< 2 Wafalme 20 >

1 Katika siku hizo Hezekia aliugua akawa kwenye hatari ya kufa. Hivyo Isaya mwana wa Amozi, akaja, na kumwambia, “Yahwe asema, 'Weka nyumba yako kwenye mpangilio; kwa kuwa utakufa, na hutapona.'”
In those days Hezekiah has been sick to death, and Isaiah son of Amoz the prophet comes to him and says to him, “Thus said YHWH: Give a charge to your house, for you are dying, and do not live.”
2 Kisha Ahazi akageuza uso wake kwenye ukuta na kumuomba Yahwe, akisema,
And he turns around his face to the wall, and prays to YHWH, saying,
3 “Tafadhali, Yahwe, ukumbuke jinsi nilivyo mwaminifu kutembea mbele yako kwa moyo wangu wote, na jinsi nilivyofanya yaliyo mazuri usoni kwako.” Kisha Hezekia akalia kwa sauti.
“Ah, now, O YHWH, please remember how I have habitually walked before You in truth and with a perfect heart, and I have done that which [is] good in Your eyes”; and Hezekiah weeps [with] a great weeping.
4 Kabla ya Isaya hajatoka nje kwenye mji wa kati, neno la Yahwe likamjia, kusema,
And it comes to pass, [when] Isaiah has not [yet] gone out to the middle court, that the word of YHWH has been to him, saying,
5 '“Rudi, na umwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, 'Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Daudi babu yako, asemavyo: “Nimesikia maombi yako, na nimeyaona machozi yako. Nitakuponya katika siku ya tatu, na utapanda juu kwenye nyumba ya Yahwe.
“Return, and you have said to Hezekiah, leader of My people, Thus said YHWH, God of your father David: I have heard your prayer, I have seen your tear, behold, I give healing to you. On the third day you go up to the house of YHWH;
6 Nitakuongeza miaka kumi na tano ya maisha yako, na nitakulinda na huu mji kwa ajili yangu na kwa ajili ya mtumishi wangu."”'
and I have added fifteen years to your days, and I deliver you and this city out of the hand of the king of Asshur, and have covered over this city for My own sake, and for the sake of My servant David.”
7 Hivyo Isaya akasema, “Chukueni mkate wa tini.” Walifanya hivyo na kuweka kwenye jipu lake, na akapona.
And Isaiah says, “Take a cake of figs”; and they take and lay [it] on the boil, and he revives.
8 Hezekia akamwambia Isaya, “Je kutakuwa na alama gani ambayo Yahwe ataniponya, na kwamba nitapanda juu hadi kwenye hekalu la Yahwe katika siku ya tatu?”
And Hezekiah says to Isaiah, “What [is] the sign that YHWH gives healing to me, that I have gone up to the house of YHWH on the third day?”
9 Isaya akajibu, “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako kutoka kwa Yahwe, kwamba Yahwe atafanya kitu amacho alichokisema. Je kivuli kitaenda mbele hatua saba, au kurudi nyuma hatua saba?”
And Isaiah says, “This [is] the sign to you from YHWH, that YHWH does the thing that He has spoken—[will] the shadow have gone on ten degrees, or does it turn back ten degrees?”
10 Hezekia akajibu, “Ni kitu chepesi kwa kivuli kwenda mbele hatua kumi. Hapana, hicho kivuli kirudi nyuma hatua kumi.”
And Hezekiah says, “It has been light for the shadow to incline ten degrees; no, but let the shadow turn backward ten degrees.”
11 Hivyo Isaya nabii akamlilia Yahwe, na akaleta kivuli hatua kumi nyuma, kutoka pale ambapo zilikuwa zimevuka kwenye ngazi za Ahazi.
And Isaiah the prophet calls to YHWH, and He brings back the shadow by the degrees that it had gone down in the degrees of Ahaz—backward ten degrees.
12 Katika kipindi hicho Merodak Baladani mfalme wa Babeli alituma barua na zawadi kwa Hezekia, kwa kuwa alisikia kwamba Hezekia alikuwa anaumwa.
At that time Berodach-Baladan son of Baladan, king of Babylon, has sent letters and a present to Hezekiah, for he heard that Hezekiah had been sick;
13 Hezekia akasikiliza hizo barua, na kisha kuwaonyesha wajumbe sehemu zote na sehemu zake za thamani, fedha, dhahabu, manukato na marhamu na nyumba yenye ghala la silaha zake, na yote yaliyokutwa kwenye ghala za nyumba zake. Hapakuwa na kitu kwenye nyumba, wala kwenye ufalme wake wote, ambao Hezekia hakuwaonyesha.
and Hezekiah listens to them, and shows them all the house of his treasury, the silver, and the gold, and the spices, and the good ointment, and all the house of his vessels, and all that has been found in his treasuries; there has not been a thing that Hezekiah has not showed them in his house and in all his dominion.
14 Kisha Isaya akaja kwa Hezekia na kumuuliza, “Hawa watu walikuwa wanakwambiaje? Wanatokea wapi?” Hezekia aksema, “Wamekuja kutoka nchi ya mbali ya Babeli.
And Isaiah the prophet comes to King Hezekiah and says to him, “What did these men say? And from where do they come to you?” And Hezekiah says, “They have come from a far-off land—from Babylon.”
15 Isaya akauliza, “Wameona nini kwenye nyumba yako?” Hezekia akajibu, “Wameona kila kitu kwenye nyumba yangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha.”
And he says, “What did they see in your house?” And Hezekiah says, “They saw all that [is] in my house; there has not been a thing that I have not showed them among my treasures.”
16 Basi Isaya akamwambia Hezekia, “Sikiliza neno la Yahwe:
And Isaiah says to Hezekiah, “Hear a word of YHWH:
17 'Tazama siku zinakuja wakati kila kitu kwenye kwenye nyumba yako ya kifalme, vitu ambavyo babu zako walivitunza huko hadi leo, vitabebwa kwenda Babeli. Hakuna kitakachobakia, Yahwe asema.
Behold, days are coming, and all that [is] in your house, and [all] that your father has treasured up until this day, has been carried to Babylon; there is not a thing left, said YHWH;
18 Watoto waliozaliwa na wewe, ambao umewazaa wewe mwenyewe-watawachukua mbali, na watakuwa matowashi kwenye nyumba ya kifalme ya mfalme wa Babeli.'”
and of your sons who go out from you, whom you beget, they take away, and they have been eunuchs in the palace of the king of Babylon.”
19 Hezekia akamwambia Isaya, “neno la Yahwe uliloliongea ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, Je sivyo ikiwapo amani na kweli katika siku zangu?”
And Hezekiah says to Isaiah, “The word of YHWH that you have spoken [is] good”; and he says, “Why not, if there is peace and truth in my days?”
20 Kama kwa mambo mengine yanamuhusu Hezekia, na ushujaa wake wote, na jinsi alivyotengeza bwawa la maji na mfereji, na kuleta maji kwenye mji-hayakuandikwa kwenye kitabu cha ya matukio ya wafalme wa Yuda?
And the rest of the matters of Hezekiah, and all his might, and how he made the pool, and the conduit, and brings in the waters to the city, are they not written on the scroll of the Chronicles of the Kings of Judah?
21 Hezekia akalala na babu zake, na Manase mwanae akawa mfalme katika sehemu yake.
And Hezekiah lies with his fathers, and his son Manasseh reigns in his stead.

< 2 Wafalme 20 >