< 2 Wafalme 18 >

1 Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
And it was in year three of Hoshea [the] son of Elah [the] king of Israel he became king Hezekiah [the] son of Ahaz [the] king of Judah.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala; alitawala miaka ishirini na tisa katika Yerusalemu. Jina la mama yake alikuwa anaitwa Abija; alikuwa binti wa Zekaria.
A son of twenty and five year[s] he was when became king he and twenty and nine year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Abi [the] daughter of Zechariah.
3 Alifanya yaliyo mema usoni pa Yahwe, kufuata mfano wa yote ambayo Daudi, babu yake, aliyoyafanya.
And he did the right in [the] eyes of Yahweh according to all that he had done David ancestor his.
4 Alipaondoa mahali pa juu, akaiharibu nguzo ya jiwe, akaikata hiyo nguzo ya Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ambayo Musa aliyokuwa ameifanya, kwa sababu siku zile wana wa Israeli walikuwa wakichoma ubani katika hiyo; ilikuwa inaitwa “Nehushtani.”
He - he removed the high places and he broke the sacred pillars and he cut down the Asherah pole and he crushed to pieces [the] snake of bronze which he had made Moses for until the days those they were [the] people of Israel making smoke to it and someone had called it Nehushtan.
5 Hezekia alimwamini Yahwe, Mungu wa Israeli, hivyo basi baada ya yeye hapakuwa kama yeye miongoni mwa wafalme wote wa Yuda, wala miongoni mwa wafalme ambao walikuwa kabla yake.
In Yahweh [the] God of Israel he trusted and after him not anyone was like him among all [the] kings of Judah and [those] who they were before him.
6 Aliambatana na Yahwe. Hakuacha kumfuata lakini alizifuata amri zake, ambazo Yahwe alimwamuru Musa.
And he clung to Yahweh not he turned aside from after him and he kept commandments his which he had commanded Yahweh Moses.
7 Hivyo Yahwe alikuwa na Hezekia, kila alipokwenda alifanikiwa. Akaasi dhidi ya mfalme wa Ashuru na hakumtumikia.
And he was Yahweh with him in all that he went out he prospered and he rebelled against [the] king of Assyria and not he served him.
8 Akawashambulia Wafilisti hadi Gaza na mipaka inayoizunguka, kutoka mnara wa walinzi hadi hadi mji wenye ngome.
He he struck down [the] Philistines to Gaza and territories its from a tower of watchmen unto a city of fortification.
9 Katika mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru akapanda hadi Samaria na kuizunguka.
And it was in the year fourth of the king Hezekiah it [was] the year seventh of Hoshea [the] son of Elah [the] king of Israel he came up Shalmaneser [the] king of Assyria on Samaria and he laid siege on it.
10 Mwishoni mwa miaka mitatu wakaichukua, katika mwaka wa sita wa Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa Hoshea mfalme wa Israeli; hivi ndivyo Samaria ilivyotekwa.
And they captured it from [the] end of three years in year six of Hezekiah it [was] year nine of Hoshea [the] king of Israel it was captured Samaria.
11 Basi mfalme wa Ashuru akawachukua Israeli kwenda Ashuru na kuwaweka kwenye Hala, na katika mto Habori katika Gozani, na katika mji wa Wamedi.
And he took into exile [the] king of Assyria Israel Assyria towards and he led them in Halah and on [the] Habor [the] river of Gozan and [the] cities of Media.
12 Alifanya hivi kwasababu hakutii sauti ya Yahwe Mungu wao, lakini walikiuka makubaliano ya agano lake, yote yale ambayo Musa yule mtumishi wa Yahwe aliwaamuru. Walikataa kuyasikiliza au kuyafanya.
On - that not they had listened to [the] voice of Yahweh God their and they had transgressed covenant his all that he had commanded Moses [the] servant of Yahweh and not they listened and not they did.
13 Kisha katika mwaka wa kumi na nne wa mfalme Hezekia, Senakerebu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote yenye boma na kuwateka mateka.
And in four-teen year of the king Hezekiah he came up Sennacherib [the] king of Assyria on all [the] cities of Judah fortified and he seized them.
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akatuma neno kwenda kwa mfalalme wa Yuda akatuma neno kwa mfalme wa Ashuru, ambaye alikuwa Lachishi, akisema, “Nimekuudhi. Nichukue. Popote utakaponiweka nitavumulia”. Mfalme wa Ashuru akamtaka Hezekia mfalme wa Yuda kulipa talanta mia tatu za fedha na talanta thelathini za dhahabu.
And he sent Hezekiah [the] king of Judah to [the] king of Assyria - Lachish towards - saying - I have sinned turn back from on me [that] which you will put on me I will bear and he imposed [the] king of Assyria on Hezekiah [the] king of Judah three hundred talent[s] of silver and thirty talent[s] of gold.
15 Hivyo Hezekia akampatia fedha zote ambazo zilikuwa zimepatikana kwenye nyumba ya Yahwe na kawenye hazina nyumba ya mfalme.
And he gave Hezekiah all the silver which was found [the] house of Yahweh and in [the] treasuries of [the] house of the king.
16 Kisha Hezekia akaikata ile dhahabu kutoka kwenye milango ya hekalu la Yahwe na kutoka juu ya nguzo; akampatia dhahabu mfalme wa Ashuru.
At the time that he cut off Hezekiah [the] doors of [the] temple of Yahweh and the door-posts which he had overlaid Hezekiah [the] king of Judah and he gave them to [the] king of Assyria.
17 Lakini mfalme wa Ashuru akalihamasisha jeshi lake kubwa, akawatuma Tartani na Rabsarisi na amiri jeshi mkuu kutoka Lakishi kwenda kwa Hezekia huko Yerusalemu. Wakasafiri hadi kwenye mabarabara na kufika nje ya Yerusalemu. Wakakaribia karibu na mfereji wa birika la juu, kwenye barabara kuu ya shamba la dobi, na kusimama hapo.
And he sent [the] king of Assyria [the] commander in chief and [the] chief court-official - and [the] chief commander from Lachish to the king Hezekiah with an army massive Jerusalem and they went up and they came Jerusalem and they went up and they came and they stood at [the] conduit of the pool upper which [is] on [the] highway of [the] field of [the] washer.
18 Wakati walipokuwa wamemwita Mfalme Hezekia, Eliakimu mwana wa Hilkia, ambaye alikuwa kiongozi wa nyumba ya mfalme na Shebna mwandishi, na Joa mwana wa Asafu, anayeandika kumbukumbu, wakatoka nje kwenda kuwalaki
And they called out to the king and he went out to them Eliakim [the] son of Hilkiah who [was] over the house and Shebna the scribe and Joah [the] son of Asaph the recorder.
19 Basi yule amiri jeshi mkuu akawaambia wamwambie Hezekia kile alichosema mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru, amesema: “Nini chanzo cha ujasiri wako?
And he said to them [the] chief commander say please to Hezekiah thus he says the king great [the] king of Assyria what? [is] the trust this which you trust.
20 Unaongea maneno yasiyo na maana, kusema lipo neno na nguvu ya vita. Sasa unamtumainia nani? Nani anakupa ujasiri wa kuasi dhidi yangu?
You have said only a word of lips counsel and strength for war now on whom? do you rely that you have rebelled against me.
21 Tazama, unatumainia kutembelea fimbo ya mwanzi huu uliopondeka wa Misri, lakini kama mtu akiutegemea, utamchapa kwenye mkono wake na kuutoboa. Hicho ndicho Farao mfalme wa Misri kwa ymtu yeyote ambaye anayemtumainia.
Now there! you rely yourself on [the] staff of reed crushed this on Egypt which he will support himself anyone on it and it will go in palm his and it will pierce it [is] thus Pharaoh [the] king of Egypt to all those [who] rely on him.
22 Lakini kama ukiniambia, 'Tunamwamini Yahwe Mungu watu; je si yeye ambaye mahali pa juu na madhabahu Hezekia amezichukua, na kumwambia Yuda na kwa Yerusalemu, 'Lazima uabudu mbele ya hii madhabahu katika Yerusalemu'?
And if you will say! to me to Yahweh God our we trust ¿ not [is] he [the one] whom he has removed Hezekiah high places his and altars his and he has said to Judah and to Jerusalem before the altar this you will bow down in Jerusalem.
23 Basi kwa hiyo, nataka kukufanyia ahadi nzuri kutoka kwa bwana wangu mfalme wa Ashuru. Nitakupatia farasi elfu mbili, kama unaweza kuwatafuta kuwaendesha kwa ajili yao.
And therefore make a wager please with master my with [the] king of Assyria and let me give to you two thousand horses if you will be able to put yourself riders on them.
24 Wanawezaje kumpinga hata nahodha mmoja wa watumishi walio wadogo? Mmeweka tumaini lenu katika Misri kwa magari ya farasi na waendesha farasi!
And how? will you turn back [the] face of [the] governor one of [the] servants of master my small and you have been relying yourself on Egypt for chariotry and for horsemen.
25 Je nimesafiri kwenda huko juu bila Yahwe kupapigania hapa mahali na kupaharibu? Yahwe ameniambia, 'Ishambulie hii nchi na uiharibu.”'
Now ¿ from without Yahweh have I come up on the place this to destroy it Yahweh he said to me go up on the land this and destroy it.
26 Kisha Elikana mwana wa Hilkia, na Shebna, na Joa wakamwambia amiri jeshi mkuu, “Tafadhali ongea na watumishi wako katika lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaielewa. Usiongee nasi katika lugha ya Yuda katika masikio ya watu ambao wako ukutani.”
And he said Eliakim [the] son of Hilkiah and Shebna and Joah to [the] chief commander speak please to servants your Aramaic for [are] understanding we and may not you speak with us [in] Judean in [the] ears of the people which [is] on the wall.
27 Lakini yule amiri jeshi mkuu akawaambia, “Je bwana wangu amenituma kwa bwana wako na kuwachukua kuongea haya maneno? Je hajanituma kwa hawa watu ambao wameketi kwenye ukuta, ambao watakula kinyesi chao na kunywa mkojo wao wenyewe?”
And he said to them [the] chief commander ¿ to master your and to you has he sent me master my to speak the words these ¿ not to the men who are sitting on the wall to eat (own excrement their *Q(K)*) and to drink ([the] water of feet their *Q(K)*) with you.
28 Kisha yule amiri jeshi mkuu akasimama na akapiga kelele kubwa kwa lugha ya Kiyahudi, akisema, “Sikilizeni neno la mfalme mkuu, mfale wa Ashuru.
And he stood [the] chief commander and he called out with a voice great [in] Judean and he spoke and he said hear [the] word of the king great [the] king of Assyria.
29 Mfalme asema, 'Msimwache Hezekia akawadanganya, kwa kuwa hataweza kuwaokoa kwenye nguvu yangu.
Thus he says the king may not he deceive you Hezekiah for not he will be able to deliver you from hand his.
30 Msimwache Hezekia akawatumainisha katika Yahwe, akisema, “Yahwe atatuokoa hakika, na huu mji hautawekwa kwenye mkono wa mfalme wa Ashuru.'”
And may not he make trust you Hezekiah to Yahweh saying certainly he will deliver us Yahweh and not it will be given the city this in [the] hand of [the] king of Assyria.
31 Msikilize Hezekia, kwa kuwa hivi ndivyo mfalme wa Ashuru asemavyo: 'Fanyeni amani pamoja nami na njooni kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwenye mzabibu wake mwenyewe na kutoka kwenye mtini wake mwenyewe, na kunywa kutoka kwenye maji kwenye maji ya birika lake mwenyewe.
May not you listen to Hezekiah for thus he says [the] king of Assyria make with me a blessing and come out to me and eat everyone own vine his and everyone own fig tree his and drink everyone [the] water of own cistern his.
32 Mtafanya hivyo hadi nitakapokuja na kuwachukua kwenda kwenye nchi kama nchi yenu, nchi ya nafaka na divai, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya miti ya mizaituni na asali, ili muweze kuishi na sio kufa.' Msimsikilize Hezekia wakati atakapojaribu kuwashawishi, akisema, 'Yahwe atatuokoa.'
Until come I and I will take you to a land like own land your a land of grain and new wine a land of bread and vineyards a land of olive tree of fresh oil and honey and live and not you will die and may not you listen to Hezekiah for he misleads you saying Yahweh he will deliver us.
33 Je miungu yeyote ya watu inayewaokoa kutoka kwenye nchi ya mfalme wa Ashuru?
¿ Really have they delivered [the] gods of the nations anyone land its from [the] hand of [the] king of Assyria.
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na Arpadi? iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena, na Iva? Je imeiokoa Samaria kutoka mkono wangu?
Where? [were] [the] gods of Hamath and Arpad where? [were] [the] gods of Sepharvaim Hena and Ivvah that they have delivered Samaria from hand my.
35 Miongoni mwa miungu yote ya nchi, je kuna mungu ambaye ameiokoa nchi yake kutoka kwenye nguvu yangu? Inawezekanaje Yahwe akaiokoa Yerusalemu kutoka kwenye uwezo wangu?”
Who? among all [the] gods of the lands [are those] which they have delivered land their from hand my that he will deliver Yahweh Jerusalem from hand my.
36 Lakini watu wakabaki kimya na hawakujibu, kwa kuwa mfalme alikuwa ameamuru, “Msimjibu.”
And they kept silent the people and not they answered him anything for [was] [the] command of the king it saying not you must answer him.
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia, ambaye alikuwa juu ya nyumba ya mfalme; Shebna yule mwandishi; na Joa mwana wa Asafu, mtunza kumbukumbu, akaja kwa Hezekia pamoja na nguo zao zilizoraruliwa, na kumpatia taarifa ya maneno ya yule amiri mkuu.
And he went Eliakim [the] son of Hilkiah who [was] over the house and Shebna the scribe and Joah [the] son of Asaph the recorder to Hezekiah torn of clothes and they told to him [the] words of [the] chief commander.

< 2 Wafalme 18 >