< 2 Wafalme 14 >
1 Katika mwaka wa pili wa Yehoashi mwana wa Yehoazi, mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.
La deuxième année de Joas, fils de Joachaz, roi d’Israël, régna Amasias, fils de Joas, roi de Juda.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tanao wakati alipoanza kutawala; alitawala kwa mda wa miaka ishirini na tisa katika Yerusalemu.
Il avait vingt-cinq ans, lorsqu’il devint roi, et il régna vingt-neuf ans à Jérusalem. Sa mère s’appelait Joadan, de Jérusalem.
3 Mama yake alikuwa anaitwa Yehoyadani, wa Yerusalemu. Alifanya yale yaliyo mema usoni mwa macho ya Yahwe, sio kama baba yake Daudi. Alifanya kila kitu ambacho Yoashi, baba yake, alichukuwa amekifanya.
Il fit ce qui est droit aux yeux de Yahweh, non pas toutefois comme David, son père; il se conduisit en tout comme avait Joas, son père.
4 Lakini sehemu ya juu haikuondolewa. Watu wakaendelea kutoa dhabihu na kufukiza ubani katika sehemu mahala pa juu.
Seulement les hauts lieux ne disparurent point; le peuple continuait d’offrir des sacrifices et des parfums sur les hauts lieux.
5 Ikawa mara utawala wake ulipokuwa imara, aliwaua watumishi ambao waliokuwa wamemuua baba yake, mfalme.
Lorsque la royauté fut affermie dans sa main, il frappa ses serviteurs, qui avaient tué le roi, son père.
6 Ila hakuwaweka watoto wa wale wauaji kwenye kifo; isipokuwa, alifanya kutokana na kile kilichokuwa kimeandikwa kwenye sheria, kwenye kitabu cha Musa, kama Yahwe alivyokuwa ameamuru, akisema, “Wababa wasife kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasife kwa ajili ya makosa ya wazazi wao. Isipokuwa, kila mtu atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
Mais il ne fit pas mourir les fils des meurtriers, selon ce qui est écrit dans le livre de la loi de Moïse, où Yahweh donne ce commandement: « Les pères ne seront pas mis à mort pour les enfants, et les enfants ne seront pas mis à mort pour les pères; mais on fera mourir chacun pour son péché. »
7 Aliua maaskari elfu kumi wa Edomi kwenye bonde la chumvi; pia alimchukua Sela kwenye vita na kuiita Yoktheeli, ndivyo paitwavyo hadi leo.
Il battit dix mille Edomites dans la vallée du Sel, et il prit d’assaut Séla, et lui donna le nom de Jectéhel, qu’elle a conservé jusqu’à ce jour.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tuonane kila mmoja macho kwa macho kwenye mashinadano.”
Alors Amasias envoya des messagers à Joas, fils de Joachaz, fils de Jéhu, roi d’Israël, pour lui dire: « Viens, et voyons-nous en face. »
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akawatuma wajumbe kurudi kwa Amazia mfalme wa Yuda, akisema, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma kwa mwerezi katika Lebanuni, kusema, 'Mpatie mwanangu binti yako amuoe; lakini hayawani aliyekuwako Lebanoni akaukanyaga chini ule mbaruti.
Et Joas, roi d’Israël, envoya répondre à Amasias, roi de Juda: « L’épine qui est au Liban envoya dire au cèdre qui est au Liban: Donne ta fille pour femme à mon fils! Et les bêtes sauvages qui sont au Liban passèrent et foulèrent aux pieds l’épine.
10 Umempiga sana Edomu, na moyo wako umekuinua. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani, kwa nini unataka kujisababishia mataizo na kuanguka, wote wewe na Yuda pamoja nawe?”
Tu as, en vérité, battu les Edomites, et ton cœur s’est élevé. Glorifie-toi, et reste chez toi. Pourquoi t’engager dans le malheur, pour tomber, toi, et Juda avec toi? »
11 Lakini Amazia hakutaka kusikia. Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth Shemeshi, ambayo ilikuwa ya Yuda.
Mais Amasias ne l’écouta pas. Et Joas, roi d’Israël, monta, et ils se virent en face, lui et Amasias, roi de Juda, à Bethsamès, qui est à Juda.
12 Yuda walishindwa mbele ya Israeli, na kila mtu akakimbia nyumbani.
Juda fut battu devant Israël, et chacun s’enfuit dans sa tente.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli, akamchukua Amazia, mfalme wa Yuda mwana wa Yehoashi mwana wa Ahazia, huko Beth Shemeshi. Akaja Yerusalemu na kuuangusha chini ukuta wa Yerusalemu kutoka lango la Efraimu mpaka kwenye pembe ya lango, urefu wa mbali wa dhiraa mia nne.
Joas, roi d’Israël, prit à Bethsamès Amasias, roi de Juda, fils de Joas, fils d’Ochozias. Il vint à Jérusalem et fit une brèche de quatre cents coudées dans la muraille de Jérusalem, depuis la porte d’Ephraïm jusqu’à la porte de l’angle.
14 Akachukua dhahabu na fedha zote, na vitu vyote ambavyo vilipatikana katika nyumba ya Yahwe, na vitu vya thamani kwenye nyumba ya mfalme, pamoja na mateka pia, na kurudi samaria.
Il prit tout l’or et l’argent et tous les ustensiles qui se trouvaient dans la maison de Yahweh et dans les trésors de la maison du roi; il prit aussi des otages, et retourna à Samarie.
15 Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Yehoashi, yote aliyoyafanya, ushujaa wake, na jinsi alivyopigana na Amazia mfalme wa Yuda, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Israeli?
Le reste des actes de Joas, ce qu’il a fait, et comment il combattit avec Amasias, roi de Juda, cela n’est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois d’Israël?
16 Kisha Yehoashi akalala na wazee wake na ailizikwa katika Samaria pamoja na wafalme wa Israeli, na Yeroboamu, mwanaye, akawa mfalme katika eneo lake.
Joas se coucha avec ses pères, et il fut enterré à Samarie, avec les rois d’Israël. Jéroboam, son fils, régna à sa place.
17 Amazia mwana wa Yoashi, mfalme wa Yuda, akaishi miaka kumi na tano baada ya Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mfalme wa Israeli.
Amasias, fils de Joas, roi de Juda, vécut quinze ans après la mort de Joas, fils de Joachaz, roi d’Israël.
18 Kama ilivyo kwa mambo mengine yanayomhusu Amazia, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Yuda?
Le reste des actes d’Amasias n’est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
19 Wakafanya njama dhidi ya Amazia katika Yerusalimu, akakimbilia Lakishi. Akakimbia hadi Lakishi, lakini wakawatuma watu kumfuata hadi Lakishi na kumuua huko.
On ourdit contre lui une conspiration à Jérusalem, et il s’enfuit à Lachis; mais on envoya après lui des hommes à Lachis, et on l’y mit à mort.
20 Wakamrudisha kwa farasi, na alizikwa pamoja na wazee wake katika mji wa Saudi.
On le transporta sur des chevaux, et il fut enterré à Jérusalem avec ses pères, dans la cité de David.
21 Watu wote wa Yuda wakamchukua Uzaria, ambaye alikuwa na umri wa miaka kumi na minne, na walimfanya kuwa mfalme katika nyumba ya kifalme wa baba yake Uzaria.
Et tout le peuple de Juda prit Azarias, qui était âgé de seize ans; et on l’établit roi à la place de son père Amasias.
22 Alikuwa Uzaria ambaye alijenga Elathi na kuirudisha kwa Yuda, baada ya mfalme Uzaria akalala pamoja na mababu zake.
Azarias rebâtit Elath et la ramena à Juda, après que le roi fut couché avec ses pères.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala katika Samaria; alitawala kwa muda wa miaka arobaini na moja.
La quinzième année d’Amasias, fils de Joas, roi de Juda, Jéroboam, fils de Joas roi d’Israël, régna à Samarie; son règne fut de quarante et un ans.
24 Akafanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Hakuziacha dhambi zake za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye aliisababisha Israeli kuasi.
Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahweh; il ne se détourna d’aucun des péchés de Jéroboam, fils de Nabat, qui avait fait pécher Israël.
25 Akairudisha mipaka ya Israeli kutoka Lebo Hamathi mpaka kwenye Bahari ya Araba, kufuata amri ya neno la Yahwe, Mungu wa Israeli, ambalo aliongea kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, yule nabii, ambaye alitokea Gathi Heferi.
Il rétablit les limites d’Israël depuis l’entrée d’Emath jusqu’à la mer de l’Arabah, selon la parole de Yahweh, Dieu d’Israël, qu’il avait dite par l’organe de son serviteur Jonas, le prophète, fils d’Amathi, qui était de Geth-Chépher.
26 Kwa kuwa Yahwe aliyaona mateso ya Israeli, ambayo yalikuwa makali kwa kila mmoja, wote mtumwa na asyemtumwa, na kwamba hapakuwa na ulinzi kwa ajili ya Israeli.
Car Yahweh vit l’affliction très amère d’Israël, où il n’y avait plus ni homme marié, ni homme libre, ni personne pour venir au secours d’Israël.
27 Basi Yahwe akasema kwamba hatoweza kulifuta jina la Israeli chini ya mbingu; badala yake, aliwaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
Et Yahweh n’avait pas encore résolu d’effacer le nom d’Israël de dessous les cieux, mais il les délivra par la main de Jéroboam, fils de Joas.
28 Kama ilivyo kwa mambo mengine yamhusuyo Yeroboamu, yote aliyoyafanya, ushujaa wake, jinsi alivyo pigana vita na kuipata tena Damaskasi na Hamathi, ambayo ilikuwa ya Yuda, kwa Israeli, je hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
Le reste des actes de Jéroboam, tout ce qu’il a fait, ses exploits, comment il combattit et comment il ramena à Israël Damas et Emath qui avait appartenu à Juda, cela n’est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois d’Israël?
29 Yeroboamu akalala na mababu zake, pamoja na mfalme wa Israeli, na Zekaria mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.
Jéroboam se coucha avec ses pères, avec les rois d’Israël; et Zacharias, son fils, régna à sa place.