< 2 Wafalme 12 >

1 Katika mwaka wa saba wa Yehu, utawala wa Yoashi ulianza; alitawala kwa mda wa miaka arobaini huko Yerusalimu. Mama yake alikuwa anaitwa Sibia, wa Beersheba.
Roku siódmego Jehu począł królować Joaz, a czterdzieści lat królował w Jeruzalemie; imię matki jego było Sebija z Beersaby.
2 Yoashi akafanya yaliyo mema usoni mwa Yahwe siku zote, kwa sababu Yehoyada kuhani alimfundisha.
I czynił Joaz, co dobrego było w oczach Pańskich, po wszystkie dni swoje, których go uczył Jojada kapłan.
3 Lakini sehemu ya juu haikuchukuliwa. Watu wakaendelea kutoa sadaka na kuchoma ubani kwenye sehemu za juu.
Wszakże wyżyny nie były zniesione; jeszcze lud ofiarował i kadził na onych wyżynach.
4 Yoashi akamwambia kuhani, “Pesa zote zilizokuja kama sadaka takatifu kwenye nyumba ya Yahwe, pesa ya matumizi pesa ya watu kadiri alivyoandikiwa kila mtu, na pesa yote aonayo moyoni mwake kuileta kwenye nyumba ya Yahwe-
I rzekł Joaz do kapłanów: Wszystkie pieniądze poświęcone, które przychodzą do domu Pańskiego, pieniądze tych, którzy idą w liczbę, pieniądze każdego z osobna według szacunku jego, i wszystkie pieniądze, które ktokolwiek dobrowolnie znosi do domu Pańskiego,
5 makuhani watapokea pesa kutoka miongoni mwa mmoja wa watunza pesa na kutengeneza kila sehemu itakayoonekana imeharibika kwenye hekalu.”
Te wezmą do siebie kapłani każdy od znajomego swego; a oni naprawią skazę domu Pańskiego wszędy, gdzieby się znalazła skaza.
6 Lakini kama mwaka wa ishirini na tatu wa mfalme Yoashi, makuhani hawakuwa wameandaa kitu chochote kwenye hekalu.
I stało się roku dwudziestego i trzeciego króla Joaza, gdy jeszcze nie poprawili byli kapłani skazy domu,
7 Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na kuhani mwingine; akawaambia, “Kwa nini hamjaandaa kitu chochote kwenye hekalu? Sasa msichukue tena pesa kutoka kwa walipa kodi wenu, lakini chukueni kile kilichokuwa kikikusanywa kwa ajili ya matengenezo ya hekalu na uwapatia wale wanaoweza kufanya matengenezo.
Że wezwał król Joaz Jojady kapłana, i innych kapłanów, i mówił do nich: Przecz nie oprawujecie skazy domu? Przetoż teraz nie bierzcie pieniędzy od znajomych waszych, ale one na poprawę skazy domu oddawajcie.
8 Hivyo makuhani wakakubaliana wasichukue pesa tena kutoka kwa watu na wasitengeneze wenyewe.
I zezwolili na to kapłani; żeby nie brali pieniędzy od ludu, i żeby nie poprawiali skazy domu.
9 Badala yake, Yehoyada yule kuhani akachukua kasha, akatoboa tundu kwenye kifuniko chake, na kuliweka karibu na madhabahu, upande wa kulia kama mtu anaingia kwenye madhabahu ya Yahwe. Makuhani ambao walikuwa wakilinda mlango wa hekalu wakatumbukiza pesa zote ambazo zilizokuwa zimeletwa kwenye nyumba ya Yahwe.
Przetoż wziąwszy Jojada kapłan skrzynię jednę, uczynił dziurę w wieku jej, a postawił ją przy ołtarzu po prawej stronie, kędy wchodzono do domu Pańskiego. I kładli w nię kapłani, którzy strzegli progu, wszystkie pieniądze, które wnoszono do domu Pańskiego.
10 Ikawa walipoona kwamba kulikuwa na pesa za kutosha kwenye kasha, mwadishi wa mfalme na kuhani mkuu wakaja na kuweka pesa kwenye mifuko na kisha kuhesabu, pesa ikaonekana kwenye nyumba ya Yahwe.
A gdy widzieli, że było wiele pieniędzy w skrzyni, tedy przychodził pisarz królewski, i kapłan najwyższy, którzy zliczywszy chowali one pieniądze, które się znajdowały w domu Pańskim.
11 Wakawapa pesa ambayo ilikuwa imepimwa kwenye mikono ya watu ambao waliokuwa wanatunza nyumba ya Yahwe. Wakawalipa mafundi seremala na wajenzi ambao walikuwa wemefanya kazi kwenye nyumba ya Yahwe,
I dawali pieniądze gotowe w ręce rzemieślników, przełożonych nad robotą domu Pańskiego; a ci je wydawali na cieśle, i na robotniki, którzy poprawiali domu Pańskiego;
12 na waashi na wakata mawe, kwa ajili ya kununua mbao na kukata mawe kwa ajili ya kutengenezea nyumba ya Yahwe, na yote iliyokuwa inahitajika kulipwa kwa ajili ya kuitengeneza.
I na murarze, i na te, co ciosali kamienie, i na kupowanie drzewa, i ciosanego kamienia, ku poprawie skazy domu Pańskiego, i na wszystek nakład ku poprawie domu onego.
13 Lakini ile pesa iliyokuwa imeletwa kwenye nyumba ya Yahwe haikulipwa kwa ajili ya vikombe vya fedha, mabeseni, au dhahabu au fedha yoyote ya vyombo.
Wszakże nie sprawowano do domu Pańskiego kubków srebrnych, naczynia do muzyki, miednic, i trąb, żadnego naczynia złotego, i naczynia srebrnego, z pieniędzy, które przynoszono do domu Pańskiego;
14 Waliwapa hizi fedha wale ambao waliokuwa wamefanya kazi ya kutengeneza nyumba ya Yahwe.
Ale rzemieślnikom przełożonym nad robotą dawali je, i poprawiali za nie domu Pańskiego.
15 Pia, hakukuhitajika zile pesa zilipwe kwa ajili ya matengenezo ili kuwajibika kwa kuwa watu walizipokea nakuzilipa kwa watenda kazi, kwa sababu hawa watu walikuwa waadilifu.
A nie słuchano liczby tych ludzi, którym dawano pieniądze w ręce ich, aby wydawali rzemieślnikom, ponieważ to oni wiernie odprawowali.
16 Lakini pesa kwa ajili ya matoleo ya hatia na pesa kwa ajili ya matoleo ya dhambi hazikuwa zimeletwa kwenye hekalu la Yahwe, kwa sababu zilikuwa mali ya makuhani.
Ale pieniądze za występek, i pieniądze za grzechy, nie były wnoszone do domu Pańskiego; kapłanom się dostawały.
17 Kisha Hazaeli mfalme wa Shamu akashambuliwa na kupigana dhidi ya Gathi, na kuichukua.
Tedy wyciągnął Hazael, król Syryjski, a walczył przeciwko Giet, i wziął je. Potem obrócił Hazael twarz swoję, aby ciągnął przeciwko Jeruzalemowi.
18 Ndipo Hazaeli akageuka kuishambulia Yerusalemu. Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vitu vyote ambavyo Yehoshefati na Yehoramu na Ahazia, baba zake, wafalme wa Yuda, na kuviweka wakfu, na vile alivyokuwa ameviweka wakfu, na dhahabu zote zilizokuwa zimeonekana kwenye gala la nyumba ya Yahwe na la mfalme akawatuma kwenda kwa Ahazi mfalme wa Shamu. Kisha Hazaeli akaenda zake kutoka Yerusamu.
Przetoż wziął Joaz, król Judzki, wszystkie rzeczy poświęcone, które byli poświęcili Jozafat i Joram, i Ochozyjasz, ojcowie jego, królowie Judzcy, i to, co był sam poświęcił, i wszystko złoto, które się znalazło w skarbach domu Pańskiego, i domu królewskiego, a posłał to do Hazaela, króla Syryjskiego, i odciągnął od Jeruzalemu.
19 Kama mambo mengine yanayomuhusu Yoashi, yote aliyoyafanya, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
Ale insze sprawy Joazowe, i wszystko co czynił, azaż to nie jest napisane w kronikach o królach Judzkich?
20 Watumishi wake wakainuka na kupanga pamoja; wakamteka Yoashi katika Bethi Milo, kwenye njia ya kushukia kwa Sila.
Potem powstawszy słudzy jego sprzysięgli się między sobą i zabili Joaza w Betmello, którędy chodzą do Selli;
21 Yozakari mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri, watumishi wake, wakamshambulia na akafa. Wakamzika Yoashi pamoja na mababu zake katika mji wa Daudi, na Amazia, mtoto wake, akawa mfalme kwenye sehemu yake.
To jest, zabili go Josachar, syn Semaatowy, i Jozabad, syn Sommerowy; ci słudzy jego zabili go, i umarł. A pochowali go z ojcami jego w mieście Dawidowem, i królował Amazyjasz, syn jego, miasto niego.

< 2 Wafalme 12 >