< 2 Wakorintho 6 >
1 Na kwa hiyo, kufanya kazi pamoja, tunawasihi ninyi msiipokee neema ya Mungu pasipo matokeo.
As a worker with him I beseech you not to receive the grace of God in vain.
2 Kwa kuwa anasema, “Wakati uliokubalika nilikuwa makini kwenu, na katika siku ya wokovu niliwasaidia.” Tazama, sasa ni wakati uliokubalika. Tazama, sasa ni siku ya wokovu.
For he said. In an acceptable time have I heard thee, And in the day of salvation have I succored thee. Behold, now is the acceptable time! behold, now is the day of salvation!
3 Hatuweki jiwe la kizuizi mbele ya mtu yeyote, kwa kuwa hatuitakii huduma yetu iletwe katika sifa mbaya.
I am giving no one a cause of stumbling in order that my ministry may not be discredited;
4 Badala yake, tunajihakiki wenyewe kwa matendo yetu yote, kwamba tu watumishi wa Mungu. Tu watumishi wake katika wingi wa ustahimilivu, mateso, dhiki, ugumu wa maisha,
but in every way I am striving to commend myself as God’s minister by stedfast endurance, by afflictions, by troubles, by distresses,
5 kupigwa, vifungo, ghasia, katika kufanya kazi kwa bidii, katika kukosa usingizi usiku, katika njaa,
by floggings, by imprisonment; in riots, in labors, in sleepless watching, in hunger and thirst;
6 katika usafi, maarifa, uvumilivu, wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo halisi.
with purity, understanding, patience, and kindness; by the Holy Spirit, by love sincere,
7 Tu watumishi wake katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu. Tuna silaha ya haki kwa ajili ya mkono wa kuuume na wa kushoto.
by a true teaching and an energy divine; by the weapons of righteousness, for attack or for defense,
8 Tunafanya kazi katika heshima na kudharauliwa, katika kashfa na sifa. Tunatuhumiwa kuwa wadanganyifu na wakati tu wakweli.
amid honor or dishonor, amid evil report and good report; as a deceiver and yet true;
9 Tunafanya kazi kana kwamba hatujulikani na bado tunajulikana vizuri. Tunafanya kazi kama wanaokufa na -Tazama! - bado tunaishi. Tunafanya kazi kama tunaoadhibiwa kwa ajili ya matendo yetu lakini sio kama waliohukumiwa hata kufa.
as unknown and yet well known; as at death’s door, yet, strange to tell, I live on; as chastened, but not killed;
10 Tunafanya kazi kama wenye masikitiko, lakini siku zote tuna furaha. Tunafanya kazi kama maskini, lakini tunatajirisha wengi. Tunafanya kazi kana kwamba hatupati kitu bali kama tunaomiliki kila kitu.
as grieved, but always glad; as poor, but making many rich; as having nothing, yet possessing everything.
11 Tumezungumza ukweli wote kwenu, Wakorintho, na mioyo yetu imefunguka kwa upana.
O Corinthians, I am unsealing my lips to you; my heart is wide open to you.
12 mioyo yenu haizuiliwi na sisi, bali mnazuiliwa na hisia zenu wenyewe.
There is no narrowness in my love; but the narrowness is in your own.
13 Sasa katika kubadilishana kwa haki - ninaongea kama kwa watoto - fungueni mioyo yenu kwa upana.
I pray you, therefore, in fair exchange (I speak as to my children), let your hearts also be wide open to me.
14 Msifungamanishwe pamoja na wasioamini. Kwa kuwa kuna uhusiano gani kati ya haki na uasi? Na kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
Be not unequally yoked with unbelievers; for what fellowship has righteousness with lawlessness? what communion has light with darkness?
15 Ni makubaliano gani Kristo anaweza kuwa nayo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na asiyeamini?
What concord has Christ with Belial? What portion has a believer with an unbeliever?
16 Na kuna makubaliano gani yapo kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi ni hekalu la Mungu aliye hai, kama ambavyo Mungu alisema: “Nitakaa kati yao na kutembea kati yao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
And what compact has God’s temple with idols? For we are a temple of the living God, as he has said. I will dwell among them, and walk about among them; I will be their God, and they will be my people.
17 Kwa hiyo, “Tokeni kati yao, na mkatengwe nao,” asema Bwana. “Msiguse kitu kichafu, na nitawakaribisha ninyi.
Therefore, Come out from among them and separate yourselves, saith the Lord, touch not what is unclean;
18 Nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu wa kiume na wa kike,” asema Bwana Mwenyezi.
then I will receive you and will be to you a Father, and you shall be to me sons and daughters, saith the Lord Almighty.