< 2 Wakorintho 5 >

1 Tunajua kwamba kama maskani ya ulimwenguni ambayo tunaishi humo yanaharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu. Ni nyumba isiyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu, bali ni nyumba ya milele, katika mbingu. (aiōnios g166)
For I know, if this earthly tent of mine were struck, I have a mansion built by God, a house not made with hands, eternal in the heavens. (aiōnios g166)
2 Kwa kuwa katika hema hii tunaugua, tukitamani kuvikwa kwa maskani yetu mbinguni.
For in this tent I am groaning, earnestly longing to be under the cover of my heavenly habitation; if so be that being so covered,
3 Tunatamani kwa ajili ya hii kwa sababu kwa kuivaa hatutaonekana kuwa tu uchi.
I shall not be found naked.
4 Kwa hakika wakati tuko ndani ya hema hii, twaugua tukilemewa. Hatutaki kuvuliwa. Badala yake, tunataka kuvalishwa, ili kwamba kile kilicho kufa kiweze kumezwa na uzima.
For in this tent of mine I am groaning in deep trouble; not that I wish to be unclothed, but to be clothed upon, that what is mortal may be swallowed up in life.
5 Yule aliyetuandaa sisi kwa kitu hiki ni Mungu, ambaye alitupa sisi Roho kama ahadi ya kile kitakacho kuja.
And He who has wrought me out for this very end is God, who has given me his Spirit as pledge.
6 Kwa hiyo muwe na ujasiri siku zote. Muwe macho kwamba wakati tuko nyumbani katika mwili, tuko mbali na Bwana.
Therefore I am always of good courage, because I well know that while I am at home in the body, I am in banishment from the Lord,
7 Kwa kuwa tunatembea kwa imani, sio kwa kuona. Kwa hiyo tunaujasiri.
for I am walking by faith, not by sight.
8 Ni bora tuwe mbali kutoka kwenye mwili na nyumbani pamoja na Bwana.
So I have good courage, and am well pleased rather, to be in banishment from the body and to be at home with the Lord.
9 Kwa hiyo tunaifanya kuwa lengo letu, kama tukiwa nyumbani au mbali, tumpendeze yeye.
And for this reason I also make it home with the Lord.
10 Kwa kuwa lazima wote tuonekane mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kwamba kila mmoja aweze kupokea kile kinachostahili kwa mambo yaliyofanyika katika mwili, ikiwa ni kwa uzuri au kwa ubaya.
For we must all be made manifest, in our true characters, before the Judgment-seat of Christ; so that each one may receive according to that which he has done in his body, whether good or evil.
11 Kwa hiyo, kwa kuijua hofu ya Bwana, tunawashawishi watu. Jinsi tulivyo, inaonekana wazi na Mungu. Ninatumaini kuwa inaeleweka pia kwenye dhamiri zenu.
So, because I know the fear of God, I "persuade men." What I am is manifest to God, and I hope manifest also to your conscience.
12 Hatujaribu kuwashawishi ninyi tena kutuona sisi kama wakweli. Badala yake, tunawapa ninyi sababu ya kujivuna kwa ajili yetu, ili kwamba muweze kuwa na jibu kwa wale wanaojivunia kuhusu mwonekano lakini sio kile kilicho ndani ya moyo.
I am not "commending myself to you again," but I am giving you an occasion of boasting on my behalf, so that you may have an answer ready for those who boast in externals, and not in the heart.
13 Kwa kuwa ikiwa kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu. Na kama tuko kwenye akili zetu timamu, ni kwa ajili yenu.
For if I was "beside myself," it was to God; of if I am now "of sound mind," it is for you.
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo watushurutisha, kwa sababu tuna uhakika na hili: kuwa mtu mmoja alikufa kwa ajili ya wote, na kwa hiyo wote wamekufa.
For the love of Christ overmasters me; because I thus judge that if One has died for all, then all have died;
15 Na Kristo alikufa kwa ajili ya wote, ili kwamba wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe. Badala yake, lazima waishi kwa ajili yake yeye ambaye alikufa na alifufuliwa.
and that he died for all in order that the living may live no longer for themselves, but for Him who died and rose again for them.
16 Kwa sababu hii, kuanzia sasa na kuendelea hatumuhukumu mtu kulingana na viwango vya wanadamu, ingawa hapo kwanza tulimtazama Kristo katika namna hii. Lakini sasa hatumuhukumu yeyote kwa namna hii tena.
Therefore henceforth I know no one simply as a man - even if I have known Christ as a man, yet now I do so no longer.
17 Kwa hiyo, ikiwa mtu yeyote yuko ndani ya Kristo, yeye ni kiumbe kipya. Mambo ya kale yamepita. Tazama, yamekuwa mapya.
So there is a new creation when any man is in Christ. The old life has passed away, behold, the new is come.
18 Vitu vyote hivi vyatoka kwa Mungu. Alitupatanisha sisi kwake mwenyewe kupitia Kristo, na ametupatia huduma ya upatanisho.
And all this is from God, who through Christ reconciled me to himself, and gave me the ministry of reconciliation;
19 Hiyo ni kusema, katika Kristo, Mungu anaupatanisha ulimwengu kwake mwenyewe, sio kuhesabu makosa yao dhidi yao. Anawekeza kwetu ujumbe wa upatanisho.
how that God was in Christ reconciling a world to himself, not reckoning to men their trespasses; and that to me he has entrusted the message of that reconciliation.
20 Kwa hiyo tunateuliwa kama wawakilishi wa Kristo, kana kwamba Mungu alikuwa anafanya rufaa yake kupitia sisi. Tunawasihi ninyi kwa ajili ya Kristo: “Mpatanishwe kwa Mungu!”
On Christ’s behalf, then, I come as ambassador. It is as though God was entreating you, through me, on Christ’s behalf I beg you to be reconciled to God.
21 Alimfanya Kristo kuwa sadaka kwa ajili ya dhambi zetu. Yeye ndiye ambaye hakutenda dhambi. Alifanya hivi ili tuweze kufanyika haki ya Mungu katika yeye.
Him who knew no sin, in our behalf he has made to be sin; so that in him we might become the righteousness of God.

< 2 Wakorintho 5 >