< 2 Wakorintho 7 >

1 Wapendwa wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizi, na tujitakase wenyewe kwa kila jambo ambalo linatufanya kuwa wachafu katika miili yetu na katika roho. Na tuutafute utakatifu katika hofu ya Mungu.
Dear friends, since we have these promises, we should wash ourselves clean from all that makes both body and spirit dirty, aiming for complete holiness out of reverence for God.
2 Fanyeni nafasi kwa ajili yetu! Hatujamkosea mtu yeyote. Hatukumdhuru mtu yeyote. Hatujajinufaisha kwa faida ya mtu yeyote.
Please accept us as your friends! We haven't done anyone wrong, we haven't corrupted anyone, and we haven't taken advantage of anyone.
3 Nasema hili siyo kwa kuwalaumu. Kwa kuwa nimeshasema kwamba mmo mioyoni mwetu, kwetu sisi kufa pamoja na kuishi pamoja.
I'm not saying this to condemn you—as I already told you, you mean so much to us that we live and die together with you!
4 Nina ujasiri mwingi ndani yenu, na ninajivuna kwa ajili yenu. Nimejawa na faraja. Ninajawa na furaha hata katikati ya mateso yetu yote.
I speak up very strongly for you because I am so proud of you. You are such an encouragement to me. I am so happy for you despite all our troubles.
5 Tulikuja Makedonia, miili yetu haikuwa na pumziko. Badala yake, tulipata taabu kwa namna zote kwa kupigwa vita upande wa nje na hofu upande wa ndani.
When we arrived in Macedonia we didn't have a minute's peace. We were attacked from every direction, with external conflicts and inner fears.
6 Lakini Mungu, anayefariji waliokata tamaa, alitufariji kwa ujio wa Tito.
Even so, God who encourages the downhearted, encouraged us with Titus' arrival.
7 Haikuwa kwa ujio wake tu kwamba Mungu alitufariji. ilikuwa pia faraja zile Tito alizopokea kutoka kwenu. Yeye alituambia upendo mkuu mlionao, huzuni yenu, na mlivyokuwa na wasiwasi kwa ajili yangu. Hivyo nimezidi kuwa na furaha zaidi.
Not just by his arrival, but also by the encouragement you gave him. He told us how you were longing to see me, how sorry you were, and how concerned you were about me, which made me even happier.
8 Hata ingawa waraka wangu uliwafanya kusikitika, mimi siujutii. lakini ninaujutia wakati nilipoona waraka huo uliwafanya ninyi kuwa na huzuni. lakini mlikuwa na huzuni kwa muda mfupi.
Even though I made you sorry by the letter I wrote, I don't regret it—though I did regret it because the letter did hurt you, but just for a while.
9 Sasa nina furaha, si kwa sababu mlikuwa na shida, lakini kwa sababu huzuni zenu iliwaleta kwenye toba. Mlipatwa na huzuni ya kiungu, hivyo mliteswa si kwa hasara kwa sababu yetu.
I'm happy now, not for hurting you, but because this pain led you to change your minds. You were made sorry in a way God would want, and so weren't harmed by us in any way.
10 Kwa kuwa huzuni ya kiungu huleta toba ambayo hukamilisha wokovu bila ya kuwa na majuto. Huzuni ya kidunia, hata hivyo, huleta mauti.
The kind of sorrow God wants us to have makes us change our minds and brings salvation. This kind of sorrow leaves no sense of regret, but worldly sorrow brings death.
11 Angalieni huzuni hii ya kiungu ilizalisha azma gani kubwa ndani yenu. Jinsi gani azma ilikuwa kubwa ndani yenu kuthibitisha kuwa hamkuwa na hatia. Kwa jinsi gani uchungu wenu ulivyokuwa mkubwa, hofu yenu, matamanio yenu, bidii yenu, na shauku yenu kuona kwamba haki inapaswa kutendeka! Katika kila jambo mmethibitisha wenyewe kutokuwa na hatia.
See what happened to you when you had this very same experience of sorrow that God wants. Remember how enthusiastic you became, how keen you were to defend yourselves, how angry you were at what had happened, how seriously you took it, how you longed to do right, how concerned you were, how you wanted justice to be done. In all of this you showed that you were sincere in wanting to make things right.
12 Ingawa niliwaandikia ninyi, sikuandika kwa ajili ya mkosaji, wala si kwa mtu aliyeteswa na maovu. Nimeandika ili kwamba udhati wa mioyo yenu kwa ajili yetu ifanywe kujulikana kwenu mbele ya macho ya Mungu.
So when I wrote to you, I wasn't writing about who did the wrong or who was wronged, but to show you how devoted you are to us in God's sight.
13 Ni kwa ajili ya hii kwamba tunafarijika. Katika nyongeza ya faraja yetu wenyewe, tunafurahi pia, hata zaidi kwa sababu ya furaha ya Tito, kwa kuwa roho yake iliburudishwa na ninyi nyote.
We are so encouraged by this. Added to our own encouragement, we were so pleased to see how happy Titus was, because you set his mind at rest.
14 Kwa kuwa kama nilijivuna kwake kuhusiana na ninyi, sikuwa na aibu. Kinyume chake, kama tu kila neno tulilolisema kwenu lilikuwa kweli, Majivuno yetu kuhusu ninyi kwa Tito yalithibitisha kuwa kweli.
I boasted to him about you, and you didn't let me down. Just as all I've told you is true, my boasting about you to Titus has proved to be true too!
15 Upendo wake kwa ajili yenu hata ni mkubwa zaidi, kama akumbukapo utii wenu nyote, jinsi mlivyomkaribisha yeye kwa hofu na kutetemeka.
Titus cares for you even more as he remembers how you did what he told you, how you welcomed him with great respect.
16 Ninafurahi kwa sababu nina ujasiri kamili ndani yenu.
I am so happy that I can be completely confident of you.

< 2 Wakorintho 7 >