< 2 Wafalme 15 >
1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
In the twenty-seventh year of Jeroboam, the king of Israel: Azariah, the son of Amaziah, reigned as king of Judah.
2 Azaria alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, na alitawala kwa mda wa miaka hamsini na mbili katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Yekolia, na alikuwa anatokea Yerusalemu.
He was sixteen years old when he had begun to reign, and he reigned for fifty-two years in Jerusalem. The name of his mother was Jecoliah of Jerusalem.
3 Alifanya yaliyo mema machoni pa Yahwe, kama baba yake Amazia alivyofanya.
And he did what was pleasing before the Lord, in accord with all that his father, Amaziah, did.
4 Lakini, mahali pa juu hapakuwa pameondolewa. Watu wakaendelea kutoa sadaka na kufukiza ubani katika mahala pa juu.
Yet truly, he did not demolish the high places. And still the people were sacrificing, and burning incense, in the high places.
5 Yhawe akampiga mfalme hivyo basi akawa na ukoma mpaka siku ya kifo chake na alikaa kwenye nyumba ya pekee. Yothamu, mtoto wa mfalme, alikuwa juu ya watu na kuwaongoza watu wa nchi.
Now the Lord struck the king, and he became a leper, even until the day of his death. And he was living in a separate house by himself. And truly, Jotham, the son of the king, governed the palace, and he judged the people of the land.
6 Kama kwa mambo mengine yanayomhusu Azaria, yote aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
Now the rest of the words of Azariah, and all that he did, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Judah?
7 Hivyo Azaria alilala pamoja na babu zake katika mji wa Daudi. Yothamu, mtoto wake, akawa mfalme katika mahala pake.
And Azariah slept with his fathers, and they buried him with his ancestors in the city of David. And Jotham, his son, reigned in his place.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane mwaka wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akatawala juu ya Israeli katika Samaria kwa miezi sita.
In the thirty-eighth year of Azariah, the king of Judah: Zechariah, the son of Jeroboam, reigned over Israel, in Samaria, for six months.
9 Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe, kama baba zake waliyoyafanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye alisababisha Israeli kuasi
And he did what is evil before the Lord, just as his fathers had done. He did not withdraw from the sins of Jeroboam, the son of Nebat, who caused Israel to sin.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya njama dhidi ya Zekaria, akamshambulia katika Ibleamu, na kumuua. Kisha akawa mfalme katika mahala pake.
Then Shallum, the son of Jabesh, conspired against him. And he struck him openly, and killed him. And he reigned in his place.
11 Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Zekaria, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
Now the rest of the words of Zechariah, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
12 Hili ndilo lililokuwa neno la Yahwe ambalo aliongea na Yehu, kusema, “Kizazi chako kitakaa katika kiti cha Israeli mpaka kizazi cha nne.” Hiyo ikatokea.
This was the word of the Lord, which he spoke to Jehu, saying: “Your sons, even to the fourth generation, shall sit upon the throne of Israel.” And so it happened.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akaanza kutawala katika mwaka wa thelathini na tisa wa Azaria mfalme wa Yuda, na kutawala kwa mwezi mmoja tu katika Samaria.
Shallum, the son of Jabesh, reigned in the thirty-ninth year of Azariah, the king of Judah. And he reigned for one month, in Samaria.
14 Menahemu mwana wa Gadi akapanda kutoka Tirza kwenda Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi hapo, katika Samria. Akamuua na kuwa mfalme katika mahali pake.
And Menahem, the son of Gadi, ascended from Tirzah. And he went into Samaria, and he struck Shallum, the son of Jabesh, in Samaria. And he killed him, and reigned in his place.
15 Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Shalumu na njama aliyoifanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafle wa Israeli.
Now the rest of the words of Shallum, and his conspiracy, by which he carried out treachery, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
16 Ndipo Menahemu akamshambulia Tifsa na wote waliokuwa pale, na mipaka yote kuzunguka Tizra, kwasababu hawakufungua kwenye mji. Hivyo akaushambulia, na akawapasua wanawake wajawazito wote katika hicho kijiji.
Then Menahem struck Tirzah, and all who were in it, and its borders around Tirzah. For they were not willing to open to him. And he killed all of its pregnant women, and he tore them open.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa Ahazia mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akaanza kutawala; alitawala kwa miaka kumi katika Samaria.
In the thirty-ninth year of Azariah, the king of Judah: Menahem, son of Gadi, reigned over Israel for ten years, in Samaria.
18 Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Katika maisha yake yote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye alifanya Israeli kufanya dhambi.
And he did what was evil before the Lord. He did not withdraw from the sins of Jeroboam, the son of Nebat, who caused Israel to sin, during all his days.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaja kinyume cha nchi, na Menahemu akampatia Pulu talanta elfu moja za fedha, hivyo msaada wa Pulu ungeweza kuwa na yeye kuimarisha utawala wa Israeli katika nchi yake.
Then Pul, the king of the Assyrians, came into the land. And Menahem gave Pul one thousand talents of silver, so that he would be a help to him, and so that he might strengthen his kingdom.
20 Menahemu akatoza hii pesa kutoka Israeli kwa kumtaka kila mtu tajiri alipe shekeli hamsini za fedha kwake kumpatia mfalme wa Ashura. Hivyo mfalme wa Ashuru akarudi na hakukaa pale katika ile nchi.
And Menahem proclaimed a tax upon Israel, on all who were powerful and wealthy, so that each one would give to the king of the Assyrians fifty shekels of silver. Then the king of the Assyrians turned back, and he did not remain in the land.
21 Kama kwa mabo mengine yanayomuhusu Menahemu, na yote aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya waflme wa Israeli?
Now the rest of the words of Menahem, and all that he did, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
22 Hivyo Menahemu akalala pamoja na babu zake, na Pekahia mtoto wake akawa mfalme katika mahala pake.
And Menahem slept with his fathers. And Pekahiah, his son, reigned in his place.
23 Katika mwaka wa hamsini wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akaanza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; alitawala kwa muda wa miaka miwili.
In the fiftieth year of Azariah, the king of Judah: Pekahiah, the son of Menahem, reigned over Israel, in Samaria, for two years.
24 Alifanya yaliyo maovu usoni pa Yahwe. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambazo kwa hizo alisababisha Israeli kufanya dhambi.
And he did what was evil before the Lord. He did not withdraw from the sins of Jeroboam, the son of Nebat, who caused Israel to sin.
25 Pekahia alikuwa na afisa aliyekuwa anaitwa Peka mwana wa Remalia, ambaye alifanya njama dhidi yake. Pamoja na watu hamsini wa Gileadi, Peka akamuua Pekahia pamoja na Argobu na Arie katika Samaria, katika ngome ya nyumba ya mfalme. Peka akamuua alipomua Pekahia akawa mfalme katika mahala pake.
Then Pekah, the son of Remaliah, his commander, conspired against him. And he struck him in Samaria, in the tower of the king’s house, near Argob and Arieh, and with him fifty men from the sons of the Gileadites. And he killed him, and reigned in his place.
26 Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Pekahia, yote aliyoyafanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
Now the rest of the words of Pekahiah, and all that he did, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa Azia mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akaanza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; alitawala miaka Ishirini.
In the fifty-second year of Azariah, the king of Judah: Pekah, the son of Remaliah, reigned over Israel, in Samaria, for twenty years.
28 Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabati, ambaye alisababisha Israeli kufanya dhambi.
And he did what was evil before the Lord. He did not withdraw from the sins of Jeroboam, the son of Nebat, who caused Israel to sin.
29 Katika siku za Peka mfalme wa Israeli, Tiglath Pileseri mfalme wa Ashuru akaja na kuichukua Iyoni, Abel Beth Maaka, Yanoa, Kadeshi, Hazori, Gileadi, na nchi yote ya Naftali. Akawachukua hao watu hadi Ashuru.
In the days of Pekah, the king of Israel, Tiglath-pileser, the king of Assyria, arrived and captured Ijon, and Abel Bethmaacah, and Janoah, and Kedesh, and Hazor, and Gilead, and Galilee, and the entire land of Naphtali. And he took them away into Assyria.
30 Hivyo Hoshea mwana wa Ela akafanya njama dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akaishambulia na kisha kumuua. Kisha akawa mfalme katika mahali pake, katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Then Hoshea, the son of Elah, conspired and carried out treachery against Pekah, the son of Remaliah. And he struck him, and killed him. And he reigned in his place, in the twentieth year of Jotham, the son of Uzziah.
31 Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Peka, yote aliyoyafanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
Now the rest of the words of Pekah, and all that he did, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Israel?
32 Katika mwaka wa pili wa Peka mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Azaria, mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
In the second year of Pekah, the son of Remaliah, the king of Israel: Jotham, son of Uzziah, reigned as king of Judah.
33 Alikuwa na umri wa miaka ishirini alipoanza kutawala; alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita katika Yerusalimu. Mama yake alikuwa anaitwa Yerusha; alikuwa binti ya Sadoki.
He was twenty-five years old when he had begun to reign, and he reigned for sixteen years in Jerusalem. The name of his mother was Jerusha, the daughter of Zadok.
34 Yotahmu alifanya yaliyo sahihi usoni pa Yahwe. Alifuata mfano wa yote baba yake Azaria aliyofanya.
And he did what was pleasing before the Lord. In accord with all that his father, Uzziah, had done, so he did.
35 Ila, mahali pa juu hapakuchukuliwa. Watu walikuwa wakitio sadaka na kufukiza ubani katika mahali pa juu. Yothamu akajenga lango la juu la nyumba ya Yahwe.
Yet truly, he did not take away the high places. And still the people were immolating, and burning incense, in the high places. But he edified the gate of the house of the Lord to be very sublime.
36 Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Yothamu, na yote aliyoyafanya, je yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
Now the rest of the words of Jotham, and all that he did, have these not been written in the book of the words of the days of the kings of Judah?
37 Katika zamani hizo Yahwe akaanza kumtuma dhidi ya Yuda Rezini mfalme wa Sahmu, na Peka mwana wa Remalia.
In those days, the Lord began to send, into Judah, Rezin, the king of Syria, and Pekah, the son of Remaliah.
38 Yothamu akalala pamoja na babu zake na akazikwa pamoja na babu zake katika mji wa Daudi, babu yake. Kisha Ahazi, mtoto wake, akwa mfalme katika mhali pake.
And Jotham slept with his fathers, and he was buried with them in the city of David, his father. And Ahaz, his son, reigned in his place.