku zake, Farao Neko, mfalme wa Misri, alienda kupigana dhidi ya mfalme wa Ashuru huko mto Frati. Mfalme Yosia akaenda kuonana na Neco katika mapigano, na Neko akamuua huko Megido.
In his days, Pharaoh Necho, king of Egypt, went to fight against the king of Assyria at the Euphrates River. King Josiah went to meet Necho in battle, and Necho killed him at Megiddo.
30 Watumishi wa Yosia wakambeba kwenye gari la farasi akiwa amekufa kutoka Migido, kumleta Yerusalemu, na kumzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta, na kumfanya kuwa mfalme katika mahali pake.
Josiah's servants carried him dead in a chariot from Megiddo, brought him to Jerusalem, and buried him in his own grave. Then the people of the land took Jehoahaz son of Josiah, anointed him, and made him king in his father's place.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na tatu alipoanza kutawala, na alitawala miezi mitatu katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Hamutali; alikuwa binti wa Yeremia wa Libana.
Jehoahaz was twenty-three years old when he began to reign, and he reigned three months in Jerusalem. His mother's name was Hamutal; she was the daughter of Jeremiah of Libnah.
32 Yehoahazi alifanya yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama kila kitu ambacho babu zake walichokifanya.
Jehoahaz did what was evil in the sight of Yahweh, like everything that his ancestors had done.
33 Farao Neko akamfunga gerezani huko Ribla katika nchi ya Hamathi, hivyo asiweze kutawala katika Yerusalemu. Kisha Neko akaitoza Yuda talanta mia moja za fedha na talanta moja ya dhahabu.
Pharaoh Necho put him in chains at Riblah in the land of Hamath, so that he might not reign in Jerusalem. Then Necho fined Judah one hundred talents of silver and one talent of gold.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia mfalme katika mahali pa Yosia baba yake, na kubadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua mfalme Yehoahazi kwenda Misri, na Yehoahazi akafia huko.
Pharaoh Necho made Eliakim son of Josiah king in the place of Josiah his father, and changed his name to Jehoiakim. But he took Jehoahaz away to Egypt, and Jehoahaz died there.
35 Yehoyakimu akalipa fedha na dhahabu kwa Farao. Ili akutane na amri ya Farao, Yehoyakimu akaitoza nchi na kulazimisha kila mtu miongoni mwa watu wa nchi wamlipe fedha na dhahabu kulingana na makadirio yao.
Jehoiakim paid the silver and gold to Pharaoh. In order to meet the demand of Pharaoh, Jehoikim taxed the land and he forced each man among the people of the land to pay him the silver and gold according to their assessments.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, na alitawala miaka kumi na moja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Zebida; alikuwa binti wa Pedaia wa Ruma.
Jehoiakim was twenty-five years old when he began to reign, and he reigned eleven years in Jerusalem. His mother's name was Zebidah; she was the daughter of Pedaiah of Rumah.
37 Yehoyakimu akafanya yale yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama waliyoyafanya babu zake.
Jehoiakim did what was evil in the sight of Yahweh, just as his ancestors had done.

< 2 Wafalme 23 >