< 2 Wakorintho 1 >
1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, na kwa waumini wote walioko katika mkoa wote wa Akaya.
Paul, an apostle of Jesus Christ, by the will of God, and Timothy my brother, to the church of God which is in Corinth, with all the saints that are in all Achaia:
2 Neema na iwe kwenu na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
grace be to you and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
3 Na asifiwe Mungu na Baba wa Bwana Yesu Kristo. Yeye ni Baba wa rehema na Mungu wa faraja yote.
Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, the Father of mercies, and the God of all comfort,
4 Mungu hutufariji sisi katika mateso yetu yote, ili kwamba tuweze kuwafariji wale walio katika mateso. Tunawafariji wengine kwa faraja ileile ambayo Mungu alitumia kutufariji sisi.
who con soles us in all our afflictions, so that we are able to comfort those who are in any affliction, with the comfort with which we ourselves are comforted by God.
5 Kwa kuwa kama vile mateso ya Kristo huongezeka kwa ajili yetu, vile vile faraja yetu huongezeka kupitia Kristo.
For as the sufferings for the Christ abound in us, so also through Christ abounds our consolation.
6 Lakini kama tunataabishwa, ni kwa ajili ya faraja yenu na wokovu wenu. Na kama tunafarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu. Faraja yenu inafanya kazi kikamilifu mnaposhiriki mateso kwa uvumilivu kama sisi pia tunavyoteseka.
And if we are afflicted, it is for your consolation and salvation, which salvation is effected by your patient endurance of the same sufferings that we also suffer; (and our hope in you is steadfast; ) or if we are consoled, it is for your comfort and salvation;
7 Na ujasiri wetu juu yenu ni thabiti. Tunajua kwamba kama vile ambavyo mnashiriki mateso, vile vile mnashiriki faraja.
because we know, that as you are partakers of the sufferings, so also you shall be partakers of the comfort.
8 Kwa kuwa hatutaki ninyi muwe wajinga, ndugu, kuhusu matatizo tuliyokuwa nayo huko Asia. Tulionewa zaidi ya vile tuwezavyo kubeba, kana kwamba hatukuwa hata na tumaini la kuishi tena.
For we do not wish you to be ignorant, brethren, concerning our affliction which came upon us in Asia, that we were exceedingly oppressed, beyond our strength, so that we despaired even of life.
9 Kweli, tulikuwa na hukumu ya kifo juu yetu. Lakini hiyo ilikuwa ni kutufanya sisi tusiweke tumaini juu yetu wenyewe, badala yake tuweke tumaini katika Mungu, afufuaye wafu.
But we have in ourselves the sentence of death, that we may not trust in ourselves, but in God, who raises the dead;
10 Alituokoa sisi kutoka hayo maafa ya mauti, na atatuokoa tena. Tumeweka ujasiri wetu katika yeye ya kwamba atatuokoa tena.
who delivered us from so great a death, and does still deliver us: in whom we have confidence, that he will continue to deliver us,
11 Atafanya hivi kama vile ninyi pia mtusaidiavyo kwa maombi yenu. Hivyo wengi watatoa shukurani kwa niaba yetu kwa ajili ya upendeleo wa neema tuliyopewa sisi kupitia maombi ya wengi.
if you also unite in prayer for our aid, that the favor bestowed on us, through the intercession of many persons, may cause thanks to be given by many for us.
12 Tunajivunia hili: ushuhuda wa dhamiri yetu. Kwa kuwa ni katika nia safi na usafi wa Mungu kwamba tulienenda wenyewe katika dunia. Tumefanya hivi hasa na ninyi, na sio katika hekima ya ulimwengu, lakini badala yake ni katika neema ya Mungu.
For the ground of our rejoicing is this: the testimony of our conscience that we have lived in the world more―abundantly, indeed, for you―in sincerity and godly purity, not in carnal wisdom, but in the grace of God.
13 Hatuwaandikii chochote ambacho hamwezi kukisoma au kuelewa. Ninaujasiri
For we write to you nothing else than what you recognize, or even acknowledge; and which I hope you will acknowledge to the end;
14 kwamba kwa sehemu mumekwisha kutuelewa. Na ninaujasiri kwamba katika siku ya Bwana Yesu tutakuwa sababu yenu kwa ajili ya kiburi chenu, kama vile mtakavyokuwa kwetu.
as some of you also acknowledge us, that we are the cause of your rejoicing, even as you, also, are of ours, in the day of the Lord Jesus.
15 Kwa sababu nilikuwa na ujasiri kuhusu hili, nilitaka kuja kwenu kwanza, ili kwamba muweze kupokea faida ya kutembelewa mara mbili.
And in this confidence I intended to go to you before, that you might have a second benefit;
16 Nilikuwa napanga kuwatembelea wakati nikielekea Makedonia. Tena nilitaka kuwatembelea tena wakati nikirudi kutoka Makedonia, na kisha ninyi kunituma mimi wakati nikielekea Uyahudi.
and by you, to pass through into Macedonia, and to come again to you from Macedonia, and be conducted by you into Judea.
17 Nilipokuwa nafikiria namna hii, je, nilikuwa nasitasita? Je ninapanga mambo kulingana na viwango vya kibinadamu, ili kwamba niseme “Ndiyo, ndiyo” na “Hapana, hapana” kwa wakati mmoja?
In forming this purpose, did I, therefore, behave with levity? or do I purpose what I purpose, according to the flesh, that there may be with me, yes yes, and no, no?
18 Lakini kama vile Mungu alivyo mwaminifu, hatusemi vyote “Ndiyo” na “Hapana.”
But God is true; for our preaching to you was not yes and no:
19 Kwa kuwa mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ambaye Silvano, Timotheo na mimi tulimtangaza miongoni mwenu, siyo “Ndiyo” na “Hapana.” Badala yake, yeye wakati wote ni “Ndiyo.”
for the Son of God, Jesus Christ, who was preached among you by us, by me and Sylvanus and Timothy, was not yes and no, but in him was yes.
20 Kwa kuwa ahadi zote za Mungu ni “Ndiyo” katika yeye. Hivyo pia kupitia yeye tunasema “Amina” kwa utukufu wa Mungu.
For whatever promises of God there are, are in him yes, and in him amen, to the glory of God by us.
21 Sasa ni Mungu ambaye hututhibitisha sisi pamoja nanyi katika Kristo, na alitutuma sisi.
For he who establishes us with you in Christ, and has anointed us, is God,
22 Aliweka muhuri juu yetu na alitupa Roho katika mioyo yetu kama dhamana ya kile ambacho angetupatia baadaye.
who has also set his seal upon us, and given us the earnest of the Spirit in our hearts.
23 Badala yake, namsihi Mungu kunishuhudia mimi kwamba sababu iliyonifanya nisije Korintho ni kwamba nisiwalemee ninyi.
But I call on God as a witness against my soul, that wishing to spare you, I did not go to Corinth;
24 Hii sio kwa sababu tunajaribu kudhibiti jinsi imani yenu inavyotakiwa kuwa. Badala yake, tunafanya pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kama mnavyosimama katika imani yenu.
not that we are lords over your faith, but fellow-workers for your joy: for by faith you stand.