< 2 Wafalme 2 >
1 Hivyo ilipokuja kuhusu, wakati Yahwe alipokuwa akienda kumchukua Eliya kwenda mbinguni kwa uvumi, ambapo Eliya aliondoka pamoja na Elisha kutoka Gigali.
Now it happened that, when the Lord willed to lift up Elijah into heaven by a whirlwind, Elijah and Elisha were going out of Gilgal.
2 Eliya akamwambia Elisha, '“kaa hapa, tafadhali, kwa sababu Yahwe alinituma kwa Betheli.'” Elisha akajibu, “Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.'” Hivyo wakashuka chini kulekea Betheli.
And Elijah said to Elisha: “Remain here. For the Lord has sent me as far as Bethel.” And Elisha said to him, “As the Lord lives, and as your soul lives, I will not forsake you.” And when they had descended to Bethel,
3 Wana wa manabii ambao walikuwa Betheli walikuja kwa Elisha na kumwambia, je unajua kwamba Yahwe atamwondoa bwana wako kuanzia leo?”' Elisha akajibu, “Ndiyo, nalijua hilo, ila msizungumze kuhusu hilo.”'
the sons of the prophets, who were at Bethel, went out to Elisha. And they said to him, “Do you not know that today the Lord will take away your lord from you?” And he responded: “I know it. Be silent.”
4 Eliya akamwambia, “Elisha, subiri hapa, tafadhali, kwa kuwa Yahwe amenituma niende Yeriko.” Kisha Elisha akajibu, '“Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
Then Elijah said to Elisha: “Remain here. For the Lord has sent me to Jericho.” And he said, “As the Lord lives, and as your soul lives, I will not forsake you.” And when they had arrived at Jericho,
5 Kisha wana wa manabii ambao walikuwa Yeriko wakaja kwa Elisha na kumwambia, “'Je unajua kwamba Yahwe atamwondoa bwana wako kutoka kwako leo?” Elisha akajibu, “Ndiyo, nalijua hilo, lakini msilizungumzie hilo.”
the sons of the prophets, who were at Jericho, drew near to Elisha. And they said to him, “Do you not know that today the Lord will take away your lord from you?” And he said: “I know it. Be silent.”
6 Kisha Eliya akamwambia, '“kaa hapa, tafadhali, kwa kuwa Yahwe amenituma kwenda Yeriko.” Elisha akajibu, “Kama Yahwe ishivyo, na kama uishivyo, sintokuacha.” Hivyo wawili wakaenda mbele.
Then Elijah said to him: “Remain here. For the Lord has sent me as far as the Jordan.” And he said, “As the Lord lives, and as your soul lives, I will not forsake you.” And so, the two of them continued on together.
7 Baadaye watu hamsini wa watoto wa wale manabii wakasimama kuwakabili kwa mbali kidogo wale wawili wakasimama karibu na Yordani.
And fifty men from the sons of the prophets followed them, and they stood opposite them, at a distance. But the two of them were standing above the Jordan.
8 Eliya akachukua vazi lake, akaliviringisha, na kuyapiga maji kwa kutumia lile vazi. Ule mto ukagawanyika katika sehemu mbili hivyo basi wawili hao wakatembea hadi nchi kavu.
And Elijah took his cloak, and he rolled it up, and he struck the waters, which were divided into two parts. And they both went across on dry ground.
9 Ilitokea, walipokwisha kuvuka, kwamba Eliya akamwambia Elisha, “Niambie unachotaka nifanye kwako kabla sijaondolewa kutoka kwako.” Elisha akajibu, “Naomba sehemu kubwa ya roho yako ije kwangu.
And when they had gone across, Elijah said to Elisha, “Ask what you wish that I may do for you, before I am taken from you.” And Elisha said, “I beg you, that twice your spirit may be accomplished in me.”
10 Eliya akajibu, “Umeomba jambo gumu. Hata hivyo, kama ukiniona wakati nitakapoondolewa kutoka kwako, hii itatokea kwako, lakini kama sivyo, haitatokea.”
And he responded: “You have requested a difficult thing. Nevertheless, if you see me when I am taken from you, you will have what you requested. But if you do not see, it shall not be.”
11 Ikawa walipokuwa bado wakienda mbele na kuzungumza, gari la kukokotwa na farasi lenye moto na farasi wa moto ikatokea, ambapo iliwatenga wale watu wawili kutoka kila mmoja, na Eliya akaenda juu kwa uvumi wa upepo kwenda mbinguni.
And as they continued on, they were conversing while walking. And behold, a fiery chariot with fiery horses divided the two. And Elijah ascended by a whirlwind into heaven.
12 Elisha akaiona akalia kwa sauti, “Baba yangu, baba yangu, gari la kukokotwa na farasi la Israeli na waendesha farasi!'” Hakumwona Eliya tena, na akashikilia nguo zake mwenyewe na kugawanya kwenye vipande viwili.
Then Elisha saw it, and he cried out: “My father, my father! The chariot of Israel with its driver!” And he saw him no more. And he took hold of his own garments, and he tore them into two parts.
13 Akachukua vazi la Eliya lililokuwa limemwangukia, na kurudi kusimama kwenye ukingo wa Yordani.
And he picked up the cloak of Elijah, which had fallen from him. And turning back, he stood above the bank of the Jordan.
14 Akayapiga maji pamoja na lile vazi la Eliya alilokuwa ameliangusha na kusema, “Yahwe yuko wapi, Mungu wa Eliya?'” Wakati alipoyapiga yale maji, yaligawanyika katika pande mbili na Elisha akavuka.
And he struck the waters with the cloak of Elijah, which had fallen from him, and they were not divided. And he said, “Where is the God of Elijah, even now?” And he struck the waters, and they were divided here and there. And Elisha went across.
15 Wakati hao wana wa manabii ambao walitoka Yeriko walipomuona akikatiza kwao, wakasema, “roho ya Eliya imepumzika kwa Elisha!” Hivyo wakaja kuonana naye, na wakasujudu aridhini mbele yake.
Then the sons of the prophets, who were at Jericho, watching from a distance, said, “The spirit of Elijah has rested upon Elisha.” And approaching to meet him, they reverenced him prone on the ground.
16 Wakamwambia, “Ona sasa, miongoni mwa watumishi wako kuna watu hamsini hodari. Tunakuomba Waache waende, na kumtafuta bwana wako, endapo huyo Roho wa Yahwe alipomchukua juu na kumtupa juu ya mlima mmoja au kwenye bonde moja.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
And they said to him, “Behold, with your servants there are fifty strong men, who are able to go forth and to seek your lord. For perhaps, the Spirit of the Lord has taken him up and cast him upon some mountain, or into some valley.” But he said, “Do not send them.”
17 Lakini walimsihi Elisha hadi akaona aibu, akasema, “Watume.”Ndipo wakawatuma watu hamsini, na wakatafuta kwa mda wa siku tatu, lakini hawakumpata.
And they urged him, until he acquiesced and said, “Send them.” And they sent fifty men. And after they had searched for three days, they did not find him.
18 Wakarudi kwa Elisha, wakati alipokuwa bado yuko Yeriko, na akasema, “Je sikusema, 'msiende'?”
And they returned to him, for he was living in Jericho. And he said to them: “Did I not say to you, ‘Do not send them?’”
19 Watu wa mjini wakamwambia Elisha, “Ona, tunakuomba, hali ya mjini hapa ni pazuri, kama bwana wangu awezavyo kuona, lakini maji ni mabaya na hiyo nchi haiwezi kuzaa matunda.”
Also, the men of the city said to Elisha: “Behold, this city is a very good habitation, as you yourself perceive, O lord. But the waters are very bad, and the ground is barren.”
20 Elisha akajibu, “Nileteeni bakuli jipya na muweke chumvi ndani ya hilo bakuli,” hivyo wakamletea.
And so he said, “Bring a new vessel to me, and place salt in it.” And when they had brought it,
21 Elisha akaenda hadi kwenye chemichemi za maji na kutupia chumvi ndani; halafu akasema, “Yahwe asema hivi, 'Nimeyaponya haya maji. Kuanzia mda huu, hakutakuwa na kifo au nchi isiyozaa matunda.
he went out to the source of the waters, and he cast the salt into it. And he said: “Thus says the Lord: I have healed these waters, and no longer shall there be death or barrenness in them.”
22 “Hivyo hayo maji yakaponya hata leo, kwa lile neno ambalo Elisha aliongea.
Then the waters were healed, even to this day, in accord with the word of Elisha, which he spoke.
23 Ndipo Elisha akapanda kutoka pale mpaka Betheli. Naye alipokuwa akienda hadi kwenye barabara, wakatokea vijana nje ya mji na kumtania, wakamwambia, “Panda juu, wewe mwenye kipara! Panda juu, wewe mwenye kipara!”
Then he went up from there into Bethel. And as he was ascending along the way, little boys departed from the city. And they were mocking him, saying: “Go up, bald head! Go up, bald head!”
24 Elisha alipotazama nyuma yake na kuwaona; alimwambia Yahwe awalaani. Ndipo dubu wa kike wawili wakatokea kichakani na kuwajeruhi vijana arobaini na mbili.
And when he had looked back, he saw them, and he cursed them in the name of the Lord. And two bears went out from the forest, and they wounded forty-two boys among them.
25 Ndipo Elisha alipoondoka pale na kuelekea Mlima Karmeli, na kutoka huko alirudi samaria.
Then he went away from there to mount Carmel. And he returned from there into Samaria.