< 2 Yohana 1 >
1 Kutoka kwa mzee kwenda kwa mwanamke mteule na watoto wake, ambao niwapendao katika kweli na si mimi tu, bali na wote wale wanao ifahamu kweli,
The Elder to the elect lady and her children. Truly I love you all, and not I alone, but also all who know the truth,
2 kwa sababu ya kweli iliyomo ndani yetu na itakayodumu pamoja nasi milele. (aiōn )
for the sake of the truth which is continually in our hearts and will be with us for ever. (aiōn )
3 Neema, rehema, amani zitakuwa nasi kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, katika kweli na pendo.
Grace, mercy and peace will be with us from God the Father, and from Jesus Christ the Son of the Father, in truth and love.
4 Ninafurahi sana kwamba nimegundua baadhi ya watoto wanaenenda katika kweli, kama vile tu tulivyoipokea amri hii kutoka kwa Baba.
It is an intense joy to me to have found some of your children living true Christian lives, in obedience to the command which we have received from the Father.
5 Na sasa nakusihi wewe, mwanamke, siyo kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tokea mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana sisi kwa sisi. Na huu ndiyo upendo, tunaopaswa kuenenda, kulingana na amri yake.
And now, dear lady, I pray you--writing to you, as I do, not a new command, but the one which we have had from the very beginning--let us love one another.
6 Hii ndiyo ile amri, kama mlivyoisikia tokea mwanzo, kwamba mnapaswa kuenenda katika hiyo.
The love of which I am speaking consists in our living in obedience to God's commands. God's command is that you should live in obedience to what you all heard from the very beginning.
7 Kwa kuwa wadanganyifu wengi wamesambaa katika ulimwengu, na hawakiri kwamba Yesu Kristo alikuja katika mwili. Huyu ndiye mdanganyifu na mpinga Kristo.
For many deceivers have gone out into the world--men who do not acknowledge Jesus as Christ who has come in human nature. Such a one is 'the deceiver' and 'the anti-Christ.'
8 Jiangalieni wenyewe kwamba hampotezi mambo yale tuliyokwisha fanyia kazi, lakini ili kwamba mweze kuipokea tuzo kamili.
Keep guard over yourselves, so that you may not lose the results of your good deeds, but may receive back a full reward.
9 Yeyote aendeleae mbele na hadumu katika fundisho la Kristo, hana Mungu. Yeye adumuye katika fundisho anaye Baba na Mwana pia.
No one has God, who instead of remaining true to the teaching of Christ, presses on in advance: but he who remains true to that teaching has both the Father and the Son.
10 Kama mtu anakuja kwenu na haleti fundisho hili, msimkaribishe katika nyumba zenu na msimsalimie.
If any one who comes to you does not bring this teaching, do not receive him under your roof nor bid him Farewell.
11 Kwa kuwa amsalimuye hushiriki katika matendo yake maovu.
He who bids him Farewell is a sharer in his evil deeds.
12 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, na sikutaka kuyaandika kwa karatasi na wino. Lakini natumaini kuja kwenu na kuongea uso kwa uso, kwamba furaha yetu ipate kufanywa kamili.
I have a great deal to say to you all, but will not write it with paper and ink. Yet I hope to come to see you and speak face to face, so that your happiness may be complete.
13 Watoto wa dada yenu mteule wanawasalimia.
The children of your elect sister send greetings to you.