< 2 Wafalme 17 >
1 Katika mwaka wa kumi na moja wa Ahazi mfalme Yuda, utawala wa Hoshea mwana wa Elahi ulianza. Alitawala katika Samaria juu ya Israeli kwa muda wa miaka minane.
In the twelfth year of Ahaz king of Judah, the reign of Hoshea son of Elah began. He ruled in Samaria over Israel for nine years.
2 Alifanya yaliyo maovu usoni pa Yahwe, ila sio kama waflme wa Israeli ambao ulikuwa kabla yake.
He did what was evil in the sight of Yahweh, yet not as the kings of Israel who were before him.
3 Shalmanesa mfalme wa Ashuru akamshambulia, na Hoshea akawa mtumishi na kumletea kodi.
Shalmaneser king of Assyria attacked him, and Hoshea became his servant and brought him tribute.
4 Kisha mfalme wa Ashuru akaona kwamba Hoshea alikuwa na njama dhidi ya yake, kwa kuwa Hoshea aliwatuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri; pia, hakumpatia kodi mfalme wa Ashuru, kama alivyofanya mwaka hadi mwaka.
Then the king of Assyria realized that Hoshea had been plotting against him, for Hoshea had sent messengers to So king of Egypt; also, he offered no tribute to the king of Assyria, as he had done year by year. So the king of Assyria shut him up and bound him in prison.
5 Basi mfalme wa Ashuru akamfunga akamtia kifungoni. Kisha mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akaishambulia Samaria na kuizunguka kwa miaka mitatu.
Then the king of Assyria attacked throughout all the land, and attacked Samaria and besieged it for three years.
6 Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaichukua Samaria na akawapeleka Israeli hadi Ashuru. Akawaweka kwenye Hala, kwenye Habori Mto wa Gozani, na katika mji wa Wamedi.
In the ninth year of Hoshea, the king of Assyria took Samaria and carried Israel away to Assyria. He put them in Halah, at the Habor River of Gozan, and in the cities of the Medes.
7 Utekwaji huu ulitokea kwa sababu wana wa Israeli walifanya dhambi dhidi ya Yahwe Mungu wao, ambaye aliwaleta kutoka nchi ya Misri, kutoka chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri. Watu walikuwa wakiabudu miungu mingine
This captivity happened because the people of Israel had sinned against Yahweh their God, who had brought them up from the land of Egypt, from under the hand of Pharaoh king of Egypt. The people had been worshiping other gods
8 na kutembea katika matendo ya wamataifa ambao Yahwe aliwafukuza mbele ya watu wa Israeli, na katika matendo ya wafalme wa Israeli ambayo waliyokuwa wameyafanya.
and walking in the practices of the nations whom Yahweh had driven out before the people of Israel, and in the practices of the kings of Israel that they had done.
9 Wana wa Israeli wakafanya kwa siri mambo mabaya dhidi ya Yahwe Mungu wao. Wakajijengea mahala pa juu katika miji yao yote, kutoka mnara wa walinzi hadi mji wenye boma.
The people of Israel did secretly—against Yahweh their God—things that were not right. They built for themselves high places in all their cities, from the watchtower to the fortress.
10 Pia wakasimamisha nguzo za mawe na Ashera juu ya kila mlima chini ya kila mti mbichi.
They also set up stone pillars and Asherah poles on every high hill and under every green tree.
11 Huko wakafukiza ubani katika mahali pa juu pote, kama mataifa walivyokuwa wamefanya, ambao Yahwe aliwafukuza mbele yao. Waisraeli wakafanya mambo maovu ili kuchochea hasira ya Yahwe,
There they burned incense in all the high places, as the nations had done, those whom Yahweh had carried away before them. The Israelites performed wicked things to provoke Yahweh to anger;
12 wakaabudu sanamu, ambazo Yahwe alizokuwa amewaambia, “Msifanye jambo hili.”
they worshiped idols, about which Yahweh had said to them, “You will not do this thing.”
13 Bado Yahwe aliwashuhudia Israeli na Yuda kwa kila nabii na kila muonaji, kusema, “Geukeni kutoka nija zenu mbaya na kuzishika amri zangu na hukumu zangu, na kuwa makini kufuata ile sheria yote niliyowaamuru baba zenu, na ambayo niliwapelekea kwa watumishi wangu manabii.”
Yet Yahweh had testified to Israel and to Judah by every prophet and every seer, saying, “Turn from your evil ways and keep my commandments and my statutes, and be careful to keep all the law I commanded your fathers, and that I sent to you by my servants the prophets.”
14 Lakini hawakuweza kusikia; badala yake walikuwa wakaidi kama baba zao ambao hawakumwamini Yahwe Mungu wao.
But they would not listen; instead they were very stubborn like their fathers who did not trust in Yahweh their God.
15 Walizikataa sheria zake na lile agano ambalo alilifanya pamoja na babu zao, na hilo agano wakakubaliana wapewe. Wakafuata mambo yao yasiyofaa na wakawa hawafai. Wakawafuata mataifa ya kipagani ambao waliwazunguka, ambao Yahwe alikuwa amewaamuru wasiige.
They rejected his statutes and the covenant that he had made with their ancestors, and the covenant decrees that he had given to them. They followed useless practices and they themselves became useless. They followed the pagan nations who were around them, those that Yahweh had commanded them not to imitate.
16 Wakazipuuza amri zote za Yahwe Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za kusubu za ndama wawili kuziabudu. Wakatengeza nguzo ya Ashera, na wakaziabudu nyota zote za mbinguni na Baali.
They ignored all the commandments of Yahweh their God. They made cast metal figures of two calves to worship. They made an Asherah pole, and they worshiped all the stars of the heavens and Baal.
17 Wakawatupia watoto wao wakike kwa wakiume kwenye moto, wakapiga ramli na uchawi, wakajiuza wenyewe kufanya yale ambayo yalikuwa maovu usoni pa Yahwe, na kuichochea hasira yake.
They made their sons and daughters pass through the fire, they used divination and enchantments, they sold themselves to do that which was evil in the sight of Yahweh, and they provoked him to anger.
18 Kwa hiyo Yahwe alikuwa na hasira na Israeli na kuwaondoa usoni mwake. Hakubakia mtu hata mmoja isipokuwa kabila la Yuda peke yake.
Therefore Yahweh was very angry with Israel and removed them out of his sight. There was no one left but the tribe of Judah alone.
19 Hata watu wa Yuda hawakushika amri za Yahwe Mungu wao, lakini badala yake walifuata mambo hayo hayo ya kipagani ambayo Israeli walifuata.
Even Judah did not keep the commandments of Yahweh their God, and they followed the practices that Israel had done.
20 Hivyo Yahwe akawakataa vizazi vyote vya Israeli; akawatesa na kuwatia kwenye mkono wa wale wenye kuwateka nyara, hadi atakapokuwa amewatupa usoni mwake.
So Yahweh rejected all the descendants of Israel; he afflicted them and gave them into the hand of those who would take the possession as spoil, until he had cast them out of his sight.
21 Akawatoa Israeli kutoka kwenye mstari wa kifalme wa Daudi, na wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nabeti mfalme. Yeroboamu akawapeleka Israeli mbali kutoka kumfuata Yahwe na kuwafanya wafanye dhambi kubwa.
He tore Israel from the royal line of David, and they made Jeroboam son of Nebat king. Jeroboam drove Israel away from following Yahweh and made them commit a great sin.
22 Wana wa Israeli wakafuata dhambi zote za Yeroboamu na hawakujiepusha nazo,
The people of Israel followed all the sins of Jeroboam and they did not depart from them,
23 basi Yahwe akawaondoa Israeli kutoka usoni pake, kama alivyokuwa amesema kupitia watumishi wake wote manabii kwamba angeweza kufanya. Hivyo Israeli walichukuliwa kutoka nchi yao kwenda Ashuru, na iko hivyo hata leo.
so Yahweh removed Israel from his sight, as he had said through all his servants the prophets that he would. So Israel was carried away out of their own land to Assyria, and it is this way to this present day.
24 Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli na kutoka Kutha, na kutoka Ava, na kutoka Hamathi na Sefarvaimu, na kuwaweka katika mji wa Samaria na kuishi katika huo mji wake.
The king of Assyria brought people from Babylon and from Kuthah, and from Avva, and from Hamath and Sepharvaim, and placed them in the cities of Samaria in place of the people of Israel. They took over Samaria and lived in its cities.
25 Ikatokea wakati walipoanza kuishi huko hawakumcha Yahwe. Hivyo Yahwe akatuma simba miongoni mwao ambao waliwaua baadhi yao.
It happened at the beginning of their residence there that they did not honor Yahweh. So Yahweh sent lions among them which killed some of them.
26 Basi wakaongea na mfalme wa Ashuru, wakisema, “Wale mataifa uliowaamisha na kuwaweka kwenye miji ya Samaria hawayajui mambo wanayotakiwa kuyafanya kutokana na mungu wa nchi. Hivyo alikuwa amewatuma simba kwenda kwao, na, tazama, wale simba walikuwa wakiwauua watu huko kwa sababu hawakufahamu yale mambo waliyokuwa wanatakiwa kuyafanya kwa mungu wa nchi.”
So they spoke to the king of Assyria, saying, “The nations that you have carried away and placed in the cities of Samaria do not know the practices required by the god of the land. So he has sent lions among them, and, see, the lions are killing people there because they do not know the practices required by the god of the land.”
27 Kisha mfalme wa Ashuru akatoa amri, akisema, “Mchukueni mmoja wa makuhani hapo ambaye mmemleta kutoka huko, na mumwache aende na kuishi huko, na mumwache awafundishe mambo yanayotakiwa kwa mungu wa nchi.”
Then the king of Assyria commanded, saying, “Take one of the priests there whom you brought from there, and let him go and live there, and let him teach them the practices required by the god of the land.”
28 Hivyo mmoja wa makuhani ambaye walimchukua kutoka Samaria akaja na kuishi katika Betheli; akawafundisha jinsi wavyotakiwa mcha Yahwe.
So one of the priests whom they had carried away from Samaria came and lived in Bethel; he taught them how they should honor Yahweh.
29 Watu wa kila kabila wakajifanyia miungu yao wenyewe, na kuiweka mahala pa juu ambapo Wasamaria walifanya kila kabila katika mji ambako walipoishi.
Every ethnic group made gods of their own, and put them in the high places that the Samaritans had made—every ethnic group in the cities where they lived.
30 Watu wa Babeli wakatengeneza Sakoth Benithi; watu wa Sakoth wakatengeneza Nergali; watu wa Hamathi wakatengeza Ashima;
The people of Babylon made Succoth Benoth; the people of Kuthah made Nergal; the people of Hamath made Ashima;
31 Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki. Nao Wasefarvi wakwachoma watoto wao kwenye moto kwa Adrameleki na Anameleki, wale miungu wa Sefarvaimu.
the Avvites made Nibhaz and Tartak. The Sepharvites burned their children in the fire to Adrammelek and Anammelek, the gods of the Sepharvites.
32 Pia wakamcha Yahwe, na kuwateua kutoka miongoni mwao makuhani wa mahali pa juu, ambao waliteketeza kwa ajili yao kwenye hekalun mahali pa juu.
They also honored Yahweh, and appointed from among themselves priests of the high places, who sacrificed for them in the temples at the high places.
33 Wakamcha Yahwe na pia kuabudu miungu yao wenyewe, sawa sawa na tamaduni za mataifa kutoka miongoni mwao waliokuwa wamewachukua.
They honored Yahweh and also worshiped their own gods, in the customs of the nations from among whom they had been taken away.
34 Hadi siku hii ya leo wameshikilia tamaduni zao za zamani. Wala hawamwogopi Yahwe, wala hawazifuati sheria zake, torati, au amri ambazo Yahwe aliwapa watu wa Yakobo ambaye alemwita jina Israeli
To this day they persist in their old customs. They neither honor Yahweh, nor do they follow the statutes, decrees, the law, or the commandments that Yahweh gave to the people of Jacob—whom he named Israel—
35 pamoja na ambao Yahwe alifanya agano nao na kuwaamuru, “Msiiche miungu mingine, wala kuisujudia, wala kuiabudu, wala kuitolea sadaka.
and with whom Yahweh had made a covenant and commanded them, “You will not fear other gods, nor bow yourselves to them, nor worship them, nor sacrifice to them.
36 Lakini Yahwe, ambaye aliwatoa kutoka nchi ya Misri kwa nguvu kubwa na mkono ulionyooshwa, yeye ndiye mnayetakiwa kumwabudu, yeye ndiye manayetakiwa kumsujudia, na yeye ndiye mnayetakiwa kumtolea sadaka.
But Yahweh, who brought you up from the land of Egypt with great power and a raised arm, is the one you must honor; it is to him that you will prostrate yourselves, and it is to him that you will sacrifice.
37 Na sheria na hukumu, na torati na amri ambazo alizoziandika kwa ajili yenu, mtazishika milele. Hivyo msiiche miungu mingine,
The statutes and the decrees, the law and the commandments that he wrote for you, you will keep them forever. So you must not fear other gods,
38 na agano ambalo nimelifanya pamoja nanyi, hamtalisahau; wala kuicha miungu mingine.
and the covenant that I have made with you, you will not forget; neither will you honor other gods.
39 Lakini Yahwe Mungu wenu, ndiye ambaye mtakayemcha. Atawalinda mbali na nguvu ya maadui zenu,”
But Yahweh your God is who you will honor. He will rescue you from the might of your enemies.”
40 Hawatasikia, kwasababu waliendelea kufanya yale waliyokuwa wameyafanya nyuma.
They would not listen, because they continued to do what they had done in the past.
41 Hivyo haya mataifa wakamcha Yahwe na pia wakaabudu sanamu zao za kuchonga, na watoto wao wakafanya hivyo hivyo na watoto wa watoto wao. Wakaendelea kufanya yale ambayo babu zao waliyoyafanya, hata leo.
So these nations feared Yahweh and they also worshiped their carved figures, and their children did the same—as did their children's children. They continue to do what their ancestors did, up to this day.