< 2 Wafalme 21 >
1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na mbili wakati alipoanza kutawala; alitawala miaka hamsini na tano katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Hefziba.
Manasseh was twelve years old when he had begun to reign, and he reigned for fifty-five years in Jerusalem. The name of his mother was Hephzibah.
2 Alifanya maovu usoni kwa Yahwe, kama machukizo ya mataifa ambayo Yahwe aliyafukuza nje mbele ya wana wa Israeli.
And he did evil in the sight of the Lord, in accord with the idols of the nations that the Lord destroyed before the face of the sons of Israel.
3 Kwa kupajenga tena mahala pa juu ambapo Hezekia baba yake alipaharibu, na akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali, akafanya Ashera, kama Ahabu mfalme wa Israeli alivyofanya, akasujudu kwa nyota zote za mbinguni na kuwaabudu wao.
And he turned away. And he built up the high places that his father, Hezekiah, had destroyed. And he erected altars to Baal, and he made sacred groves, just as Ahab, the king of Israel, had done. And he adored the entire army of heaven, and he served them.
4 Manase akajenga madhabahu za kipagani kwenye nyumba ya Yahwe, ingawaje Yahwe aliamuru, “Jina langu litakuwa Yerusalemu daima.”
And he constructed altars in the house of the Lord, about which the Lord said: “In Jerusalem, I will place my name.”
5 Akajenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika behewa mbili za nyumba ya Yahwe.
And he constructed altars, for the entire army of heaven, within the two courts of the temple of the Lord.
6 Akamuweka mtoto wake wa kiume kwenye moto; akatazama bao ushirikina na kujishuhulisha pamoja wale ambao wenye pepo wa utambuzi na wale wachawi. Akafanya maovu mengi usoni kwa Yahwe na kuchochea hasira kwa Mungu.
And he led his son through fire. And he used divinations, and observed omens, and appointed soothsayers, and multiplied diviners, so that he did evil before the Lord, and provoked him.
7 Sanamu ya kuchongwa ya Ashera ambayo aliitnegeneza, akaiweka kwenye nyumba ya Yahwe. Nyumba hii ndiyo ambayo Yahwe alimwambia Daudi na Sulemani mwanawe; alisema: “Ni nyumba hii na katika Yerusalemu, ambayo nimeichagua kutoka makabila yote ya Isaraeli, ambako nitaliweka jina langu milele.
Also, he set up an idol, of the sacred grove that he had made, in the temple of the Lord, about which the Lord said to David, and to his son Solomon: “In this temple, and in Jerusalem, which I have chosen out of all the tribes of Israel, I will place my name forever.
8 Sintofanya miguu ya Israeli kushindwa tena nje ya nchi ambayo niliwapa babu zao, kama tu watakuwa makini kutii yale yote niliyowaamuru, na kufuata sheria zote ambazo mtumishi wangu Musa aliwaamuru.”
And I will no longer cause the feet of Israel to be moved from the land that I gave to their fathers: if only they will take care to do all that I have instructed them, and the entire law that my servant Moses commanded to them.”
9 Lakini watu hawakusikia, na Manase akawaongoza kufanya maovu zaidi kuliko yale ya mataifa ambayo Yahwe aliyaharibu mbele ya watu wa Israeli.
Yet truly, they did not listen. Instead, they were seduced by Manasseh, so that they did evil, more so than the nations that the Lord crushed before the face of the sons of Israel.
10 Basi Yahwe akaongea na watumishi wake manabii, akisema,
And so the Lord spoke, by the hand of his servants, the prophets, saying:
11 Kwasababu Manase mfalme wa Yuda amefanya haya machukizo, na kutenda maovu zaidi kuliko yote waliyoyatenda Waamori ambao walikuwa mbele yake walikubali, na pia aliwafanya Yuda kuasi kwa sanamu zake,
“Since Manasseh, the king of Judah, has committed these wicked abominations, beyond all that the Amorites before him have done, and also has caused Judah to sin by his defilements,
12 kwa hiyo Yahwe, Mungu wa Israeli, akasema hivi: Tazama, nakaribia kuleta uovu juu ya Yerusalemu na Yuda ambayo kila mtu asikiapo kuhusu hilo, masikio yake yote yatang'aa.
because of this, thus says the Lord, the God of Israel: Behold, I will lead evils over Jerusalem and over Judah, such that, whoever will hear of these things, both his ears will ring.
13 Nitanyoosha juu ya Yerusalemu kipimo kilichotumika dhidi ya Samaria, na kuangusha msatari utakaotumika dhidi ya nyumba ya Ahabu; Nitaifuta Yerusalemu safi, kama kufuta sahani, kuifuta na kuifunika juu chini.
And I will extend the measuring line of Samaria over Jerusalem, with the scale of the house of Ahab. And I will erase Jerusalem, just as writing tablets are usually erased. And after erasing, I will turn it and repeatedly drag a stylus over its surface.
14 Nitawatupa masalia ya urithi wangu na kuwaweka mikononi mwa maadui zao. Watakuwa nyara na mateka kwa maadui zao wote,
And truly, I will send away the remnants of my inheritance, and I will deliver them into the hands of their enemies. And they will be devastated and plundered by all their adversaries.
15 kwa sababu wamefanya yaliyo maovu usoni kwangu, na kunichochea hasira, tangu siku babu zao walipotoka Misri, hadi leo.”
For they have done evil before me, and they have persevered in provoking me, from the day when their fathers departed from Egypt, even to this day.
16 Aidha, Manase akazimwaga damu nyingi za wasio na hatia, hadi alipoijaza Yerusalemu kutoka upande huu kwenda mwingine kwa kifo. Hii ilikuwa ni kuongeza kwenye dhambi ambayo aliifanya Yuda kuasi, wakati walipofanya uovu mbele za Yahwe.
Moreover, Manasseh also has shed an exceedingly great amount of innocent blood, until he filled Jerusalem even to the mouth, aside from his sins by which he caused Judah to sin, so that they did evil before the Lord.”
17 Kama kwa mambo mengine yamhusuyo Manase, yote aliyoyafanya, na dhambi ambayo aliyoifanya, je haya hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafalme wa Yuda?
Now the rest of the words of Manasseh, and all that he did, and his sin that he sinned, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Judah?
18 Manase akalala pamoja na babu zake na alizikwa kwenye bustani ya nyumba yake, katika bustani ya Uza. Amoni mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.
And Manasseh slept with his fathers, and he was buried in the garden of his own house, in the garden of Uzza. And Amon, his son, reigned in his place.
19 Amoni alikuwa na miaka kumi na mbili alipoanza kutawala; alitawala miaka miwili katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Meshlemethi; alikuwa binti wa Haruzi wa Yotba.
Amon was twenty-two years old when he had begun to reign, and he reigned for two years in Jerusalem. The name of his mother was Meshullemeth, the daughter of Haruz, from Jotbah.
20 Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe, kama manase baba yake alivyofanya.
And he did evil in the sight of the Lord, just as his father, Manasseh, had done.
21 Amoni alifuata njia zote ambazo baba yake alizotembelea na kuabudu sanamu ambazo baba yake aliziabudu, na kuzisujudia.
And he walked in all the ways in which his father had walked. And he served the unclean things that his father had served, and he adored them.
22 Akajitenga na Yahwe, Mungu wa baba zake, na hakutembea katika njia ya Yahwe.
And he abandoned the Lord, the God of his fathers, and he did not walk in the way of the Lord.
23 Watumishi wa Amoni wakafanya njama dhidi yake na kumuua mfalme kwenye nyumba yake mwenyewe.
And his servants undertook treachery against him. And they killed the king in his own house.
24 Lakini watu wa nchi wakawaua watu wote waliofanya njama dhidi ya mfalme Amoni, na wakamfanya Yosia mtoto wake kuwa mfalme katika sehemu yake.
But the people of the land slew all those who had conspired against king Amon. And they appointed for themselves Josiah, his son, as king in his place.
25 Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Amoni yale aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
But the rest of the words of Amon, which he did, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Judah?
26 Watu wakamzika kwenye kaburi lake katika bustani ya Uza, na Yosia mwanawe akawa mfalme katika sehemu yake.
And they buried him in his sepulcher, in the garden of Uzza. And his son, Josiah, reigned in his place.