< 2 Wakorintho 5 >
1 Tunajua kwamba kama maskani ya ulimwenguni ambayo tunaishi humo yanaharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu. Ni nyumba isiyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu, bali ni nyumba ya milele, katika mbingu. (aiōnios )
For we have known that if the tent of our earthly house may be thrown down, we have a building from God, a house not made with hands—perpetual—in the heavens, (aiōnios )
2 Kwa kuwa katika hema hii tunaugua, tukitamani kuvikwa kwa maskani yetu mbinguni.
for also in this we groan, earnestly desiring to clothe ourselves with our dwelling that is from Heaven,
3 Tunatamani kwa ajili ya hii kwa sababu kwa kuivaa hatutaonekana kuwa tu uchi.
if so be that, having clothed ourselves, we will not be found naked,
4 Kwa hakika wakati tuko ndani ya hema hii, twaugua tukilemewa. Hatutaki kuvuliwa. Badala yake, tunataka kuvalishwa, ili kwamba kile kilicho kufa kiweze kumezwa na uzima.
for we also who are in the tent groan, being burdened, seeing we do not wish to unclothe ourselves, but to clothe ourselves, that the mortal may be swallowed up of life.
5 Yule aliyetuandaa sisi kwa kitu hiki ni Mungu, ambaye alitupa sisi Roho kama ahadi ya kile kitakacho kuja.
And He who worked us to this very thing [is] God, who also gave to us the deposit of the Spirit;
6 Kwa hiyo muwe na ujasiri siku zote. Muwe macho kwamba wakati tuko nyumbani katika mwili, tuko mbali na Bwana.
having courage, then, at all times, and knowing that being at home in the body, we are away from home from the LORD—
7 Kwa kuwa tunatembea kwa imani, sio kwa kuona. Kwa hiyo tunaujasiri.
for we walk through faith, not through sight—
8 Ni bora tuwe mbali kutoka kwenye mwili na nyumbani pamoja na Bwana.
we have courage, and are well pleased, rather, to be away from the home of the body, and to be at home with the LORD.
9 Kwa hiyo tunaifanya kuwa lengo letu, kama tukiwa nyumbani au mbali, tumpendeze yeye.
We are also ambitious for this reason, whether at home or away from home, to be well pleasing to Him,
10 Kwa kuwa lazima wote tuonekane mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kwamba kila mmoja aweze kupokea kile kinachostahili kwa mambo yaliyofanyika katika mwili, ikiwa ni kwa uzuri au kwa ubaya.
for it is necessary for all of us to have appeared before the judgment seat of the Christ, that each one may receive the things [done] through the body, in reference to the things that he did, whether good or evil;
11 Kwa hiyo, kwa kuijua hofu ya Bwana, tunawashawishi watu. Jinsi tulivyo, inaonekana wazi na Mungu. Ninatumaini kuwa inaeleweka pia kwenye dhamiri zenu.
having known, therefore, the fear of the LORD, we persuade men, and we are revealed to God, and I also hope to have been revealed in your consciences;
12 Hatujaribu kuwashawishi ninyi tena kutuona sisi kama wakweli. Badala yake, tunawapa ninyi sababu ya kujivuna kwa ajili yetu, ili kwamba muweze kuwa na jibu kwa wale wanaojivunia kuhusu mwonekano lakini sio kile kilicho ndani ya moyo.
for we do not again recommend ourselves to you, but we are giving occasion to you of glorifying in our behalf, that you may have [something] in reference to those glorifying in face and not in heart;
13 Kwa kuwa ikiwa kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu. Na kama tuko kwenye akili zetu timamu, ni kwa ajili yenu.
for whether we were beside ourselves, [it was] to God; whether we be of sound mind, [it is] to you,
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo watushurutisha, kwa sababu tuna uhakika na hili: kuwa mtu mmoja alikufa kwa ajili ya wote, na kwa hiyo wote wamekufa.
for the love of the Christ constrains us, having judged thus: that if one died for all, then the whole died,
15 Na Kristo alikufa kwa ajili ya wote, ili kwamba wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe. Badala yake, lazima waishi kwa ajili yake yeye ambaye alikufa na alifufuliwa.
and He died for all, that those living may no longer live to themselves, but to Him who died for them, and was raised again.
16 Kwa sababu hii, kuanzia sasa na kuendelea hatumuhukumu mtu kulingana na viwango vya wanadamu, ingawa hapo kwanza tulimtazama Kristo katika namna hii. Lakini sasa hatumuhukumu yeyote kwa namna hii tena.
So that we, from now on, have known no one according to the flesh, and even if we have known Christ according to the flesh, yet now we know Him [thus] no longer;
17 Kwa hiyo, ikiwa mtu yeyote yuko ndani ya Kristo, yeye ni kiumbe kipya. Mambo ya kale yamepita. Tazama, yamekuwa mapya.
so that if anyone [is] in Christ—[he is] a new creature; the old things passed away, behold, all things have become new.
18 Vitu vyote hivi vyatoka kwa Mungu. Alitupatanisha sisi kwake mwenyewe kupitia Kristo, na ametupatia huduma ya upatanisho.
And all things [are] of God, who reconciled us to Himself through Jesus Christ, and gave to us the ministry of the reconciliation,
19 Hiyo ni kusema, katika Kristo, Mungu anaupatanisha ulimwengu kwake mwenyewe, sio kuhesabu makosa yao dhidi yao. Anawekeza kwetu ujumbe wa upatanisho.
how that God was in Christ—reconciling the world to Himself, not reckoning to them their trespasses; and having put in us the word of the reconciliation,
20 Kwa hiyo tunateuliwa kama wawakilishi wa Kristo, kana kwamba Mungu alikuwa anafanya rufaa yake kupitia sisi. Tunawasihi ninyi kwa ajili ya Kristo: “Mpatanishwe kwa Mungu!”
in behalf of Christ, then, we are ambassadors, as if God were calling through us, we implore, in behalf of Christ, “Be reconciled to God”;
21 Alimfanya Kristo kuwa sadaka kwa ajili ya dhambi zetu. Yeye ndiye ambaye hakutenda dhambi. Alifanya hivi ili tuweze kufanyika haki ya Mungu katika yeye.
He made Him having not known sin [to be] sin in our behalf, that we may become the righteousness of God in Him.