< 2 Wafalme 19 >

1 Ikawa kuhusu kwamba wakati Mfalme Hezekia aliposikia taazrifa zao, akararua mavazi yake, akavaa nguo za magunia, na kwenda kwenye nyumba ya Yahwe.
And it came to pass, when king Hezekiah heard it, that he tore his clothes, and covered himself with sackcloth, and went into the house of Jehovah.
2 Akamtuma Elkana, ambaye alikua msimamizi wa nyumba ya mfalme, na Shebna yule mwandishi, na wazee wa makuhani, wote walikuwa wamefunikwa na nguo za magunia, kwenda kwa Isaya mwana wa Amozi, yule nabii.
And he sent Eliakim, who was over the household, and Shebna the scribe, and the elders of the priests (covered with sackcloth) to Isaiah the prophet the son of Amoz.
3 Wakamwambia, “Hezekia wakisema, 'siku hii ni siku ya mateso, shutuma, na fedheha, kwa kuwa wakati umewadia watoto kuzaliwa, lakini hakuna nguvu ili wazaliwe.
And they said to him, Thus says Hezekiah, This day is a day of trouble, and of rebuke, and of blasphemy, for the sons have come to the birth, and there is no strength to bring forth.
4 Inaweza kuwa Yahwe Mungu wako atasikia maneno yote ya amiri jeshi mkuu, ambaye mfalme wa Ashuru bwana wake amemtuma kumkaidi Mungu aliye hai, naye atayakemea yale maneno ambayo Yahwe Mungu wako aliyasikia. Sasa inua maombi yako juu kwa ajili ya mabaki yaliyo bakia hapo.”'
It may be that Jehovah thy God will hear all the words of Rabshakeh whom the king of Assyria his master has sent to defy the living God, and will rebuke the words which Jehovah thy God has heard. Therefore lift up thy prayer for the remnant that is left.
5 Hivyo watumishi wa mfalme Hezekia wakaja kwa Isaya,
So the servants of king Hezekiah came to Isaiah.
6 na Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu: 'Yahwe asema hivi, “Usiyaogope maneno ambayo uliyoyasikia, pamoja na kwamba watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana.
And Isaiah said to them, Thus shall ye say to your master, Thus says Jehovah, Do not be afraid of the words that thou have heard, with which the servants of the king of Assyria have blasphemed me.
7 Tazama, nitaweka roho ndani yake, na yamkini atasikia taarifa na kurudi kwenye nchi yake mwenyewe. Nitamfanya aanguke kwa upanga katika nchi yake mwenyewe."”'
Behold, I will put a spirit in him, and he shall hear news, and shall return to his own land. And I will cause him to fall by the sword in his own land.
8 Kisha amiri jeshi mkuu akarudi na kumkuta mfalme wa Ashuru akipigana dhidi ya Libna, kwa kuwa alisikia kwamba mfalme alikuwa ameenda kutoka Lakishi.
So Rabshakeh returned, and found the king of Assyria warring against Libnah, for he had heard that he was departed from Lachish.
9 Kisha Senakeribu akasikia kwamba Tirhaka mfalme wa Kushi na Misri alihamasisha kupigana dhidi yake, hivyo akatuma wajumbe tena kwa Hezekia pamoja na ujumbe:
And when he heard say of Tirhakah king of Ethiopia, Behold, he comes out to fight against thee, he sent messengers again to Hezekiah, saying,
10 “Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda, 'Asikudanganye Mungu wako unayemwamini, kusema, “Yerusalemu haitawekwa kwenye mikono ya mikono ya mfalme wa Ashuru.”
Thus shall ye speak to Hezekiah king of Judah, saying, Do not let thy God in whom thou trust deceive thee, saying, Jerusalem shall not be given into the hand of the king of Assyria.
11 Tazama, umesikia kwamba wafalme wa Ashuru wamemaliza nchi zote kwa kuziharibu kabisa. Kwa hiyo je utaokoka?
Behold, thou have heard what the kings of Assyria have done to all lands, by destroying them utterly. And shall thou be delivered?
12 Je wale miungu wa mataifa wamewaokoa, mataifa ambao baba zangu waliyaharibu: Gozani, Harani, Resefu, na watu wa Edeni katika Telasari?
Have the gods of the nations delivered them, which my fathers have destroyed, Gozan, and Haran, and Rezeph, and the sons of Eden that were in Telassar?
13 Je yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme Arpadi, mfalme wa miji ya Sefarvaimu, wa Hena, na Iva?”'
Where is the king of Hamath, and the king of Arpad, and the king of the city of Sepharvaim, of Hena, and Ivvah?
14 Hezekia akapokea hii barua kutoka wale wajumbe na kuisoma. Kisha akapanda hata kwenye nyumba ya Yahwe na kuukunjua mbele yake.
And Hezekiah received the letter from the hand of the messengers, and read it. And Hezekiah went up to the house of Jehovah, and spread it before Jehovah.
15 Kisha Hezekia akaomba mbele ya Yahwe na kusema, “Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya makerubi, wewe ni Mungu wa pekee juu ya tawala zote za dunia. Uliyeziumba mbingu na nchi.
And Hezekiah prayed before Jehovah, and said, O Jehovah, the God of Israel, who sits above the cherubim, thou are the God, even thou alone, of all the kingdoms of the earth. Thou have made heaven and earth.
16 Tega sikio lako, Yahwe, na usikie. Fungua macho yako, Yahwe, na tazama, na sikia maneno ya Senakeribu, ambayo ameyatuma kumdhihaki Mungu aliye hai.
Incline thine ear, O Jehovah, and hear. Open thine eyes, O Jehovah, and see. And hear the words of Sennacherib, with which he has sent for him to defy the living God.
17 Ni kweli, Yahwe, wafalme wa Ashuru ameyaharibu mataifa na nchi zao.
Of a truth, Jehovah, the kings of Assyria have laid waste the nations and their lands,
18 Wameiweka miungu yao kwenye moto, kwa kuwa hawakuwa miungu lakini ilikuwa kazi ya mikono ya watu, ilikuwa miti na mawe. Hivyo Waashuru wamewaharibu.
and have cast their gods into the fire, for they were no gods, but the work of men's hands, wood and stone. Therefore they have destroyed them.
19 Basi sasa, Yahwe Mungu wetu, tuokoe, nakusihi, kutoka kwenye nguvu zake, ili kwamba mamlaka zote za dunia zipate kujua yakwamba wewe, Yahwe, ndiye Mungu wa pekee.”
Now therefore, O Jehovah our God, save thou us, I beseech thee, out of his hand, that all the kingdoms of the earth may know that thou Jehovah are God alone.
20 Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe kwa Hezekia, akisema, “Yahwe, Mungu wa Israeli asema, 'Kwasababu umeomba kwangu kuhusiana na Senakeribu mfalme wa Ashuru, nimekusikia.
Then Isaiah the son of Amoz sent to Hezekiah, saying, Thus says Jehovah, the God of Israel, Whereas thou have prayed to me against Sennacherib king of Assyria, I have heard.
21 Hili ndilo neno ambalo Yahwe ameliongea kuhusu yeye: “Bikira binti Sayuni amekudharau na kukucheka kwa dharau. Binti wa Yerusalemu akatikisa kichwa juu yako.
This is the word that Jehovah has spoken concerning him: The virgin daughter of Zion has despised thee and laughed thee to scorn. The daughter of Jerusalem has shaken her head at thee.
22 Je ni nani uliyemchokoza na kumtukana? Dhidi ya nani umeinua sauti yako na kuinua macho yako katika majivuno? Juu ya Mtakatifu wa Israeli!
Whom have thou defied and blasphemed? And against whom have thou exalted thy voice and lifted up thine eyes on high? Even against the Holy One of Israel.
23 Kupitia wajumbe wako wamemdharau Bwana, na kusema, 'Pamoja na wingi wa magari yangu ya farasi nimeenda juu ya vilele ya milima, hata juu ya kilele cha Lebanoni. Nitaikata mierezi mirefu na kuchagua miti ya mivinje huko. Nitaingia sehemu za makazi yake yaliyo mbali, msitu wake uzaao sana.
By thy messengers thou have defied the Lord, and have said, With the multitude of my chariots I have come up to the height of the mountains, to the innermost parts of Lebanon. And I will cut down the tall cedars of it, and the choice fir trees of it. And I will enter into his farthest lodging-place, the forest of his fruitful field.
24 Nimechimba visima na kunywa maji mageni. Nimekausha mito yote ya Misri chini ya soli ya miguu yangu.'
I have dug and drunk strange waters, and with the sole of my feet I will dry up all the rivers of Egypt.
25 Je hukusikia jinsi nilivyoagiza tangu zamani, na kuyafanya tangu siku za zamani? Sasa ninalileta kupita. Uko hapa kupunguza miji isiyoingilika kwenye rundo la maangamizi.
Have thou not heard how I have done it long ago, and formed it of ancient times? Now I have brought it to pass, that thou should be to lay waste fortified cities into ruinous heaps.
26 Makazi yao, ya nguvu kidogo, imevunjwa vunjwa na aibu. Wamekuwa mimea katika shamba, majani ya kijani, majani juu kwenye dari au kwenye shamba, lililochomwa kabla halijakua.
Therefore their inhabitants were of small power, they were dismayed and confounded. They were as the grass of the field, and as the green herb, as the grass on the housetops, and as grain blasted before it is grown up.
27 Lakini najua kuketi kwako chini, na kutoka kwako, kuingia kwako dhidi yangu.
But I know thy sitting down, and thy going out, and thy coming in, and thy raging against me.
28 Kwasababu kiburi chako kimeyafikia masikio yangu, Nitaweka kulabu yangu kwenye pua yako, na hatamu yangu kwenye mdomo wako; nitakurudisha nyuma kwa njia ile ile uliyoijia.”
Because of thy raging against me, and because thine arrogance has come up into my ears, therefore I will put my hook in thy nose, and my bridle in thy lips, and I will turn thee back by the way by which thou came.
29 Hii ndiyo itakuwa ishara kwako: Mwaka huu mtakula vitu viotavyo porini, na katika mwaka wa pili vile vikuavyo katika huo. Lakini katika mwaka wa tatu ni lazima mpande na kuvuna, kupanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.
And this shall be the sign to thee: Ye shall eat this year that which grows of itself, and in the second year that which springs of the same. And in the third year sow ye, and reap, and plant vineyards, and eat the fruit of it.
30 Mabaki ya nyumba ya Yuda ambayo yataokoka yatachukua tena mizizi na kuzaa matunda.
And the remnant that is escaped of the house of Judah shall again take root downward, and bear fruit upward.
31 Kwa kuwa mabaki yatatoka Yerusalemu, kutoka Mlima Sayuni wenye kuokoka utakuja. Wivu wa Yahwe wa majeshi utafanya hivyo.
For out of Jerusalem shall go forth a remnant, and out of mount Zion those who shall escape. The zeal of Jehovah shall perform this.
32 Kwa hiyo Yahwe asema hivi kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hatakuja kwenye huu mji wala kupiga mshale hapa. Wala hatakuja mbele yake na ngao au kujenga boma dhidi yake.
Therefore thus says Jehovah concerning the king of Assyria, He shall not come to this city, nor shoot an arrow there, neither shall he come before it with shield, nor cast up a mound against it.
33 Njia ile ile aliyoijia ndiyo njia atakayoondokea; hatoingia mji huu - hivi ndivyo asemavyo Yahwe.”
By the way that he came, by the same shall he return, and he shall not come to this city, says Jehovah.
34 Kwa maana nitaulinda huu mji na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”'
For I will defend this city to save it, for my own sake, and for my servant David's sake.
35 Ikawa kuhusu usiku huo ambao malaika wa Yahwe alitoka na kuvamia kambi ya Waashuru, akawaua maaskari 185, 000. Kisha watu wakaamka asubuhi na mapema, miili ya watu waliokuwa wamekufa ilikuwa imelala kila mahali.
And it came to pass that night, that the agent of Jehovah went forth, and smote in the camp of the Assyrians a hundred eighty-five thousand. And when men arose early in the morning, behold, these were all dead bodies.
36 Hivyo Senakeribu mfalme wa Ashuru akaondoka Israeli na kwenda nyumbani na kuishi katika Ninawi.
So Sennacherib king of Assyria departed, and went and returned, and dwelt at Nineveh.
37 Baadaye, alipokuwa akiabudu kwenye nyumba ya Nisroki mungu wake, watoto wake Adramaleki na Shareza wakamuua kwa upanga. Kisha wakakimbilia kwenye nchi ya Ararati. Kisha Esarhodani mwanaye akawa mfalme katika mahali pake.
And it came to pass, as he was worshiping in the house of Nisroch his god, that Adrammelech and Sharezer smote him with the sword, and they escaped into the land of Ararat. And Esar-haddon his son reigned in his stead.

< 2 Wafalme 19 >