< 2 Wafalme 21 >

1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala miaka hamsini na tano katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Hefziba.
[was] a son of Two [plus] ten year[s] Manasseh when became king he and fifty and five year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Hephzi-bah.
2 Alifanya maovu usoni kwa Yahwe, kama machukizo ya mataifa ambayo Yahwe aliyafukuza nje mbele ya wana wa Israeli.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh according to [the] abominations of the nations which he had dispossessed Yahweh from before [the] people of Israel.
3 Kwa kupajenga tena mahala pa juu ambapo Hezekia baba yake alipaharibu, na akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali, akafanya Ashera, kama Ahabu mfalme wa Israeli alivyofanya, akasujudu kwa nyota zote za mbinguni na kuwaabudu wao.
And he returned and he built the high places which he had destroyed Hezekiah father his and he set up altars to Baal and he made an Asherah pole just as he had done Ahab [the] king of Israel and he bowed down to all [the] host of the heavens and he served them.
4 Manase akajenga madhabahu za kipagani kwenye nyumba ya Yahwe, ingawaje Yahwe aliamuru, “Jina langu litakuwa Yerusalemu daima.”
And he built altars in [the] house of Yahweh which he had said Yahweh in Jerusalem I will put name my.
5 Akajenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika behewa mbili za nyumba ya Yahwe.
And he built altars to all [the] host of the heavens in [the] two [the] courtyards of [the] house of Yahweh.
6 Akamuweka mtoto wake wa kiume kwenye moto; akatazama bao ushirikina na kujishuhulisha pamoja wale ambao wenye pepo wa utambuzi na wale wachawi. Akafanya maovu mengi usoni kwa Yahwe na kuchochea hasira kwa Mungu.
And he made pass son his in the fire and he practiced soothsaying and he practiced divination and he dealt with necromancer and soothsayers he increased to do the evil in [the] eyes of Yahweh to provoke [him] to anger.
7 Sanamu ya kuchongwa ya Ashera ambayo aliitnegeneza, akaiweka kwenye nyumba ya Yahwe. Nyumba hii ndiyo ambayo Yahwe alimwambia Daudi na Sulemani mwanawe; alisema: “Ni nyumba hii na katika Yerusalemu, ambayo nimeichagua kutoka makabila yote ya Isaraeli, ambako nitaliweka jina langu milele.
And he put [the] image of Asherah which he had made in the house which he had said Yahweh to David and to Solomon son his in the house this and in Jerusalem which I have chosen from all [the] tribes of Israel I will put name my for ever.
8 Sintofanya miguu ya Israeli kushindwa tena nje ya nchi ambayo niliwapa babu zao, kama tu watakuwa makini kutii yale yote niliyowaamuru, na kufuata sheria zote ambazo mtumishi wangu Musa aliwaamuru.”
And not I will repeat to make wander [the] foot of Israel from the ground which I gave to ancestors their only - if they will take care to do according to all that I have commanded them and to all the law which he commanded them servant my Moses.
9 Lakini watu hawakusikia, na Manase akawaongoza kufanya maovu zaidi kuliko yale ya mataifa ambayo Yahwe aliyaharibu mbele ya watu wa Israeli.
And not they listened and he misled them Manasseh to do evil more than the nations which he had destroyed Yahweh from before [the] people of Israel.
10 Basi Yahwe akaongea na watumishi wake manabii, akisema,
And he spoke Yahweh by [the] hand of servants his the prophets saying.
11 Kwasababu Manase mfalme wa Yuda amefanya haya machukizo, na kutenda maovu zaidi kuliko yote waliyoyatenda Waamori ambao walikuwa mbele yake walikubali, na pia aliwafanya Yuda kuasi kwa sanamu zake,
Because that he has done Manasseh [the] king of Judah the abominations these he has done evil more than all that they did the Amorite[s] who [was] before him and he has caused to sin also Judah with idols his.
12 kwa hiyo Yahwe, Mungu wa Israeli, akasema hivi: Tazama, nakaribia kuleta uovu juu ya Yerusalemu na Yuda ambayo kila mtu asikiapo kuhusu hilo, masikio yake yote yatang'aa.
Therefore thus he says Yahweh [the] God of Israel here I [am] about to bring calamity on Jerusalem and Judah which every ([one who] hears of it *Q(K)*) they will tingle [the] two ears his.
13 Nitanyoosha juu ya Yerusalemu kipimo kilichotumika dhidi ya Samaria, na kuangusha msatari utakaotumika dhidi ya nyumba ya Ahabu; Nitaifuta Yerusalemu safi, kama kufuta sahani, kuifuta na kuifunika juu chini.
And I will stretch out over Jerusalem [the] measuring-line of Samaria and [the] leveling tool of [the] house of Ahab and I will wipe clean Jerusalem just as someone wipes clean the bowl he wipes [it] clean and he turns [it] over on face its.
14 Nitawatupa masalia ya urithi wangu na kuwaweka mikononi mwa maadui zao. Watakuwa nyara na mateka kwa maadui zao wote,
And I will abandon [the] remnant of inheritance my and I will give them in [the] hand of enemies their and they will become spoil and plunder to all enemies their.
15 kwa sababu wamefanya yaliyo maovu usoni kwangu, na kunichochea hasira, tangu siku babu zao walipotoka Misri, hadi leo.”
Because that they have done the evil in view my and they have been provoking to anger me since the day when they came out ancestors their from Egypt and until the day this.
16 Aidha, Manase akazimwaga damu nyingi za wasio na hatia, hadi alipoijaza Yerusalemu kutoka upande huu kwenda mwingine kwa kifo. Hii ilikuwa ni kuongeza kwenye dhambi ambayo aliifanya Yuda kuasi, wakati walipofanya uovu mbele za Yahwe.
And also blood innocent he shed Manasseh much very until that he had filled Jerusalem mouth to mouth apart from sin his which he caused to sin Judah to do the evil in [the] eyes of Yahweh.
17 Kama kwa mambo mengine yamhusuyo Manase, yote aliyoyafanya, na dhambi ambayo aliyoifanya, je haya hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Manasseh and all that he did and sin his which he sinned ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
18 Manase akalala pamoja na babu zake na alizikwa kwenye bustani ya nyumba yake, katika bustani ya Uza. Amoni mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.
And he lay down Manasseh with ancestors his and he was buried in [the] garden of house his in [the] garden of Uzzah and he became king Amon son his in place of him.
19 Amoni alikuwa na miaka kumi na mbili alipoanza kutawala; alitawala miaka miwili katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Meshlemethi; alikuwa binti wa Haruzi wa Yotba.
[was] a son of Twenty and two year[s] Amon when became king he and two years he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Meshullemeth [the] daughter of Haruz from Jotbah.
20 Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe, kama manase baba yake alivyofanya.
And he did the evil in [the] eyes of Yahweh just as he had done Manasseh father his.
21 Amoni alifuata njia zote ambazo baba yake alizotembelea na kuabudu sanamu ambazo baba yake aliziabudu, na kuzisujudia.
And he walked in all the way which he had walked father his and he served the idols which he had served father his and he bowed down to them.
22 Akajitenga na Yahwe, Mungu wa baba zake, na hakutembea katika njia ya Yahwe.
And he forsook Yahweh [the] God of ancestors his and not he walked in [the] way of Yahweh.
23 Watumishi wa Amoni wakafanya njama dhidi yake na kumuua mfalme kwenye nyumba yake mwenyewe.
And they conspired [the] servants of Amon on him and they killed the king in own house his.
24 Lakini watu wa nchi wakawaua watu wote waliofanya njama dhidi ya mfalme Amoni, na wakamfanya Yosia mtoto wake kuwa mfalme katika sehemu yake.
And it struck down [the] people of the land all those [who] had conspired on the king Amon and they made king [the] people of the land Josiah son his in place of him.
25 Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Amoni yale aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
And [the] rest of [the] matters of Amon which he did ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Judah.
26 Watu wakamzika kwenye kaburi lake katika bustani ya Uza, na Yosia mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.
(And someone buried *LB(ah)*) him in grave his in [the] garden of Uzzah and he became king Josiah son his in place of him.

< 2 Wafalme 21 >