< 2 Wakorintho 8 >

1 Tunawataka ninyi mjue, kaka na dada, kuhusu neema ya Mungu ambayo imetolewa kwa makanisa ya Makedonia.
Nous voulons, frères, vous faire connaître la grâce que Dieu a faite aux fidèles des Églises de Macédoine:
2 Wakati wa jaribu kubwa la mateso, wingi wa furaha yao na ongezeko la umaskini wao umezaa utjiri mkubwa wa ukarimu.
éprouvés par beaucoup d'afflictions, ils ont, dans l'abondance de leur joie et dans leur pauvreté profonde, répandu largement les richesses de leur libéralité.
3 Kwa maana nashuhudia kwamba walitoa kwa kadiri ya walivyoweza, na hata zaidi ya walivyoweza.
En effet, je leur rends ce témoignage, qu'ils ont donné de leur propre mouvement, selon leur pouvoir, et même au-delà de leur pouvoir,
4 Na kwa hiari yao wenyewe kwa kutusihi kwingi, walituomba kwa ajili ya kushiriki katika huduma hii kwa waumini.
nous demandant très instamment de leur accorder la grâce de prendre part à l'assistance destinée aux saints.
5 Hii haikutokea kama tulivyokuwa tunatarajia. Badala yake, kwanza walijitoa wao wenyewe kwa Bwana. Kisha wakajitoa wao wenyewe kwetu kwa mapenzi ya Mungu.
Et ils ont dépassé nos espérances; car ils se sont donnés eux-mêmes premièrement au Seigneur, et ensuite à nous, par la volonté de Dieu.
6 Hivyo tulimsihi Tito, aliyekuwa tayari ameanzisha kazi hii, kuleta katika utimilifu tendo hili la ukarimu juu yenu.
Aussi avons-nous prié Tite d'aller chez vous pour achever cette oeuvre de charité, comme il l'avait commencée.
7 Lakini ninyi mna wingi katika kila kitu- katika imani, katika usemi, katika maarifa, katika bidii, na katika upendo wenu kwa ajili yetu. Hivyo hakikisheni kwamba ninyi mnakuwa na wingi pia katika tendo hili la ukarimu.
Ainsi donc, comme vous excellez, à tous égards, dans la foi, dans l'éloquence, dans la connaissance, en zèle de tout genre, en amour pour nous, appliquez-vous à exceller aussi dans cette oeuvre de charité.
8 Nasema hili si kama amri. Badala yake, nasema hili ili kupima uhalisi wa upendo wenu kwa kuulinganisha na shauku ya watu wengine.
Je ne dis pas cela pour vous donner un ordre; mais, par l'exemple du zèle des autres, je voudrais mettre à l'épreuve la sincérité de votre charité.
9 Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo. Hata kama alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikuwa maskini. Ili kwamba kupitia umaskini wake mweze kuwa tajiri.
Car vous connaissez la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ, qui, étant riche, s'est fait pauvre pour vous, afin que par sa pauvreté vous fussiez rendus riches.
10 Katika jambo hili nitawapa ushauri ambao utawasaidia. Mwaka mmoja uliopita, hamkuanza tuu kufanya jambo. Lakini mlitamani kulifanya.
C'est donc un avis que je donne; et il s'adresse à vous d'autant mieux que, dès l'année dernière, vous avez été les premiers, non seulement à entreprendre cette oeuvre, mais à la vouloir.
11 Sasa likamilisheni. Kama tu kulivyokuwa na shauku na nia ya kulifanya, kisha, je, mngeweza pia kulileta katika ukamilifu, kwa kadri ya mnavyoweza.
Achevez donc maintenant votre oeuvre, afin qu'à l'ardeur de votre bonne volonté réponde aussi l'exécution, suivant vos moyens.
12 Kwa kuwa mnashauku ya kufanya tendo hili, ni jambo zuri na linakubalika. Lazima lisimame juu ya kile alichonacho mtu, siyo juu ya asichokuwa nacho mtu.
Car, si l'on donne de bon coeur, suivant ce qu'on a, — et non suivant ce qu'on n'a pas, — on est agréable à Dieu.
13 Kwa kuwa kazi hii siyo kwa ajili kwamba wengine waweze kupata nafuu na ninyi mweze kulemewa. Badala yake, kuwe na usawa.
Je ne vous demande pas, pour soulager les autres, de vous mettre vous-mêmes dans la gêne, mais je voudrais qu'il y eût de l'égalité entre vous.
14 Wingi wenu wa wakati wa sasa utasaidia kwa kile wanachohitaji. Hii ni hivyo pia ili kwamba wingi wao uweze kusaidia mahitaji yenu, na kwamba kuwe na usawa.
Dans les circonstances présentes, votre abondance suppléera à leur indigence, afin que leur abondance supplée aussi à votre indigence, et qu'ainsi il y ait égalité,
15 Hii ni kama ilivyoandikwa; “Yeye aliye na vingi hakuwa na kitu chochote kilichobaki na yeye aliyekuwa na kidogo hakuwa na uhitaji wowote.”
comme il est écrit: «Celui qui avait beaucoup recueilli n'avait pas trop, et celui qui avait peu recueilli ne manquait de rien.»
16 Lakini ashukuriwe Mungu, aliyeweka ndani ya moyo wa Tito moyo uleule wa bidii ya kujali ambyo ninayo kwa ajili yenu.
Grâces soient rendues à Dieu de ce qu'il a mis au coeur de Tite le même zèle pour vous;
17 Kwa kuwa si tu alipokea maombi yetu, bali pia alikuwa na bidii kuhusiana na maombi hayo. Alikuja kwenu kwa hiari yake mwenyewe.
car il a accueilli ma prière, et même, dans l'ardeur de son zèle, il est parti de son propre mouvement pour aller vous voir.
18 Tumemtuma pamoja naye ndugu ambaye anasifiwa miongoni mwa makanisa kwa ajili ya kazi yake katika kutangaza injili.
Nous avons envoyé avec lui le frère dont l'éloge est répandu dans toutes les Églises, à cause de ce qu'il a fait pour l'Evangile.
19 Si hivi tu, lakini pia alichaguliwa na makanisa kusafiri nasisi katika kulibeba sehemu mbalimbali tendo hili la ukarimu. Hii ni kwa utukufu wa Bwana mwenyewe na kwa shauku yetu ya kusaidia.
Bien plus, il a été choisi par les suffrages des Eglises, pour être notre compagnon de voyage dans cette oeuvre de charité que nous accomplissons à la gloire du Seigneur lui-même, et pour montrer notre bonne volonté.
20 Tunaepuka uwezekano kwamba yeyote napaswa kulalamika kuhusiana na sisi kuhusiana na ukarimu huu ambao tunaubeba.
Nous voulons éviter par là tout reproche au sujet de l'administration de cette abondante collecte;
21 Tunachukua uangalifu kufanya kilicho cha heshima, sio tu mbele za Bwana, lakini pia mbele za watu.
car nous recherchons ce qui est bien, non seulement devant le Seigneur, mais aussi devant les hommes.
22 Pia tunamtuma ndugu mwingine pamoja nao. Tumempima mara nyingi, na tumemwona ni mwenye shauku for ajili ya kazi nyingi. Hata sasa ana bidii zaidi kwa sababu ya ujasiri mkubwa alionao ndani yenu.
Nous avons encore envoyé avec eux l'un de nos frères dont nous avons plusieurs fois, en diverses occasions, éprouvé le zèle, et qui en aura beaucoup plus encore cette fois-ci, à cause de la grande confiance qu'il a en vous.
23 Kwa habari ya Tito, yeye ni mshirika mwenza wangu na mtendakazi mwenzangu kwa ajili yenu. Kama kwa ndugu zetu, wanatumwa na makanisa. Ni waheshima kwa Kristo.
Ainsi, en ce qui concerne Tite, il est mon compagnon et mon collaborateur auprès de vous; en ce qui concerne nos frères, ils sont les envoyés des Églises, la gloire du Christ.
24 Hivyo, waonesheni upendo wenu, na muoneshe kwa makanisa sababu ya majivuno yetu kwa ajili yenu.
Donnez-leur donc, à la face des Églises, des preuves de votre chanté, et montrez-leur que nous avons eu raison de leur faire un si grand éloge de vous.

< 2 Wakorintho 8 >