< 2 Wakorintho 5 >
1 Tunajua kwamba kama maskani ya ulimwenguni ambayo tunaishi humo yanaharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu. Ni nyumba isiyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu, bali ni nyumba ya milele, katika mbingu. (aiōnios )
Nous savons, en effet, que si la maison terrestre qui nous sert de tente est détruite, nous avons un édifice qui vient de Dieu, une maison non faite de main d'homme, éternelle, dans les cieux. (aiōnios )
2 Kwa kuwa katika hema hii tunaugua, tukitamani kuvikwa kwa maskani yetu mbinguni.
C'est là, en effet, que nous gémissons, désirant ardemment être revêtus de la demeure qui est dans les cieux,
3 Tunatamani kwa ajili ya hii kwa sababu kwa kuivaa hatutaonekana kuwa tu uchi.
si toutefois, étant revêtus, nous ne devons pas être trouvés nus.
4 Kwa hakika wakati tuko ndani ya hema hii, twaugua tukilemewa. Hatutaki kuvuliwa. Badala yake, tunataka kuvalishwa, ili kwamba kile kilicho kufa kiweze kumezwa na uzima.
En effet, nous qui sommes dans cette tente, nous gémissons et nous sommes accablés, non que nous désirions être dépouillés, mais nous désirons être revêtus, afin que la vie engloutisse ce qui est mortel.
5 Yule aliyetuandaa sisi kwa kitu hiki ni Mungu, ambaye alitupa sisi Roho kama ahadi ya kile kitakacho kuja.
Or, celui qui nous a créés pour cela, c'est Dieu, qui nous a aussi donné l'acompte de l'Esprit.
6 Kwa hiyo muwe na ujasiri siku zote. Muwe macho kwamba wakati tuko nyumbani katika mwili, tuko mbali na Bwana.
C'est pourquoi nous sommes toujours confiants et nous savons que, pendant que nous sommes chez nous dans le corps, nous sommes absents du Seigneur;
7 Kwa kuwa tunatembea kwa imani, sio kwa kuona. Kwa hiyo tunaujasiri.
car nous marchons par la foi et non par la vue.
8 Ni bora tuwe mbali kutoka kwenye mwili na nyumbani pamoja na Bwana.
Nous sommes courageux, dis-je, et nous voulons plutôt être absents du corps et être chez nous avec le Seigneur.
9 Kwa hiyo tunaifanya kuwa lengo letu, kama tukiwa nyumbani au mbali, tumpendeze yeye.
C'est pourquoi nous nous efforçons de lui être agréables, que nous soyons chez nous ou absents.
10 Kwa kuwa lazima wote tuonekane mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kwamba kila mmoja aweze kupokea kile kinachostahili kwa mambo yaliyofanyika katika mwili, ikiwa ni kwa uzuri au kwa ubaya.
Car il faut que nous soyons tous révélés devant le tribunal du Christ, afin que chacun reçoive ce qui lui revient dans le corps selon ce qu'il a fait, en bien ou en mal.
11 Kwa hiyo, kwa kuijua hofu ya Bwana, tunawashawishi watu. Jinsi tulivyo, inaonekana wazi na Mungu. Ninatumaini kuwa inaeleweka pia kwenye dhamiri zenu.
Connaissant donc la crainte du Seigneur, nous persuadons les hommes, mais nous sommes révélés à Dieu, et j'espère que nous sommes aussi révélés dans vos consciences.
12 Hatujaribu kuwashawishi ninyi tena kutuona sisi kama wakweli. Badala yake, tunawapa ninyi sababu ya kujivuna kwa ajili yetu, ili kwamba muweze kuwa na jibu kwa wale wanaojivunia kuhusu mwonekano lakini sio kile kilicho ndani ya moyo.
Car nous ne nous recommandons pas de nouveau à vous, mais nous parlons comme pour vous donner l'occasion de vous glorifier en notre faveur, afin que vous ayez de quoi répondre à ceux qui se glorifient en apparence et non dans le cœur.
13 Kwa kuwa ikiwa kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu. Na kama tuko kwenye akili zetu timamu, ni kwa ajili yenu.
Car si nous sommes hors de nous-mêmes, c'est pour Dieu. Et si nous sommes sobres d'esprit, c'est pour vous.
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo watushurutisha, kwa sababu tuna uhakika na hili: kuwa mtu mmoja alikufa kwa ajili ya wote, na kwa hiyo wote wamekufa.
Car l'amour du Christ nous y contraint; car nous jugeons ainsi: un seul est mort pour tous, donc tous sont morts.
15 Na Kristo alikufa kwa ajili ya wote, ili kwamba wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe. Badala yake, lazima waishi kwa ajili yake yeye ambaye alikufa na alifufuliwa.
Il est mort pour tous, afin que ceux qui vivent ne vivent plus pour eux-mêmes, mais pour celui qui, pour eux, est mort et ressuscité.
16 Kwa sababu hii, kuanzia sasa na kuendelea hatumuhukumu mtu kulingana na viwango vya wanadamu, ingawa hapo kwanza tulimtazama Kristo katika namna hii. Lakini sasa hatumuhukumu yeyote kwa namna hii tena.
C'est pourquoi nous ne connaissons désormais personne selon la chair. Si nous avons connu le Christ selon la chair, maintenant nous ne le connaissons plus ainsi.
17 Kwa hiyo, ikiwa mtu yeyote yuko ndani ya Kristo, yeye ni kiumbe kipya. Mambo ya kale yamepita. Tazama, yamekuwa mapya.
Ainsi, si quelqu'un est en Christ, il est une nouvelle création. Les choses anciennes ont disparu. Voici, toutes choses sont devenues nouvelles.
18 Vitu vyote hivi vyatoka kwa Mungu. Alitupatanisha sisi kwake mwenyewe kupitia Kristo, na ametupatia huduma ya upatanisho.
Or, tout vient de Dieu, qui nous a réconciliés avec lui par Jésus-Christ, et qui nous a confié le ministère de la réconciliation,
19 Hiyo ni kusema, katika Kristo, Mungu anaupatanisha ulimwengu kwake mwenyewe, sio kuhesabu makosa yao dhidi yao. Anawekeza kwetu ujumbe wa upatanisho.
c'est-à-dire que Dieu a réconcilié le monde avec lui-même en Christ, sans leur imputer leurs fautes, et qu'il nous a confié la parole de la réconciliation.
20 Kwa hiyo tunateuliwa kama wawakilishi wa Kristo, kana kwamba Mungu alikuwa anafanya rufaa yake kupitia sisi. Tunawasihi ninyi kwa ajili ya Kristo: “Mpatanishwe kwa Mungu!”
Nous sommes donc ambassadeurs au nom du Christ, comme si Dieu priait par nous: nous vous en supplions au nom du Christ, soyez réconciliés avec Dieu.
21 Alimfanya Kristo kuwa sadaka kwa ajili ya dhambi zetu. Yeye ndiye ambaye hakutenda dhambi. Alifanya hivi ili tuweze kufanyika haki ya Mungu katika yeye.
Car celui qui n'a pas connu le péché, il l'a fait devenir péché à notre place, afin que nous devenions en lui la justice de Dieu.