< 2 Wafalme 11 >
1 Basi Athalia, mama yake na Ahazia, alipoona kwamba mtoto wake amekufa, aliinuka na kuwaua watoto wote wa kifalme.
И Гофолиа мати Охозиина виде, яко умре сын ея, и воста и погуби все семя царево.
2 Lakini Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu na dada wa Ahazia, akamchukua Yoashi mwana wa Ahazia, na kumficha mbali mwa miongoni mwa watoto wa mfalme waliokuwa wameuawa, wakati wote pamoja na mlezi wake; akawaweka kwenye chumba cha kulala. Wakamficha kutoka Athalia kwa hiyo hakuuawa.
Иосавееф же дщи царя Иорама, сестра Охозиина, поя Иоаса сына брата своего, и украде его от среды сынов царевых избиеных, того и доилицу его в клети постельней, и утаи его от лица Гофолиина, и не умертвиша его:
3 Alikuwa pamoja na Yehosheba, wamejificha kwenye nyumba ya Yahwe, kwa mda wa miaka sita, wakati Athalia alipotawala juu ya nchi.
и бе с нею крыемь в дому Господни шесть лет: и Гофолиа бе царствующи в земли той.
4 Katika mwaka wa saba, Yehoyada alituma ujumbe na kuleta maamiri jeshi mamia wa Wakari na wa walinzi, na kuwaleta kwake mwenyewe, ndani ya nyumba ya Yahwe. Akafanya agano pamoja nao, na kuwaapisha kiapo katika nyumba ya Yahwe. Kisha akawaonyesha mtoto wa mfalme.
И в седмое лето посла Иодай жрец, и поят стоначалники хорримски и расимски, и возведе я к себе в дом Господень, и завеща им завет Господень, и закля их пред Господем: и показа им Иодай сына царска,
5 Akawaamuru, akisema, “Hivi ndivyo mnavyotakiwa kufanya. Theluthi yenu mtakaokuja kwenye Sabato mtakuwa mkiiangalia nyumba ya mfalme,
и заповеда им, глаголя: сие слово, еже сотворите: третия часть от вас да снидет в субботу, и да стрежете стражбу дому царева во вратех,
6 na theluthi mtakuwa langoni mwa Suri, na theluthi langoni nyuma ya walinzi.”
и третия часть у дверий Пути, и третия часть у врат созади протекаюшнх, и да устрежете стражбу дому:
7 Makundi mengine mawili ambayo hayatumikii Sabato, Mtayalinda juu ya nyumba ya Yahwe kwa ajili ya mfalme.
и две части в вас, всяк исходяй в субботу, и да хранят стражбу дому Господня при цари:
8 Ni lazima mumzunguke mfalme, kila mmoja na silaha zake kwenye mkono wake. Yeyote aingiaye ndani ya safu, auwawe. Lazima mkae pamoja na mfalme kila atokapo na kila aingiapo.
и обступите царя около, кийждо оружие свое имый в руце своей, и входяй в садироф и да умрет: и будите с царем, егда входити ему и исходити.
9 Hivyo mamia ya maamri jeshi wakatii kila kitu Yehoyada kuhani alichokiamuru. Kila mmoja akachukua watu wake, wale ambao walitakiwa kuja kutumika siku ya hiyo Sabato, na wale ambao wataacha kuitumika kwenye hiyo Sabato; ndipo wakaja kwa Yehoyada kuhani.
И сотвориша стоначалницы вся, елика заповеда Иодай смысленый: и поя кийждо мужы своя, и входящыя в субботу со исходяшими в субботу, и внидоша ко Иодаю жерцу.
10 Kisha Yehoyada yule kuhani akawapa mikuki na ngao mamia wa maamri jeshi ambayo ilikuwa mali ya mfalme Daudi ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe.
И даде жрец сотником копия и щиты царя Давида, яже быша в дому Господни:
11 Basi walinzi wakasimama, kila mtu na silaha kwenye mkono wake, kutoka upande wa kuume wa hekalu, kwenda upande wa kushoto, karibu na madhabahu ya hekelu, wakimzunguka mfalme.
и быша в руках воевод и предтекущих, и сотвориша сотницы и предходящии по всему, елико заповеда им жрец. И собра жрец Господень вся люди земли в дом Господень: и сташа предтекущии, кийждо их оружие имый в руце своей, от страны дому десныя, даже да страны дому шуия жертвенныя, и дому царева около:
12 Kisha Yehoyada akamleta nje mtoto wa mfalme Yoashi, na kumvalisha taji la kifalme, na kumpatia mikataba ya agano. Kisha wakamfanya mfalme na kummiminia mafuta. Wakapiga makofi wakisema, “Mfalme na aishi!”
и изведе сына царева, и возложи на него венец (царский) и свидение, и воцари его, и помаза его. И восплескаша руками и реша: да живет царь.
13 Wakati Athalia aliposikia sauti za walinzi na za watu, alikuja kwa wale watu kwenye nyumba ya Yahwe.
И услыша Гофолиа глас предтекущих людий, и вниде к народу в дом Господень,
14 Akatazama, na, kisha, yule mfalme alikuwa amesimama kwenye nguzo, kama ilivyokuwa desturi, na manahodha na wapiga mabaragumu walikuwa karibu na mfalme. Watu wote wa nchi hiyo walikuwa wakifurahi na kupiga matarumbeta. Kisha Athalia akachana mavazi yake kwa hasira na kupiga kelele, “Uhaini! Uhaini!”
и виде, и се, царь стояше на столпе по обычаю: и бяху пред царем певцы и трубы, и вси людие земли радующеся и трубяще в трубы. И раздра Гофолиа ризы своя и возопи: измена, измена.
15 Ndipo Yehoyada yule kuhani akawaagiza maamri jeshi wa mamia ambao waliokuwa juu ya jeshi, akisema, “Mtoeni kwenye safu.” Atakayemfuata, muueni kwa upanga.” Kwa kuwa kuhani alisema, “Msimwache auawe kwenye nyumba ya Yahwe.”
И заповеда Иодай жрец стоначалником и властелем силы, и рече к ним: изведите ю вон из полков, и входяй вслед ея смертию да умрет от оружия: понеже рече жрец, да не умрет в дому Господни.
16 Hivyo wakamtwaa kadiri walivyokuwa wakiikaribia hiyo sehemu iliyokuwa na farasi wakaingia chini, na akauawa huko.
И возложиша на ню руце, и изведоша ю скопцы путем исхода коней дому царева, и умре ту.
17 Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yahwe na mfalme na watu, ambao wangekuwa watu wa Yahwe, na pia kati ya mfalme na watu.
И завеща Иодай завет между Господем и между царем и между людьми, яко быти им в люди Господни: и между царем и между людьми.
18 Basi watu wote wa nchi wakaenda kwenye nyumba ya Baali na kuingusha chini. Wakaangusha madhabahu ya Baali na sanamu zake wakazivunja vipande vipande, na kumuua Matani, mfalme wa Baali, mbele ya haya madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawachagua walinzi juu ya hekalu la Yahwe.
И внидоша вси людие земли в дом Ваалов и разбиша его, и жертвенники его и образы его сокрушиша добре, и Мафана жерца Ваалова убиша пред лицем жертвенников. И постави жрец властели в дому Господни,
19 Yehoyada akawachukua maamiri jeshi wa mamia, Wakari, walinzi, na watu wote wa nchi, na kwa pamoja wakamleta chini mfalme kutoka kwenye nyumba ya Yahwe na wakaenda kwenye nyumba ya mfalme, wakaingia kwa njia ya lango la walinzi. Yoashi akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi cha mfalme.
и взя стоначалники, и хоррима и расима, и вся люди земли, и изведе царя от дому Господня: и внидоша путем врат предтекущих дому царева, и посадиша его на престоле цареве.
20 Hivyo watu wote wa nchi wakamsifu, na nchi ilikuwa kimya baada ya Athalia kuuawa kwa upanga kwenye nyumba ya mfalme.
И возрадовашася вси людие земли, и град умолче: и Гофолию умертвиша мечем в дому цареве.
21 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba tangu alipoanza kutawala.
Сын седми лет Иоас егда нача царствовати.