< 2 Wafalme 19 >
1 Ikawa kuhusu kwamba wakati Mfalme Hezekia aliposikia taazrifa zao, akararua mavazi yake, akavaa nguo za magunia, na kwenda kwenye nyumba ya Yahwe.
И бысть егда услыша царь Езекиа, и раздра ризы своя, и облечеся во вретище, и вниде в дом Господень.
2 Akamtuma Elkana, ambaye alikua msimamizi wa nyumba ya mfalme, na Shebna yule mwandishi, na wazee wa makuhani, wote walikuwa wamefunikwa na nguo za magunia, kwenda kwa Isaya mwana wa Amozi, yule nabii.
И посла Елиакима строителя, и Сомнаса книгочиа и старейшины жерцев облечены во вретище ко Исаии пророку сыну Амосову.
3 Wakamwambia, “Hezekia wakisema, 'siku hii ni siku ya mateso, shutuma, na fedheha, kwa kuwa wakati umewadia watoto kuzaliwa, lakini hakuna nguvu ili wazaliwe.
И реша ему: сице глаголет Езекиа: день скорби и обличения и прогневания день сей, яко приидоша сынове даже до болезнорождения, и крепости несть раждающей:
4 Inaweza kuwa Yahwe Mungu wako atasikia maneno yote ya amiri jeshi mkuu, ambaye mfalme wa Ashuru bwana wake amemtuma kumkaidi Mungu aliye hai, naye atayakemea yale maneno ambayo Yahwe Mungu wako aliyasikia. Sasa inua maombi yako juu kwa ajili ya mabaki yaliyo bakia hapo.”'
аще како послушает Господь Бог твой всех словес Рапсаковых, егоже и посла царь Ассирийский господин его поносити Богу живому и хулити словесы, ихже слыша Господь Бог твой, и приими молитву о останце обретающемся.
5 Hivyo watumishi wa mfalme Hezekia wakaja kwa Isaya,
И приидоша отроцы царя Езекии и ко Исаии.
6 na Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu: 'Yahwe asema hivi, “Usiyaogope maneno ambayo uliyoyasikia, pamoja na kwamba watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana.
И рече им Исаиа: сице рцыте господину вашему: тако глаголет Господь: не убойся от лица словес, ихже слышал еси, имиже похулиша Мя отроцы царя Ассирийска:
7 Tazama, nitaweka roho ndani yake, na yamkini atasikia taarifa na kurudi kwenye nchi yake mwenyewe. Nitamfanya aanguke kwa upanga katika nchi yake mwenyewe."”'
се, Аз даю ему духа, и услышит возвещение и возвратится в землю и свою: и низложу его оружием в земли и его.
8 Kisha amiri jeshi mkuu akarudi na kumkuta mfalme wa Ashuru akipigana dhidi ya Libna, kwa kuwa alisikia kwamba mfalme alikuwa ameenda kutoka Lakishi.
И возвратися Рапсак и обрете и царя Ассирийска воююща на Ловну: услыша бо, яко отступи от Лахиса.
9 Kisha Senakeribu akasikia kwamba Tirhaka mfalme wa Kushi na Misri alihamasisha kupigana dhidi yake, hivyo akatuma wajumbe tena kwa Hezekia pamoja na ujumbe:
И слыша о Фараке цари Ефиопстем, глаголя: се, изыде ратоватися с тобою. И возвратися и посла послы ко Езекии, глаголя: тако рцыте Езекии царю Иудейску:
10 “Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda, 'Asikudanganye Mungu wako unayemwamini, kusema, “Yerusalemu haitawekwa kwenye mikono ya mikono ya mfalme wa Ashuru.”
да не возносит тя Бог твой, на негоже ты надеешися глаголя: не имать предан быти Иерусалим в руце и царя Ассирийска:
11 Tazama, umesikia kwamba wafalme wa Ashuru wamemaliza nchi zote kwa kuziharibu kabisa. Kwa hiyo je utaokoka?
се, ты слышал еси вся, елика и сотвориша царие Ассирийстии всем землем, еже прокляти их, и ты ли избудеши?
12 Je wale miungu wa mataifa wamewaokoa, mataifa ambao baba zangu waliyaharibu: Gozani, Harani, Resefu, na watu wa Edeni katika Telasari?
Еда избавляюще избавиша их и бози языков, ихже расточиша отцы и мои, Гозану и Харану, и Фаресу и сыны Едомли, иже во Фалассаре?
13 Je yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme Arpadi, mfalme wa miji ya Sefarvaimu, wa Hena, na Iva?”'
Где есть царь Емафов и царь и Арфадов? И где есть царь града Сепфаруима, Ана и Ава?
14 Hezekia akapokea hii barua kutoka wale wajumbe na kuisoma. Kisha akapanda hata kwenye nyumba ya Yahwe na kuukunjua mbele yake.
И прият царь Езекиа книги от руки послов и прочте я: и вниде в храм Господень, и разгну их Езекиа пред Господем,
15 Kisha Hezekia akaomba mbele ya Yahwe na kusema, “Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya makerubi, wewe ni Mungu wa pekee juu ya tawala zote za dunia. Uliyeziumba mbingu na nchi.
и молися Езекиа пред Господем и рече: Господи Боже Израилев, седяй на Херувимех, Ты еси и Бог един бо всех царствиих земли, Ты сотворил еси небо и землю:
16 Tega sikio lako, Yahwe, na usikie. Fungua macho yako, Yahwe, na tazama, na sikia maneno ya Senakeribu, ambayo ameyatuma kumdhihaki Mungu aliye hai.
приклони, Господи, ухо Твое и услыши мя: отверзи, Господи, очи Твои и виждь, и услыши словеса Сеннахирима, яже посла поношая Тебе Богу живу:
17 Ni kweli, Yahwe, wafalme wa Ashuru ameyaharibu mataifa na nchi zao.
яко поистинне, Господи, опустошиша царие Ассирийстии языки,
18 Wameiweka miungu yao kwenye moto, kwa kuwa hawakuwa miungu lakini ilikuwa kazi ya mikono ya watu, ilikuwa miti na mawe. Hivyo Waashuru wamewaharibu.
и даша боги их на огнь, яко не бози беша, но дела руку человечу, древа и камения, и погубиша я:
19 Basi sasa, Yahwe Mungu wetu, tuokoe, nakusihi, kutoka kwenye nguvu zake, ili kwamba mamlaka zote za dunia zipate kujua yakwamba wewe, Yahwe, ndiye Mungu wa pekee.”
и ныне, Господи Боже наш, спаси ны из руки его, и уразумеют вся царствия земли, яко Ты еси Господь Бог един.
20 Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe kwa Hezekia, akisema, “Yahwe, Mungu wa Israeli asema, 'Kwasababu umeomba kwangu kuhusiana na Senakeribu mfalme wa Ashuru, nimekusikia.
И посла Исаиа сын Амосов ко Езекии, глаголя: тако глаголет Господь Бог Сил, Бог Израилев: слышах, о нихже молился еси ко Мне, о Сеннахириме царе Ассирийсте.
21 Hili ndilo neno ambalo Yahwe ameliongea kuhusu yeye: “Bikira binti Sayuni amekudharau na kukucheka kwa dharau. Binti wa Yerusalemu akatikisa kichwa juu yako.
Сие слово, еже глагола Господь на него: уничижи тя и поругася тебе девица и дщи Сионя, над тобою главою своею покива дщи Иерусалимля:
22 Je ni nani uliyemchokoza na kumtukana? Dhidi ya nani umeinua sauti yako na kuinua macho yako katika majivuno? Juu ya Mtakatifu wa Israeli!
кому поносил еси, и кого похулил еси? И на кого вознесл еси глас, и воздвигл еси на высоту очи твои? На Святаго Израилева.
23 Kupitia wajumbe wako wamemdharau Bwana, na kusema, 'Pamoja na wingi wa magari yangu ya farasi nimeenda juu ya vilele ya milima, hata juu ya kilele cha Lebanoni. Nitaikata mierezi mirefu na kuchagua miti ya mivinje huko. Nitaingia sehemu za makazi yake yaliyo mbali, msitu wake uzaao sana.
Рукою послов твоих поносил еси Господу, и рекл еси: со множеством колесниц моих взыду аз на вышнюю часть горы Ливанския, и усеку величество от кедр ея и избранныя кипарисов ея, и прииду в средину чащи Кармилския:
24 Nimechimba visima na kunywa maji mageni. Nimekausha mito yote ya Misri chini ya soli ya miguu yangu.'
аз изсуших, и пиях воды чуждыя, и опустоших стопами ног моих вся реки окрестныя:
25 Je hukusikia jinsi nilivyoagiza tangu zamani, na kuyafanya tangu siku za zamani? Sasa ninalileta kupita. Uko hapa kupunguza miji isiyoingilika kwenye rundo la maangamizi.
еда не слышал еси? Издавна ю сотворих, от дний первых создах ю и принесох ю: и бысть в холмы преселников воююших грады тверды:
26 Makazi yao, ya nguvu kidogo, imevunjwa vunjwa na aibu. Wamekuwa mimea katika shamba, majani ya kijani, majani juu kwenye dari au kwenye shamba, lililochomwa kabla halijakua.
и живущии в них изнемогоша рукою, сотрясошася и постыдешася, быша (яко) трава селная, или злачно былие, злак иже на зданиих, и попрания противу стоящаго:
27 Lakini najua kuketi kwako chini, na kutoka kwako, kuingia kwako dhidi yangu.
и седение твое, и исход твой, и вход твой разумех, и гнев твой на Мя,
28 Kwasababu kiburi chako kimeyafikia masikio yangu, Nitaweka kulabu yangu kwenye pua yako, na hatamu yangu kwenye mdomo wako; nitakurudisha nyuma kwa njia ile ile uliyoijia.”
занеже разгневался еси на Мя и шум твой вниде во ушы Мои, и вложу удицу Мою в ноздри твоя и бразду во устне твои, и возвращу тя по пути, имже пришел еси.
29 Hii ndiyo itakuwa ishara kwako: Mwaka huu mtakula vitu viotavyo porini, na katika mwaka wa pili vile vikuavyo katika huo. Lakini katika mwaka wa tatu ni lazima mpande na kuvuna, kupanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
И сие тебе знамение, (Езекие): яждь в сие лето прозябающая самородная, и в лето второе прозябающая, и в лето третие сейте семена и жните, садите винограды, и да ясте плод их:
30 Mabaki ya nyumba ya Yuda ambayo yataokoka yatachukua tena mizizi na kuzaa matunda.
и приложит спасшееся дому Иудова, оставшееся, корень доле, и сотворит плод горе,
31 Kwa kuwa mabaki yatatoka Yerusalemu, kutoka Mlima Sayuni wenye kuokoka utakuja. Wivu wa Yahwe wa majeshi utafanya hivyo.
яко из Иерусалима изыдет останок, и спасаемый из горы Сиони: ревность Господа Сил сотворит сие.
32 Kwa hiyo Yahwe asema hivi kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hatakuja kwenye huu mji wala kupiga mshale hapa. Wala hatakuja mbele yake na ngao au kujenga boma dhidi yake.
Сего ради тако глаголет Господь (Сил) на царя Ассирийска: не имать внити во град сей, и не имать устрелити нам стрелы, и не достигнет к нему щит, и не имать осыпати его землею:
33 Njia ile ile aliyoijia ndiyo njia atakayoondokea; hatoingia mji huu - hivi ndivyo asemavyo Yahwe.”
но путем, имже прииде темже возвратится, и во град сей не имать внити, глаголет Господь,
34 Kwa maana nitaulinda huu mji na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”'
и защищу град сей, еже спасти его Мене ради и Давида ради раба Моего.
35 Ikawa kuhusu usiku huo ambao malaika wa Yahwe alitoka na kuvamia kambi ya Waashuru, akawaua maaskari 185, 000. Kisha watu wakaamka asubuhi na mapema, miili ya watu waliokuwa wamekufa ilikuwa imelala kila mahali.
И бысть в нощь ону, и сниде Ангел Господнь и уби от полка Ассирийскаго сто осмьдесят и пять тысящ. И восташа заутра, и се, вся трупия мертва.
36 Hivyo Senakeribu mfalme wa Ashuru akaondoka Israeli na kwenda nyumbani na kuishi katika Ninawi.
И воста, и отиде, и возвратися Сеннахирим царь Ассирийский, и вселися в Ниневию.
37 Baadaye, alipokuwa akiabudu kwenye nyumba ya Nisroki mungu wake, watoto wake Adramaleki na Shareza wakamuua kwa upanga. Kisha wakakimbilia kwenye nchi ya Ararati. Kisha Esarhodani mwanaye akawa mfalme katika mahali pake.
И бысть ему кланяющуся во храме Месераха бога своего, и Адрамелех и Сарасар сынове его убиста его мечем: сами же бежаста в землю Араратску. И воцарися Асордан сын его вместо его.