< 2 Wafalme 17 >

1 Katika mwaka wa kumi na moja wa Ahazi mfalme Yuda, utawala wa Hoshea mwana wa Elahi ulianza. Alitawala katika Samaria juu ya Israeli kwa muda wa miaka minane.
En la douzième année du règne d'Achaz, en Juda, Osée, fils d'Ela, commença en Samarie, sur Israël, un règne de neuf ans.
2 Alifanya yaliyo maovu usoni pa Yahwe, ila sio kama waflme wa Israeli ambao ulikuwa kabla yake.
Et il fit le mal aux yeux du Seigneur, mais non comme les rois d'Israël qui avaient existé avant lui.
3 Shalmanesa mfalme wa Ashuru akamshambulia, na Hoshea akawa mtumishi na kumletea kodi.
Salmanasar, roi des Assyriens, marcha contre lui; Osée lui fut asservi, et il lui paya un tribut.
4 Kisha mfalme wa Ashuru akaona kwamba Hoshea alikuwa na njama dhidi ya yake, kwa kuwa Hoshea aliwatuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri; pia, hakumpatia kodi mfalme wa Ashuru, kama alivyofanya mwaka hadi mwaka.
Ensuite, Salmanasar trouva en Osée une iniquité, en ce qu'il avait envoyé des messagers à Ségor, roi d'Égypte, et n'avait point payé cette année-là le tribut au roi des Assyriens; et celui-ci l'assiégea et le jeta, enchaîné, dans une prison.
5 Basi mfalme wa Ashuru akamfunga akamtia kifungoni. Kisha mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akaishambulia Samaria na kuizunguka kwa miaka mitatu.
Puis, il parcourut toute la terre d'Israël, et monta à Samarie, qu'il assiégea trois ans.
6 Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaichukua Samaria na akawapeleka Israeli hadi Ashuru. Akawaweka kwenye Hala, kwenye Habori Mto wa Gozani, na katika mji wa Wamedi.
Ce fut en la neuvième année du règne d'Osée, que Salmanasar prit Samarie, et transporta Israël en Assyrie, où il l'établit en Hala, en Habor, sur le fleuve Gozan, et sur les montagnes des Mèdes.
7 Utekwaji huu ulitokea kwa sababu wana wa Israeli walifanya dhambi dhidi ya Yahwe Mungu wao, ambaye aliwaleta kutoka nchi ya Misri, kutoka chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri. Watu walikuwa wakiabudu miungu mingine
Et cela arriva, parce que les fils d'Israël avaient péché contre le Seigneur leur Dieu, qui les avait tirés de l'Égypte, et délivrés des mains du roi Pharaon; parce qu'ils avaient craint d'autres dieux.
8 na kutembea katika matendo ya wamataifa ambao Yahwe aliwafukuza mbele ya watu wa Israeli, na katika matendo ya wafalme wa Israeli ambayo waliyokuwa wameyafanya.
Car ils avaient marché dans les voies des nations que le Seigneur avait exterminées devant les fils d'Israël, et dans celles des rois d'Israël qui avaient fait de tels péchés,
9 Wana wa Israeli wakafanya kwa siri mambo mabaya dhidi ya Yahwe Mungu wao. Wakajijengea mahala pa juu katika miji yao yote, kutoka mnara wa walinzi hadi mji wenye boma.
Et dans celles des enfants d'Israël, adonnés à des coutumes qui n'étaient point selon le Seigneur leur Dieu; ils s'étaient bâti des hauts lieux en toutes les villes, depuis les tours des guetteurs jusqu'aux cités entourées de remparts.
10 Pia wakasimamisha nguzo za mawe na Ashera juu ya kila mlima chini ya kila mti mbichi.
Et ils s'étaient dressé des colonnes dans des bois sacrés sur toutes les hautes collines, et sous tous les arbres touffus.
11 Huko wakafukiza ubani katika mahali pa juu pote, kama mataifa walivyokuwa wamefanya, ambao Yahwe aliwafukuza mbele yao. Waisraeli wakafanya mambo maovu ili kuchochea hasira ya Yahwe,
Et ils avaient fait des sacrifices sur tous les hauts lieux, comme les nations que le Seigneur avait expulsées de devant leur face; ils avaient formé de honteuses associations, ils avaient gravé des images pour irriter le Seigneur.
12 wakaabudu sanamu, ambazo Yahwe alizokuwa amewaambia, “Msifanye jambo hili.”
Et ils avaient servi des idoles au sujet desquelles le Seigneur leur avait dit: Ne faites point cette offense au Seigneur.
13 Bado Yahwe aliwashuhudia Israeli na Yuda kwa kila nabii na kila muonaji, kusema, “Geukeni kutoka nija zenu mbaya na kuzishika amri zangu na hukumu zangu, na kuwa makini kufuata ile sheria yote niliyowaamuru baba zenu, na ambayo niliwapelekea kwa watumishi wangu manabii.”
Cependant, le Seigneur protestait en Israël et en Juda par la bouche de tous ses voyants et de tous ses prophètes, disant: Détournez-vous de vos mauvaises voies, observez mes commandements et mes préceptes; suivez en toutes choses la loi que j'ai donnée à vos pères, et tout ce que je leur ai mandé par mes serviteurs les prophètes.
14 Lakini hawakuweza kusikia; badala yake walikuwa wakaidi kama baba zao ambao hawakumwamini Yahwe Mungu wao.
Mais ils ne l'écoutaient point; ils s'endurcissaient le cœur plus que ne l'avaient fait leurs pères.
15 Walizikataa sheria zake na lile agano ambalo alilifanya pamoja na babu zao, na hilo agano wakakubaliana wapewe. Wakafuata mambo yao yasiyofaa na wakawa hawafai. Wakawafuata mataifa ya kipagani ambao waliwazunguka, ambao Yahwe alikuwa amewaamuru wasiige.
Ils ne gardaient aucun des témoignages que portait le Seigneur; ils marchaient à la suite des vanités, étant vains eux-mêmes; à la suite des nations qui les entouraient, au sujet desquelles le Seigneur leur avait dit: Ne faites pas comme elles.
16 Wakazipuuza amri zote za Yahwe Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za kusubu za ndama wawili kuziabudu. Wakatengeza nguzo ya Ashera, na wakaziabudu nyota zote za mbinguni na Baali.
Ils abandonnaient les commandements du Seigneur leur Dieu; ils s'étaient fait deux génisses jetées en fonte; ils plantaient des bois sacrés; ils adoraient toute l'armée du ciel, et ils servaient Baal.
17 Wakawatupia watoto wao wakike kwa wakiume kwenye moto, wakapiga ramli na uchawi, wakajiuza wenyewe kufanya yale ambayo yalikuwa maovu usoni pa Yahwe, na kuichochea hasira yake.
Et ils faisaient passer dans la flamme de Moloch leurs fils et leurs filles; ils usaient de la divination et des présages, et ils s'attachaient à faire le mal aux yeux du Seigneur et à l'irriter.
18 Kwa hiyo Yahwe alikuwa na hasira na Israeli na kuwaondoa usoni mwake. Hakubakia mtu hata mmoja isipokuwa kabila la Yuda peke yake.
Et le Seigneur conçut un grand courroux contre Israël; il le rejeta de devant sa face, et il ne resta que la seule tribu de Juda.
19 Hata watu wa Yuda hawakushika amri za Yahwe Mungu wao, lakini badala yake walifuata mambo hayo hayo ya kipagani ambayo Israeli walifuata.
Et Juda lui-même n'observa point les commandements du Seigneur son Dieu; il marcha dans les voies d'Israël, et il répudia le Seigneur.
20 Hivyo Yahwe akawakataa vizazi vyote vya Israeli; akawatesa na kuwatia kwenye mkono wa wale wenye kuwateka nyara, hadi atakapokuwa amewatupa usoni mwake.
Et le Seigneur se courrouça contre toute la race d'Israël; il les ébranla, il les livra à tous ceux qui vinrent les piller, jusqu'à ce. qu'il les rejetât de devant sa face.
21 Akawatoa Israeli kutoka kwenye mstari wa kifalme wa Daudi, na wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nabeti mfalme. Yeroboamu akawapeleka Israeli mbali kutoka kumfuata Yahwe na kuwafanya wafanye dhambi kubwa.
Il le fit surtout parce qu'Israël ayant rejeté la maison de David, et s'étant donné pour roi Jéroboam, fils de Nabat, Jéroboam entraîna Israël hors des voies du Seigneur, et lui fit commettre un grand péché.
22 Wana wa Israeli wakafuata dhambi zote za Yeroboamu na hawakujiepusha nazo,
Car, les fils d'Israël tombèrent tous dans le péché de Jéroboam, et ils ne s'en retirèrent point,
23 basi Yahwe akawaondoa Israeli kutoka usoni pake, kama alivyokuwa amesema kupitia watumishi wake wote manabii kwamba angeweza kufanya. Hivyo Israeli walichukuliwa kutoka nchi yao kwenda Ashuru, na iko hivyo hata leo.
Jusqu'à ce que le Seigneur eût expulsé Israël de devant sa face, comme il l'en avait menacé par la voix de tous ses serviteurs les prophètes. Et Israël fut emmené en la terre des Assyriens, où il est encore de nos jours.
24 Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli na kutoka Kutha, na kutoka Ava, na kutoka Hamathi na Sefarvaimu, na kuwaweka katika mji wa Samaria na kuishi katika huo mji wake.
Ensuite, le roi des Assyriens amena des hommes de Babylone, de Chuth, d'Aïa, d'Emath, de Sepharvaïm, et il les établit en Samarie à la place des fils d'Israël; ils se partagèrent son territoire, et ils demeurèrent dans ses villes.
25 Ikatokea wakati walipoanza kuishi huko hawakumcha Yahwe. Hivyo Yahwe akatuma simba miongoni mwao ambao waliwaua baadhi yao.
Dans les premiers temps de leur séjour, ils ne craignaient point le Seigneur, et le Seigneur envoya contre eux des lions qui en tuèrent quelques- uns.
26 Basi wakaongea na mfalme wa Ashuru, wakisema, “Wale mataifa uliowaamisha na kuwaweka kwenye miji ya Samaria hawayajui mambo wanayotakiwa kuyafanya kutokana na mungu wa nchi. Hivyo alikuwa amewatuma simba kwenda kwao, na, tazama, wale simba walikuwa wakiwauua watu huko kwa sababu hawakufahamu yale mambo waliyokuwa wanatakiwa kuyafanya kwa mungu wa nchi.”
Ils le firent savoir au roi des Assyriens, disant: Les nations que tu as transportées et assises dans les villes de Samarie, ne connaissaient point les jugements du Dieu de cette terre; et il a envoyé contre eux des lions; et voilà que ces lions les tuent, parce qu'ils ne savent pas les jugements du Dieu de cette terre.
27 Kisha mfalme wa Ashuru akatoa amri, akisema, “Mchukueni mmoja wa makuhani hapo ambaye mmemleta kutoka huko, na mumwache aende na kuishi huko, na mumwache awafundishe mambo yanayotakiwa kwa mungu wa nchi.”
Et le roi des Assyriens donna ses ordres, disant: Emmenez d'ici des gens, qu'ils partent, qu'ils demeurent avec vous; ils vous éclaireront sur les jugements du Dieu de cette terre.
28 Hivyo mmoja wa makuhani ambaye walimchukua kutoka Samaria akaja na kuishi katika Betheli; akawafundisha jinsi wavyotakiwa mcha Yahwe.
Et ils emmenèrent un des prêtres qu'on avait transportés de Samarie; il s'établit à Béthel; il les éclaira, et il leur apprit comme ils devaient craindre le Seigneur.
29 Watu wa kila kabila wakajifanyia miungu yao wenyewe, na kuiweka mahala pa juu ambapo Wasamaria walifanya kila kabila katika mji ambako walipoishi.
Mais, chaque nation fabriqua ses dieux; on les plaça dans les temples des hauts lieux que les Samaritains avaient construits; chaque nation eut les siens dans les villes qu'elle habitait.
30 Watu wa Babeli wakatengeneza Sakoth Benithi; watu wa Sakoth wakatengeneza Nergali; watu wa Hamathi wakatengeza Ashima;
Ceux de Babylone avaient fabriqué Soccoth-Benith; ceux de Chuth, Ergel; ceux d'Emath, Asimath;
31 Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki. Nao Wasefarvi wakwachoma watoto wao kwenye moto kwa Adrameleki na Anameleki, wale miungu wa Sefarvaimu.
Les Evéens fabriquèrent Eblazer et Tharthac; ceux de Sepharvaïm firent le mal quand ils brûlèrent leurs fils dans les flammes d'Adra-Moloch et d'Ana- Moloch, leurs dieux.
32 Pia wakamcha Yahwe, na kuwateua kutoka miongoni mwao makuhani wa mahali pa juu, ambao waliteketeza kwa ajili yao kwenye hekalun mahali pa juu.
Ils craignaient le Seigneur; mais ils avaient établi leurs abominations dans les temples des hauts lieux qu'avaient construits les Samaritains, chacun dans la ville que sa nation habitait; ils craignaient le Seigneur; mais ils avaient institué pour eux des prêtres des hauts lieux, et ils sacrifiaient dans les temples des hauts lieux.
33 Wakamcha Yahwe na pia kuabudu miungu yao wenyewe, sawa sawa na tamaduni za mataifa kutoka miongoni mwao waliokuwa wamewachukua.
Ils craignaient le Seigneur, mais ils servirent leurs dieux selon l'usage des nations dont ils avaient été tirés.
34 Hadi siku hii ya leo wameshikilia tamaduni zao za zamani. Wala hawamwogopi Yahwe, wala hawazifuati sheria zake, torati, au amri ambazo Yahwe aliwapa watu wa Yakobo ambaye alemwita jina Israeli
Jusqu'à ce jour, ils ont agi selon leurs usages; les mêmes gens craignent le Seigneur et agissent selon leurs mœurs, selon leurs usages, et en même temps selon la loi et les préceptes que le Seigneur a donnés aux fils de Jacob, qu'il a appelé aussi Israël;
35 pamoja na ambao Yahwe alifanya agano nao na kuwaamuru, “Msiiche miungu mingine, wala kuisujudia, wala kuiabudu, wala kuitolea sadaka.
Avec qui le Seigneur fit jadis alliance, disant: Vous ne craindrez point d'autres dieux, vous ne les adorerez pas, vous ne les servirez point, vous ne leur ferez point de sacrifices.
36 Lakini Yahwe, ambaye aliwatoa kutoka nchi ya Misri kwa nguvu kubwa na mkono ulionyooshwa, yeye ndiye mnayetakiwa kumwabudu, yeye ndiye manayetakiwa kumsujudia, na yeye ndiye mnayetakiwa kumtolea sadaka.
Vous ne craindrez, vous n'adorerez, vous n'honorerez par des sacrifices que le Seigneur qui vous a ramenés d'Égypte par sa toute-puissance, et par son bras très-haut.
37 Na sheria na hukumu, na torati na amri ambazo alizoziandika kwa ajili yenu, mtazishika milele. Hivyo msiiche miungu mingine,
Vous observerez toujours les ordonnances, les jugements, la loi et les commandements qu'il a écrits, pour que vous les pratiquiez; vous ne craindrez point d'autres dieux.
38 na agano ambalo nimelifanya pamoja nanyi, hamtalisahau; wala kuicha miungu mingine.
Et vous n'abandonnerez point l'alliance qu'il a faite avec vous, et vous ne craindrez point d'autres dieux;
39 Lakini Yahwe Mungu wenu, ndiye ambaye mtakayemcha. Atawalinda mbali na nguvu ya maadui zenu,”
Vous ne craindrez que le Seigneur votre Dieu, et il vous délivrera de tous vos ennemis;
40 Hawatasikia, kwasababu waliendelea kufanya yale waliyokuwa wameyafanya nyuma.
Vous ne suivrez point les pratiques que suivent les Gentils.
41 Hivyo haya mataifa wakamcha Yahwe na pia wakaabudu sanamu zao za kuchonga, na watoto wao wakafanya hivyo hivyo na watoto wa watoto wao. Wakaendelea kufanya yale ambayo babu zao waliyoyafanya, hata leo.
Ces nations nouvelles craignaient donc le Seigneur, et elles servaient leurs idoles; et leurs fils, et les fils de leurs fils, ont fait comme leurs pères jusqu'à nos jours.

< 2 Wafalme 17 >