< 2 Wafalme 20 >

1 Katika siku hizo Hezekia aliugua akawa kwenye hatari ya kufa. Hivyo Isaya mwana wa Amozi, akaja, na kumwambia, “Yahwe asema, 'Weka nyumba yako kwenye mpangilio; kwa kuwa utakufa, na hutapona.'”
In those days was Hezekiah sick to death. Isaiah the prophet the son of Amoz came to him, and said to him, "Thus says the LORD, 'Set your house in order; for you shall die, and not live.'"
2 Kisha Ahazi akageuza uso wake kwenye ukuta na kumuomba Yahwe, akisema,
Then he turned his face to the wall, and prayed to the LORD, saying,
3 “Tafadhali, Yahwe, ukumbuke jinsi nilivyo mwaminifu kutembea mbele yako kwa moyo wangu wote, na jinsi nilivyofanya yaliyo mazuri usoni kwako.” Kisha Hezekia akalia kwa sauti.
"Remember now, LORD, I beg you, how I have walked before you in truth and with a perfect heart, and have done that which is good in your sight." Hezekiah wept bitterly.
4 Kabla ya Isaya hajatoka nje kwenye mji wa kati, neno la Yahwe likamjia, kusema,
It happened, before Isaiah had gone out of the middle court, that the word of the LORD came to him, saying,
5 '“Rudi, na umwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, 'Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Daudi babu yako, asemavyo: “Nimesikia maombi yako, na nimeyaona machozi yako. Nitakuponya katika siku ya tatu, na utapanda juu kwenye nyumba ya Yahwe.
"Turn back, and tell Hezekiah the prince of my people, 'Thus says the LORD, the God of David your father, "I have heard your prayer. I have seen your tears. Look, I will heal you. On the third day, you shall go up to the house of the LORD.
6 Nitakuongeza miaka kumi na tano ya maisha yako, na nitakulinda na huu mji kwa ajili yangu na kwa ajili ya mtumishi wangu."”'
I will add to your days fifteen years. I will deliver you and this city out of the hand of the king of Assyria. I will defend this city for my own sake, and for my servant David's sake."'"
7 Hivyo Isaya akasema, “Chukueni mkate wa tini.” Walifanya hivyo na kuweka kwenye jipu lake, na akapona.
Isaiah said, "Take a cake of figs." They took and laid it on the boil, and he recovered.
8 Hezekia akamwambia Isaya, “Je kutakuwa na alama gani ambayo Yahwe ataniponya, na kwamba nitapanda juu hadi kwenye hekalu la Yahwe katika siku ya tatu?”
Hezekiah said to Isaiah, "What shall be the sign that the LORD will heal me, and that I shall go up to the house of the LORD the third day?"
9 Isaya akajibu, “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako kutoka kwa Yahwe, kwamba Yahwe atafanya kitu amacho alichokisema. Je kivuli kitaenda mbele hatua saba, au kurudi nyuma hatua saba?”
Isaiah said, "This shall be the sign to you from the LORD, that the LORD will do the thing that he has spoken: shall the shadow go forward ten steps, or go back ten steps?"
10 Hezekia akajibu, “Ni kitu chepesi kwa kivuli kwenda mbele hatua kumi. Hapana, hicho kivuli kirudi nyuma hatua kumi.”
Hezekiah answered, "It is a light thing for the shadow to go forward ten steps. Nay, but let the shadow return backward ten steps."
11 Hivyo Isaya nabii akamlilia Yahwe, na akaleta kivuli hatua kumi nyuma, kutoka pale ambapo zilikuwa zimevuka kwenye ngazi za Ahazi.
Isaiah the prophet cried to the LORD; and he brought the shadow ten steps backward, by which it had gone down on the dial of Ahaz.
12 Katika kipindi hicho Merodak Baladani mfalme wa Babeli alituma barua na zawadi kwa Hezekia, kwa kuwa alisikia kwamba Hezekia alikuwa anaumwa.
At that time Marduk-Baladan the son of Baladan, king of Babylon, sent letters and a present to Hezekiah, for he had heard that Hezekiah had been sick, and had recovered.
13 Hezekia akasikiliza hizo barua, na kisha kuwaonyesha wajumbe sehemu zote na sehemu zake za thamani, fedha, dhahabu, manukato na marhamu na nyumba yenye ghala la silaha zake, na yote yaliyokutwa kwenye ghala za nyumba zake. Hapakuwa na kitu kwenye nyumba, wala kwenye ufalme wake wote, ambao Hezekia hakuwaonyesha.
Hezekiah was delighted at this, and showed them all the house of his precious things, the silver, and the gold, and the spices, and the precious oil, and the house of his armor, and all that was found in his treasures: there was nothing in his house, nor in all his dominion, that Hezekiah did not show them.
14 Kisha Isaya akaja kwa Hezekia na kumuuliza, “Hawa watu walikuwa wanakwambiaje? Wanatokea wapi?” Hezekia aksema, “Wamekuja kutoka nchi ya mbali ya Babeli.
Then Isaiah the prophet came to king Hezekiah, and said to him, "What did these men say? From where did they come to you?" Hezekiah said, "They have come from a far country, even from Babylon."
15 Isaya akauliza, “Wameona nini kwenye nyumba yako?” Hezekia akajibu, “Wameona kila kitu kwenye nyumba yangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha.”
He said, "What have they seen in your house?" Hezekiah answered, "They have seen all that is in my house. There is nothing among my treasures that I have not shown them."
16 Basi Isaya akamwambia Hezekia, “Sikiliza neno la Yahwe:
Isaiah said to Hezekiah, "Hear the word of the LORD.
17 'Tazama siku zinakuja wakati kila kitu kwenye kwenye nyumba yako ya kifalme, vitu ambavyo babu zako walivitunza huko hadi leo, vitabebwa kwenda Babeli. Hakuna kitakachobakia, Yahwe asema.
'Look, the days come, that all that is in your house, and that which your fathers have laid up in store to this day, shall be carried to Babylon. Nothing shall be left,' says the LORD.
18 Watoto waliozaliwa na wewe, ambao umewazaa wewe mwenyewe-watawachukua mbali, na watakuwa matowashi kwenye nyumba ya kifalme ya mfalme wa Babeli.'”
'Of your sons who shall issue from you, whom you shall father, shall they take away; and they shall be eunuchs in the palace of the king of Babylon.'"
19 Hezekia akamwambia Isaya, “neno la Yahwe uliloliongea ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, Je sivyo ikiwapo amani na kweli katika siku zangu?”
Then Hezekiah said to Isaiah, "The word of the LORD which you have spoken is good." He said moreover, "Isn't it so, if peace and truth shall be in my days?"
20 Kama kwa mambo mengine yanamuhusu Hezekia, na ushujaa wake wote, na jinsi alivyotengeza bwawa la maji na mfereji, na kuleta maji kwenye mji-hayakuandikwa kwenye kitabu cha ya matukio ya wafalme wa Yuda?
Now the rest of the acts of Hezekiah, and all his might, and how he made the pool, and the conduit, and brought water into the city, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Judah?
21 Hezekia akalala na babu zake, na Manase mwanae akawa mfalme katika sehemu yake.
Hezekiah slept with his fathers; and Manasseh his son reigned in his place.

< 2 Wafalme 20 >