< 2 Wafalme 18 >

1 Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
After King Hoshea had been ruling Israel for almost three years, Hezekiah, the son of Ahaz, began to rule Judah.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala; alitawala miaka ishirini na tisa katika Yerusalemu. Jina la mama yake alikuwa anaitwa Abija; alikuwa binti wa Zekaria.
He was 25 years old when he became the king [of Judah] and he ruled from Jerusalem for 29 years. His mother was Abijah, the daughter of [a man whose name was] Zechariah.
3 Alifanya yaliyo mema usoni pa Yahwe, kufuata mfano wa yote ambayo Daudi, babu yake, aliyoyafanya.
Hezekiah did things that Yahweh considered to be right, like his ancestor King David had done.
4 Alipaondoa mahali pa juu, akaiharibu nguzo ya jiwe, akaikata hiyo nguzo ya Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ambayo Musa aliyokuwa ameifanya, kwa sababu siku zile wana wa Israeli walikuwa wakichoma ubani katika hiyo; ilikuwa inaitwa “Nehushtani.”
He destroyed the places where people worshiped Yahweh on the tops of hills, and he broke into pieces the stone pillars [for worshiping the goddess Asherah]. He also broke into pieces the bronze [replica/statue of a] snake that Moses had made. He did that because the people had named it Nehushtan, and they were burning incense in front of it to honor it.
5 Hezekia alimwamini Yahwe, Mungu wa Israeli, hivyo basi baada ya yeye hapakuwa kama yeye miongoni mwa wafalme wote wa Yuda, wala miongoni mwa wafalme ambao walikuwa kabla yake.
Hezekiah trusted in Yahweh, the God whom the Israelis [worshiped.] There was no king who ruled Judah before him or after him who was as [devoted to Yahweh as] he was.
6 Aliambatana na Yahwe. Hakuacha kumfuata lakini alizifuata amri zake, ambazo Yahwe alimwamuru Musa.
He remained loyal to Yahweh and never disobeyed him. He carefully obeyed all the commandments that Yahweh had given to Moses.
7 Hivyo Yahwe alikuwa na Hezekia, kila alipokwenda alifanikiwa. Akaasi dhidi ya mfalme wa Ashuru na hakumtumikia.
Yahweh always (helped/was with) him. He was successful in everything that he did. He rebelled against the king of Assyria and refused to (pay taxes to him/do what the king of Assyria wanted him to do).
8 Akawashambulia Wafilisti hadi Gaza na mipaka inayoizunguka, kutoka mnara wa walinzi hadi hadi mji wenye ngome.
His army defeated [the soldiers of] Philistia as far [south] as Gaza [city] and the nearby villages. They conquered the entire area, from the smallest watchtower to the largest cities surrounded by walls.
9 Katika mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru akapanda hadi Samaria na kuizunguka.
After King Hezekiah had been ruling Judah for almost four years, and when King Hoshea had been ruling Israel for almost seven years, [the army of] King Shalmaneser of Assyria invaded Israel and surrounded Samaria [city].
10 Mwishoni mwa miaka mitatu wakaichukua, katika mwaka wa sita wa Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa Hoshea mfalme wa Israeli; hivi ndivyo Samaria ilivyotekwa.
In the third year they captured the city. That was when Hezekiah has been ruling Judah for almost six years, and when Hoshea had been ruling Israel for almost nine years.
11 Basi mfalme wa Ashuru akawachukua Israeli kwenda Ashuru na kuwaweka kwenye Hala, na katika mto Habori katika Gozani, na katika mji wa Wamedi.
The king of Assyria commanded that the people of Israel be taken to Assyria. Some of them were taken to Halah [town], some were taken to a place near the Habor [River] in [the] Gozan [region], and some were taken to cities where the Mede people-group live.
12 Alifanya hivi kwasababu hakutii sauti ya Yahwe Mungu wao, lakini walikiuka makubaliano ya agano lake, yote yale ambayo Musa yule mtumishi wa Yahwe aliwaamuru. Walikataa kuyasikiliza au kuyafanya.
That happened because the Israelis did not obey Yahweh their God. They disobeyed the agreement that Yahweh had made with their ancestors, and all the laws that Moses, the man who served Yahweh [very well], had told them to obey. They would not obey those laws; they would not even listen to them.
13 Kisha katika mwaka wa kumi na nne wa mfalme Hezekia, Senakerebu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote yenye boma na kuwateka mateka.
After King Hezekiah had been ruling Judah for almost 14 years, [the army of] King Sennacherib of Assyria attacked all the cities in Judah that had walls around them. They [did not capture Jerusalem, but they] captured all the other cities.
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akatuma neno kwenda kwa mfalalme wa Yuda akatuma neno kwa mfalme wa Ashuru, ambaye alikuwa Lachishi, akisema, “Nimekuudhi. Nichukue. Popote utakaponiweka nitavumulia”. Mfalme wa Ashuru akamtaka Hezekia mfalme wa Yuda kulipa talanta mia tatu za fedha na talanta thelathini za dhahabu.
King Hezekiah sent a message to Sennacherib, while Sennacherib was in Lachish, saying “What I have done was wrong. Please [tell your soldiers to] stop attacking us. If you do that, I will pay you whatever you tell me to.” So the king of Assyria said that Hezekiah must pay to him (ten tons/9,000 kg.) of silver and (one ton/900 kg.) of gold.
15 Hivyo Hezekia akampatia fedha zote ambazo zilikuwa zimepatikana kwenye nyumba ya Yahwe na kawenye hazina nyumba ya mfalme.
So Hezekiah gave to him all the silver that was in the temple and that was stored in the king’s palace.
16 Kisha Hezekia akaikata ile dhahabu kutoka kwenye milango ya hekalu la Yahwe na kutoka juu ya nguzo; akampatia dhahabu mfalme wa Ashuru.
Hezekiah’s men also stripped the gold from the doors of the temple and the gold that he himself had put on the doorposts, and he sent all that gold to the king of Assyria.
17 Lakini mfalme wa Ashuru akalihamasisha jeshi lake kubwa, akawatuma Tartani na Rabsarisi na amiri jeshi mkuu kutoka Lakishi kwenda kwa Hezekia huko Yerusalemu. Wakasafiri hadi kwenye mabarabara na kufika nje ya Yerusalemu. Wakakaribia karibu na mfereji wa birika la juu, kwenye barabara kuu ya shamba la dobi, na kusimama hapo.
But the king of Assyria sent a large army with some of his important officials from Lachish [city] to [persuade] King Hezekiah [to surrender]. When they arrived at Jerusalem, they stood alongside the aqueduct/channel in which water flows from the upper pool into Jerusalem, near the road to the field where the women wash clothes.
18 Wakati walipokuwa wamemwita Mfalme Hezekia, Eliakimu mwana wa Hilkia, ambaye alikuwa kiongozi wa nyumba ya mfalme na Shebna mwandishi, na Joa mwana wa Asafu, anayeandika kumbukumbu, wakatoka nje kwenda kuwalaki
They sent a message requesting King Hezekiah to come to them, but the king sent three of his officials [to talk to them]. He sent Hilkiah’s son Eliakim, who supervised the palace; Shebna, the official secretary; and Asaph’s son Joah, who communicated the king’s messages to the people.
19 Basi yule amiri jeshi mkuu akawaambia wamwambie Hezekia kile alichosema mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru, amesema: “Nini chanzo cha ujasiri wako?
One of Sennacherib’s important officials told them to take this message to Hezekiah: “This is what the king of Assyria, the great king, says: ‘What are you trusting in [to rescue you] [RHQ]?
20 Unaongea maneno yasiyo na maana, kusema lipo neno na nguvu ya vita. Sasa unamtumainia nani? Nani anakupa ujasiri wa kuasi dhidi yangu?
You say that you have weapons to fight us, and some country promises [to help you], [and that will enable you to defeat us, ] but that is only talk [RHQ]. Who do you think will help you to rebel against my [soldiers from Assyria]?
21 Tazama, unatumainia kutembelea fimbo ya mwanzi huu uliopondeka wa Misri, lakini kama mtu akiutegemea, utamchapa kwenye mkono wake na kuutoboa. Hicho ndicho Farao mfalme wa Misri kwa ymtu yeyote ambaye anayemtumainia.
Listen to me! You are relying on [the army of] Egypt. But that is like [MET] using a broken reed for a walking stick on which you could lean. But it would pierce the hand of anyone who would lean on it! That is what the king of Egypt would be like for anyone who relied on him [for help].
22 Lakini kama ukiniambia, 'Tunamwamini Yahwe Mungu watu; je si yeye ambaye mahali pa juu na madhabahu Hezekia amezichukua, na kumwambia Yuda na kwa Yerusalemu, 'Lazima uabudu mbele ya hii madhabahu katika Yerusalemu'?
But perhaps you will say to me, “No, we are (relying on/trusting in) Yahweh our God [to help us].” [I would reply, ] “Is he not the one whom you [insulted by] tearing down his shrines and altars and forcing everyone in Jerusalem and [other places in] Judah to worship only in front of the altar [in Jerusalem]?”’
23 Basi kwa hiyo, nataka kukufanyia ahadi nzuri kutoka kwa bwana wangu mfalme wa Ashuru. Nitakupatia farasi elfu mbili, kama unaweza kuwatafuta kuwaendesha kwa ajili yao.
So I suggest that you make a deal between you and my master/boss, the king of Assyria. I will give you 2,000 horses, but [I do not think that] you are able to find 2,000 of your men who can ride on them!
24 Wanawezaje kumpinga hata nahodha mmoja wa watumishi walio wadogo? Mmeweka tumaini lenu katika Misri kwa magari ya farasi na waendesha farasi!
You are expecting the king of Egypt to send chariots and men riding horses [to assist you]. But they certainly would not [RHQ] be able to resist/defeat even the most insignificant/unimportant official in the army of Assyria!
25 Je nimesafiri kwenda huko juu bila Yahwe kupapigania hapa mahali na kupaharibu? Yahwe ameniambia, 'Ishambulie hii nchi na uiharibu.”'
Furthermore, (do you think that we have come to destroy Jerusalem without Yahweh’s help?/do not think that we have come to Jerusalem without Yahweh’s help.) [RHQ] It is Yahweh himself who told us to come here and destroy this land!”
26 Kisha Elikana mwana wa Hilkia, na Shebna, na Joa wakamwambia amiri jeshi mkuu, “Tafadhali ongea na watumishi wako katika lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaielewa. Usiongee nasi katika lugha ya Yuda katika masikio ya watu ambao wako ukutani.”
Then Eliakim, Shebna and Joah said to the official from Assyria, “Sir, please speak to us in your Aramaic language, because we understand it. Do not speak to us in our Hebrew language, because the people who are standing on the wall will understand it [and be frightened].”
27 Lakini yule amiri jeshi mkuu akawaambia, “Je bwana wangu amenituma kwa bwana wako na kuwachukua kuongea haya maneno? Je hajanituma kwa hawa watu ambao wameketi kwenye ukuta, ambao watakula kinyesi chao na kunywa mkojo wao wenyewe?”
But the official replied, “Do you think [RHQ] that my master sent me to say these things only to you and not to the people who are standing on the wall? [If you reject this message, ] the [people in this city] will soon need to eat their own dung and drink their own urine, just like you will, [because there will be nothing more for you to eat or drink].”
28 Kisha yule amiri jeshi mkuu akasimama na akapiga kelele kubwa kwa lugha ya Kiyahudi, akisema, “Sikilizeni neno la mfalme mkuu, mfale wa Ashuru.
Then the official stood up and shouted in the Hebrew language [to the people sitting on the wall]. He said, “Listen to this message from the great king, the king of Assyria. He says,
29 Mfalme asema, 'Msimwache Hezekia akawadanganya, kwa kuwa hataweza kuwaokoa kwenye nguvu yangu.
‘Do not allow Hezekiah to deceive you. He will not be able to rescue you from my power [MTY].
30 Msimwache Hezekia akawatumainisha katika Yahwe, akisema, “Yahwe atatuokoa hakika, na huu mji hautawekwa kwenye mkono wa mfalme wa Ashuru.'”
Do not allow him to persuade you to rely on Yahweh, saying that Yahweh will rescue you, and that the army of Assyria will never capture this city!’
31 Msikilize Hezekia, kwa kuwa hivi ndivyo mfalme wa Ashuru asemavyo: 'Fanyeni amani pamoja nami na njooni kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwenye mzabibu wake mwenyewe na kutoka kwenye mtini wake mwenyewe, na kunywa kutoka kwenye maji kwenye maji ya birika lake mwenyewe.
“Do not pay attention to what Hezekiah says! This is what the king of Assyria says: ‘Come out of the city and surrender to me. If you do that, I will arrange for each of you to drink the juice from your own grapevines, and to eat figs from your own trees, and to drink water from your own wells.
32 Mtafanya hivyo hadi nitakapokuja na kuwachukua kwenda kwenye nchi kama nchi yenu, nchi ya nafaka na divai, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya miti ya mizaituni na asali, ili muweze kuishi na sio kufa.' Msimsikilize Hezekia wakati atakapojaribu kuwashawishi, akisema, 'Yahwe atatuokoa.'
You will be able to do that until we come and take you to a land that is like your land—a land where there is grain to make bread and vineyards to [produce grapes for making] wine. It will be a land that has plenty of olive trees and honey. If you do what the king of Assyria commands, you will not die. You will continue to live. ‘Do not allow Hezekiah to persuade you to trust in Yahweh saying that he will rescue you!
33 Je miungu yeyote ya watu inayewaokoa kutoka kwenye nchi ya mfalme wa Ashuru?
The gods that people of other nations worship have never rescued them from the power [MTY] of the king of Assyria [RHQ]!
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na Arpadi? iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena, na Iva? Je imeiokoa Samaria kutoka mkono wangu?
Why were the gods of Hamath and Arpad [cities] unable to rescue their people from the king of Assyria [RHQ]? What happened to the gods of Sepharvaim, Hena, and Ivvah, [towns that we completely destroyed and their gods disappeared] [RHQ]? Did any god rescue Samaria from my power?
35 Miongoni mwa miungu yote ya nchi, je kuna mungu ambaye ameiokoa nchi yake kutoka kwenye nguvu yangu? Inawezekanaje Yahwe akaiokoa Yerusalemu kutoka kwenye uwezo wangu?”
No, none of the gods of the countries [that my army attacked] rescued their people [RHQ] from me! So why do you think that Yahweh will rescue you people of Jerusalem from my power [MTY]?’”
36 Lakini watu wakabaki kimya na hawakujibu, kwa kuwa mfalme alikuwa ameamuru, “Msimjibu.”
But the people [who were listening] stayed silent. No one said anything, because King Hezekiah had told them, “[When the official from Assyria talks to you, ] do not answer him.”
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia, ambaye alikuwa juu ya nyumba ya mfalme; Shebna yule mwandishi; na Joa mwana wa Asafu, mtunza kumbukumbu, akaja kwa Hezekia pamoja na nguo zao zilizoraruliwa, na kumpatia taarifa ya maneno ya yule amiri mkuu.
Then Eliakim the palace administrator and Shebna the court secretary and Joah the royal historian went back to Hezekiah with their clothes torn [because they were extremely distressed], and they told him what the official from Assyria had said.

< 2 Wafalme 18 >